Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,494
- 113,590
RIP Mke wa Freetown.
Heroes never die because their ideas will live for ever - R.I.PWakuu,
Nimetaarifiwa sasa hivi kwamba mke wa member mwenzetu Freetown ameaga dunia mchana huu saa7.30 kwenye hospitali ya KCMC-Moshi.
Freetown ni member 'legend' hapa majukwaani, na kwa wale waliofika Arusha mwaka jana (27/12/2010) tulipoenda safari ya Tarangire wanapata hisia zaidi juu ya kuondokewa na mkewe kwa huyu member mwenzetu, maana tulikuwa pamoja nae bega kwa bega, na alisafiri na wanae, mabinti wawili.
Mipango ya Mazishi bado haijawekwa wazi, na zaidi inasubiri kuwasili kwa Freetown mwenyewe toka Ughaibuni anakomtumikia mkoloni, na kwa taarifa nilizopewa ni kwamba anatarajiwa kuondoka huko leo usiku, na atawasili kesho alasiri, Mungu akipenda.
Tutajuzana zaidi kinachoendelea, kwa sasa tunachoweza kusema ni kwamba Mungu ailaze pema roho ya Marehemu mke wa Freetown.
Amen.
Pole sana Freetown kwa msiba mkubwa uliokufika. Mwenyezi Mungu awape nguvu na faraja katika kipindi hiki kigumu kwenu na ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi~AMEN