Tafakuri ya FaizaFoxy: CCM imetegwa ikategeka?

Tafakuri ya FaizaFoxy: CCM imetegwa ikategeka?

Kuanzia mwaka 2016 mpaka Leo kuna hujuma kubwa sana kwa wafanyabiashara hasa wale waliokuwa wanamshangilia Team nywele nyeupe au wazee wa mabadiliko, Utafanyiwa kila aina ya fugisu za kodi na utasalimu amri tu,

Kadi imenifanya nionekane nipo Team pendwa kwa sasa, wakisikia mzigo wa mtoto wa fulani haina shida

Kumbuka kwa biashara zetu Tanzania ni wachache wanaweza kodi meli yote peke yako, Tunashare meli sasa watu wakiona Team nywele nyeupe kwenye mzigo utapata tabu sana

HIZI BIASHARA ZINAFUNGWA KUNA MAMBO MENGI FAIZA, MENGINE TUNAUMIA NDANI, KUSEMA TUNAOGOPA
FITINA NA UJINGA UMEJAA KATI YA TIMU MBILI ZA MPIRA

Nchi moja tumeamua kuharibu biashara kisa Team za mpira za 2015
Hakuna hujuma yoyote. Ukisoma ilani ya uchaguzi ya CCM utagundua kuwa awamu hii imefikia katika kupambana na ufisadi na hata kwenye ilani kuna mpaka kufunguliwa mahakama ya ufisadi. Na ndicho serikali inachokifanya.

Serikali inajitahidi kupambana na kuzini mia nay ya ufisadi (corruption). Unataka kunambia hakuna wana CCM walioshikwa kwa ufisadi?

Bado hujanijibu, bandarini ukienda kuitoa mizigo yako unaulizwa kadi ya CCM?
 
Ukiwa kwenye madaraka ya kuendesha nchi kuna mengi sana unayoyajuwa kuliko ukiwa nje ya madaraka ya nchi, kuna mengine fitna kuna mengine kweli.

Nnakumbuka Kikwete aliwahi kusema kuna watu "wana viwanda vya uongo". Kwa hiyo usifikiri kila baya linafanywa na chama tawala, kuna watu wana mitego ili tu wakuchafulie. Pia kuna watu wako so "aggressive" wanaweza kufanya chochote ili wakupokonye tonge lako.

Fikra za kuwa mtu anakwenda kwenye kibanda cha kupigia kura huku analazimishwa mpigie fulani ni potofu. Waliochaguliwa ni watu na wamechaguliwa na watu kwa kura za halali kabisa.

Mbona kuna wapinzani bungeni, na wengi walikuwa CCM walipohamia upinzani wakachaguliwa vile vile? Kungekuwa kuna mabavu ungekaa a kina Bulaya, Slaa, Shibuda bungeni?

Fikiri.
FF najua unajua mengi, lakini lazima tukubaliane kuwa CCM ya JK kilikuwa chama cha siasa cha kisiasa na CCM ya JPM ni chama cha siasa cha kidola, kisicho na ushawishi wowote.
Hao wapinzani walio bungeni maeneo mengi waliingia bungeni kwa nguvu kubwa wakati wa JK, na jambo hilo kwa utawala huu ambao unawaambia wasimamizi "nakulipa, nakupa gari ni kisha unamtangaza mpinzani?"haliwezekani
 
Hakuna hujuma yoyote. Ukisoma ilani ya uchaguzi ya CCM utagundua kuwa awamu hii imefikia katika kupambana na ufisadi na hata kwenye ilani kuna mpaka kufunguliwa mahakama ya ufisadi. Na ndicho serikali inachokifanya.

Serikali inajitahidi kupambana na kuzini mia nay ya ufisadi (corruption). Unataka kunambia hakuna wana CCM walioshikwa kwa ufisadi?

Bado hujanijibu, bandarini ukienda kuitoa mizigo yako unaulizwa kadi ya CCM?
Kwa ufupi siwezi ongea hapa yote, Mimi ufisadi na rushwa sijui maana yake Katika maisha yangu

Kama kutoa pesa ili mtoto wangu afanikiwe au biashara zangu ziwe vizuri ni rushwa au ufisadi, Nitaendelea kutoa rushwa

Na kama mzazi wangu kanisomesha kupitia pesa za uwizi toka ccm na kanipa mtaji wa uwizi toka ccm, Bora awe fisadi ili maisha yetu yasiyumbe

Kama kuna tafsiri tofauti na hapo basi nitarudi tena Udsm niwe kama profesa Lipumba au kabudi
 
CCM is dying slowly.
Daniel: 24 Ndipo kile kitanga cha ule mkono kikaletwa kutoka mbele zake, na maandiko haya yameandikwa.
25 Na maandiko yaliyoandikwa ni haya; MENE, MENE, TEKELI, NA PERESI.
26 Na tafsiri ya maneno haya ni hii; MENE, Mungu ameuhesabu ufalme wako na kuukomesha.
27 TEKELI, umepimwa katika mizani nawe umeonekana kuwa umepunguka.
28 PERESI, ufalme wako umegawanyika, nao wamepewa Wamedi na Waajemi.
 
Kwa mtu yeyote aneifahamu Kusini ya mkoa wa Dar Es Salaam ataelewa kuwa ukianza kufika Mtoni (kwa Aziz Ali) kushuka Kusini utakutana na mchezo wa bao la kete (solo).

Bao la kete Kusini ya Tanzania ni mchezo unaochezwa na takriban jamii nzima, kuanzia watoto, vijana hadi wazee, wote, akina mama na akina baba. Bao lina aina ya michezo mingi tofauti. Lakini maarufu ni ule wa kusafiri, kutaka ta, kutembea, kulala na kuulinda Miraji. Ambao hufanyiwa mashindano ya kitaifa. Marehemu Mzee Nyerere alikuwa ni mpenzi wa mchezo huu wa bao.

Licha ya mchezo wa bao kuwepo takriban Tanzania nzima, lakini mchezo huo Kusini umekuwa maarufu zaidi kwa kuwa kwanza inajulikana wachongaji mabao mazuri ya nakshi ni wamakonde, na kusini ndiyo kwao. Pili, mikete, miti ambayo hudondosha kokwa za kete zinazochezewa bao ipo mingi Kusini.

Kwanini nimelikumbuka bao? Bao Lina mitago na mahesabu ya hali ya juu sana kwa wenye kulijuwa kulicheza vizuri, wanaweza kumtega mtu mpaka mizunguko mitano ijayo na kila mzunguko aliyetegwa atakuwa anahisi anashinda tu lakini ndiyo anazidi kumtengenezea njia ya ushindi aliyemtega.

CCM siku za nyuma kidogo imepokea wapinzani wengi sana waliotokea vyama vya upinzani kutoka kada mbali mbali, kuanzia washabiki na wanachama wa kawaida, wenyeviti wa serikali za mitaa, madiwani, wabunge na wengi wengine.

Jee, huu siyo mtego wa upinzani kupandikiza mapandikizi ya kuja kuisambaratisha CCM? Jee, CCM imetegwa ikategeka? CCM tunachezewa "chess" au bao?

Upinzani wa Tanzania unaweza kuwa na vichwa na mahesabu na mitago ya kisiasa kama mahesabu na mitego ya mabingwa wa bao kama Mzee Nyerere, vya kuweza kutega mizunguko mitano ijayo?

Ni tafakuri tu ya FaizaFoxy.
Mke wangu siku hizi bana ha ha ha ha ha
 
Dada Faiza .... tatizo watanzania wengi wanasiasa wanaitikadi za kuedekeza njaa zao zaidi kuliko kutetea maslahi ya wananchi tena walio masikini na wahitaji ..... bado sana
 
Habari za siku bibi?pole na kazi bibi,tangu awamu yako pendwa itoke madarakani umekuwa kmya sana bibi
 
Hakuna wapinzani waliohamia ccm, ila kuna wapinzani waliomfuata Magufuli ndio maana wengi hata wakijaribu kuchangamana na wana CCM asilia wanaonekana kabisa hawana mikia.

Uhai wa Wanaccm Magufuli ni uwepo wa Magufuli, siku Magufuli akiondoka na wao hawana chao.

Ndio maana wanasema tunaunga mkono juhudi za Rais sio juhudi za CCM, wengi CCM hawaiheshimu kabisa sababu sio ndio iliyowapa kula.

Kuhusu CCM kutegwa, sijaona upinzani wenye nguvu hizo kwa sasa.... Maana mamluki lazima uwe na uwezo wa kumlipa....

Sasa wapinzani wenye uwezo wa kuwalipa mamluki hawapo kwa sasa.

Wanasiasa wetu wengi wao ni njaa tu.
 
Si kweli. Ingekuwa hivyo tusingeona wenyeviti wa serikali za mitaa, vijiji, madiwani na wabunge wa upinzani.

CCM ni chama cha kupigiwa mfano duniani.

Ccm sio chama cha siasa bali ni taasisi ya kidola iliyojivika koti la chama cha siasa. Chama kinachotegemea madaraka ya rais kuagiza tume ya uchaguzi na vyombo vya dola kuhakikisha wanatangazwa washindi utasema hicho ni chama cha siasa. Chama cha siasa ni ushawishi wa hoja na sio matumizi ya nguvu.
 
Ungesubiri ufungue na kupata service ya mumeo ndo ulete huu uchafu wako Faiza Foxy.
 
Mitego ya CCM ni ipi zaidi ya;
- Time isiyo huru
- Polisi walio chini ya mamlaka ya CCM
- Wasimamizi wa uchaguzi ni wateule wa Mwenyekiti wa CCM
- Wizi wa hela za uma kuendesha kampeni za chama
- Kujipa madaraka zaidi ya katiba, upinzani no siasa no mkutano; CCM mikutano ruksa
- Kuhodhi maamuzi kwenye usimamizi wa vyombo vya habari.
 
Ule ushindi wa asubuhi aliotabiri lowasa na mbowe 2015 upo wapi

Nakumbuka tambo za wanasiasa wa upinzani kwenye kila uchaguzi kuanzia 1995 ni kuwa wanakwenda kushinda uchaguzi ukishapita wanasema wameibiwa huu umekuwa wimbo wa taifa


Hata chaguzi za serkal za mitaa ambao NEC hawapo nani anawaibia

Uzi huu unaandikwa na MTU aliyeshiba daku na kuvimbiwa tu
 
Maana jinsi Magufuli na Bashiri walivyousambaratisha upinzani na tunavyoona jinsi wimbi la upinzani lililorudi CCM, inatisha, inabidi mtu ujiulize na kufikiri nje ya boksi.

Usimchanganye Bashiru maana yeye ni kenge kwenye msafara wa mamba. Na upinzani haujasambaratika bali madaraka ya rais yanatumika vibaya kuhakikisha upinzani haufanyi shughuli zake za vyama vya siasa. Kitisho kikubwa kwa upinzani ni matumizi ya risasi za moto na kutekwa. Hakuna popote mtu mwenye akili timamu anaweza kusimama na kusema upinzani unesambaratika kwa mantiki ya ushindani wa kisiasa, maana huo ushindani wa kisiasa haupo zaidi ya mabavu.

Huyo Bashiru ni kama kijakazi tu huko ccm kuhadaa umma kwamba kuna siasa inafanyika, lakini ukweli wanaofanya siasa za ccm kwa sasa ni watu wasiojulikana, akina Musiba, Makonda, vyombo vya dola nk.
 
Si kweli. Ingekuwa hivyo tusingeona wenyeviti wa serikali za mitaa, vijiji, madiwani na wabunge wa upinzani.

CCM ni chama cha kupigiwa mfano duniani.

Hao walipatikana kipindi cha JK wakati demokrasia ilipokuwa inaheshimiwa kwa mbali.
 
FaizaFoxy ukumbuke kujiunga ccm ni rahisi ila kufungamana na ccm si kazi rahisi. Ndani ya chama huwa kuna ccm core na hata nikuhakikishie mtu kama nape pamoja na wakati ule kuwa mwenezi, hakuweza kuaminiwa na core ya ccm baada ya 2010 yeye na Sitta kujaribu kunzisha CCK. Hii kitu ndiyo inamtafuna. Kwa mantiki hiyo usiwe na wasiwasi na watu kama Salary Slip, kwa mfano, watu wasiokuwa na itikadi ambao walitutangazia hapa kuwa JK tarehe atakayotoka madarakani atakuwa anaiadhimisha ingawa leo anatuaminisha kuwa alikuwa kiongozi wa kuigwa! Ajabu.
 
Back
Top Bottom