Taabu na Pombe ni Kaka na Dada

Taabu na Pombe ni Kaka na Dada

Mkuu wewe endelea kunywa soda zako.na mango passion!
Laiti ungejua izo zinavyotengenezwa wala usingeleta huo uzi hapa.!
Alafa shida sio pombe,shida ni mnywaji..!
Pombe haijawai kuwa na shida kwa waastaarabu..!
Bila kujua zinatengenezwa vipi, ujue soda sio bia, hawawezi kuwa kitu kimoja
 
Ukifuatilia vizuri watu wenye taabu fulani maishani ndio hutumia sana pombe ili wasahau uchungu walio nao moyoni ili wajiliwaze.

Uzuri ni kwamba biblia imetufunulia yote katika:
Mithali 31:

6 Mpe kileo yeye aliye karibu na kupotea; Kampe divai yeye aliye na uchungu nafsini.

7 Anywe akausahau umaskini wake; Asiikumbuke tena taabu yake.

Utakunywa pombe utasahau machungu kwa muda tu asubuhi ikifika pombe itaisha utaendelea kuyakumbuka machungu yako.

Dawa ni kumrudia Yesu, akutue mzigo wako. Acha pombe haitoi machungu.
Kunyweni kwa kiasi.
 
Nakubali mtumishi,

Pombe inaweza kukufanya usahau kwa muda, lakini haiwezi kuondoa sababu iliyokufanya uumie. Usiku unaweza kulewa ukasahau, lakini asubuhi ukiamka, tatizo bado lipo. Kileo kinapokwisha, maumivu yanaweza kurudi. Ndiyo maana dawa ya kweli si kukimbia maumivu kwa pombe, bali kumrudia Yesu na kumkabidhi mzigo wako. Pombe inaweza kuzima hisia kwa muda Yesu ndiye anayebadilisha moyo na kukupa nguvu ya kukabiliana na maisha.

Mithali 31:6–7 haisemi kwamba pombe ndiyo dawa ya kudumu ya huzuni, inaeleza matumizi ya kileo kwa mtu mwenye uchungu ili kwa muda asikumbuke taabu yake.
 
Ukifuatilia vizuri watu wenye taabu fulani maishani ndio hutumia sana pombe ili wasahau uchungu walio nao moyoni ili wajiliwaze.

Uzuri ni kwamba biblia imetufunulia yote katika:
Mithali 31:

6 Mpe kileo yeye aliye karibu na kupotea; Kampe divai yeye aliye na uchungu nafsini.

7 Anywe akausahau umaskini wake; Asiikumbuke tena taabu yake.

Utakunywa pombe utasahau machungu kwa muda tu asubuhi ikifika pombe itaisha utaendelea kuyakumbuka machungu yako.

Dawa ni kumrudia Yesu, akutue mzigo wako. Acha pombe haitoi machungu.
Uko sahihi
 
Mkuu wewe endelea kunywa soda zako.na mango passion!
Laiti ungejua izo zinavyotengenezwa wala usingeleta huo uzi hapa.!
Alafa shida sio pombe,shida ni mnywaji..!
Pombe haijawai kuwa na shida kwa waastaarabu..!
Hahaha
 
Hukatazwi kuamini unachoamini, ila huruhusiwi kujumuisha wote kwenye kundi lako la kutokuamini.
Kwani nimemjumuisha mtu hapa? Mpaka watu wameenda kutatua matatizo kwa kunywa pombe, wengine kujiuza na wengine hadi kujiua huyo Yesu anakuwa wapi?
 
Nimepitia comments za watu niwakali haswa wanatetea ulaji. Nina ndugu yangu hata yeye mwenyewe anatamani kuacha pombe. Naomba mbinu mtumishi.
 
Yesu Hana Msaada wowote kwenye maisha ya watu, usipopambana mwenyewe
Ana msaada ndugu 100%. Akili za binadamu zina mwisho. Kuna vitu haziwezi kufanya kutokana na mazingira au muda uliopo. Hapo sasa ndio Yesu anahitajika sana.
 
Mtakatifu Kambarage akipiga vombo...
Ahahahhaha 😅😅😅😅kama wafuasi wa Yesu walipiga na wakapungukiwa na akayabariki maji yakawa pombe kwanini mtakatifu kambarage asijipigie...
 
Back
Top Bottom