LINITATIZALO TANGU ZAMA....yupo mwenye jibu mwanana?????

Anyisile Obheli

JF-Expert Member
Dec 13, 2009
3,398
319
Wayebusi hodi naja, Waperizi sichukie,
Mkaananii kwako naja, Nawe Kushi unisikie,
Mwamori andaa hoja, Nzuri na nizisikie,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadiri kula.

Nauliza tangu zama, majibu sijayapata,
Nisijeleta dhahama, na jibu kutopata,
Angalizo la mapema, kwa wale wenye utata,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadiri kula.

Chonde chonde waungwana, jazba tuweke mbali,
Tukwepe kusuguana, elimu ikawa mbali,
Midomo tukaishona, na likawa chungu swali,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadili kula.

Nimehoji tangu zama, majibu hayaridhishi,
Milo yote kutokwama, kutafuna hamuishi,
Chapatti mwazisukuma, na uji mkijinakshi,
Ramadhani ni mfungo am mwabadili kula.

Milo mitatu ya mchana, mwaipeleka usiku,
Tena mwasutama mchana, mwaomba fika usiku,
Ili kuulipiza mchana, kwa masaa ya usiku,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadili kula.

Tena mwaanza futari, pale saa za jioni,
Tena mkiwa munkari, kujikunjua usoni,
Na mmejaa tafakari, zile za daku sahani,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadiri kula.

Mwakandamiza majimbi, tena vyakula vizito,
Bila kusahau tambi, ili tumbo liwe zito,
Mwajilaza kwanye kumbi, na mkitoa hewa nzito,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadili kula.

Mwisrael namaliza, Masadukayo kwaheri,
Jazba kuzipunguza, mwanakureshi tafadhari,
Mfilisti we chomoza, sitaki zako kejeri,
Hivi kweli mnafunga, au mwabadiri ratiba.
 
Wayebusi hodi naja, Waperizi sichukie,
Mkaananii kwako naja, Nawe Kushi unisikie,
Mwamori andaa hoja, Nzuri na nizisikie,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadiri kula.

Nauliza tangu zama, majibu sijayapata,
Nisijeleta dhahama, na jibu kutopata,
Angalizo la mapema, kwa wale wenye utata,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadiri kula.

Chonde chonde waungwana, jazba tuweke mbali,
Tukwepe kusuguana, elimu ikawa mbali,
Midomo tukaishona, na likawa chungu swali,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadili kula.

Nimehoji tangu zama, majibu hayaridhishi,
Milo yote kutokwama, kutafuna hamuishi,
Chapatti mwazisukuma, na uji mkijinakshi,
Ramadhani ni mfungo am mwabadili kula.

Milo mitatu ya mchana, mwaipeleka usiku,
Tena mwasutama mchana, mwaomba fika usiku,
Ili kuulipiza mchana, kwa masaa ya usiku,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadili kula.

Tena mwaanza futari, pale saa za jioni,
Tena mkiwa munkari, kujikunjua usoni,
Na mmejaa tafakari, zile za daku sahani,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadiri kula.

Mwakandamiza majimbi, tena vyakula vizito,
Bila kusahau tambi, ili tumbo liwe zito,
Mwajilaza kwanye kumbi, na mkitoa hewa nzito,
Ramadhani ni mfungo ama mwabadili kula.

Mwisrael namaliza, Masadukayo kwaheri,
Jazba kuzipunguza, mwanakureshi tafadhari,
Mfilisti we chomoza, sitaki zako kejeri,
Hivi kweli mnafunga, au mwabadiri ratiba.


Mimi pia litatizwa, dhimaye lishindwa jua
Ramadhani ikabezwa, kila ilipowadia
Utadhani wakimbizwa, jioni ikiwadia
Ramadhani megundua, ni zaidi ya mfungo.

Jioni kikaribia, wanawaza kufuturu
Uji ni wa kuanzia, tumbo kuliweka huru
Zafuata na bagia, na viazi vya Luguru
Kumbe Ramadhani bwana, ni zaidi ya mfungo.

Usiku wote tafuna, tumbo likae sawia
Jua zikichomozana, mbavu zote zi sawia
Hapo mchana kichuna, hakuna sababu kulia
Ulaji wa Ramadhani, ratiba tu badili

Lakini mimejifunza, dhimaye sio chakula
Msingi matendo kwanza, na sio hiyo ratiba
Basi! Swaumu ikiwa kali, kwa nini wanalalama?
Ramadhani ni ibada, si adhabu asilani

Gulioni ukienda, tajua ni Ramadhani
Bei zote zimepanda, badala ya kushukani
Kuelewa lanishinda, walaji meongezeka?
Tutazame Ramadhani, kwa kiimani zaidi.

Najua nimekanganya, unaweza sielewe
Nakubali funga hiyo, na ninaiamini pia
Lakini waifanyao, wasiifaanye adhabu
Raamadhani Kareem, waungwana natakia.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom