Mimi nitaendelea kukumbusha tu, hiyo heshima unayompa mtu asiyeistahili sijui unalenga kitu gani.
Ukimwita tu Samia haitoshi hadi umpe heshima na cheo kisichoendana kabisa na hadhi yake?
Hilo moja.
Mbona unakuwa na mashaka juu ya anachoamini Samia hadi utake kumlazimisha afanye kinyume na uamini wake.
Hujasikia kauli zake mbalimbali juu ya swala hilo hilo la "kujutia"?
Au labda nikupe mfano ulio karibu naye:
Bi Asha Migiro ambaye ni Katibu Mkuu wa Chama kasema waziwazi kwamba "vyombo vya dola vilifanya kazi ya kutukuka", unaeleewa maana ya maneno hayo?
hayo anaweza kuyasema Katibu Mkuu wa chama; na Mwenyekiti wake awe na msimamo tofauti?
Jameni, kwa nini mnatafuta kumlazimisha Samia jambo ambalo haliamini kabisa. Aguswe na watu waliotaka kumnyima fursa ya kuwa mtawala (kwa uamini na fikra zake)?