Taarifa: Usalama Wangu Hatarini

Taarifa: Usalama Wangu Hatarini

Kuna watu hata ukiwaambia CCM wanataka kumpa Rais wa China mlima Kilimanjaro aondoke nao kwenye ndege yake wataamini...
 
mkuu Mchambuzi kuwa makini sana na vitu vyenye ncha kali au pollonium 210.just a word of advice you can heed if you like.
 
Mchambuzi bado hujanishawishi nikukubali na masuala yako, wewe kama umetishiwa ni kwamba hawataki/hawakutaki mada zako wala wewe hutakiwi ndiyo maana kuna vyama vingi, ukiweza hamia kingine kama hutaki achana na haya mambo ya siasa na mada unazoandika.
CCM ni mama yako au baba yako?
 
maslahi ya watanzania wote kwa ujumla si ya sehemu flani au kabila au dini.
Chama cha ccm kina wajali wananchi wake si chama cha kusacrifice watu kwa manufaa ya wachache.

na huyu anayelalamika ni Mkenya? Nyerere alivyouliwa na Mkwapa je?
 
Tanzania kila mmoja kwa sasa "akitishwa/maisha kuwa hatarini" mashitaka anapeleka JAMII FORUM.

Kuna watu wameanza kuuza propaganda za njia ya kijasusi.

Siasa kwa sasa imeingiliwa na wenyewe.

SOMETHING'S FISHY
 
Mchambuzi,lifie taifa usiifie ccm mkuu!Sitaki kuwa rude lakini haustahili huruma kwenye hili mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Kuna watu hata ukiwaambia CCM wanataka kumpa Rais wa China mlima Kilimanjaro aondoke nao kwenye ndege yake wataamini...

That's true bro!!!

Wana CCM wanaamini kila kitu kinachosemwa na CCM kiasi kwamba wanaamini serikali ya CCM imeweza kutuletea maendeleo ndani ya miaka 50. Kama unabisha kuuliza Ritz!!!
 
nani amekutishia maisha? Mtaje

Kama ameamua kuja hapa kutoa taarifa basi ingekuwa vizuri taalifa yake akaikamilisha.

Kama anasema mpaka ana majina na sijui hayo majina amepewa na nani?

Tatizo liko wapi mpaka anashindwa kuyataja.
 
Kama ameamua kuja hapa kutoa taarifa basi ingekuwa vizuri taalifa yake akaikamilisha.

Kama anasema mpaka ana majina na sijui hayo majina amepewa na nani?

Tatizo liko wapi mpaka anashindwa kuyataja.

Anajua watu wanalaghaika kirahisi. Na kwa kiasi fulani amefanikiwa...
 
Kuna watu hata ukiwaambia CCM wanataka kumpa Rais wa China mlima Kilimanjaro aondoke nao kwenye ndege yake wataamini...
Mkiongelea mambo ya uzinzi mbele ya mzinzi.......ni lazima michango ya mzinzi katika mazungumzo yatajawa na hofu na kujihami.........wewe ni mfuasi wa Magaidi
 
Pole sana,
Chukua hatua za haraka za kujihakikishia usalama wako. Baada ya hapo wasiliana na wadau wengine wakusaidie kuwa salama na kuendeleza unayodhani ni azma yako kwa faida ya nchi yako. Karibu Tanzania: Mungu akulinde.

Marcossy umepotea, nasikia na wewe ulikuwa chimboni poelni wote mnaosema ukweli. Najua wewe hawakuwezi. kama bado uko morogoro karibu tena.
 
Ndugu wana JF, hasa wadau wenzangu jukwaa la siasa,nimeona kuna umuhimu wa kuwapa tu taarifa kwamba nimepotea kidogo humu ili kujipanga kutokana na vitisho navyokumbana navyo kutokana na michango yangu mbalimbali humu,hasa kuhusiana na misimamo yangu dhidi ya madhaifu ya chama changu cha CCM kuelekea 2015;kwa wengi,naamini watakubaliana nami kwamba lengo langu limekuwa ni kujenga,sasa hawa wachache kwa mtazamo wao ni kwamba nabomoa chama (CCM) kuelekea 2015; vitisho hivi havijaanza


wamejuaje kwamba wewe ndio Mchambuzi? au hata huko mtaani unatumia jina hilo hilo?

Huyu jamaa anatumia picha yake halisi na ameshawahi kujitaja jina hapa
 
I salute you Mchambuzi. Kama ni mkuki kwenye moyo umegonga katikati! Kwanza pole na vitisho na hiyo ni kawaida kwa wale wanoleta fikra mpya katika chombo ambacho kimezoea kufanya mambao kwa utamaduni bila kujaili alama za nyakati. Wazee wengi wa CCM pamoja na busara zao wamefika mahali wakawa waoga wa kukosoa mambo yanavyoendeshwa na chama kwa hofu ya kuitwa wasaliti. Hivyo wamekaa kimya ili kulinda uwepo wao kwenye uongozi na muhimu kabisa kwao kulinda maslahi binafsi.Huu ni unafiki uliokamaa ambao sasa umezaa mkwamo wa mawazo wa namna bora ya kukiendesha chama. Na kuongeza maumivu kwenye kidonda tulidhani kwamba walau akina Nape wangetukwamua hapa tulipo na kuanza kusema na kutenda "revolutionary ideas" ndani ya chama lakini hapo napo tumekwama.

Sasa tunahitaji wana CCM waliopandwa na wendawazimu kama wewe ili tuweze kutoka hapa tulipo. Hii ni kukifanya chama kijitafakari na kutengeneza mipango ya miaka 100 ijayo. Hii haiwezi kufanyika kwa njia ya propaganda kama invyofanyika sasa. Inabibidi chama kivue ngue zote na kujitazama kikiwa uchi ili kuona katika umbile lake ni wapi pamekosewa na nini kifanyike ili kirudishe umbile la awali. Kama ni kufanya mazoezi ili nyama za uzembe zilizoota ziondoke na kifanye hivyo.

Kwa hali ilivyo hivi sasa na kuzingatia uelewa wa watanzania wa kawaida unaokua kila kukicha,kasi ya Chadema na utamu wa madaraka CCM itatuingiza kwenye vurugu kubwa na kusababisha damu imwagike kama wataendelea kung'ang'ania na kukumbatia mambo ambayo yanakifu mioyo ya watanzania. Angalizo watu wengi wamejiunga na Chadema si kwa sababu wakemekaa chini na kusoma sera zake na kuzikubali bali ni kwa kuichukia CCM. Pia wapo wale ambao si wanachama wa Chadema kwa kadi na kuhudhuria mikutano(unachama wao upo moyoni) ila wanaiunga mkono kwa sababu ya mambo ya kipuuzi na ya kishenzi yanayofanywa na CCM.
 
ccm ni devil worshipers!! watatuua mwili, lakini hawataimaliza mbegu yetu kuing'oa ccm tuliyoipanda! watuue wote basi, maana ni dhahiri HATUWAPENDI NA WANALIJUA HILO!
 
Mchambuzi pole. Hakika ni kutoitakia nchi yetu memo kwa watu kuendelea kufikiria na kufanya ujuma ili chama Fulani cha siasa kife! Tunahitaji kuondokana na mawazo hayo baada ya kuingia kwenye mfumo wa vyama vingi. Pia tunatakiwa sasa kufanya siasa za kistaarabu ambazo zinakubali kuwa chama chochote kinachoshinda kinaweza kutawala nchi yetu. Hizi kauli zinazoendelea kusemwa na kuwaaminisha wananchi kuwa ni chama Fulani tu kinaweza kuongoza au chama Fulani hakistahili hata kikishinda zinapaswa kuachwa vinginevyo tunafuata mfumo tusiouamini.
 
Tanzania kila mmoja kwa sasa "akitishwa/maisha kuwa hatarini" mashitaka anapeleka JAMII FORUM.

Kuna watu wameanza kuuza propaganda za njia ya kijasusi.

Siasa kwa sasa imeingiliwa na wenyewe.

SOMETHING'S FISHY
Huyu Mlevi wa dengelua kumbe yupo hapa twende kwenye jukwaa la jokes kwasababu hapa hoja zako ni hafifu sana
 
Inavyoonekana hizi propaganda kwa sasa zimeanza kushika kasi na kufanya kazi.

Kuna mwingine naye alipotea lakini juzi akaibuka na matamko.

kuna mwingine anaishi Uskochi, naye alidai amepata vitisho

Mchambuzi na yeye amekuja na malalamiko.

kwa mtazamo wa haraka. Hawa watu wanafanya nini kikubwa ambacho wanaweza kuiogopesha CCM mpaka iwatumie ujumbe wa vitisho?.

Kuna watu wako nyuma ya hizi propaganda chafu. TIME WILL TELL.
 
Back
Top Bottom