Ndugu yangu Mchambuzi ; hamia CHADEMA. Hao CCM si watu wema. Mimi nimewasoma kwa muda mrefu na nimewatumikia kwa hali na mali kwa nguvu zangu zote lakini kwa kipindi chote tangu niwe na akili mpaka sasa nimekuwa nikiwasoma kwa makini na nimegundua CCM ni chama kinacho dhibitiwa na watu
wachache wenye siri kubwa na malengo ambayo ni ya kutia shaka na pengine ya kuogopesha kwa mtu wa kawaida pale anapoyagundua..
kama mtu anania ya kukudhuru hawezi kuja kukutishia, huo unaitwa mkwara. Jamaa kama anania mbaya na wewe anafanya kweli.
Huko nako kuna "GAIDI" Lwakatare?? Labda Nchemba
Hili jambo la kumtaja alietishia maisha ni jambo zuri na lenye manufaa.Waswahili husema "ukishamjua mchawi na ukamuambia (ukamuweka wazi ) hawezi kukuloga tena".Mkuu Mchambuzi ; ukiwataja wahusika wataogopa kuendelea kufanya njama za kukuhujumu kwani ikitokea ukidhurika, bundi atalia upande wao.Kadhalika wale wasiojua kwamba ni nani adui wa nchi hii nao watajua sasa! mkuu Mtambuzi wataje watu hao maana hata hivyo hakuna haja ya kumuonea haya mtu asiyekuwa na utu.Kwa kufanya hivyo pia utaviweka vyombo vya usalama katika hali ya tahadhari.Ila usifanye hivyo kama huna ushahidi wa kutosha na wakuaminika maana inaweza kukugharimu vibaya.nani amekutishia maisha? Mtaje
Mkuu,
Umeingia shirika na wachawi, leo unawasema hadharani, sasa unashangaa nini kusikia ya kuwa sasa wanapanga kukutoa kafara na wewe?
Pole sana lakini hivyo ndivyo ngoma ya wanga inavyochezwa!
Tunakuombea mkuu Mungu Akulinde na kukuepusha na mabaya yote wanayoyapanga.
Siku ingine ukisikia watu tunalalamika kuhusu magamba na umafia uliokithiri kwenye serikali ya ccm nafikiri utatuelewa na kukubaliana nasi ya kuwa muda umefika wa kuwaondoa kabla hatujatolewa kafara wote kwa uchu wa watu wachache!
Mungu Ibariki Tanzania!
Nimeagiza container mbili toka China yamejaa meno bandia na kucha bandia. Najua soon biashara hii itakuwa inalipa sana hapa Bongo.
By Mchambuzi
...vijana tuna haja ya kuacha kuiga siasa za wazee zilizojaa majungu,fitina na visasi,badala yake...