X-PASTER
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 11,610
- 1,810
Kwa kitu gani haswa...!? Wacha jazba ndugu!Bro vp!!! mbona unanifuatilia sana??? ushairi sio gypsum au vigae mpaka inishughulishe.
Kwa kitu gani haswa...!? Wacha jazba ndugu!Bro vp!!! mbona unanifuatilia sana??? ushairi sio gypsum au vigae mpaka inishughulishe.
Kwa kitu gani haswa...!? Wacha jazba ndugu!
umechelewa naona,Nimekupata muungwana vipi walalama'
Kuachama hujaacha tangu enzizo za kula kwa mama'
Kipi chakuudhi watu wengine kula nyama'
Ikiwa meno huna mifupa yetu mate waitema?
Ramadhan mwezi wetu katujalia karima.
Kufunga ni lazima na twajifunga kwa hikima.
Huko kula kwa kuhama ndo nasikia ukisema.
Hujasoma zetu sunna kula na njaa ndio dhima'
Weye chako wakipima kwa vijiko nazo uma'
Wapotoka kutuama umagharibi wakupa cha kusema'
Twabadili mida ya kumung'unya na thawaze chungu mzima'
U mpotevu weye mwana,
Islamu hutaijua kwa kusakama'
Tabakia na hizo dhana ukweliwe hutoweza kuuzima'
Chakula ndicho hasa kila ufikapo shahar wa rehema'
Sijakaa niko wima na wasaa nkipata yapo mengi ningetema'
Nakana ulodhani na usije tamba hadharani, sie twala vilo vywetu hatuibi na kuazima'
Kitabuni tulisoma na nabii kashadidia, ukweli huu sije kwacha macho pima'
Nakwachia hizo taadhima nawe je nijibia ukisoma.
Nimekusoma ewe mshika tama unowaka na kuzima'
Mmahiri wa kusema ulokosa kauli zilo wima'
Ramadhan shurti uijue ndo waeza kemakema'
Misosi ya haja ndo sababu wa weye kutupima?
Thawabuze tupatazo ndaniye hujazisema'
Masaa twabadili na hiyo yake adili, mchana wenu nyie makobe kuachama'
Tangu enzi twaamrishwa fungeni mfudhu kwa yalo mema'
Saumu ni kipimo kwa muumini na kujua vipi njaa huuma'
Walaji mchana kama nyie hamtojali hii ahadi kwani mu wakosa huruma'
Twajifundisha kugawana na kuepuka ya dhuluma'
Kisa chako nshakisoma Mwezini Biasharazo zenda mrama'
Imani yao waifwatiza wasiwachwe siku ya kiama'
Twabadili ulaji na twatafuna kwa nudhuma'
Kobe la mchana endeleza zako fitina na uchokapo yakungoja kwaresima'
hakuna kitu thawabu,kwa kubadili ratiba
mchana unakauka,usiku washindilia,
chakula kikiwa kingi,kwatumbo usiku kucha
ramadhani kubadili,ratiba ya kutafunaaa
mchana kwenye mkeka, usiku ndio shuguli
tandika misosi mingi,kulipiza ya mchana
najuta kwa siku hizi, misosi sokoni kwisha
ramadhani kubadili,ratiba ya kutafuna
mfungo kabla yake,vyakula vingu sokoni
mfungo ukiashaanza,vyakula sokoni isha
hii inadhihirisha,mwezi wa kula kwa sana
ndio maana tunaona,misosi sokoni kwisha
chapati na maandazi,kacho nazo kababu
sambusa nazo chachandu,maharage yenye nazi
mihogo nayo magimbi,mbatata na malimao
nakupa pole jamani,ewe tumbo kusaganaaaaaa
Ukigagadua vizuri mistari hiyo inamaanisha funga sio mateso bali ibada na malipo yake ni kwa Mwenyezi Mungu. Ndo maana inasisitizwa kuwahi kufuturu na kuchelewa kula daku.Mathayo 6:16,...tena ninyi mfungapo msiwe kama wenye uso wa kukunjamana; maana hujisumbua nyuso zao ili waonekane na watu kuwa wanafunga Mathayo 16:17,....bali wewe ufungapo jipake mafuta kichwani, unawe uso Mathayo 16:18.....ili usionekane na watu kuwa unafunga, ila baba yako iliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.
any way turudi kwenye somo husika,
Kuhusu kubadili ratiba ya kula mwezi wa Ramadhan ni lazima kwa sababu mafundisho yanasema:X-Paster hodi nakuja, Jinius sichukie,
Tumaini kwako naja, Sadeeq unisikie,
Hafif andaa hoja, MziziMkavu nisikie,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadiri kula.
Nauliza tangu zama, majibu sijayapata,
Nisijeleta dhahama, na jibu kutopata,
Angalizo la mapema, kwa wale wenye utata,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadiri kula.
Chonde chonde waungwana, jazba tuweke mbali,
Tukwepe kusuguana, elimu ikawa mbali,
Midomo tukaishona, na likawa chungu swali,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadili kula.
Nimehoji tangu zama, majibu hayaridhishi,
Milo yote kutokwama, kutafuna hamuishi,
Chapatti mwazisukuma, na uji mkijinakshi,
Ramadhani ni mfungo am mwabadili kula.
Milo mitatu ya mchana, mwaipeleka usiku,
Tena mwasutama mchana, mwaomba fika usiku,
Ili kuuulipiza mchana, kwa masaa ya usiku,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadili kula.
Tena mwaanza futari, pale saa za jioni,
Tena mkiwa munkari, kujikunjua usoni,
Na mmejaa tafakari, zile za daku sahani,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadiri kula.
Mwakandamiza majimbi, tena vyakula vizito,
Bila kusahau tambi, ili tumbo liwe zito,
Mwajilaza kwanye kumbi, na mkitoa hewa nzito,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadili kula.
Tumaini namaliza, X-Paster tafadhari,
Talmud kupunguza, Sadeeq tahadhari,
Maralia we chomoza, sitaki zako kejeri,
Hivi kweli mnafunga, au mwabadiri ratiba.
Miongoni mwa fadhila za mwezi mtukufu wa Ramadhan ni kufuturishana na kulisha maskini, ndo maana futari zinaliwa nje mabarazani ili hata wapita njia waweze kushiriki. Kwa hali hiyo mwezi wa Ramadhan watu wanapika chakula cha ziada kwa ajili hiyo.hakuna kitu thawabu,kwa kubadili ratiba
mchana unakauka,usiku washindilia,
chakula kikiwa kingi,kwatumbo usiku kucha
ramadhani kubadili,ratiba ya kutafunaaa
mchana kwenye mkeka, usiku ndio shuguli
tandika misosi mingi,kulipiza ya mchana
najuta kwa siku hizi, misosi sokoni kwisha
ramadhani kubadili,ratiba ya kutafuna
mfungo kabla yake,vyakula vingu sokoni
mfungo ukiashaanza,vyakula sokoni isha
hii inadhihirisha,mwezi wa kula kwa sana
ndio maana tunaona,misosi sokoni kwisha
chapati na maandazi,kacho nazo kababu
sambusa nazo chachandu,maharage yenye nazi
mihogo nayo magimbi,mbatata na malimao
nakupa pole jamani,ewe tumbo kusaganaaaaaa
1 - Kwa Myahudi ili Kuuponya mwili wake ni lazima achukue vumbi la udongo ndani ya kivuli cha choo cha nje, changanya na asali halafu kula" Gittin 69a.
2 -Akitoka mtu nje ya mlango wa choo hapaswi kufanya ngono mpaka asubiri kwa muda wa kutosha kutembea nusu maili, kwa sababu pepo wa choo yuko pamoja naye kwa wakati huo, kama akifanya hivyo (akifanya ngono), watoto wake watakuwa kifafa. "83- Gittin 70a.
3 -Mwanamke ambaye alikuwa anafanya ngono na mnyama anastahiki kuolewa na kuhani wa Kiyahudi. Mwanamke ambaye anafanya ngono na pepo pia hustahiki kuolewa na kuhani wa Kiyahudi Yebamoth 59b
Ooovyoooo!
ramadhani ni shuruba, alizoweka shetwanMiongoni mwa fadhila za mwezi mtukufu wa Ramadhan ni kufuturishana na kulisha maskini, ndo maana futari zinaliwa nje mabarazani ili hata wapita njia waweze kushiriki. Kwa hali hiyo mwezi wa Ramadhan watu wanapika chakula cha ziada kwa ajili hiyo.