Swali la weekend kwa wanafamilia...

Swali la weekend kwa wanafamilia...

inategemeana na mfumo wao wa ndoa.
kwani kuna ndoa zingine zinaona hela ya baba ndio ya familia na ya mke ni ya mke.
lakini zingine kama yangu ni kwamba hela ya mke ni yetu na hela ya mme ni yetu .hivyo tunaziweka pamoja na kufanyia jambo la kimaendeleo kama tunavyopanga pamoja.
ni mtazamo wa familia yetu maana kila mtu ana ndoa yake.
hivyo inaweza kuwa laki mbili au milioni tano na laki mbili kulingana na mfumo tajwa hapo juu
Labda wewe mwenzetu ni mudhungu, muulizaji analenga Muafrika mwenyeji wa Tanzania. Hapo familia ina akiba ya laki mbili tu kibindoni, si kama napenda bali sheria yetu ya ndoa inamtwika mume majukumu yote ya kugharamia ndoa, mke anayo hiyari kuchangia ama la! Sheria haimbani.
 
Then mkiji mnasema.mnataka mwanamke anayejali. Kiujumla tuna wake lakini walio wengi ni wabinafsi. Ni bora mwanaume uweke wazi sehemu ya kipato na nyingine haitakiwi kujulikana maana utaleta expectations za matumizi ya hela uliyonayo ma mara nyingi interest kunwa zikiwa ni za ke.
Hivi alowapelekea wawe wabinafsi hivyo ni akina nani?
 
Jumla ni laki mbili kwenye matumizi ya familia, mwanamke hata kama Ana million wewe Una 50,000/= ni lazima utoe hela ya matumizi kwaajili ya familia
Hivi haya mnayoyaongea ndio yanayotokea kwenye hizo familia zenu au ni assumptions tu!!
 
Kwa hiyo nikitaka niende vicoba, sherehe, labda nna vipodozi vimeniishia, nahitaji kutengeneza nywele na vingine natakiwa niombe hela? yaani hiyo milion 4 niliyotoa utakua ujaridhika nayo? Kingine ambacho unaeza usijue wanawake lazima tubakishe hela ya emergency likitokea tatizo lolote lile, so hiyo milion 1 usistuke kuona sijaitoa inaeza kuja kusave baadae
Mkuu kila kitu kiwe hadharani kama ni cha familia hata vikoba na vipodozi maana hata ya bia name itatolewa hapo hapo,Pia kama nikusave kwa emergency lazima ziwepo hadharani tujue tunasave sh ngapi pia!
 
Laki mbili na ikizingatiwa wanaume wa kiafrika kwa asilimia kubwa hawapendi kulelewa au kutumia hela ya mwanamke. Ila kwa wale waliojiwekea utaratibu mzuri ni milioni 5.2
 
wanaokwenda club ijumaa ndio hao hao wanaokwenda kanisani jumapili.

so pa kukutana sio ishu... bar tunaenda jioni na kanisani asubuhi.. ila watu ni wale wale
Nakataa mkuu, sio watu wote wanakwenda Bar na Club. Kwa wengine hizo sehemu hawaingii kabisa. Mkuu kumbuka kwamba ukitaka kuchuma "zabibu" ni lazima uende ulipo mzabibu, huwezi kuchuma zabibu kwenye "mchongoma"!

Mwanamke utakayekutana naye "Night Club" saa tisa za usiku, kamwe hawezi kuwa mke bora kwako, wala wewe huwezi kuwa mume bora kwake. Huo ndiyo ukweli. Najua utabisha sana lakini ukweli utabakia kuwa ukweli.
 
Huwa nafakarigi tu IQ na miaka ya boss siipatii jibu... Ni kutokana na mada zake tu na si vingine..
 
Huwa nafakarigi tu IQ na miaka ya boss siipatii jibu... Ni kutokana na mada zake tu na si vingine..

nimeshindwa kuelewa ni compliment au dongo...
unahisi nina low iq au high? au labda umri wangu miaka mingapi?
be free..
 
Back
Top Bottom