Anyisile Obheli
JF-Expert Member
- Dec 13, 2009
- 3,398
- 319
Wayebusi hodi naja, Waperizi sichukie,
Mkaananii kwako naja, Nawe Kushi unisikie,
Mwamori andaa hoja, Nzuri na nizisikie,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadiri kula.
Nauliza tangu zama, majibu sijayapata,
Nisijeleta dhahama, na jibu kutopata,
Angalizo la mapema, kwa wale wenye utata,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadiri kula.
Chonde chonde waungwana, jazba tuweke mbali,
Tukwepe kusuguana, elimu ikawa mbali,
Midomo tukaishona, na likawa chungu swali,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadili kula.
Nimehoji tangu zama, majibu hayaridhishi,
Milo yote kutokwama, kutafuna hamuishi,
Chapatti mwazisukuma, na uji mkijinakshi,
Ramadhani ni mfungo am mwabadili kula.
Milo mitatu ya mchana, mwaipeleka usiku,
Tena mwasutama mchana, mwaomba fika usiku,
Ili kuulipiza mchana, kwa masaa ya usiku,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadili kula.
Tena mwaanza futari, pale saa za jioni,
Tena mkiwa munkari, kujikunjua usoni,
Na mmejaa tafakari, zile za daku sahani,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadiri kula.
Mwakandamiza majimbi, tena vyakula vizito,
Bila kusahau tambi, ili tumbo liwe zito,
Mwajilaza kwanye kumbi, na mkitoa hewa nzito,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadili kula.
Mwisrael namaliza, Masadukayo kwaheri,
Jazba kuzipunguza, mwanakureshi tafadhari,
Mfilisti we chomoza, sitaki zako kejeri,
Hivi kweli mnafunga, au mwabadiri ratiba.
Mkaananii kwako naja, Nawe Kushi unisikie,
Mwamori andaa hoja, Nzuri na nizisikie,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadiri kula.
Nauliza tangu zama, majibu sijayapata,
Nisijeleta dhahama, na jibu kutopata,
Angalizo la mapema, kwa wale wenye utata,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadiri kula.
Chonde chonde waungwana, jazba tuweke mbali,
Tukwepe kusuguana, elimu ikawa mbali,
Midomo tukaishona, na likawa chungu swali,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadili kula.
Nimehoji tangu zama, majibu hayaridhishi,
Milo yote kutokwama, kutafuna hamuishi,
Chapatti mwazisukuma, na uji mkijinakshi,
Ramadhani ni mfungo am mwabadili kula.
Milo mitatu ya mchana, mwaipeleka usiku,
Tena mwasutama mchana, mwaomba fika usiku,
Ili kuulipiza mchana, kwa masaa ya usiku,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadili kula.
Tena mwaanza futari, pale saa za jioni,
Tena mkiwa munkari, kujikunjua usoni,
Na mmejaa tafakari, zile za daku sahani,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadiri kula.
Mwakandamiza majimbi, tena vyakula vizito,
Bila kusahau tambi, ili tumbo liwe zito,
Mwajilaza kwanye kumbi, na mkitoa hewa nzito,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadili kula.
Mwisrael namaliza, Masadukayo kwaheri,
Jazba kuzipunguza, mwanakureshi tafadhari,
Mfilisti we chomoza, sitaki zako kejeri,
Hivi kweli mnafunga, au mwabadiri ratiba.