Tabia za wanawake kuchukiana bila sababu.

Tabia za wanawake kuchukiana bila sababu.

Girl wangu akirudi magetoni kutoka kwenye mihangaiko yake kazi yake inakua ni kuwapiga madongo rafiki zake, mimi nakua naitikia tu ee ndio, aisee mpaka nashangaa hawa watu ni marafiki gani? Na mwenzie akija magetoni wanaungana tena wanaanza kuwapiga mdomo wenzao wengine hapo ndio hua nachoka
 
Kabisaa au hawajazaliwa bado

Humu JF chuki zipo wazi wazi makundi yapo wazi wazi. Ule uzi uliosababisha picha za mdada mmoja humu kutupiwa,wanawake waliongoza kuchekelea na kufurahia mwenzao akidhalilishwa

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]baraka za hali ya juu
Niliupinga ule uzi kwa nguvu zote kujaribu kummaliza nguvu kile kivulana na bado baadhi ya ID za kike zilinishambulia pm na jukwaani nikazushiwa na mengineyo lukuki,,, wanawake hatupendani sijui tukoje hapa
 
Niliwahi kuambiwa kwamba , sababu ya wanawake kutokupendana ni wanaume.
Kila mtu anajitahidi aonekane bora kuliko mwenzake, aonekani mzuri kuliko mwenzake na kadhalika machoni pa wanaume.
Nilisoma shule ya girls tuu , tulipendana sana sana, ule upendo wenyewe.
Nikahamia mchanganyiko, ndipo nilipodhibitisha kwamba sababu ni wanaume.
 
Kuna mahala unavuka

Chuki kati ke na ke haihusiani na 50 kwa 50,,
Uko sahihi kabisa lkn jaribu hata kuangalia miongoni mwa mahusiano ya kikazi, biashara utagundua 7bu kubwa ni uwepo wa 50 kwa 50 kutakikana kwa haki sawa.

Picha halisi inaonesha ni lazima m1 awe juu na mwingine awe chini ili pawepo na Mtawala/kiongozi na atoaye ushauri, asikilizaye au kutekeleza kazi kufikia malengo husika.

So nime-generalize 50 kwa 50 ni jipu kubwa kiuhalisia na popote ktk maisha wala siyo ktk ndoa pekee.
 
Habari za jioni wana jukwaa.

Ni hivi kwenye ofisi ninayofanya kazi tuko watumishi kama 15 hivi,kati ya hao wanawake tuko saa watano pamoja na ps,walobaki ni wanaume.

Basi kuna kipindi tulipewa zawadi ofisini,nami nilikuwepo miongoni mwa waliopata,tukiwa wanawake wawil tu tuliobahatika ,nikajipost kwenye group ya ofisini wanaume almost wote walikuwa happy na kunipongeza,ikaja kwa wanawake Sasa,mtu unakutana naye koridoni anakuuliza nimeona bana umepewa cheti,unamjibu ndio,anakwambia hongera huku ikiambatana na kicheko Cha kebehi na kejeli.

Ukija kwenye groups za wasap, comments wanazotoa wanaume kwetu wanawake si za kubeza,hata kama kukukosoa atakukosoa kistaarabu.Ila wanawake mtu atoa comments kama mna ugomvi,ama aweza comment neno la kukudhalilisha ilmradi usijisikie vizuri.Hadi wajiuliza ,tatizo nini?

Kuna wakati mwenzetu mmoja alikuwa mjamzito, jamaa mmoja wa ofisin akapiga naye picha akaipost kwa group,most of men walikuwa happy na walikuwa wanacomment positively,na matani ya hapa na pale,ila upande wa wanawake sasa wakatoa maneno ya kejeli na kuonyesha kutofurahia hilo jambo,as if wamechangia mume .Mwingine akaandika ,,ahhh mama kijaaa hongera bwana,then hehehehe halooo
,Like what the f@ck?

Hata kwenye ishu za deals ni mara chache,mwanamke akushirikishe hata kama una uwezo wa kulifanikisha,but kwa upande wa wanaume wako so smooth na washirikishaji wazuri.Tena wanawake hao wakigundua kuna kaishu unafatilia yuko radhi hata akuharibie kwa client,ili tu mkose wote.

Ishu ni nyingi,ila wanawake mostly hatupendani maofisini,Hatuko professional mostly,Tunasemana vibaya,tunaoneana wivu wa kijinga (siyo wa kimaendeleo),tunachafuana Wala hatusapotiani kwenye ishu positive.Nashindwa elewa tatizo ni nini.

So swali ni kwanini wanawake hatupendani?ni nature?Ni laana?Na suala la kutaka unnecessary competition na wanawake wengine sababu ni nini?
Wanaume kwenye mambo ya kawaida ndo huwa wana ubinadamu ila kwenye mapenzi ndo huwa wanaongoza kwa unyama
 
Girl wangu akirudi magetoni kutoka kwenye mihangaiko yake kazi yake inakua ni kuwapiga madongo rafiki zake, mimi nakua naitikia tu ee ndio, aisee mpaka nashangaa hawa watu ni marafiki gani? Na mwenzie akija magetoni wanaungana tena wanaanza kuwapiga mdomo wenzao wengine hapo ndio hua nachoka
Jaribu kumchunguza vzr huyo demu wako asijekuwa anakupiga madongo pia akiwa na mashosti wake, ni mtizamo tu Mzee Baba wala usipanikc... [emoji87]
 
Hupaswi kuangalia nani hataki kumpisha nani! Wewe kuamua kumpisha inatosha!

Kwani wanaume wangapi walikuwa kwa hiyo gari na hawakupisha?! Tunatofautiana tabia na malezi!
Mimi hata hii sakaya nimekuwa nikikutana nayo sana na kwangu huwa nachukulia kama credit na baraka pia.... na hii huwa naitumia kama opportunity ya kuhakikisha ninyi wanawake mnaendelea kutokupendana na kupatana na muendelee kugombana na kuonana wabaya...

Kuna siku nilipanda gari sehemu fulani .....wakati gari linaanza kuondoka lakini kuna mdada aliyekuwa na mtoto akasimamisha gari......akaingia kwenye gari kila akicheki seat zote zimejaa akaendelea kusimama uku gari linakwenda na alipokuwa amesimama kulikuwa na wamama na wasichana wamekaa karibu na yeye ....mimi nikawa nacheki mchezo tuuu....... bahati mbaya yule mtoto akaanza kulia yule binti akawa ana mbembeleza uku ameshikilia chuma ....

Hakuna aliyekuwa ana jali kuhusu yule binti si wale waliokuwa karibu nae wala sisi tuliokuwa nyuma ....wote tulikumbatia siti kama hatumuoni vile........
Moyo ukawa unaniambia wagombanishe, mara mpishe akae, wagombanishe, wagawe....
Ilibidi ni muite yule dada nikamwambia njoo ukae huku dada...... unajua aligeuka fasta nusura aanguke na mtoto..... yani alishukuru huyo....oooh ubarikiwe sana kaka...oooh Mungu akutunze... .
Mimi nikabaki naitikia tuu Amina,amina, amina lakini moyoni nasema bado jambo langu halijatimia la kuhakisha hawa wanawake wanapeana adabu humu....na kitchen party..hahaha

Mara mapepo yakaanza kulipuka....konda akanza kusema hakika wanawake hampendani kabisa yani mmemuacha mwanamke mwenzenu ana teseka mmeshindwa kumpisha mpaka mtu mwingine tena mwanaume ndio anashikwa uchungu ana muonea huruma? hahahahha
basi na wanaume wengine wakalipuka......oooh hawa wanawake wanaongoza kwa roho mbaya kabisa yani hata hao wambele wameshindwa kumpisha mpaka mtu wa huku nyuma ampishe kweli halafu mnatwambia kuwa huwa mnasikia uchungu wa kuzaaa..... jamaa akaongeza kwa kusema nani kawaroga nyinyi? watu vicheko daladala nzima hahahha

Mimi moyoni nikawa nasema bado sijafanikisha ninalolitaka......hatujakaa dakika moja vicheko vinaendeleaa...... Mara mwanamke mmoja kalipuka nakusema ni kweli wanawake hatupendani kabisa na hatuna huruma kabisa yani mtu unakaa na mtu karibu hapo anataka kukuangukia unashindwa kumuonea huruma? wanawake tubadilike kabisa hii ni aibu...........

Moyoni nikasema yes....yes....yes.... hapa ndipo nilikuwa napataka....hahahha
Sasa wale waliokuwa karibu na yule dada wakati amesimama na hakumpisha ...... nao wakalipuka na kumvaa mwanamke mwezao...........oooooh wewe mwanamke acha unafiki wewee.....na matusi juuu siyakumbuki....... wakamuuliza kwanini hukumpisha mpaka ukamuacha huyo kaka ampishe? Wanawake wengine nao wakalipuka wakasema mwambieni huyo mnafiki anajipendekeza ili watu wamuone mwemwa wakati sura yake inaonesha kabisa ana roho mbaya......hahahaha

Sasa kwakuwa daladala ilianza kuwaka moto wa wanawake kwa wanawake wakirushiana matusi mimi nikakaa kimya sikuchangia lolote na nikamwambie yule binti anyamaze asichangie..... kwakweli moto uliwaka wakaanza kutukanana matusi ya nguoni.......uku wanaume tuko kimya na wengine wanacheka tuu jinsi wanavyorushiana madongo....

Mara konda akaanza kukusanya nauli uku anasema endeleeni kugombana uku mnanipa nauli yangu.......
Mimi moyoni nikasema hapa ni kuongeza kuni na kuchochea moto..... hahahaha
Konda akafika niliposimama akaomba nauli nikampa buku na kumwambia ni ya wawili mimi na huyu dada..... hahahahah hapo ndipo nilichochea moto zaidi.....
Kumbe kuna mama pembeni alisikia nampa konda nauli na kumlipia yule dada....... mara akamuita konda konda akamwambia chukua hii buku tano naomba umrudishie yule kaka hela yake nitalipa mimi na ya yule dada halafu na wale mashakumpe wawili pale mbele ntawalipia.....hahahaha.....moto ukawaka tena.....

Konda akanirudishia buku yangu nikaweka mfukoni moto ukaendelea kuwaka baada ya wale wadada kusikia wanalipiwa na wameitwa mashakumpe hahahahaha yani ilikuwa timbwili ni kutukanana matusi tuu.....umlipie nani wewe ......acha kujipendekeza kama unamtaka huyo kaka mwambie sio kutumia migongo yetu....hahahahahahhahha
Mimi moyoni nasema hapa ndipo nilipopataka acha wafunzane adabu..... walikuwa wanaambiana maneno aiseee hadi wanaume tulikuwa tuna shangaa.....hahahaha.... ugomvi uliendelea muda mrefu...sana hadi nashuka bado walikuwa wanagombana.....

Hakika naendelea kufurahi kwakuwa dawa ya matatizo yao hawajeweza kuijua....
Mimi siingili ugomvi wa wanawake bali nikipata nafasi naongeza kuni moto uwake.......
Lazima wanawake wajifunze wenyewe kupatana na kutatua matatizo yao.....
 
Back
Top Bottom