Tafakuri ya FaizaFoxy 2: Korosho

Tafakuri ya FaizaFoxy 2: Korosho

Kweli kabisa viongozi wateuliwa awamu ya tano wamefanya mlolongo wa maamuzi yasiyo na tija kwa ki-Spaniola tuna kausemi : Estar como una cabra.

Ushauri wako FaizaFoxy, wauzingatie maana wameshafanya maamuzi mengi yanayoligharimu taifa kiuchumi na kijamii na sasa hali ni mbaya sana.
. Vamos de puta Madre
 
Hao akina Bakhressa hawakopi wakafungie viwanda vya kusaka political millage, wanakopa na kufungua viwanda vinavyolipa. Mimi niliwahi kushauri kwakuwa sera ya viwanda ni ilani ya ccm, basi ccm waanze kuwa mfano, wao kuanzia rais na mawaziri wakope na kufungua viwanda kisha wazalishe, tukishaona mfano toka kwao tutavutika.

Maana wanaccm huwa tunawaona kwenye chaguzi kuanzia rais, wabunge na mawaziri wakitumia nguvu zao zote na kusaidiwa na vyombo vya dola kuhakikisha hawapotezi madaraka. Nguvu hizo hizo wazitumie kufungua viwanda tuone ubora wao maana viwanda vinalipa kuliko urais, uwaziri, ubunge nk. Sio ushauri akina Mo wakope kufungua viwanda, halafu nyie muue, mloge, mtoe rushwa kuhakikisha mnapata madaraka.
Unatumia kinywaji gani mkuu wakuongezee hapo round mbili kwa Bill yangu.
 
Kama unaziona fursa kelele za nini? Nenda kafunguwe kiwanda ubangue korosho uuze Saudia. Shida za hii nchi zinaletwa na wazee wa itikadi. Sioni KIPYA kwenye mada yako cha kukiita ushauri.
Hapo ulipoandika "Sioni kipya" umepatia kwa asilimia mia. Sijawahi kutegemea mwenye macho yasiyoona akaona.
 
Kuhusu malipo Kassim Majaliwa ameshatolea ufafanuzi na kwa sasa siyo issue tena.

India ndiyo moja ya soko kuu la asili la mazao yetu, historia inatufundisha hata Vasco Da Gama alikuta tayari tuna biashara kati ya India na Kilwa toka enzi na enzi.

Unapokuwa na soko la zamani namna hiyo si hasha unakuwa umejijengea uwezo, uaminifu, mbinu na wateja wa kudumu wa biashara zako.

Mambo matatu makuu India imejijengea kwenye zao la korosho, uaminifu ambao wateja wao wanaamini kuwapa pesa za manunuzi mpaka asilimia mia moja "in advance". Gharama nafuu za ubanguaji kwa mkono kutumia watu kubangua badala ya mashine (hili siku zinavyokwenda linaanza kutoweka huko India). Nidhamu ya kazi na matumizi.

Hizo ndiyo sababu kuu za India kuwa kitovu cha biashara ya korosho.

Sababu hizo ni rahisi kuzipata kwa wafanya biashara wachache wazoefu Tanzania. Tuwatumie.
Inawezekana sio issue kwa sababu ufafanuzi umetolewa lakini ni issue kwa maskini wale kama hawalipwi kwa wakati... ilhali wana mahitaji ya kielimu, afya, makazi nk. "...aaah HAYATUKHUSU!!!"
Hivi kwanini wanaopewa nafasi "HATUJIFUNZI?"
Korosho zitaendelea kuwa korosho na si korosho hata kahawa tunarudi nyuma... achilia mbali cash crop zingine!!!
China leo wanaleta samaki wanaowafuga hapa kwetu ilhali wao wakiagiza kwetu hapo awali...
Kuna tatizo mahala...
 
Matatizo ya nchi hii hayako kwenye mitaji, yapo kwenye sera. Post yangu ilikuwa inajibu post yake ambayo ilikuwa inajibu post ya member mwingine kwa kuyaita mawazo yake ni mawazo duni.

Shida yetu ni kupenda kufumba macho na kuvuka barabara tukijisahaulisha uwepo wa magari. Tunashuhudia biashara ngapi zikifungwa na 'wazee wa itikadi' wanaishia kusema hao walikuwa wapiga dili?

Tumeshasikia matamko mangapi yenye ukakasi ambayo hamkani yakaleta kigugumizi kwa wawekezaji kuwekeza hapa nchini? Tatizo halipo hapo anaposema. Hivi kuna serikali hapa duniani ambayo haijui umuhimu wa kuwawezesha raia wake kutumia fursa zinazopatikana ndani ya nchi husika?

Hata ile ahadi ya MILIONI 50 KILA KIJIJI si ililenga muktadha huu? That means wanajua. Ndugu yangu, mambo ni mengi...muda ndio mchache. Kama tuna balozi India, na India ndio inaongoza kwa kula dengu na mbaazi, umeshawahi kujiuliza ni zipi kazi za mabalozi wetu huko nje?
Kama umeona fursa ya dengu na mbaazi kwanini usiitumie umngoje balozi?

Huo ndiyo muono wako ulipoishia kungoja kufanyiwa.
 
Narudia tena, ilani ya viwanda ni ya ccm, na viwanda vinalipa kuliko udiwani, ubunge na urais. Kwakuwa wanaccm huwa tunaona wanafanya lolote kuhakikisha wanapata madaraka, kwanini wasikope bila riba wafungue hivyo viwanda kisha tuone matokeo ya wanachoamini?

Tena kwa kuanzia mawaziri wajiunge wanne wanne kila kundi lianzishe kiwanda watoe ajira tuone matokeo. Na funga kazi rais ajiunge na mawaziri watatu wa viwanda, wawili aliowatumbua na huyu mpya wajenge kiwanda kisha tuone mfano halisi wa hicho wanachohubiri. Akina Mo, Bakhresa and the likes hawahitaji ushauri wako kwenye viwanda maana tayari wanavyo, hawa wanaohubiri sasa ndio watoe shamba darasa la mahubiri yao.
Ongeza mbili mkuu
 
Waache ubunge wajikite kwenye biashara maana huko kwenye siasa ndio wameharibu kwa kutoa rushwa, kufanya ukatili nk ili washinde. Kama unaweza kunisaidia unaweza kuniambia Profesa Kabudi kiwanda chake kiko wapi? Ukiweza nitajie na kiwanda cha Makonda kilipo nikaombe ajira.
 
Inawezekana sio issue kwa sababu ufafanuzi umetolewa lakini ni issue kwa maskini wale kama hawalipwi kwa wakati... ilhali wana mahitaji ya kielimu, afya, makazi nk. "...aaah HAYATUKHUSU!!!"
Hivi kwanini wanaopewa nafasi "HATUJIFUNZI?"
Korosho zitaendelea kuwa korosho na si korosho hata kahawa tunarudi nyuma... achilia mbali cash crop zingine!!!
China leo wanaleta samaki wanaowafuga hapa kwetu ilhali wao wakiagiza kwetu hapo awali...
Kuna tatizo mahala...
Hilo ni tatizo lililokuja ghafla na kwa muda tu, mada yangu imelenga suluhisho la muda mrefu kuepukana na matatizo ya kupangiwa bei na wabangua korosho wa India. Tutoke huko tukapambane na wapanga bei za walaji wa korosho.

Mfano, India wanalima aina nzuri ya mchele wa Basmati lakini nenda India kanunuwe mpunga kama utaupata. At the same time, nenda kanunuwe mchele, watakuuzia hata kwa brand yako na namna ya vifungashio uvitakavyo. Huko ndiyo ku add value ya mazao nilipopalenga mimi.
 
Hayo utayaona kwenye Mazao yote hapa kwetu Tanzania
AISEEEE, nimekusoma sana mkuu.
Jambo la ziada kidogo: hivi inakuwaje tunao wataalam chungu nzima wizarani (kilimo na kwingineko); hivi hawa wastu wanafanya kazi gani huko?

Baada ya kuweka bandiko langu la mwanzo katika mada hii, likaniijia swali: hivi nchi kama Vietnam ambao ndio wanaoongoza katika zao hili wao wakoje? Nika-'google' "Vietnam Cashewnut Processing Industry" Nikakuta taarifa nyingi tu, na hata wao wanavyohangaikia kupata mali ghafi za kulisha viwanda vyao, na jinsi wanavyolinda 'technology' yao ili waendelee kuwa vinara. Waliwanyima Nigeria teknologia hiyo walipoiomba 2007 kwa sababu za ushindani huo.

Nimesoma dakika chache tu na kupata picha ya yanayotusumbua sisi, moja wapo likiwa hilo la kukosa teknologia sahihi. Sasa najiuliza, pamoja na kuwa na wasomi wote hawa tulionao sasa tunashindwa kabisa angalao kujua matatizo yetu yanatokana na nini, tunabaki kuwa watu wa kubahatisha tu? Juzi Rais Magufuli akadhani Jeshi litatumia vile viwanda kuuku tulivyokuwa navyo, jamaa (wataalam wetu) wanamwangalia tu, pengine wakichekelea! Nilliona picha ya wanajeshi wamepinda migongo wakibeba mashine, sijui walikuwa wanaipeleka wapi!

Magufuli angependa kuwa Dikteta wa ukweli, udikteta wake ulitakiwa ufanyike huko huko kwa watu wake huko serikalini, na sio huku uraiani. Hata mimi ningemuunga mkono. Hawa wasomi tulionao ni lazima wafanye kazi kama punda kama hawawezi kujituma wenyewe.

Kwa hiyo inawezekana sana kwa hawa wafanya biashara wetu hapa wanasita kuingia katika biashara hiyo kwa kujua ugumu huo. We have no technology needed to process the damn thing efficiently, and those who have the technology are reluctant to share!
No wonder, we hardly see any of those companies willing to set up here, even with the available incentives.

Narudi huko huko nilikoanzia. Suluhisho la matatizo yetu haya ni kuwapa wakulima uwezo. Acha waunde Ushirika wao na wawe na uwezo wa kila namna katika shughuli za mazao wanayoyalima.
 
AISEEEE, nimekusoma sana mkuu.
Jambo la ziada kidogo: hivi inakuwaje tunao wataalam chungu nzima wizarani (kilimo na kwingineko); hivi hawa wastu wanafanya kazi gani huko?

Baada ya kuweka bandiko langu la mwanzo katika mada hii, likaniijia swali: hivi nchi kama Vietnam ambao ndio wanaoongoza katika zao hili wao wakoje? Nika-'google' "Vietnam Cashewnut Processing Industry" Nikakuta taarifa nyingi tu, na hata wao wanavyohangaikia kupata mali ghafi za kulisha viwanda vyao, na jinsi wanavyolinda 'technology' yao ili waendelee kuwa vinara. Waliwanyima Nigeria teknologia hiyo walipoiomba 2007 kwa sababu za ushindani huo.

Nimesoma dakika chache tu na kupata picha ya yanayotusumbua sisi, moja wapo likiwa hilo la kukosa teknologia sahihi. Sasa najiuliza, pamoja na kuwa na wasomi wote hawa tulionao sasa tunashindwa kabisa angalao kujua matatizo yetu yanatokana na nini, tunabaki kuwa watu wa kubahatisha tu? Juzi Rais Magufuli akadhani Jeshi litatumia vile viwanda kuuku tulivyokuwa navyo, jamaa (wataalam wetu) wanamwangalia tu, pengine wakichekelea! Nilliona picha ya wanajeshi wamepinda migongo wakibeba mashine, sijui walikuwa wanaipeleka wapi!

Magufuli angependa kuwa Dikteta wa ukweli, udikteta wake ulitakiwa ufanyike huko huko kwa watu wake huko serikalini, na sio huku uraiani. Hata mimi ningemuunga mkono. Hawa wasomi tulionao ni lazima wafanye kazi kama punda kama hawawezi kujituma wenyewe.

Kwa hiyo inawezekana sana kwa hawa wafanya biashara wetu hapa wanasita kuingia katika biashara hiyo kwa kujua ugumu huo. We have no technology needed to process the damn thing efficiently, and those who have the technology are reluctant to share!
No wonder, we hardly see any of those companies willing to set up here, even with the available incentives.

Narudi huko huko nilikoanzia. Suluhisho la matatizo yetu haya ni kuwapa wakulima uwezo. Acha waunde Ushirika wao na wawe na uwezo wa kila namna katika shughuli za mazao wanayoyalima.
Mengine yote nakubaliana na wewe lakini Ushirika kwa maana ya vyama vya ushirika siyo suluhisho. Vyama vya ushirika ndiyo chanzo kikuu kilichoitoa nchi hii kutoka msafirishaji wa kwanza wa mazao nje wa Afrika hadi kufikia omba omba wa kwanza.

Ushirika kama kampuni, Bakhresa na MO ni mfano mzuri nimeweka juu hapo. Hiyo ndiyo solution.

Kuhusu teknolojia, hilo si tatizo kubwa sana ingawa tunalo. Makampuni binafsi yana njia zao za ki intelijensia binafsi za kutatua hayo, yatapopewa fursa yataweza tu.
 
Kuna swali hujajiuliza, ni kwa vipi hao Wafanyabiashara hawajaiona hiyo fursa hiyo kwa miaka yote. Unadhani ni kwa sababu ya kutokuwa na fedha?
Swali zuri. Jibu ni rahisi; vyama vya msingi na vile vikuu pamoja na ushirika viliaminika na kuopewa chapuo zaidi na serikali. Kuwa, vingeweza kusimamia biashara hiyo jambo linaloonekana wazi kushindwa.
 
Hivi yule dada wa nyumbani kwako aliyekuwa anampenda Magu mpaka akawa anajishaua bibi bibi hatujawahi pata rais kama huyu bado unaye au ndo ushamtumbua

Samahani kwa kutoka nje ya mada maana mimi ata mkorosho sijawahi kuuona mimi najua mibuni ya kahawa ambayo ma ccm yaliua basi tena kila mtu apambane kivyake

Samahani bibi kwa kutoka nje ya mada
Ma shaa Allah, kaolewa yupo kwa mumewe.

Jikumbushe: https://www.jamiiforums.com/threads/bibi-nisamehe-najuta.971224/
 
Mengine yote nakubaliana na wewe lakini Ushirika kwa maana ya vyama vya ushirika siyo suluhisho. Vyama vya ushirika ndiyo chanzo kikuu kilichoitoa nchi hii kutoka msafirishaji wa kwanza wa mazao nje wa Afrika hadi kufikia omba omba wa kwanza.

Ushirika kama kampuni, Bakhresa na MO ni mfano mzuri nimeweka juu hapo. Hiyo ndiyo solution.

Kuhusu teknolojia, hilo si tatizo kubwa sana ingawa tunalo. Makampuni binafsi yana njia zao za ki intelijensia binafsi za kutatua hayo, yatapopewa fursa yataweza tu.
Faiza, usisahau kale kakero ka slogan za Kijamaa bado kapo! Kuwa mnunuzi binafsi wa mazao huitwa " mlanguzi". Hadi wakulima husikika wakisema "tumelanguliwa" mazao yetu na mnunuzi fulani.
Bado kuna imani ndani ya serikali kuwa ushirika ndo kilakitu. Ushauri wako ni mzuri.
 
Hajweka pembeni hapo... We hauon kila dakika mbili bakhresa..

Utadhan mfanya biashara yuko mwenyewe.
Nitajie basi wafanya biashara wa kutukuka wa "food processing" Tanzania hii niwaweke.

Tatizo nini?
 
Hajweka pembeni hapo... We hauon kila dakika mbili bakhresa..

Utadhan mfanya biashara yuko mwenyewe.
Nitajie basi wafanya biashara wa kutukuka wa "food processing" Tanzania hii niwaweke.

Tatizo nini?
 
Back
Top Bottom