Swali..!

Anyisile Obheli

JF-Expert Member
Dec 13, 2009
3,398
319
X-Paster hodi nakuja, Jinius sichukie,
Tumaini kwako naja, Sadeeq unisikie,
Hafif andaa hoja, MziziMkavu nisikie,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadiri kula.

Nauliza tangu zama, majibu sijayapata,
Nisijeleta dhahama, na jibu kutopata,
Angalizo la mapema, kwa wale wenye utata,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadiri kula.

Chonde chonde waungwana, jazba tuweke mbali,
Tukwepe kusuguana, elimu ikawa mbali,
Midomo tukaishona, na likawa chungu swali,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadili kula.

Nimehoji tangu zama, majibu hayaridhishi,
Milo yote kutokwama, kutafuna hamuishi,
Chapatti mwazisukuma, na uji mkijinakshi,
Ramadhani ni mfungo am mwabadili kula.

Milo mitatu ya mchana, mwaipeleka usiku,
Tena mwasutama mchana, mwaomba fika usiku,
Ili kuuulipiza mchana, kwa masaa ya usiku,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadili kula.

Tena mwaanza futari, pale saa za jioni,
Tena mkiwa munkari, kujikunjua usoni,
Na mmejaa tafakari, zile za daku sahani,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadiri kula.

Mwakandamiza majimbi, tena vyakula vizito,
Bila kusahau tambi, ili tumbo liwe zito,
Mwajilaza kwanye kumbi, na mkitoa hewa nzito,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadili kula.

Tumaini namaliza, X-Paster tafadhari,
Talmud kupunguza, Sadeeq tahadhari,
Maralia we chomoza, sitaki zako kejeri,
Hivi kweli mnafunga, au mwabadiri ratiba.
 
ramadhani si chakula, bali ni jina pima
na kama ni chakula, hapo siwezi pima
 
Bisimilahi naanza kwa Jina la rahmani.
Mola aliye muweza, Anaye tupa ihsani
Anipe uwezo kwanza, Kukujibu ukumbini

Ramadhani ni ibada, Sote yatulazimu

Mwezi huu wa fadhila, Na mwezi wa ihsani
Sio mwezi wa chakula, Kushindilia tumboni
Au mwezi wa kulala, Kukoroma kitandani

Ramadhani ni ibada, Sote yatulazimu

Mwezi huu wa ibada, Na kusoma Qur'aani
Ni mwezi wenye faida, Nyingi ziso na kifani
sio mwezi wa kawaida, Ni mwezi wenye thamani

Ramadhani ni ibada, Sote yatulazimu

Fadhila zake ni nyingi, Zinazovuka mipaka
Twajitahidi kwa wingi, Kamba ya Mungu kushika
Na Swalah ndio msingi, wa dini yetu hakika

Ramadhani ni ibada, Sote yatulazimu

Mungu Amesharidhika, Uislamu ndio dini
Milele tahifadhika, Kitabu cha Qur'aani
Tafuta na utachoka, Makosa ndani huoni

Ramadhani ni ibada, Sote yatulazimu

Mwezi huo wa baraka, Wa amani na imani
Ninamuomba Rabuka, Pepo iwe maskani
Ni mwisho wa kuandika, Nimefika kikomoni

Ramadhani ni ibada, Sote yatulazimu
 
Nafurahi kuipata, hii threat ya leo
namimi sitaiacha, itabidi nichangie
ramadhani yatatiza, kwangu kupata majibu
ramadhani huhamisha, masaa ya kula msosi

wengi tunajiuliza ,kwanini yanatokea
siku zile za mfungo, vifafa vinapungua
mfungo ukishaisha, ajali nyingi kuanza
ramadhani huhamisha, masaa ya kula msosi

nimeshapata majibu, majini nayo hufunga
pale yanapofungua, njaa ya damu huwaka
ndo maana ajali nyingi, vifafa na maajabu
wanadamu na majini, hufunga wote pamoja


mwezi wa kuiba nyota, hasa wakikupa daku
humwaga majini mengi, chuma ulete kazini
mchana kupiga soga, jioni ni mahesabu
mwezi wa changa la macho, siri kubwa yafichika

ni mwezi wa maagano, shetwani na wanadamu
mwezi kuabudu nyota, mwezi nayo maruhani
kuipanga mikakati, ya kuuongeza majini
mwezi huu ni hatari, shetwani kuabudiwa


uhamishaji masaa, kula msosi mzito
magimbi tambi chapati,mihogo na vitumbua
vyote hivi kusanyia, kwenye hili tumbo moja
matumbo kuunguruma, kwa misosi shindiliwa


siku zile za mfungo,nyumba ndogo hufukuzwa
mfungo ukishaisha, nyumbandogo karibia
sehemu zile za beach, condom hadi gunia
zote hizi hutumika, kufungua huu mwezi

nawashauri wenzangu, kuwa ni changa la macho
mwamedi kawazingua, hamtakuja elewa
mwapata njaa ya bure, hakuna hata thawabu
mungu mnayemwabudu, kweli ananichekesha.
 
1 - Kwa Myahudi ili Kuuponya mwili wake ni lazima achukue vumbi la udongo ndani ya kivuli cha choo cha nje, changanya na asali halafu kula" Gittin 69a.

2 -Akitoka mtu nje ya mlango wa choo hapaswi kufanya ngono mpaka asubiri kwa muda wa kutosha kutembea nusu maili, kwa sababu pepo wa choo yuko pamoja naye kwa wakati huo, kama akifanya hivyo (akifanya ngono), watoto wake watakuwa kifafa. "83- Gittin 70a.


3 -Mwanamke ambaye alikuwa anafanya ngono na mnyama anastahiki kuolewa na kuhani wa Kiyahudi. Mwanamke ambaye anafanya ngono na pepo pia hustahiki kuolewa na kuhani wa Kiyahudi Yebamoth 59b

Ooovyoooo!
 
1 - Kwa Myahudi ili Kuuponya mwili wake ni lazima achukue vumbi la udongo ndani ya kivuli cha choo cha nje, changanya na asali halafu kula" Gittin 69a.

2 -Akitoka mtu nje ya mlango wa choo hapaswi kufanya ngono mpaka asubiri kwa muda wa kutosha kutembea nusu maili, kwa sababu pepo wa choo yuko pamoja naye kwa wakati huo, kama akifanya hivyo (akifanya ngono), watoto wake watakuwa kifafa. "83- Gittin 70a.


3 -Mwanamke ambaye alikuwa anafanya ngono na mnyama anastahiki kuolewa na kuhani wa Kiyahudi. Mwanamke ambaye anafanya ngono na pepo pia hustahiki kuolewa na kuhani wa Kiyahudi Yebamoth 59b

Ooovyoooo!

nakupa pole sideeq, kwa kutuletea soga
wenzio twaleta point, we watuletea hewa
kati yetu sisi sote, yupi kwetu myahudi
kama waishiwa point, bora unyamaze kimya

ukiingia vitani, usikimbie risasi
kwa kulipua jirani, badala ya mpiganwa
we ukiishiwa point, hukimbilia yahudi
kama waishiwa point, bora unyamaze kimyaa
 
nakupa pole sideeq, kwa kutuletea soga
wenzio twaleta point, we watuletea hewa
kati yetu sisi sote, yupi kwetu myahudi
kama waishiwa point, bora unyamaze kimya

ukiingia vitani, usikimbie risasi
kwa kulipua jirani, badala ya mpiganwa
we ukiishiwa point, hukimbilia yahudi
kama waishiwa point, bora unyamaze kimyaa
1 - Myahudi ni lazima ale kiapo cha uongo wakati goyim anapouliza kama vitabu vyetu vin kitu chochote dhidi yao."Szaaloth-Utszabot, The Book of Jore Via 17.
2 -Akum (asiye Myahudi) ni kama mbwa. Ndiyo, Maandiko Matakatifu yanasema tumuheshimu mbwa zaidi kuliko wasio-Wayahudi. "Ereget Raschi Erod, 22 30
.......atafutaye hupata.
 
1 - Myahudi ni lazima ale kiapo cha uongo wakati goyim anapouliza kama vitabu vyetu vin kitu chochote dhidi yao."Szaaloth-Utszabot, The Book of Jore Via 17.
2 -Akum (asiye Myahudi) ni kama mbwa. Ndiyo, Maandiko Matakatifu yanasema tumuheshimu mbwa zaidi kuliko wasio-Wayahudi. "Ereget Raschi Erod, 22 30
.......atafutaye hupata.

sideeq wahangaika, kama vile mfa maji
hakosi kutapatapa, lazima miguu arushe
hatuongei yahudi, ongelea ramadhani
kama waishiwa point, bora unyamaze kimya

kitabu cheni koran, kinaruhusu uwongo
kudanganya makafiri, unapoyaconvert
kutetea wislam, uongo waruhusiwa
kama waishiwa point, bora unyamaze kimya

jihad itatukuzwa, na hawa wana wa kambo
uwongo utatukuzwa, ili kudanganya umma
wakirsto wayahudi, wakamatwe wauawe
kama hawatakubali, hii dini ya mtume

dunia inashangazwa, ugaidi ongezeka
kitabu chawafundisha, kujilipua mabom
kumpigania mola, waweza kujilipua
kama waishiwa point, bora unyamaze kimya

mihadhara inazidi, kona nyingi daslamu
kuhubiri maugomvi,chuki kwa dini zingine
mmeikosa elimu, kumkichwa kombolewa
kama waishiwa point, bora unyamaze kimyaaaaaa
 
1 - Kwa Myahudi ili Kuuponya mwili wake ni lazima achukue vumbi la udongo ndani ya kivuli cha choo cha nje, changanya na asali halafu kula" Gittin 69a.

2 -Akitoka mtu nje ya mlango wa choo hapaswi kufanya ngono mpaka asubiri kwa muda wa kutosha kutembea nusu maili, kwa sababu pepo wa choo yuko pamoja naye kwa wakati huo, kama akifanya hivyo (akifanya ngono), watoto wake watakuwa kifafa. "83- Gittin 70a.


3 -Mwanamke ambaye alikuwa anafanya ngono na mnyama anastahiki kuolewa na kuhani wa Kiyahudi. Mwanamke ambaye anafanya ngono na pepo pia hustahiki kuolewa na kuhani wa Kiyahudi Yebamoth 59b

Ooovyoooo!
sadeeq ewe pole,
na tena nakupa pole,
ilombatana na ole,
kutuletea gobole.

angalizo nimetoa,
na sikutaka potoa,
zaidi ilimu toa,
talmud acha toa.

si mahali pa hasira,
bali ni hoja kuchora,
iache ikikukera,
usiruke kama chura
 
Bisimilahi naanza kwa Jina la rahmani.
Mola aliye muweza, Anaye tupa ihsani
Anipe uwezo kwanza, Kukujibu ukumbini

Ramadhani ni ibada, Sote yatulazimu

Mwezi huu wa fadhila, Na mwezi wa ihsani
Sio mwezi wa chakula, Kushindilia tumboni
Au mwezi wa kulala, Kukoroma kitandani

Ramadhani ni ibada, Sote yatulazimu

Mwezi huu wa ibada, Na kusoma Qur'aani
Ni mwezi wenye faida, Nyingi ziso na kifani
sio mwezi wa kawaida, Ni mwezi wenye thamani

Ramadhani ni ibada, Sote yatulazimu

Fadhila zake ni nyingi, Zinazovuka mipaka
Twajitahidi kwa wingi, Kamba ya Mungu kushika
Na Swalah ndio msingi, wa dini yetu hakika

Ramadhani ni ibada, Sote yatulazimu

Mungu Amesharidhika, Uislamu ndio dini
Milele tahifadhika, Kitabu cha Qur'aani
Tafuta na utachoka, Makosa ndani huoni

Ramadhani ni ibada, Sote yatulazimu

Mwezi huo wa baraka, Wa amani na imani
Ninamuomba Rabuka, Pepo iwe maskani
Ni mwisho wa kuandika, Nimefika kikomoni

Ramadhani ni ibada, Sote yatulazimu
X-Paster e ndiyo,
sijaridhika nduguyo,
bado nahitaji moyo,
kuyajua ulonayo,

na mimi siyo kilaza,
ilimu nimekatiza,
quran lipomaliza,
maswali nikayajaza.

ni wa Mungu utukufu,
ye zaidi mtakatifu,
mwenye kufufua wafu,
ye tena ni mwaminifu,

usiletee thawabu,
zaidi nataka jibu,
je kufunga ni wajibu,
ama ni ka taratibu
 
Waungwana asalaam, ukumbini nimefika
nimekamata kalam, karatasi nimeshika
ila nakosa faham, ni nini cha kuandika,
Kufunga kweli ibada, hata Wakristo tunayo.

si kama nataka vita, bali nakwepa majungu
Sikulala na kuota, au kutumwa na Mungu
ninapatwa na utata, na moyo una machungu
Kufunga kweli ibada, hata Wakristo tunayo.

Labda niulize swali, Anyisibe na wenzako
wewe huwa ukiswali, na kuomba Mungu wako
wao huja na maswali, kuuliza nia yako
Kufunga kweli ibada, hata Wakristo tunayo.

Swali la pili jamani, pole kama nakukwaza
kufunga huwa ya nini, umeshawahi kuwaza
watu wote kila dini, sauti zao hupaza
Kufunga kweli ibada, hata Wakristo tunayo.

Nasema kweli ibada, ya kunyenyekea kwake
baba, mama hata dada, yatupasa kwenda kwake
tukidhaifisha mwili, roho inasonga kwake
Kufunga kweli ibada, hata Wakristo tunayo.

Waweza funga staftahi, ama mlo wa mchana
ukaomba asubuhi, jioni ukala pina
ukiamua kuwahi, nia yako ndo ya mana
Kufunga kweli ibada, hata Wakristo tunayo.

Usinikashifu mimi, sipofanya utakavyo
usiitukane dini, ili niheshimu yako
kufunga nafunga mimi, njaa bado ije kwako
Kufunga kweli ibada, hata Wakristo tunayo.

Nilishasema tangia, nini maana kufunga
jambo linakusumbua, ama unaomba kinga
ibada umeamua, kila mwezi nitafunga
Kufunga kweli ibada, hata Wakristo tunayo.
 
Waungwana asalaam, ukumbini nimefika
nimekamata kalam, karatasi nimeshika
ila nakosa faham, ni nini cha kuandika,
Kufunga kweli ibada, hata Wakristo tunayo.

si kama nataka vita, bali nakwepa majungu
Sikulala na kuota, au kutumwa na Mungu
ninapatwa na utata, na moyo una machungu
Kufunga kweli ibada, hata Wakristo tunayo.

Labda niulize swali, Anyisibe na wenzako
wewe huwa ukiswali, na kuomba Mungu wako
wao huja na maswali, kuuliza nia yako
Kufunga kweli ibada, hata Wakristo tunayo.

Swali la pili jamani, pole kama nakukwaza
kufunga huwa ya nini, umeshawahi kuwaza
watu wote kila dini, sauti zao hupaza
Kufunga kweli ibada, hata Wakristo tunayo.

Nasema kweli ibada, ya kunyenyekea kwake
baba, mama hata dada, yatupasa kwenda kwake
tukidhaifisha mwili, roho inasonga kwake
Kufunga kweli ibada, hata Wakristo tunayo.

Waweza funga staftahi, ama mlo wa mchana
ukaomba asubuhi, jioni ukala pina
ukiamua kuwahi, nia yako ndo ya mana
Kufunga kweli ibada, hata Wakristo tunayo.

Usinikashifu mimi, sipofanya utakavyo
usiitukane dini, ili niheshimu yako
kufunga nafunga mimi, njaa bado ije kwako
Kufunga kweli ibada, hata Wakristo tunayo.

Nilishasema tangia, nini maana kufunga
jambo linakusumbua, ama unaomba kinga
ibada umeamua, kila mwezi nitafunga
Kufunga kweli ibada, hata Wakristo tunayo.
nipo kutaka ilimu,
wala sitaki laumu,
zaidi taka fahamu,
kuuondoa ugumu.

Compaq nimekupata,
wala hakuna utata,
nadhani hujanipata,
hili swali siyo tata,

mkristo ni wake uhuru,
kufunga na kushukuru,
tena wala si kufuru,
anafunga kwa uhuru.

wengine wana lazima,
siyo baba wala mama,
sharia kuwasakama,
kwao tena ni lazima.

Compaq mi nakuomba,
na sikufungi kwa kamba,
endelea kuyachimba,
uyajue kwa kuomba.

hili swali bado liko,
na majibu yangaliko,
sijalidharau lako,
limeongezea msako.
 
Ubungoubungo said:
kitabu cheni koran, kinaruhusu uwongo
kudanganya makafiri, unapoyaconvert
kutetea wislam, uongo waruhusiwa
kama waishiwa point, bora unyamaze kimya
Tupatie hiyo aya basi, kama mimi ninavyokupa ya Talmud:
Jews may use lies ("subterfuges") to circumvent a Gentile.Baba Kamma 113a
Ubungoubungo said:
wakamatwe wauawe
kama hawatakubali, hii dini ya mtume
Tupe aya kama ninavyokupa mimi hapa:
"Even the best of the gentiles should all be killed Minor Tractates. Soferim 15, Rule 10
Ubungoubungo said:
dunia inashangazwa, ugaidi ongezeka
kitabu chawafundisha, kujilipua mabom
kumpigania mola, waweza kujilipua
"Samson said to the servant who held his hand, "Put me where I can feel the pillars that support the temple, so that I may lean against them." Now the temple was crowded with men and women; all the rulers of the Philistines were there, and on the roof were about three thousand men and women watching Samson perform. Then Samson prayed to the LORD, "O Sovereign LORD , remember me. O God, please strengthen me just once more, and let me with one blow get revenge on the Philistines for my two eyes." Then Samson reached toward the two central pillars on which the temple stood. Bracing himself against them, his right hand on the one and his left hand on the other, Samson said, "Let me die with the Philistines!" Then he pushed with all his might, and down came the temple on the rulers and all the people in it. Thus he killed many more when he died than while he lived. (From the NIV Bible, Judges 16:26-30)"
Samson alijitolea maisha yake kwa ajili ya watu wake!
Ubungoubungo said:
mihadhara inazidi, kona nyingi daslamu
Mipango inafanyika ili siku moja nianze kuja ichambua Talmud katika kona za Dar es salaam.
*Uudandao (Talmud) ndio ukubwagao.
 
Mipango inafanyika ili siku moja nianze kuja ichambua Talmud katika kona za Dar es salaam. *Uudandao (Talmud) ndio ukubwagao.
hivi kinatumiwa na watu gani hicho ki-talmud? maana mi huwa sikwelewi nalo,
hivi kina wafuasi kwa tanzania, jambo jema ukiichambua qurani ili waelewe kuwa kuna uhsiano baina yao
na majini ili kusaidia kazi yahya, lakinikwa hiyo talmud, ataaa, qurani yenyewe hujaimaliza kuirahisisha kwa wafuasi wake unakimbilia talmud kazi kweli kweli! kha!!!
 
Talmud ndio nini, mimi nashinda elewa,
talmud dini gani,mwenzenu siielewi
au ni y awahahudi, au pia ya wahindu
mwenye majibu jamani, naombeni ayalete

dar es salaama yote, masinagogi hayapo
kama yale yalojengwa, kwa wayahudi ziraeli
hatuna masinagogi, talmudi hatuhusu
umeshaishiwa point, unaleta talmudi

sideeq ninakuomba,nionyeshe sinagogi
lakutumia talmudi,ili nije kuelewa
wakristo tafadhali, hatutumii talmudi
kwahiyo haituhusu, kalete hoja ingine
 
sideeq ninakuomba,nionyeshe sinagogi
lakutumia talmudi,ili nije kuelewa
wakristo tafadhali, hatutumii talmudi
kwahiyo haituhusu, kalete hoja ingine
Hodihodi naingia, kijiweni pokeani
Sikia wangu usia ,we Yahudi namba wani
Sikughilibu rupia, Karaha ya duniani
SILIMU EWE YAHUDI; MI KWAKO NAKUUSIA

Ipi raha ya dunia?, silimu sifanye shaka
Wapata akhera pia, malipoyo takufika
Ndio dini Islamia ,Ni adhimu isi shaka
SILIMU EWE YAHUDI; MI KWAKO NAKUUSIA

Wengine wamo kundini, Uyahudi kujikisi
Yahudi si yao dini, mafatani wajihisi
Kikabila pia duni , ajabu wajirahisi
SILIMU EWE YAHUDI;MI KWAKO NAKUUSIA

Kwa kabila we yahudi?, au dini watwambia?
Sio uvumba si udi, wakutafuta kimbia
Ulaya kwao yahudi, hawataki asilia.
SILIMU EWE YAHUDI;MI KWAKO NAKUUSIA
*
Zohar (I, 160a):"Rabbi Jehuda said to him [Rabbi Cezkia]: 'He is to be praised who is able to free himself from the enemies of Israel , and the just are much to be praised who get free from them and fight against them. 'Rabbi Chezkia asked, 'How must we fight against them?' Rabbi Jehuda said, 'By wise counsel thou shalt war against them' (Proverbs, ch. 24, 6). By what kind of war? The kind of war that every son of man must fight against his enemies, which Jacob used against Esau - by deceit and trickery whenever possible. They must be fought against without ceasing, until proper order be restored. Thus it is with satisfaction that I say we should free ourselves from them and rule over them."
 
Ipi raha ya dunia?,
silimu sifanye shaka Wapata akhera pia,
malipoyo takufika Ndio dini Islamia ,
Ni adhimu isi shaka SILIMU EWE YAHUDI;
MI KWAKO NAKUUSIA
yahudi ni kitu gani,
ama ni kabila gani,
utweleweshe jamani,
tuijue kwa makini,

umekimbia swali,
umekwenda sana mbali,
sijifanye wewe mkali,
utakutana wakali,

ya topiki namba moja,
hujayajengea hoja,
kutuletea viroja,
talmud siyo hoja.
 
yahudi ni kitu gani,
ama ni kabila gani,
utweleweshe jamani,
tuijue kwa makini,
Hutuambia ni dini , kwa wengine ni kabila
Yahudi yu mashakani,hapajuwi pa kushika
Halakha yasema dini ,kabila hukubalika
SILIMU EWE YAHUDI;MI KWAKO NAKUUSIA

Wakabwabwaja wazushi , kwa kujitia mazonge
Bileshi ya matamshi , warudi kisengesenge
Uyahudi si ucheshi, chuki kwao ni vidonge.
SILIMU EWE YAHUDI;MI KWAKO NAKUUSIA
*To communicate anything to a goy about our religious relations would be equal to the killing of all Jews, for if they knew what we teach about them they would kill us openly." - Libbre David 37.
 
*To communicate anything to a goy about our religious relations would be equal to the killing of all Jews, for if they knew what we teach about them they would kill us openly." - Libbre David 37.

Samahani nikichangia bila lugha ipasavyo hapa. Namwomba sana mtaalamu wetu wa dini ya Uyahudi na kitabu cha Talmudi atueleze:
Je kile Libbre David ni nini?? Je ni sehemu ya Talmud?? Ni lugha gani?

Maana kwa njia ya kupiga google nimekuta madai eti nukuu hii ni uwongo mtupu hakuna sehemu kwa jina hili
(au jina la kufanana) katika Talmudi popote duniani!

Sasa naomba jibu:

a) Nukuu yako, mkuu, inapatikana katika toleo gani ya Talmudi?
b) wewe umeikuta wapi (yaani Talmudi kwako nyumbani - toleo gani? AU mahali kwenye intaneti kwa kopi-paste - wapi?? AU sauti ya malaika kwako wakati gani? malaika gani?)
c) Je unakubali ya kwamba jina "libbre David" inaonekana zaidi kama Kiitalia lakini haiwezekani kuwa lugha ya Kiyahudi? Unaonaje?
 
. Namwomba sana mtaalamu wetu wa dini ya Uyahudi na kitabu cha Talmudi atueleze: Je kile Libbre David ni nini?? Je ni sehemu ya Talmud?? Ni lugha gani? Maana kwa njia ya kupiga google nimekuta madai eti nukuu hii ni uwongo mtupu hakuna sehemu kwa jina hili (au jina la kufanana) katika Talmudi popote duniani! Sasa naomba jibu: a) Nukuu yako, mkuu, inapatikana katika toleo gani ya Talmudi? b) wewe umeikuta wapi (yaani Talmudi kwako nyumbani - toleo gani? AU mahali kwenye intaneti kwa kopi-paste - wapi?? AU sauti ya malaika kwako wakati gani? malaika gani?) c) Je unakubali ya kwamba jina "libbre David" inaonekana zaidi kama Kiitalia lakini haiwezekani kuwa lugha ya Kiyahudi? Unaonaje?
na asiondoke bila kutoa majibu hapa, kwa upande wangu mie nashukuru kwa ufuatiliaji wako mkuu, maana kha hii talmud nimejaribu atupatie wapi kaitoa bila mafanikio amekuwa anaruka viunzi sana
 
Back
Top Bottom