Ushuhuda wa kuhuzunisha wa Shauritanga girls boarding school.
Nakukumbuka ilikuwa ni 1994 (kama sijakosea) ulipotokea moto kwenye shule tajwa hapo juu ambao uliondoka na mabinti 41 (kama sijakosea tena) kati yao kulikuwa na ndugu wawili.
Tunafahamu ishu za kutoroka shule hasa weekend na kwenda home hasa kama sio mbali.
Weekend hiyo wale mabinti wawili walitoroka na mpango wao ilikuwa wakalale nyumbani na kurudi Shuleni Jumapili.
Wakashinda nyumbani vizuri na wazazi wao ilipofika jioni wakatakiwa kurudi shule (wazazi hawakuwa na lengo baya) mabinti walijitetea kwa nguvu zote mpaka kusaidiwa na mama lakini baba alishikilia msimamo wake..ikabidi waondoke kwa roho nzito mno kurudi Shuleni.
Usiku ule wale mabinti ni kati ya wanafunzi walioteketea na ule moto.
Hawa wazazi walikuwa wameshafunga kizazi hawakutaka kuzaa tena.
Baada ya kupata hizi taarifa na nafikiri kabla ya mazishi waliandika ushuhuda huu nao wakajiua kwa sumu.