Tafakuri ya FaizaFoxy: CCM imetegwa ikategeka?

Tafakuri ya FaizaFoxy: CCM imetegwa ikategeka?

Hakuna hujuma yoyote. Ukisoma ilani ya uchaguzi ya CCM utagundua kuwa awamu hii imefikia katika kupambana na ufisadi na hata kwenye ilani kuna mpaka kufunguliwa mahakama ya ufisadi. Na ndicho serikali inachokifanya.

Serikali inajitahidi kupambana na kuzini mia nay ya ufisadi (corruption). Unataka kunambia hakuna wana CCM walioshikwa kwa ufisadi?

Bado hujanijibu, bandarini ukienda kuitoa mizigo yako unaulizwa kadi ya CCM?
Amesema ana kadi ya CCM ,hivyo ni mwana CCM anayetambulika,kwani wewe hapo unapoishi si unafahamika kwa wenyeji wako? Sasa aulizwe kadi ya nn?
 
Kwa ufupi siwezi ongea hapa yote, Mimi ufisadi na rushwa sijui maana yake Katika maisha yangu

Kama kutoa pesa ili mtoto wangu afanikiwe au biashara zangu ziwe vizuri ni rushwa au ufisadi, Nitaendelea kutoa rushwa

Na kama mzazi wangu kanisomesha kupitia pesa za uwizi toka ccm na kanipa mtaji wa uwizi toka ccm, Bora awe fisadi ili maisha yetu yasiyumbe

Kama kuna tafsiri tofauti na hapo basi nitarudi tena Udsm niwe kama profesa Lipumba au kabudi
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
Kwa mtu yeyote aneifahamu Kusini ya mkoa wa Dar Es Salaam ataelewa kuwa ukianza kufika Mtoni (kwa Aziz Ali) kushuka Kusini utakutana na mchezo wa bao la kete (solo).

Bao la kete Kusini ya Tanzania ni mchezo unaochezwa na takriban jamii nzima, kuanzia watoto, vijana hadi wazee, wote, akina mama na akina baba. Bao lina aina ya michezo mingi tofauti. Lakini maarufu ni ule wa kusafiri, kutaka ta, kutembea, kulala na kuulinda Miraji. Ambao hufanyiwa mashindano ya kitaifa. Marehemu Mzee Nyerere alikuwa ni mpenzi wa mchezo huu wa bao.

Licha ya mchezo wa bao kuwepo takriban Tanzania nzima, lakini mchezo huo Kusini umekuwa maarufu zaidi kwa kuwa kwanza inajulikana wachongaji mabao mazuri ya nakshi ni wamakonde, na kusini ndiyo kwao. Pili, mikete, miti ambayo hudondosha kokwa za kete zinazochezewa bao ipo mingi Kusini.

Kwanini nimelikumbuka bao? Bao Lina mitago na mahesabu ya hali ya juu sana kwa wenye kulijuwa kulicheza vizuri, wanaweza kumtega mtu mpaka mizunguko mitano ijayo na kila mzunguko aliyetegwa atakuwa anahisi anashinda tu lakini ndiyo anazidi kumtengenezea njia ya ushindi aliyemtega.

CCM siku za nyuma kidogo imepokea wapinzani wengi sana waliotokea vyama vya upinzani kutoka kada mbali mbali, kuanzia washabiki na wanachama wa kawaida, wenyeviti wa serikali za mitaa, madiwani, wabunge na wengi wengine.

Jee, huu siyo mtego wa upinzani kupandikiza mapandikizi ya kuja kuisambaratisha CCM? Jee, CCM imetegwa ikategeka? CCM tunachezewa "chess" au bao?

Upinzani wa Tanzania unaweza kuwa na vichwa na mahesabu na mitago ya kisiasa kama mahesabu na mitego ya mabingwa wa bao kama Mzee Nyerere, vya kuweza kutega mizunguko mitano ijayo?

Ni tafakuri tu ya FaizaFoxy.

Sijaelewa haya maneno
1.Miraji
2.mitago
Wewe shule ulienda kuuza visheti
 
Ule ushindi wa asubuhi aliotabiri lowasa na mbowe 2015 upo wapi

Nakumbuka tambo za wanasiasa wa upinzani kwenye kila uchaguzi kuanzia 1995 ni kuwa wanakwenda kushinda uchaguzi ukishapita wanasema wameibiwa huu umekuwa wimbo wa taifa


Hata chaguzi za serkal za mitaa ambao NEC hawapo nani anawaibia

Uzi huu unaandikwa na MTU aliyeshiba daku na kuvimbiwa tu
Mbona hueleweki uko upande UPI,nyoosha maelezo.
 
Si kweli. Ingekuwa hivyo tusingeona wenyeviti wa serikali za mitaa, vijiji, madiwani na wabunge wa upinzani.

CCM ni chama cha kupigiwa mfano duniani.
Ni kweli maana hata hao wapinzan walioshinda......ni nguvu ya umma ilitumika kushinikiza atangazwe mshindi
 
Maana jinsi Magufuli na Bashiri walivyousambaratisha upinzani na tunavyoona jinsi wimbi la upinzani lililorudi CCM, inatisha, inabidi mtu ujiulize na kufikiri nje ya boksi.
Msambaratishaji anapiga na kuzeza peke yake,ana kila kinachohitajika katika uwanja wa sherehe,visivyo na nasaba ya sherehe vinajinasibisha kwa ama nguvu au kutokuelewa.
Katika mazingira hayo usipofanya sherehe ya kufana kwa tamaa yako basi wewe hujui furaha unayoitaka.
Kama ni sherehe ya kijiji basi uwanja uwe wazi,mazingira yasijali kabila hapo kijijini,imani wala itikadi na hapo ndiyo tuone kama kweli wanakijiji wote mi waumini wa sherehe hiyo au akitokea wa kuweka kigoma chake pembeni atapata wachezaji.
 
Tanzania hii CCM ni Tatizo lakini hata Upinzani ni Tatizo Pia
 
Magu ni failure sio katika uchumi tu na mambo mengine kama diplomasia,bali ni failure hata katika swala zima la kufanya siasa.

Uwezo wa huyu mtu uko katika kutumia mabavu zaidi kuliko akili, hivyo atawagharimu sana nyie masisiem na chama chenu.
Amejaa Chuki na Roho ya Kikatiri tu.
 
hakuna Mpinzani mwenye Akili hiyo kwa TZ wote ni wachunia tumbo

ukiona mpinzani amehamia CCM ujue ameenda kula nchi tu kama ilivyo kawaida ya wanasiasa wote duniani
 
Magu ni failure sio katika uchumi tu na mambo mengine kama diplomasia,bali ni failure hata katika swala zima la kufanya siasa.

Uwezo wa huyu mtu uko katika kutumia mabavu zaidi kuliko akili, hivyo atawagharimu sana nyie masisiem na chama chenu.
Analigharimu taifa pia
 
Mimi binafsi nimetafuta kadi ya CCM kwa shinikizo la Mzee wangu, Mwaka 2015 nyumba nzima Yeye pekee alikuwa anasifia ccm kisa anapata pesa na cheo kupitia huko ccm

Leo hii yeye anakumbuka bora angetusikiliza, maana alikuwa mbogo hata kwa mke wake, Anaona chama kinaharibika kimeingiliwa na mamluki wageni

Mimi binafsi nashukuru baada ya kuwa na kadi, Mzee akanitambulisha baadhi ya maeneo ya wana ccm mkakati sasa Biashara na mambo yangu yamenyooka, Sisumbuliwi sana kutoa vitu bandari

Nitaponda ccm lakini kuna muda nasifia kuangalia maslahi yangu binafsi yasiharibike
Hata mimi nina kadi ya CCM nilichukua 2017, geresha tu kuyarubuni haya majambazi ya Taifa
 
I wish 'Wapinzani' wangekuwa na uwezo wa kupanga mbinu kama hizo.
Hao unaowaona wakihama vyama vyao na kukimbilia 'CCM' ni baada ya kuona 'ulaji' waliokuwa wameandaliwa huko wanakopokelewa. Hakuna la zaidi ya hapo.
Akina Mkumbo, 'Tumbili', Mama Mgwai, na hasa watu kama Dr Mihogo walipojazwa matumbo, ni wachache tu walioko huko ndani ya upinzania ambao hawakutamani na wao wajaribu bahati yao.
Kwa hiyo, maoni yangu ni kwamba, wengi wa hao,kama sio wote waliohamia CCM kutoka upinzani ni watafuta fursa.
Napenda kuwekea uzito hoja yangu hii kwa tafakuri.
Kati ya hao waliohama, kuna mwanachama yeyote aliyezungumzia sababu yake ya kuhama iliyojikita kwenye imani yake katika jambo lolote mbali ya "kumuunga mkono Mwenyekiti?" Kuna yeyote aliyeelezea kwa kina 'sera' mpya zilizoibuliwa CCM kwamba ndizo zilizomfanya avutiwe nazo?
Hawa hawana chochote wanachokiamini katika siasa zao, bali kujaza matumbo yao.
Lawama kwa vyama vya upinzani - hawana tofauti kubwa na CCM, kwa sababu hawawaandai, na kuwapika wanachama wao wakaamini wanchokisimamia, mbali ya kuwaondoa CCM ili na wao wapate fursa ya kwenda kula!
(Itanibidi hapa niungame - hata kwa kujua hili, leo hii pakitokea uchaguzi nitawapigia wapinzani licha ya madhaifu yao). Sababu za kufanya hivyo ninazo, lakini huo ni mjadala mwingine.
Mh Lowassa alipohama CCM, hakuhama kwa sabau ya sera nzuri alizoziona huko kwenye vyama vya upinzani. Amerudi CCM, sio kwa sababu CCM sasa hivi ina sera nzuri zaidi ya zile alizokimbia wakati ule. Kama huyu mzee aliweza kufanya hivyo, hawa maskini wenye njaa wataacha kwenda kuliko na neema?
Nimalize habari hii, imekuwa ndefu: tuombe patokee muujiza Tanzania, 2020 (ndio utakuwa ni muujiza, kwa sababu haitegemewi itokee vyama vya upinzani washinde, kwa haki au kwa maguvu) Njaa itahamia CCM. Sijui tunaowaona leo hii wakijibaraguza huko watafanya sarakasi zipi ili wawe ndani ya (upinzani) ambao sasa ndio watakuwa wanagawia wenye matumbo yao shibe.

Nakuunga mkono kwa 100%. Wanasiasa karibia wote wa nchi yetu; wawe ni wa ccm, chadema, cuf, nk wamejikita zaidi kwenye kutetea kwanza matumbo yao, halafu vyama vyao, na mwisho kabisa ndipo waangalie maslahi ya nchi. Na hii imekuwa sababu kubwa kama nchi kushindwa kupiga hatua kubwa kimaendeleo na kubakia kuwa moja nchi maskini duniani huku tukiwa tumejaliwa kila aina ya utajiri.

Hivyo hao wapinzani waliokimbilia ccm kwa kigezo cha kuunga mkono juhudi, siyo mamluki! Ni wachumia tumbo tu. Njaa na maslahi binafsi ndiyo sababu kubwa. Athari yake ndani ya ccm ni furaha kwetu sisi wapenda mabadiliko! maana utakapowadia muda wa uchaguzi mkuu hasa ule wa 2025, iwapo Rais wa sasa atakubali kuondoka madarakani kwa mujibu wa sheria, basi tutegemee ccm kupitia kipindi kigumu zaidi ya kile cha 2015.
 
Upinzani hamna mkakati NDAKINDAKI wa kwenda ikulu,bali wana group la watu wenye sauti zinazofanana lakini shabaha tofauti.
 
Wapinzani hawana Mbinu kama hizo,na hawana uwezo wa kupanga suala kama hilo!!

Nashangaa uyatambui mambo kama haya, wao wako busy na siasa za matukio ya Muda mfupi mfupi
Kama vile., Magufuli hajui kizungu! Massele, CAG ,

Natamani tuupate upinzani imara usiokuwa na mizengwe,
 
Ukiwa kwenye madaraka ya kuendesha nchi kuna mengi sana unayoyajuwa kuliko ukiwa nje ya madaraka ya nchi, kuna mengine fitna kuna mengine kweli.

Nnakumbuka Kikwete aliwahi kusema kuna watu "wana viwanda vya uongo". Kwa hiyo usifikiri kila baya linafanywa na chama tawala, kuna watu wana mitego ili tu wakuchafulie. Pia kuna watu wako so "aggressive" wanaweza kufanya chochote ili wakupokonye tonge lako.

Fikra za kuwa mtu anakwenda kwenye kibanda cha kupigia kura huku analazimishwa mpigie fulani ni potofu. Waliochaguliwa ni watu na wamechaguliwa na watu kwa kura za halali kabisa.

Mbona kuna wapinzani bungeni, na wengi walikuwa CCM walipohamia upinzani wakachaguliwa vile vile? Kungekuwa kuna mabavu ungewaona akina Bulaya, Slaa, Shibuda bungeni?

Fikiri.
Umeongea kweli kabisa!

Mfano kipindi cha JK tulikuwa tunaambiwa kila lori unaloliona ni la Riz 1, kituo kipya cha mafuta kikianzishwa ni cha Riz 1, mahotel makubwa yote ya riz1.

Yani ulikuwa uongo mtupu.
 
Wakati wa JK sio ninyi watanzania mlimtuhumu kuwa amekigawa chama kwa makundi ya wanamtandao na ccm nyingine sijui zalendo?
Leo tena jk was better than?
Akiondoka jpm nina hakika atakaekuja atasemwa ni the baddest...sisi watanzania kituelewa yataka digirii ya unafiki.
FF najua unajua mengi, lakini lazima tukubaliane kuwa CCM ya JK kilikuwa chama cha siasa cha kisiasa na CCM ya JPM ni chama cha siasa cha kidola, kisicho na ushawishi wowote.
Hao wapinzani walio bungeni maeneo mengi waliingia bungeni kwa nguvu kubwa wakati wa JK, na jambo hilo kwa utawala huu ambao unawaambia wasimamizi "nakulipa, nakupa gari ni kisha unamtangaza mpinzani?"haliwezekani
 
CCM is dying slowly.
Daniel: 24 Ndipo kile kitanga cha ule mkono kikaletwa kutoka mbele zake, na maandiko haya yameandikwa.
25 Na maandiko yaliyoandikwa ni haya; MENE, MENE, TEKELI, NA PERESI.
26 Na tafsiri ya maneno haya ni hii; MENE, Mungu ameuhesabu ufalme wako na kuukomesha.
27 TEKELI, umepimwa katika mizani nawe umeonekana kuwa umepunguka.
28 PERESI, ufalme wako umegawanyika, nao wamepewa Wamedi na Waajemi.
Dah!
Nachokaga sana mnapolinganisha huu utawala wa ulimwengu huu na utawala wa Mungu kimaandiko...
Hakuna chama chochote kinachoongoza au kutarajia kuongoza kwa kanuni za kimaandiko hapa nchini, wanasiasa wote ni wanafiki plus tofauti yao na sisi ambao hatujajidhihirisha iko kwenye kujaribu kutaka kufikia matamanio yetu kimwili kimaandiko ambayo hatuyatendi...
Fursa tu!
 
Back
Top Bottom