Ushauri: Serikali ijitowe kimasomaso kuwakopesha bila riba wafanya biashara wakubwa wenye uzoefu wa viwanda kama vile akina Bakhresa na Mo kufunguwa viwanda vikubwa vya kisasa vya kubangua, kusindika na kufungasha korosho kwa kiwango cha Kimataifa na kuwasaidia kushindana na masoko ya Kimataifa.
Ni ushauri (wazo) ambalo bila shaka hao hao wafanya biashara wangekuwa na nia ya kuifanya biashara hiyo wasingekuwa wamesita kukopa kwenye mabenki na kwingineko, kama mashirika ya fedha duniani yanayokopesha na hata kuingia ushirika na wafanya biashara, kama International Finance Corp.(IFC) sehemu ya WB.
Wafanya biashara wakubwa kama hao uliowataja, wasingehitaji kamwe kutikiswa ili waione fursa iliyopo bwe(lele) (rere?) kama hiyo. Hawa wangekuwa wameichangamkia siku nyingi.
Nadhani kuna umhimu wa wanaojua biashara hii ya korosho, watueleze kwa nini inakuwa ngumu kiasi hiki.
Huko nyuma tuliwahi kuwa na viwanda kadha vya kubangua korosho, hivi viwanda ilikuwaje hadi ikashindikana visifanye kazi?
Wakulima wa korosho na mazao mengine, kwa vipi hawawezi kuunda ushirika imara na kuendesha shughuli kama hizi ili kufanikisha mazao yao?
Hapa ngoja nitoe mfano hai. KCC (Kenya Creameries Co-operative) wanatuuzia maziwa yao kwa wingi hapa kwetu. Hawa sasa karibia wanasindika Lita milioni mbili kwa siku za maziwa, na wanapambana kikwelikweli na Brookeside ya Kenyatta. Kwa nini sisi imekuwa shida sana katika kila jambo?
Tafakuri ni nzuri, lakini wazo la serikali kugawa hela ya kodi kwa hawa wafanya biashara wenye uwezo mkubwa, nasita kuukubali.
Wakopeshwe wakulima na wapewe mafunzo yanayostahili ya uendeshaji wa shughuli zao, ikiwa ni pamoja na hivyo viwanda.