Taarifa: Usalama Wangu Hatarini

Taarifa: Usalama Wangu Hatarini

Mchambuzi kwani wewe ni verified? Na hiyo picha hapo ni yako? Hata hivyo pole sana kwa hayo yanayokunyemelea. Ustawi una gharama zake. Unajulikana kwa hoja zako makini na za kufunza. Sijui ni kwa nini hao ccm wenzako watake kukudhuru wakati unajaribu kuwanyooshea njia. Mwisho karibu sana cdm.
 
I really feel sorry for u...trying to feel the ctuation and pains you are facing.

Lakini sasa, Mchambuzi... unamaanisha kwamba wanaokusaka kukung'oa kucha, kukutoa macho au kutaka uhai wako, ni WAZEE! Aisee, so vijana wote kwenye chama chenu uko pamoja nao kwenye fikra zako kwa ajili ya chama chenu. Naona kama unaanza kutokuwa makini katika kujenga premises na hatimaye conclusion.
To me it does not mater. Atishiwe na wazee au vijana, mwisho wa siku anachokipitia ni kile kile tu
 
pole sana kamanda, kuna watu wanaona hii nchi ni yao peke yao, wafanye tu wanavyotaka wao nasi tuwaangalie, walishazoeshwa hivyo miaka ya nyuma iliyopita, awasomi kwamba nyakati sasa zimebadilika, hawataweza kuzuia ata wafanye nini, mkuu unahitajika zaidi ukiwa mzima mwenye afya njema, kwa sasa pumzika ama pambana kwa njia ingine, uzima wako ni muhimu kwa ustawi wa taifa letu, pole sana mkuu
 
Wanataka kudhuru kivuli chako au, mchambuzi ndio nani katika CCM?
 
CHADEMA tulishafunga mlango, sasa hivi ni kutoa masalia TU. Nafasi hakuna ukitaka tafuta kina TPP Maendeleo. CCM hawawezi kumtisha wala kumtoa kucha mtu wao labda uniambie wewe uko CCM ipi? CCM-MEMBE, CCM-EL au CCM-6 n.k.
 
Ndugu Mchambuzi pole sana kwa maswaibu yanayokukumba. Hiyo ndio gharama ya kupigania demokrasia ya kweli katikati ya watu ambao hawataki kuona kila mwanachama ama mwananchi akiwa huru kutoa mawazo yake kwa ajili ya ustawi wa nchi yetu.

Mimi sitaki kukushauri uhame ccm na kujiunga na Chadema kwakuwa kwa vyovyote vile hao wakubwa waliokasirika watakuwa wanakutuhumu kukijenga Chadema kupitia maandiko yako. Nachokushauri ni wewe mwenyewe upime kama kuendelea kuwa ndani ya ccm kunaleta tija yoyote kwa taifa lako na chama ulichopo. Kama hakuna tija yoyote basi ni muhimu ukafanya maamuzi yenye manufaa kwako binafsi na kwa nchi yako.
 
Last edited by a moderator:
Ndugu wana JF, hasa wadau wenzangu jukwaa la siasa,nimeona kuna umuhimu wa kuwapa tu taarifa kwamba nimepotea kidogo humu ili kujipanga kutokana na vitisho navyokumbana navyo kutokana na michango yangu mbalimbali humu,hasa kuhusiana na misimamo yangu dhidi ya madhaifu ya chama changu cha CCM kuelekea 2015;kwa wengi,naamini watakubaliana nami kwamba lengo langu limekuwa ni kujenga,sasa hawa wachache kwa mtazamo wao ni kwamba nabomoa chama (CCM) kuelekea 2015; vitisho hivi havijaanza


wamejuaje kwamba wewe ndio Mchambuzi? au hata huko mtaani unatumia jina hilo hilo?
 
hata wewe huna lengo la kuikomboa nchi hii zaidi tu ya kutaka ulaji, zipo njia nyingi za kuikomboa nchi hii sio lazima uwe mwanasiasa, hebu angalia na huko, haimaanishi kuwa kila anayetaka kuikomboa nchi hii ni lazima awe mwanasiasa. unaweza kuwa hata kuni au mafiga na ukawa umeshiriki kuandaa chakula sio lazima uwe sufuria ndio uone fahari kuandaa chakula. Siku zote wanasiasa hutafuta huruma kwa jamii ili kutimiza malengo yao, nadhani na wewe ni sehemu ya hao.
 
ukiwa mwana CCM uwe mtu wa Yes-Yes- Sir!! maisha yako yatakuwa mazuri mno.... vinginevyo unaweza kujikuta una vidole 19, kucha 17 tu na meno 24.
 
Mchambuzi pole sana. swali langu ni kwamba hata huko mtaani unatumia jina hilo hilo?
 
Mkuu wangu Mchambuzi pole sana,tafadhali chukua tahadhari na mapema nchi yetu imefikia mahali pabaya.
 
Last edited by a moderator:
Nakushauri ni bora utafakari gharama za kubaki CCM.

kumbuka hata muasisi wa CCM,mwalimu Nyerere,aliwahi kunena kuwa "CCM si mama yangu" akimanisha kwamba anaweza kuihama CCM wakati wowote endapo itaacha kuzingatia misingi ya kuanzishwa kwake.

Tafakari sana kauli hii ya marehemu baba wa Taifa!

Mwambie mleta mada ajiandae kung'olewa meno na kucha bila ganzi. Aanze kutembea na vidonge vya usingizi ili vijana wa Ikulu wakimtia mikononi anavimeza faster!
 
Mengine mnajitakia
Ukiwa na Price Tag siku zote utatumika na ukishatumika lazima uondoke

Ni kama tu kwenye Muvi, mshiriki part ya mchezo ikiisha lazima aondolewe kwa kufa ama anasafiri milele.
 
Ili uwe salama ni lazima uwataje humu Jf wahusika wote unaowatilia mashaka , uhai wako ni Bora kuliko hayo Majina ya hao Maharamia unayoyahifadhi , Na ikiwa hata kwa hiyo ID yako feki wamekutambua basi bila shaka Jf siyo mahali salama na hasa kwenye hili jukwaa la siasa , lazima Members mjiulize kuhusu usalama wenu, kwa nchi kama hii ambayo watu wanaofahamika wanatobolewa macho bila hata Action yoyote ya polisi , itakuwaje kwa Jf Members ?
 
Mkuu Mchambuzi,
What is CCM For, CCM imekufanyia nini Mpaka uikumbatie kwa kiasi hiko, au hadi siku wakutoe Roho ndo utatoa Ushuhuda wako ukiwa Akherah!!!!!!!
 
Last edited by a moderator:
Jamii yetu inadanganyika kirähisi sana.
Critical thinking haipo kabisa!!!
Ndio maana misururu ya wagonjwa ilijaa Loliondo...
 
Back
Top Bottom