Taarifa: Usalama Wangu Hatarini

Taarifa: Usalama Wangu Hatarini

Mchambuzi,

Pole sana ndugu yangu kwa masahibu haya. Naomba nikupe moyo tu kuwa haya hayaishi na hayatakoma. Tawala mbili zinapogombania mioyo ya watu basi mara zote tawala ambayo inaelekea kushindwa hutumia nguvu zaidi kujipa nafasi. Gaddafi alijaribu sana kuzuia mapinduzi, Assad naye hivyo hivyo na hata Milosevic naye alijaribu sana. Lakini watu wakishaukataa utawala moyoni hakuna risasi wala visu vinavyoweza kulazimisha kinyume chake.

Kama umeamua kuwa huru kifikra na kimtazamo ujue kuwa kuna gharama yake. Gharama hiyo si ndogo na wakati mwingine hulazmisha gharama kubwa zaidi (ultimate price) mtu kulipa. Wapo wengi kabla yetu ambao kutokana na kuamua kuwa huru walijikuta wakilazimishwa kukimbia nchi zao, kuhama familia zao na hata wakati mwingine kuishi maisha ya kujificha ficha ili kupata nafasi ya kupigana tena.

Jambo kubwa na la maana ni kuwa usiwape maadui wako nafasi ya kukunyamazisha; jipange, na hakikisha unakuwa mbele yao maili mia moja! Mwenzako naendelea kusimama si kwa sababu hawakujaribu au kunijaribu; ni kwa sababu nimejitahidi mara zote kuwa mbele yao 1000 miles! So, keep on fighting, reorganize, but never surrender.

NIamini nikisema hivi; watawala waliojeruhiwa hawana msamaha. Kama kuna mtu yeyote anayepigania mabadiliko akidhania kuwa ati akigeuka watamseheme anajidanganya. Hawa watu hawana msamaha so, live free or die trying!
 
Mchambuzi, pole sana! I wish I could help but who am I! Hata hivyo hii ripoti yako hainishtui hata kidogo, hivyo ndivyo hali ilivyo. Pamoja na umri wangu, sijawahi kuwa mwana CCM na kwangu hiyo ndiyo sifa inayonifanya nijisikie huru na kutembea kifua mbele...pia sikuwahi kuwa mwanachma wa TANU pamoja na kwamba nilimpenda sana Mwalimu Nyerere kama kiongozi na kama alama ya utaifa uliotukuka. Tazama sasa CCM inavyomdhalilisha Baba wa Taifa baada ya kumnyamazisha milele tarehe 14 Octoba mwaka 1999.

Sijawahi kuwa mwananchama wa chama chochote cha siasa Tanzania ingawa hapa JF wananihusisha na Chadema kwa kuwa tu siipendi CCM kwa sababu naijua vizuri CCM. These guys will stop at nothing to retain power kwa sababu kuu moja...without power, CCM is dead with no ground or record to stand on and believe me, I know. Kila mtu ndani ya CCM anatakiwa ajue hilo lakini like always imejaa wanafiki wanaojidanganya kuwa they know better, kwamba wanaweza kuleta mabadiliko from within...No, never, not peacefully!

I dare and am prepared to call a spade a spade...I only have love for my country and my tears of sadness are a witness to its desecration. Tazama vijibwa vya CCM vinavyokukejeli na kukudhalilisha humu na comments za kipuuzi na za kijinga, they know what they are doing...Kumbuka The world is a dangerous place to live; not because of the people who are evil, but because of the people who don't do anything about it. Dont you think it is hightime we all stood together and did something? Best of luck, Adios!

Mag3.
 
Jamii yetu inadanganyika kirähisi sana.
Critical thinking haipo kabisa!!!
Ndio maana misururu ya wagonjwa ilijaa Loliondo...

babu wa loliondo ni project ya CCM, ya ku-buy time kwa matukio, wako na project lwakatare kombinenga kibanda, wakitoka hapo wanakuja na project lucifer nyingine.
 
Kama wamekukosakosa ondoka huko maana watakumaliza.Huwezi kuibadili ccm mkuu.Kolimba alijidai kuwakosoa wakamwambia sawa kabisa,njoo karibu utueleze vizuri zaidi mawazo yako murua!Alipoenda ukawa mwisho wake.

Ukiamuwa kubaki ndani kama kina Mwakyembe,basi juwa siku yako itafika tu,otherwise ukubali kula matapishi yako mwenyewe na kuwa "ndiyo mzee" kwa mafisadi ama vuvuzela kama Nape.
 
Usihofu kufa, kwa kuwa "Mtu yeyote, ambaye hatafanya kitu chochote hapa duniani, ataishi, hatimaye atakufa, bila kufanya kitu chochote" Hivyo basi, kuliko ufe bila kufanya kitu chochote hapa duniani, bora ufanye kabisa, ili ufe wakati umefanya kitu, ambacho kwake tutakukumbuka. Fanya kweli, ili u-rest in peace kwa haki.
cc-Kolimba the great.
 
Wasira naye anadanganya kuwa hakuna utekaji, wakati hadi South Africa mzee kafuatwa, kateswa
 
Wewe kuitwa mchambuzi jina feki hapa jukwaani nani anakujua? Ungekuwa unatumia jina halisi ningekuelewa, ila hii ya jina feki halafu utishiwe umebugi meen
 
Wewe kuitwa mchambuzi jina feki hapa jukwaani nani anakujua? Ungekuwa unatumia jina halisi ningekuelewa, ila hii ya jina feki halafu utishiwe umebugi meen

We jina linakuhusu nini, muhuni tu wewe unafanya JF sehemu ya kupotezea taim.......unataka kumjua ili iweje?
 
Wewe kuitwa mchambuzi jina feki hapa jukwaani nani anakujua? Ungekuwa unatumia jina halisi ningekuelewa, ila hii ya jina feki halafu utishiwe umebugi meen

Join Date : 12th February 2013

Posts : 189

Rep Power : 343

Likes Received:22
Likes Given:22

Angalia tarehe yako ya kujiunga JF halafu linganisha na hii;

Join Date : 24th August 2007

Location : Tanzania

Posts : 2,675

Rep Power : 8327

Likes Received:3411
Likes Given:2593
 
Kama unakubali tatizo kubwa ni wazee wa sasa ni bora uvute muda mpaka watakapo ondoka na kwa sasa ujikite kujiimarisha kutengeneza influnces zako una elimu ya kutosha to formulate an attacking strategy huko baadae kama unaona siasa ndio njia pekee uliyopangiwa kwa sababu uzijuazo.

Lakini kupambana na watu wanaomiliki usalama wa taifa, polisi na jeshi na kote huko kuna wazee hao hao, nadhani unakuwa too ambitious to think you can change the system abraptly. Kibaya zaidi hawa watu ni waoga, maana hata positive criticism hawataki tena kama washaanza kutishia watu.

Go back kwakuwa umeshaijua CCM kindani draw up your 'game theory' and be in the right team within na si ya waoga ambao wanataka kuwafanya wenzao chambo. Mabadiliko ndani ya CCM yataletwa na vigogo walioshiba tu kwa sasa, wengine bado wanapiga mipango ya kufikia zamu zao hawa ndio unatakiwa kujipanga hili baadae kusiwe tena na zamu. Kama zamu hiwe ya watanzania it is possible kutoa status quo and liberate the nation, siasa zetu bado changa lakini marekani walipitia huko ndio evolution yenyewe.

Party Games: Getting, Keeping, and Using Power in Gilded Age Politics - Mark W. Summers - Google Books

Pole sana.
 
Kaa mkao wa kujiandaa zaidi in case ukiweza kama unao uwezo weka mikakakti mahususi...mbaya ananjia nyingi na mpaka akutishe huwa ameshajiaandaa kitambo. Mungu akutangulie..Kumbuka yote yana mwisho as long as wote pua zinaangalia chini nao watafuata
 
Nchi itakapochukuliwa na kina Xi-Jinping hata wale wa deal za kuruka na ndege za usiku kutuuza hawatapewa uongozi watanyongwa tu hadharani (kifo wanachokikwepa kwa kuuza chuma na gesi).
 
Wewe kuitwa mchambuzi jina feki hapa jukwaani nani anakujua? Ungekuwa unatumia jina halisi ningekuelewa, ila hii ya jina feki halafu utishiwe umebugi meen

Kwa akili zako finyu unadhani kwa vile unatumia jina feki hapa basi huwezi kujulikana.

Yaani unajiona uko secure kweli kwa kutumia jina lako feki la NAKEMEAUDINI.

But the button line humjui Mchambuzi ni nani na kama humjui ni bora kuuliza kuliko kuanika hadharani ujinga wako.

Ungekuwa unamjua Mchambuzi ni nani lazima ungekula matapishi yako yote na ya wengine wote walioandika kama wewe.

Kuuliza siyo ujinga, but ignorance is bliss.
 
Jamii yetu inadanganyika kirähisi sana.
Critical thinking haipo kabisa!!!
Ndio maana misururu ya wagonjwa ilijaa Loliondo...

Mkuu, simple logic tu inaeleza kuwa mkataa wengi ni mchawi.Haiyumkiniki asilimia kubwa ya wanaochangia mada waone logic ya kilichoandikwa na Ndugu Mchambuzi lakini mwenzetu-gwiji la critical thinking- uone tofauti.

Tell you what, we are dealing with a double-headed monster. It will continue to attack the victims thrown to it by you,but, trust me, when deprived of victims, it's going to strike at you same guys who have been taking care of it. Mchawi akiishiwa na wa kumroga huigeukia familia yake mwenyewe.

Endeleeni kufurahia uharamia huu lakini mkae mkitambua kuwa kuna siku nanyi mtakuwa wahanga wa hayahaya mnayoyakenulia meno.

TIME WILL TELL
 
Hii post ndo itawafanye wakuteke mkuu, jisalimishe huko CCM hakuna watu wa aina yako wote walishakimbia ndio maana wanakuona adui!
 
Back
Top Bottom