Tafakuri ya FaizaFoxy: CCM imetegwa ikategeka?

Tafakuri ya FaizaFoxy: CCM imetegwa ikategeka?

FaizaFoxy

Platinum Member
Joined
Apr 13, 2011
Posts
100,506
Reaction score
123,802
Kwa mtu yeyote aneifahamu Kusini ya mkoa wa Dar Es Salaam ataelewa kuwa ukianza kufika Mtoni (kwa Aziz Ali) kushuka Kusini utakutana na mchezo wa bao la kete (solo).

Bao la kete Kusini ya Tanzania ni mchezo unaochezwa na takriban jamii nzima, kuanzia watoto, vijana hadi wazee, wote, akina mama na akina baba. Bao lina aina ya michezo mingi tofauti. Lakini maarufu ni ule wa kusafiri, kutakata, kutembea, kulala na kuulinda mtaji. Ambao hufanyiwa mashindano ya kitaifa. Marehemu Mzee Nyerere alikuwa ni mpenzi wa mchezo huu wa bao na alikuwa bingwa.

Licha ya mchezo wa bao kuwepo takriban Tanzania nzima, lakini mchezo huo Kusini umekuwa maarufu zaidi kwa kuwa kwanza inajulikana wachongaji mabao mazuri ya nakshi ni wamakonde, na kusini ndiyo kwao. Pili, "mikete", miti ambayo hudondosha kokwa za kete zinazochezewa bao ipo mingi Kusini.

Kwanini nimelikumbuka bao? Bao Lina mitego na mahesabu ya hali ya juu sana kwa wenye kulijuwa kulicheza vizuri, wanaweza kumtega mtu mpaka mizunguko mitano ijayo na kila mzunguko aliyetegwa atakuwa anahisi anashinda tu lakini ndiyo anazidi kumtengenezea njia ya ushindi aliyemtega.

CCM siku za nyuma kidogo imepokea wapinzani wengi sana waliotokea vyama vya upinzani kutoka kada mbali mbali, kuanzia washabiki na wanachama wa kawaida, wenyeviti wa serikali za mitaa, madiwani, wabunge na wengi wengine.

Jee, huu siyo mtego wa upinzani kupandikiza mapandikizi ya kuja kuisambaratisha CCM? Jee, CCM imetegwa ikategeka? CCM tunachezewa "chess" au bao?

Upinzani wa Tanzania unaweza kuwa na vichwa na mahesabu na mitago ya kisiasa kama mahesabu na mitego ya mabingwa wa bao kama Mzee Nyerere, vya kuweza kutega mizunguko mitano ijayo?

Ni tafakuri tu ya FaizaFoxy.
 
Upinzani hakuna mtu mwenye uwezo huo!

Kwanza kwa upinzani huu wa kina Nyarandu na Sumaye, ni rahisi sana ccm kupandikiza mapandikizi huko.

Na wangekuwa na jeuri hiyo wangekuwa wanawagundua mapema wale wanao hama kisha wana wafukuza.
 
Upinzani hakuna mtu mwenye uwezo huo!

Kwanza kwa upinzani huu wa kina Nyarandu na Sumaye, ni rahisi sana ccm kupandikiza mapandikizi huko.

Na wangekuwa na jeuri hiyo wangekuwa wanawagundua mapema wale wanao hama kisha wana wafukuza.
Maana jinsi Magufuli na Bashiri walivyousambaratisha upinzani na tunavyoona jinsi wimbi la upinzani lililorudi CCM, inatisha, inabidi mtu ujiulize na kufikiri nje ya boksi.
 
CCM siku za nyuma kidogo imepokea wapinzani wengi sana waliotokea vyama vya upinzani kutoka kada mbali mbali, kuanzia washabiki na wanachama wa kawaida, wenyeviti wa serikali za mitaa, madiwani, wabunge na wengi wengine.

Jee, huu siyo mtego wa upinzani kupandikiza mapandikizi ya kuja kuisambaratisha CCM? Jee, CCM imetegwa ikategeka? CCM tunachezewa "chess" au bao?
Umefikiria nini mpaka kuja kulinganisha bao na CCM?
 
Si kweli. Ingekuwa hivyo tusingeona wenyeviti wa serikali za mitaa, vijiji, madiwani na wabunge wa upinzani.

CCM ni chama cha kupigiwa mfano duniani.
Mimi binafsi nimetafuta kadi ya CCM kwa shinikizo la Mzee wangu, Mwaka 2015 nyumba nzima Yeye pekee alikuwa anasifia ccm kisa anapata pesa na cheo kupitia huko ccm

Leo hii yeye anakumbuka bora angetusikiliza, maana alikuwa mbogo hata kwa mke wake, Anaona chama kinaharibika kimeingiliwa na mamluki wageni

Mimi binafsi nashukuru baada ya kuwa na kadi, Mzee akanitambulisha baadhi ya maeneo ya wana ccm mkakati sasa Biashara na mambo yangu yamenyooka, Sisumbuliwi sana kutoa vitu bandari

Nitaponda ccm lakini kuna muda nasifia kuangalia maslahi yangu binafsi yasiharibike
 
Mimi binafsi nimetafuta kadi ya CCM kwa shinikizo la Mzee wangu, Mwaka 2015 nyumba nzima Yeye pekee alikuwa anasifia ccm kisa anapata pesa na cheo kupitia huko ccm

Leo hii yeye anakumbuka bora angetusikiliza, maana alikuwa mbogo hata kwa mke wake, Anaona chama kinaharibika kimeingiliwa na mamluki wageni

Mimi binafsi nashukuru baada ya kuwa na kadi, Mzee akanitambulisha baadhi ya maeneo ya wana ccm mkakati sasa Biashara na mambo yangu yamenyooka, Sisumbuliwi sana kutoa vitu bandari

Nitaponda ccm lakini kuna muda nasifia kuangalia maslahi yangu binafsi yasiharibike

Kwani huko bandarini ukitoa mzigo unaulizwa kadi ya CCM?
 
Kinachotakiwa ni ccm kujitahidi kuboresha huduma vijijini na kuongeza mzunguko wa pesa, kuzingatia katiba na kuheshimu haki za binadamu, kuacha uhuru wa kuongea

Haya mambo ya Kiingereza hayana umuhimu sana

Upinzani huwezi kuufuta, Mimi mwenyewe Mzee alienilea na kunisomesha bado nilikuwa sikubaliani nae 2015 kuhusu ccm,

Lakini kwa kuwa nilinsikiliza kama mzazi niwe na kadi ya CCM nikafanya hivyo kama maslahi ya biashara zangu, Mzazi aliangalia mustakabali wa biashara zangu akanishauri nichukue kadi ya ccm

Nitaendelea kupinga makosa ya ccm, Lakini inapofika kwenye maslahi ya biashara zangu nitasifia ccm
 
Kwani huko bandarini ukitoa mzigo unaulizwa kadi ya CCM?
Kuanzia mwaka 2016 mpaka Leo kuna hujuma kubwa sana kwa wafanyabiashara hasa wale waliokuwa wanamshangilia Team nywele nyeupe au wazee wa mabadiliko, Utafanyiwa kila aina ya fugisu za kodi na utasalimu amri tu,

Kadi imenifanya nionekane nipo Team pendwa kwa sasa, wakisikia mzigo wa mtoto wa fulani haina shida

Kumbuka kwa biashara zetu Tanzania ni wachache wanaweza kodi meli yote peke yako, Tunashare meli sasa watu wakiona Team nywele nyeupe kwenye mzigo utapata tabu sana

HIZI BIASHARA ZINAFUNGWA KUNA MAMBO MENGI FAIZA, MENGINE TUNAUMIA NDANI, KUSEMA TUNAOGOPA
FITINA NA UJINGA UMEJAA KATI YA TIMU MBILI ZA MPIRA

Nchi moja tumeamua kuharibu biashara kisa Team za mpira za 2015
 
Maana jinsi Magufuli na Bashiri walivyousambaratisha upinzani na tunavyoona jinsi wimbi la upinzani lililorudi CCM, inatisha, inabidi mtu ujiulize na kufikiri nje ya boksi.
Kama wanasambaratisha upinzani woga wao wa nini hadi kutumia vitisho, ubabe na hata uhalifu wa kuteka na kujeruhi?
Nguvu ya chama cha siasa ni ushawishi wa hoja na sio mabavu, imekuwaje ccm ya sasa imeishiwa hoja imebaki na hayo mengine?
Na sasa hivi wakurugenzi wameondolewa kusimamia uchaguzi na mahakama, iweje bado serikali ya ccm inataka kuleta hila ili makada wake hao wasimamie?
Tuwe wakweli, CCM ya Jk ilikuwa Chama cha siasa lakini hii ya JPM sio chama cha siasa bali kitu kingine kabisa.
 
Kama wanasambaratisha upinzani woga wao wa nini hadi kutumia vitisho, ubabe na hata uhalifu wa kuteka na kujeruhi?
Nguvu ya chama cha siasa ni ushawishi wa hoja na sio mabavu, imekuwaje ccm ya sasa imeishiwa hoja imebaki na hayo mengine?
Na sasa hivi wakurugenzi wameondolewa kusimamia uchaguzi na mahakama, iweje bado serikali ya ccm inataka kuleta hila ili makada wake hao wasimamie?
Tuwe wakweli, CCM ya Jk ilikuwa Chama cha siasa lakini hii ya JPM sio chama cha siasa bali kitu kingine kabisa.
Ukiwa kwenye madaraka ya kuendesha nchi kuna mengi sana unayoyajuwa kuliko ukiwa nje ya madaraka ya nchi, kuna mengine fitna kuna mengine kweli.

Nnakumbuka Kikwete aliwahi kusema kuna watu "wana viwanda vya uongo". Kwa hiyo usifikiri kila baya linafanywa na chama tawala, kuna watu wana mitego ili tu wakuchafulie. Pia kuna watu wako so "aggressive" wanaweza kufanya chochote ili wakupokonye tonge lako.

Fikra za kuwa mtu anakwenda kwenye kibanda cha kupigia kura huku analazimishwa mpigie fulani ni potofu. Waliochaguliwa ni watu na wamechaguliwa na watu kwa kura za halali kabisa.

Mbona kuna wapinzani bungeni, na wengi walikuwa CCM walipohamia upinzani wakachaguliwa vile vile? Kungekuwa kuna mabavu ungewaona akina Bulaya, Slaa, Shibuda bungeni?

Fikiri.
 
Jee, huu siyo mtego wa upinzani kupandikiza mapandikizi ya kuja kuisambaratisha CCM? Jee, CCM imetegwa ikategeka? CCM tunachezewa "chess" au bao?

Upinzani wa Tanzania unaweza kuwa na vichwa na mahesabu na mitago ya kisiasa kama mahesabu na mitego ya mabingwa wa bao kama Mzee Nyerere, vya kuweza kutega mizunguko mitano ijayo?
I wish 'Wapinzani' wangekuwa na uwezo wa kupanga mbinu kama hizo.

Hao unaowaona wakihama vyama vyao na kukimbilia 'CCM' ni baada ya kuona 'ulaji' waliokuwa wameandaliwa huko wanakopokelewa. Hakuna la zaidi ya hapo.
Akina Mkumbo, 'Tumbili', Mama Mgwai, na hasa watu kama Dr Mihogo walipojazwa matumbo, ni wachache tu walioko huko ndani ya upinzania ambao hawakutamani na wao wajaribu bahati yao.
Kwa hiyo, maoni yangu ni kwamba, wengi wa hao,kama sio wote waliohamia CCM kutoka upinzani ni watafuta fursa.

Napenda kuwekea uzito hoja yangu hii kwa tafakuri.
Kati ya hao waliohama, kuna mwanachama yeyote aliyezungumzia sababu yake ya kuhama iliyojikita kwenye imani yake katika jambo lolote mbali ya "kumuunga mkono Mwenyekiti?" Kuna yeyote aliyeelezea kwa kina 'sera' mpya zilizoibuliwa CCM kwamba ndizo zilizomfanya avutiwe nazo?
Hawa hawana chochote wanachokiamini katika siasa zao, bali kujaza matumbo yao.

Lawama kwa vyama vya upinzani - hawana tofauti kubwa na CCM, kwa sababu hawawaandai, na kuwapika wanachama wao wakaamini wanchokisimamia, mbali ya kuwaondoa CCM ili na wao wapate fursa ya kwenda kula!
(Itanibidi hapa niungame - hata kwa kujua hili, leo hii pakitokea uchaguzi nitawapigia wapinzani licha ya madhaifu yao). Sababu za kufanya hivyo ninazo, lakini huo ni mjadala mwingine.

Mh Lowassa alipohama CCM, hakuhama kwa sabau ya sera nzuri alizoziona huko kwenye vyama vya upinzani. Amerudi CCM, sio kwa sababu CCM sasa hivi ina sera nzuri zaidi ya zile alizokimbia wakati ule. Kama huyu mzee aliweza kufanya hivyo, hawa maskini wenye njaa wataacha kwenda kuliko na neema?

Nimalize habari hii, imekuwa ndefu: tuombe patokee muujiza Tanzania, 2020 (ndio utakuwa ni muujiza, kwa sababu haitegemewi itokee vyama vya upinzani washinde, kwa haki au kwa maguvu) Njaa itahamia CCM. Sijui tunaowaona leo hii wakijibaraguza huko watafanya sarakasi zipi ili wawe ndani ya (upinzani) ambao sasa ndio watakuwa wanagawia wenye matumbo yao shibe.
 
Magu ni failure sio katika uchumi tu na mambo mengine kama diplomasia,bali ni failure hata katika swala zima la kufanya siasa.

Uwezo wa huyu mtu uko katika kutumia mabavu zaidi kuliko akili, hivyo atawagharimu sana nyie masisiem na chama chenu.
 
Back
Top Bottom