Taarifa: Usalama Wangu Hatarini

Taarifa: Usalama Wangu Hatarini

...pamoja na vitisho hivi ambavyo vinaweza kupelekea mtu kuteswa, kuwa sodomized na hata kuuwawa kijasusi, sitaacha kukipigania chama changu cha CCM ....

Nahitaji sana sala zenu,

Mungu ibariki Tanzania.

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Ujinga wako umefika kiwango cha kuwa mpumba.vu, yaani uko tayari kuwa kungolewa meno, kutolewa jicho, kunyofolewa kucha, kuwa-sodomized au kuuawa na wanachama wenzako wa CCM kwa ajili ya Chama 'chako' CCM? Mwalimu kilikuwa chake lakini alitaka kukitema, "na wewe ni chako!" Hao wanaotaka kuku-sodomize au kukuua watasemaje-hao si ndiyo chao?

Wewe hatuna haja ya kupoteza muda kukuombea, maana "utaangamia kwa kukoseshwa maarifa" na CCM! Muasisi wake walimuua wakashika dola, sembuse wewe uliedandia treni karibu na mwisho wa reli utusumbue! TOKA HUKO kwa wauaji hamia kwingine tuikomboe nchi!
 
ukiwa mwana CCM uwe mtu wa Yes-Yes- Sir!! maisha yako yatakuwa mazuri mno.... vinginevyo unaweza kujikuta una vidole 19, kucha 17 tu na meno 24.
Amuulize Masumbuko Lamwai.... Wakaanza na kumzuia kutoa mihadhara chuo, Wakafuata kumtimua nyumba ya chuo, wakasitisha leseni ya uwakili, akakimbilia Zanzibar, na huko nako wakahakikisha hali inakuwa mbaya.... BAADA YA KUMBANA KILA KONA, WAKAMTUMIA MTU...''mzee achana na hayo mambo rudi kundini''... Baada ya muda... ETI NI MWANASHERIA WA CCM... TZ yetu hii... wanataka kila mtu awe kama JOKA LA KIBISA.... HALING'ATI, NA LIKING'ATA HALINA SUMU....
 
Kwa ushauri jitahidi kutotembea peke yako nyakati za usiku. Ikibidi basi vaa helmet na indusrial glooves kujikinga na vitu vyenye ncha na kile cha kung'olea kucha...please zingatia
 
Mchambuzi Pole mkuu. Tanzania yetu inazidi kuwa kama a Mafia State. Bahati mbaya matukio kama haya yanapotokea bado kuna baadhi ya wenzetu hukimbilia kuhoji "dhamira" ya mhanga kuweka hadharani masahibu yanayomkumba. Jamani, hii sasa ndio hali halisi kwa kila anayediriki kutamka kisichowapendeza watawala wetu.

Inasikitisha mno lakini kama Maandiko Matakatifu yanavyosema, MWENYE HAKI ATAANGUKA SABA MARA SABINI LAKINI ATASIMAMA

Stay safe, mkuu!
 
Last edited by a moderator:
Jamii yetu inadanganyika kirähisi sana.
Critical thinking haipo kabisa!!!
Ndio maana misururu ya wagonjwa ilijaa Loliondo...

Serikali ya Chama chako si ndio iliongoza msafara chini ya kamanda wa Nyuki na Asali
 
Nilikuwa na hisia ulikuwa unawashirikisha wengine ndani ya CCM kwa hoja zako makini; hili la kutishiwa nakupa pole. Hao kwa vile unawafahamu wapime kwenye mizani yako chukua hatua.

Ni bahati mbaya baadhi yetu tunaamini hawa wanafaidi hadhi ya kulindwa hata na vyombo vya dola; kwa hiyo unapotaka kuwatolea taarifa kwenye vyombo vya dola (ambavyo hujawatathmini) unaweza kutoa fursa nyingine kwa hawa wapuuzi.

Sina sababu ya kutoiamini taarifa yako pole sana HAPO NDIPO TULIPOFIKIA umetusaidia tujitafakari na kuchukua hatua. Ili mradi umelitoa hili hadharani si ajabu nao watoa hadharani vituko vyao.
 
Machungu ya kung'olewa meno kucha, macho bila ganzi ninoma. Wosia wako mzuri ila IGP NA KOVA Wako busy kuzuia maandamano wanasubiri uuawe kinyama waje watoe matamko na kuunda Tume
 
Mchambuzi pole sana! Hakuna maisha magumu kama ya kuwindwa! Tunahitaji kufanya kitu maana inaonyesha hakuna nia ya dhati ya kusimamia haki.

Kuna watu wachache wamepania kulinda maslahi yao kwa gharama yoyote,tujihadhari sana.

Sijui miaka yote hii Mzee Mwanakijiji na wapambanaji wengine wanaishije ktk hali hii ya kuwindwa!
 
Last edited by a moderator:
Ujinga wako umefika kiwango cha kuwa mpumba.vu, yaani uko tayari kuwa kungolewa meno, kutolewa jicho, kunyofolewa kucha, kuwa-sodomized au kuuawa na wanachama wenzako wa CCM kwa ajili ya Chama 'chako' CCM? Mwalimu kilikuwa chake lakini alitaka kukitema, "na wewe ni chako!" Hao wanaotaka kuku-sodomize au kukuua watasemaje-hao si ndiyo chao?

Wewe hatuna haja ya kupoteza muda kukuombea, maana "utaangamia kwa kukoseshwa maarifa" na CCM! Muasisi wake walimuua wakashika dola, sembuse wewe uliedandia treni karibu na mwisho wa reli utusumbue! TOKA HUKO kwa wauaji hamia kwingine tuikomboe nchi!

Kwani akihama itasaidia nini kulinda usalama wake? mbona mnaandika utafikiri unakimbizwa? Kutishiwa kwake si kwasababu ya UCCM wake bali maneno yake yanawachukiza wanaoguswa! @Dr Slaa yuko Chadema mbona anawindwa kila siku?
 
Usalama wataifa wako busy kulinda Chama wanasubiri Uuawe waunde Tume. Sikuhzi kupewa Tume imekua dili kwahy R.I.P watu wanaangamia kwa kukosa maarifa
 
Jamii yetu inadanganyika kirähisi sana.
Critical thinking haipo kabisa!!!
Ndio maana misururu ya wagonjwa ilijaa Loliondo...
Critical thinking kwenye uhai wa mtu, you can't be serious!!

Hata Mwakyembe alikuwa anaripoti kutishiwa maisha na watu kama wewe walikuwa wanamdhihaki kuwa anatafuta public sympathy na wote tunajua nini kilimpata. Tuweke tofauti zetu za siasa pembeni linapokuja suala la usalama na uhai wa mtu. Safety is not a game of chance dude...
 
Wakuu,

Mchambuzi sio verified wamemjua namna gani tuongeze tahadhari?
A%20S%2039.gif
 
Ukisoma wachangiaji wa post hii utaona LIVE jinsi jamii yetu inavyoweza kuwa manipulated so easily!!!

Naona umepoteza mwelekeo kabisa, unaona ''mapicha-picha'' tu........huyu ni Great Thinker na tunamsoma toka 2007, thus unamuamini!Kama unatuonea huruma sana basi ''Toa tamko la kusitisha kumng'oa kucha''
 
Mchambuzi wamekujuaje ??kwani wewe ni verified user????
 
Last edited by a moderator:
Nawashukuru nyote kwa kunipa moyo pamoja na ushauri juu ya jinsi gani naweza kukabiliana na hili,kwa njia za kujihami lakini pia kwa njia ya sala;lakini muhimu zaidi - nafarijika sana kwamba maoni na ushauri wenu unatoka kwa watanzania wote bila ya kujali kwamba mitazamo na itikadi zetu za kisiasa zinatofautiana,kwa mfano ben saanane na wengineo,that's the revolution that we need,siasa za masimango,chuki na visasi tuwaachie wazee;sisi kama vijana tunaweza tofautiana kiitikadi na mtazani lakini tukiwea mbele maslahi ya taifa,tofauti hizi hazitabomoa bali zitajenga taifa letu kama ilivyo katika demokrasia zenye mafanikio kama marekani,uingereza,japan,s.korea n.k;

;Lakini kwa wale pia ambao wananikejeli katika hili,nachukulia kejeli hizo positively kwani zinachangiwa zaidi na kuchoka kwenu na matatiizo sugu ya kila nyanja yanayolikabili taifa letu huku waathirika wakubwa ikiwa na walipa kodi na wakulima wanaotulisha na pia kutufanya tutembee vifua mbele kwamba siku moja na sisi tutakuwa taifa linalo jitegemea na la kipato cha kati;

Mwisho,niwahakikishie tu wale wote wenye kuniunga mkono katika hili kwamba sitaacha nachofanya kwani situmikii mtu bali moyo wangu;vinginevyo kama ningekuwa mwoga na dhaifu,ningeacha siku nyingi baada ya mzee wangu balozi mwambulukutu kuvamiwa afrika kusini mwaka 2007 kwa nia ya kuuwawa kwa sababu za kisiasa huku taarifa za nyumbani Tanzania zikisambazwa kwamba ilikuwa ni tukio la ujambazi huku uchunguzi juu ya tukio husika afrika ya kusini ukishinikizwa usimamishwezi;anyways,hayo yalishapita,kikubwa ni uzima ingawa wahusika wamefaniwa kumpofua macho;

Again,shukrani na pamoja sana;

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Mkuu Mchambuzi Pole sana.Amini Mungu hatawaacha waovu hawa wajiinue.Haitawezekana kamwe.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom