Wamisionari waliofika Tanganyika walikuta watu wamestaarabika na wanajua kusoma na kuandika

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,918
30,259

Wajerumani walipofika Tanganyika waliwakuta Waislam wanafahamu kuandika, kusoma na walikuwa wameelimika katika hesabu.

Mmishionari Ludwig Krapf alipofika kwa Chifu Kimweri wa Usambaa mwaka 1848 alimkuta yeye na wanae wote wanajua kusoma na kuandika.

Krapf alikuwa na barua mkononi kutoka Zanzibar kwa Sultan Barghash ikimuomba Chief Kimweri amsaidie Krapf kwani ni "mtu wa Mungu."

Herufi walizokuwa wakitumia zilikuwa za Kiarabu.

Wajerumani kwa ajili hii basi waliwaajiri Waislam kama walimu, wakalimani na makarani serikalini.

Wamisionari na wakoloni waliona wivu kwa maendeleo haya waliyoyakuta kwa Waislam.

Kubwa zaidi ni kuwa walikuwa wamekuja kustaarabisha watu "washenzi'' badala yake wamewakuta watu walistaarabika na wanye utamaduni wa kupendeza.

Elimu hii yote na utamaduni huu wa hali ya juu ulikuwa unatokana na Uislam na elimu iliyokuwa imetolewa na madras.

Hapo ndipo zilipoaanza mbinu ya kuvunja maendeleo haya yote.

Herufi za Kiarabu zikapigwa marufuku kutumika na badala yake watu wakalazimishwa kujifunza herufi za Kirumi.

Muislam ambae jana alipoingia kulala alikuwa anaitwa ameelimika akaamka asubuhi yake mjinga, hana elimu, hajui kusoma wala kuandika.

Njama hizi zote dhidi ya Uislam ilikuwa sehemu ya makubaliano kama ilivyoandikwa katika kifungu IV cha Mkutano wa Berlin wa mwaka 1884.

Kifungu hicho kilikuwa kinasema kuwa Ukristo ni lazima ulindwe dhidi ya Uislam.

Kati ya mwaka 1888 -1892 katika kutekeleza kifungu hicho kama ilivyokubalika katia Mkutano wa Berlin, Imperial British East Africa Company ilitumia nguvu za kisiasa na kijeshi kuulinda Ukristo na taasisi zake zote katika Afrika ya Mashariki.

Ombwe lililoachwa na madrsa ikajazwa na shule zilizojengwa na Serikali na Kanisa chini ya usimamizi wa wakoloni.

Historia iliyoandikwa inasema kuwa Kanisa ndilo lililoweka msingi wa kwanza wa elimu Tanganyika.

Ukweli ni kuwa Wamisionari walifuata nyayo za madras na walimu wa kwanza katika shule za misheni walikuwa Waislam ambao hawakusoma katika shule za kanisa bali katika madras.

(Kutoka kitabu cha Abdul Sykes 1998).

Baada ya karne mbili Rais wa Tanzania kutoka Zanzibar anampa zawadi ya mlango wa Kizanzibari Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki Duniani ndani ya Vatican na kumweleza maneno haya:

"This is the door... " - Sultan opened for Christianity..."

Huu ndiyo mlango uliofunguliwa kwa Ukristo kuingia Zanzibar na Afrika ya Mashariki.
 
Ningeshangaa sana kama hii habari ingepita bila mzee Said kuianzishia mada
Mas...
Napenda kusomesha.
Haya ni mambo muhimu sana ambayo yanataka watu waelezwe kwa kina.

Umemsikia Rais Samia Hassan akimkabidhi Pope zawadi ya mfano wa mlango wa Kizanzibari anamwambia Zanzibar ilifungua mlango kwa Ukristo kuingia Germany Ostafrika.

Johann Krapf alipofika katika Barza ya Chief Kimweri anahukumu kesi huku anaandika. na kavaa kama alivyomkuta Sultan Barghash wa Zanzibar alivyovaa na anapeperusha bendera ya Sultan.

1707774351631.png

Chief Kimweri​
 
Mtu ukishakua mdini, hata uandike maandiko ya maana watu watayapuuza tu
Mr Mutuu,
Sijaandika udini.

Nakuwekea ushahidi wa picha tatu tu kuthibitisha kuwa hilo usemalo si kweli.

Nimealikwa kuzungumza vyuo kadhaa ndani na nje ya Tanzania kikubwa kupita vyote ni Northwestern University, Chicago USA ambao wao wanaongoza dunia katika African History:

1707822193054.png

Mimi ni mmoja wa waandishis zaidi ya 500 kutoka kona zote za dunia walioandika hilo Kamusi hapo chini na niliombwa kuandika maisha ya Kleist Sykes (1894 - 1949).

1707822312659.png
Naalikwa kuzungumza katika vyombo vikubwa duniani na kikubwa kupita vyote ni VoA angalia picha hiyo hapo chini:
1707822523731.png

Kote huko nilikopita wasione udini wangu ila wewe?
Sijapata kupuuzwa.

Ingekuwa rahisi kupuuza kalamu yangu ungeanza wewe.
 
Back
Top Bottom