Kwa familia zilizo nyingi hapo familia INA laki mbili! Ila unafuu ni kwamba familia haitakuwa stress ya pesa za saluni, ya michango ya kitchen party, viwalo vya kinamama na pia familia inaweza kukopa kwa "jirani wa chumbani" badala ya kuandikwa jina kwenye daftari LA Mangi!
Nimeona maisha yako hivyo kwa jamaa zangu wengi, na wamekubali matokeo kuwa ukitaka amani nyumbani inabidi ukubali chako ni chetu na chake ni chake!
Japo Mimi binafsi nyumbani kwangu hapo tuna 5,200,000/=.
Wanaume wengi wameshindwa kuthibitisha uaminifu wao kwa wake zao! Mke akikuhisi kuna mwingine anafaidi pembeni kwa pesa aliyokufadhili, huo ndio mwisho wa taarifa ya habari!