Stori ya kusisimua - Kizungumkuti!

Stori ya kusisimua - Kizungumkuti!

stori imeishia patamu[emoji23][emoji23][emoji23]

the Legend☆
Endelea kuburudika...

Kizungumkuti! - 23

Na Bishop Hiluka

Dont you trust me? I’ve told you the truth, I didnt do anything wrong,” (Huniamini? Nimeshakwambia ukweli, sijafanya chochote kibaya) Yusuf alijaribu kujitetea.

Mama Jasmine alimsogelea karibu zaidi na kusimama mbele yake huku akimkazia macho. “Baba Jasmine, hebu niangalie machoni halafu uniambie kuwa hujanisaliti.”

Yusuf alimtazama mkewe machoni na kushindwa kuongea, akayakwepesha macho yake na kutazama pembeni. “Kama huniamini basi, lakini ukweli utabaki pale pale kuwa siwezi kuisaliti ndoa yangu hata siku moja,” Yusuf alisema huku akiingia chumbani…

Endelea...

______

“Kwa kweli sijawahi kuumizwa kama alivyoniumiza Baba Jasmine leo. Hii tabia yake ya kujifanya kwenda kukutana na marafiki zake baa nilijua tu mambo kama haya lazima yatakuja kutokea,” Mama Jasmine aliwaza na kusonya kwa huzuni.

Alikuwa bado ameketi pale pale kitandani baada ya Yusuf kuondoka huku akiwaza na kuwazua lakini hakuweza kupata jibu muafaka, ingawa Yusuf alikana kufanya jambo baya lakini Mama Jasmine alikuwa na uhakika kuwa kulikuwa na jambo ambalo mumewe alikuwa akilificha.

Alitamani sana kulijua jambo lililomsibu mumewe lakini hakuwa na uwezo huo, na kutokana na maumivu makali ya moyo aliyoyapata alitamani kuondoka pale nyumbani na kurudi kwao lakini hakuwa na ushahidi wa kutosha kumhukumu Yusuf kuwa alikuwa na mwanamke mwingine…

Akiwa bado anawaza aligutushwa na sauti kali ya Jasmine aliyoisikia kwa mbali akigombana na mtoto mwingine wa chumba cha jirani kule nje ya nyumba. Mama Jasmine aliinuka pale kitandani na kujifunga khanga yake vizuri kisha akatoka nje haraka kumfuata Jasmine.

Alimkuta Jasmine akiwa amesimama aking’ang’ania andazi ambalo mtoto mwenzie alikuwa amenunuliwa na mama yake. Mama Jasmine akamchukua na kuingia naye ndani.

* * * * *

Saa mbili za asubuhi ilimkuta Yusuf akiwa ndani ya daladala lililotoka Buguruni kuelekea Mnazi Mmoja, daladala lile lilikuwa limejaza abiria kupita kiasi. Asubuhi ile abiria ndani ya daladala walikuwa wakijipepea kutokana na joto kali lililosababishwa na kujaa, hata hivyo kondakta wa daladala aliendelea kuita abiria wengine wapande kwenye kila kituo walichopita.

Yusuf alikuwa ameondoka nyumbani kwake akiwa bado ana hasira na wasiwasi kutokana na mzozo kati yake na mkewe asubuhi ile, na alikuwa akielekea ofisini kwake Mnazi Mmoja.

Yusuf alikuwa amepandia katika kituo cha Bungoni na hakuwa amepata siti hivyo kulazimika kusimama huku akiwa ameminywa na abiria wenzake, hasa wamama wawili waliokuwa na maumbo makubwa. Na muda wote aliokuwa ndani ya lile daladala alikuwa akiwaza namna ya kumfanya mkewe amwelewe na furaha irudi tena ndani ya nyumba.

Alijikuta akiwa hili na lile na kuna wakati alisonya na kuwafanya abiria wengine wageuze vichwa vyao kumtazama kwa mshangao. Aliposhtuka alishusha pumzi za ndani kwa ndani na kuwaangalia abiria wenzake, akawaona wao walikuwa na furaha sana tofauti na yeye.

Akajiuliza, huyu Belinda alikuwa wapi siku zote na kwa nini amekuja kwenye maisha yake sasa hivi? Je, aendelee na mpango wa kujipatia mamilioni ya pesa au ampigie simu na kumwambia kuwa hataki tena kuendelea na dili hilo la pesa ili kuokoa ndoa yake?

Alifikia hatua ya kuachana na dili aliloambiwa na Jacky ambaye yeye alimfahamu kwa jina la Belinda, lakini alipokumbuka ile adha ya kuminywa ndani ya daladala akajikuta akiwa njia panda. Alitakiwa achague kati ya dili la pesa au kulinda maadili ya kazi yake na kuiokoa ndoa yake.

Dah! Ahadi ya kupata mgao wa shilingi milioni mia mbili na hamsini baada ya lile dili kufanikiwa ikamfanya azidi kuchanganyikiwa, maana kwa pesa ile angeweza kujenga nyumba nzuri ya kisasa kule Kimara Temboni kwenye kiwanja alichozawadiwa na baba yake mkubwa siku ya harusi yake.

Pia angeweza kujenga nyumba nyingine kubwa nyumbani kwao Morogoro na angebakiwa na chenji ya kununulia gari, japo Toyota IST, na hivyo heshima ya ndoa yake ingerudi.

“Kila kitu kinamalizwa na pesa, hakuna mkate mgumu mbele ya chai nikishapata pesa amani kwenye ndoa yangu itarudi tu,” Yusuf aliwaza huku akiachia tabasamu laini, kisha aliinama kidogo kuangalia nje wakati daladala ikivuka eneo la soko la Boma.

Akaona vitu vikiwa vinapita mbele ya macho yake kwa kasi wakati daladala ikiwa inakwenda. Muda wote sura yake ilikuwa inaonesha huzuni na hakujua afanye nini ili kuirejesha furaha yake asubuhi ile.

Lile daladala lilipokuwa likivuka kwenye taa za kuongozea magari barabarani katika eneo la Ilala Boma, Yusuf aliwaona kinamama wakiwa wanafagia barabara kwenye vumbi bila hata kuwa na kitu cha kuwakinga. Hawakuwa na barakoa (masks), wala kitu chochote cha kuwakinga.

Baada ya kuvuka lile daladala lilisimama katika kituo cha daladala cha Karume, abiria wawili wakashuka na wengine wanne wakapanda baada ya kushawishiwa na kondakta wa lile daladala, na hapo daladala likaondoka tena.

Hapo sasa Yusuf alikuwa amepata siti baada ya abiria mmoja kushuka pale Karume na hivyo kumwachia siti aliyokuwa amekaa. Wakati wakiyapita majengo ya kiwanda cha bia (TBL) Yusuf aliwaona watoto wa mtaani wakigawana mkate karibu na kituo cha daladala cha Shule ya Sekondari ya Benjamin Mkapa.

Wakati huo watoto wengine walikuwa wanaomba fedha kwa abiria na madereva wa magari yaliyokuwa yanasimama. Yusuf aliwatazama kwa makini na kujikuta akimuwaza mwanawe Jasmine, alifikiria kuwa endapo hangefanya juhudi za kuinusuru ndoa yake, huenda Jasmine angeweza hata kuishia kuwa mtoto wa mtaani.

“Mungu aepushie mbali,” alijikuta akisema kimoyomoyo huku akivuta pumzi ndefu za ndani kwa ndani kisha akazishusha taratibu. Aliendelea kuwatazama wale watoto wa mtaani kwa makini wakati daladala likianza kuwaacha mbali wale watoto wa mtaani na mara wakajikuta wakivuka taa za kuongozea magari katika makutano ya barabara za Msimbazi na Uhuru eneo la Kariakoo.

Alishusha pumzi, akakunja sura yake na kuangalia huku na huko kwa huzuni wakati lile daladala likisimama katika kituo cha daladala cha Congo.

“Sikutegemea kabisa kama ingefikia hatua nikagombana na Mama Jasmine kiasi hiki! Hata hivyo, imenisaidia kumfahamu vizuri mke wangu, anaonekana ni mwanamke ambaye anataka kuwa na sauti ndani ya nyumba na maamuzi yake yawe ndiyo yawe ya mwisho…” Yusuf alijikuta akiwaza wakati lile daladala lilipokuwa likiondoka kutoka pale kituo cha Congo.

“Lakini mimi ndiye mwanamume ndani ya nyumba, siwezi kukubali jambo hili liendelee na siko tayari kuvumilia dharau zake. Ni kweli nimefanya kosa lakini angejaribu basi kunipa heshima yangu kama mume…” aliendelea kuwaza na mara akashtuliwa na abiria waliyekuwa wameketi siti moja baada ya lile daladala kusimama katika kituo cha Mnazi Mmoja.

Akashuka kutoka katika lile daladala na kuanza kutembea taratibu akielekea kazini kwake huku akiwa ameinamisha kichwa chake akiendelea kuwaza.

“Kichwa changu kimevurugwa kabisa, I real need someone to talk to, to comfort me,” aliwaza na mara ya Jacky ikamjia

Oh Belinda! I need to talk to her… Dah, sura ya Belinda toka niliponana naye jana asubuhi imeshindwa kabisa kunitoka kichwani. Ninamuwaza kila dakika. Yawezekana ni kutokana na uzuri wake na kasheshe zake za usiku kucha, kwa kweli sikutegemea kama ana uwezo mkubwa kiasi kile na kwa mara ya kwanza katika maisha yangu nimepata mwanamke ambaye amenikimbiza mchaka mchaka kiasi kile… isitoshe ni mtoto mzuri mno. Ameumbwa akaumbika…”

Mawazo ya Yusuf yalikatizwa na sauti kali za breki ya gari lililokuwa likiyumba kumkwepa. Yusuf aliogopa sana akajikunja na kuruka juu huku akitua kando ya ile barabara akiwa amefumba macho yake. Kutokana na kuzidiwa na mawazo alijikuta akivuka barabra ile ya Lumumba pasipo hata kuangalia kulia na kushoto kwake.

Itaendelea...
 
Asante kwa kunielewa, Jacky... Unajua ninafanya kuiba kidogo muda natupia huku episode moja kisha naendelea na kazi za ofisi, halafu sometimes internet inakuwa busy. Ila kama kawaida yangu siwezi kuwaacha na arosto...
Jamani Yusuph wangu ukipata kamda basi uwe unatupia story ni tamu mpaka imepitiliza utamu wenyewe
 
Bishop Hiluka si mtu rahisi kumpata.. Yupo na majukumu mengi sana.. Kuonekana hapa ni mara chache sana..

Ila kama kawaida, hakuna mkate mgumu mbele ya chai.. Kuna njia ya kumleta Bishop hapa tena kwa kasi ya kimbunga hata kama alikua usingizini..

the_legend kuna ndugu yetu Clkey anahitaji 'kizungumkuti' iendelee, tumpe njia.!??
Hahahaa, kwa kua Clkey ameonesha nia ya dhati muelekeze tu njia pekee ya kummudu Bishop Hiluka, njia ambayo imetumiwa na Jacky/Shunie kwa mafanikio makubwa sana

the Legend☆
 
Bishop tunaomba tena jaman
Clkey nikupe mbinu ya kumleta Bishop Hiluka..!?
Bishop Hiluka si mtu rahisi kumpata.. Yupo na majukumu mengi sana.. Kuonekana hapa ni mara chache sana..

Ila kama kawaida, hakuna mkate mgumu mbele ya chai.. Kuna njia ya kumleta Bishop hapa tena kwa kasi ya kimbunga hata kama alikua usingizini..

the_legend kuna ndugu yetu Clkey anahitaji 'kizungumkuti' iendelee, tumpe njia.!??

Hahahaa, kwa kua Clkey ameonesha nia ya dhati muelekeze tu njia pekee ya kummudu Bishop Hiluka, njia ambayo imetumiwa na Jacky/Shunie kwa mafanikio makubwa sana

the Legend☆
😀😀😀 Hahaaaa... yaani the_legend na Tater ni wambea nyie sijapata kuona, duh! Hakyanani nimewavulia kofia! Haya ngoja nishushe moja...


Kizungumkuti! - 24

Na Bishop Hiluka

“Kichwa changu kimevurugwa kabisa, I real need someone to talk to, to comfort me,” aliwaza na mara ya Jacky ikamjia

Oh Belinda! I need to talk to her… Dah, sura ya Belinda toka niliponana naye jana asubuhi imeshindwa kabisa kunitoka kichwani. Ninamuwaza kila dakika. Yawezekana ni kutokana na uzuri wake na kasheshe zake za usiku kucha, kwa kweli sikutegemea kama ana uwezo mkubwa kiasi kile na kwa mara ya kwanza katika maisha yangu nimepata mwanamke ambaye amenikimbiza mchaka mchaka kiasi kile… isitoshe ni mtoto mzuri mno. Ameumbwa akaumbika…”

Mawazo ya Yusuf yalikatizwa na sauti kali za breki ya gari lililokuwa likiyumba kumkwepa. Yusuf aliogopa sana akajikunja na kuruka juu huku akitua kando ya ile barabara akiwa amefumba macho yake. Kutokana na kuzidiwa na mawazo alijikuta akivuka barabara ile ya Lumumba pasipo hata kuangalia kulia na kushoto kwake.

Endelea...

Lile gari lilisimama katikati ya barabara na wakati huo huo dereva wa lile gari alishusha kioo cha gari na kumtazama Yusuf huku akionekana kukasirishwa sana. Lilikuwa ni gari la zuri aina ya Toyota Lexus RX la rangi nyeusi.

What’s wrong with you guy, how do you cross the road without looking right and left?” (We bwana una matatizo gani, unavukaje barabara bila kutazama kulia na kushoto kwako?) yule dereva alifoka kwa ukali huku akimkazia macho Yusuf.

Yusuf aligeuza kichwa chake kumtazama yule dereva huku akiwa na uso uliosawajika sana, mapigo ya moyo wake yalikuwa yakienda kwa kasi isivyo kawaida kutokana na mshtuko mkubwa alioupata baada ya kunusurika kugongwa.

Forgive me, brother, it’s just family problems…” (Niasamehe, kaka, ni matatizo tu ya kifamilia…)

Do not bring your family’s problems to the road…” (Matatizo ya familia yako usiyalete barabarani…) yule dereva alimkata kauli Yusuf kwa hasira lakini akaonekana kusita ghafla baada ya kuhisi kumfahamu Yusuf. Akamkazia macho akimwangalia kwa makini.

Yusuf naye alimtazama yule dereva kwa makini na kushusha pumzi za ndani kwa ndani, kikapita kitambo kifupi kila mmoja akimtazama mwenzake, na kila mmoja alihisi kumfahamu mwingine.

“Yusuf!” yule dereva aliita kwa shauku huku akizidi kumkazia macho Yusuf.

“Jacob!” Yusuf aliita huku akilisogelea lile gari, wakasalimiana kwa furaha.

What’s wrong with you, brother?” (Una shida gani, ndugu?) Jacob alimuuliza Yusuf baada ya kumtazama kwa makini na kugundua kuwa hakuwa sawa, japo alijilazimisha tabasamu lakini macho yake hawakuficha huzuni aliyokuwa nayo. Alikuwa akilengwa na machozi.

Hmm, just leave as it is. Dunia hii ina mambo, kaka,” Yusuf alisema kwa huzuni huku akishusha pumzi.

Muda ule ule madereva wa magari mengine yaliyokuwa nyuma ya gari la Jacob walianza kupiga honi kumtaka Jacob aondoe gari lake kwani alikuwa amesimamisha gari lake katikati ya barabara na hivyo kusababisha msongamano wa magari nyuma yake.

Jacob alishtuka na kuangalia nyuma yake kupitia kwenye kioo cha gari cha katikati, akayaona yale magari ya nyuma yake yakimuwashia taa kumuashiria aondoe gari lake barabarani. Jacob alishusha pumzi na haraka kutoa business card na kumpatia Yusuf.

If you get a chance, call me my brother, so we can talk,” (Ukipata nafasi nipigie ndugu yangu, ili tuongee) Jacob alisema na kuliondoa gari lake kwa mwendo wa kasi na kusababisha kelele za msuguano wa magurudumu yalipokuwa yakiserereka barabarani.

Yusuf alibaki amesimama akilisindikiza lile gari kwa macho hadi lilipopotea kwenye macho yake. kisha alishusha pumzi za ndani kwa ndani na kuitazama ile kadi aliyopewa na Jacob na kuanza kuondoka taratibu kuelekea zilipo ofisi zake.

Wakati akitembea mawazo yake yalihamia kwa Jacob, aliwaza kuhusu utofauti wa kipato uliokuwepo kati yake na Jacob, japo walisoma darasa moja na yeye Yusuf alikuwa anamzidi Jacob katika masomo ya darasani.

Jacob Haule na Yusuf walikuwa wamesoma pamoja Tambaza High School na baadaye wakaenda wote katika Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) jijini Dar es Salaam. Walipomaliza Jacob alipata nafasi ya kwenda nchini Uingereza alikosomea shahada ya umahili ya sanaa katika uongozi wa masoko (Master of Arts in Marketing Management).

Alipomaliza masomo yake alifanya kazi huko huko Uingereza kwa miaka miwili kisha akarudi nchini na kuajiriwa katika kampuni moja kubwa ya simu kama mkurugenzi wa masoko na alikuwa akilipwa mshahara mkubwa mno.

“Dah, sijui na mimi nifanye nini ili nifanikiwe kama Jacob, maana haya si maisha bali inaonekana kama sisi wengine tupo duniani kwa ajili ya kuwasindikiza wenzetu tu…” sasa kichwa cha Yusuf kilionekana kujaa mawazo mengi sana, mara akamkumbuka tena Jacky.

“Hmm! Hapa ndipo ninapoona umuhimu wa Belinda. Nikimtumia yule msichana naweza kutoka… yaani nashindwa kabisa kumtoa mawazoni mwangu na sikujua kama ni msichana mtundu kiasi kile. Sijui kajifunzia wapi yale mambo maana anaonekana ni mtoto wa geti kali,” Yusuf alizidi kuwaza na mara akajikuta akitabasamu.

She’s so sweet, I didn't even expect that one day I was going to betray my marriage, for the first time I have failed to be bold in my position before Belinda,” (Mtamu sana, sikutegemea kama siku moja ningeweza kuisaliti ndoa yangu, kwa mara ya kwanza nimeshindwa kuwa jasiri wa msimamo wangu mbele ya Belinda) Yusuf aliendelea kuwaza na muda ule ule akawa amefika ofisini kwake kwenye jengo la Benki ya Biashara tawi la Lumumba.

By the way, flies dies on the wound,” (Hata hivyo, nzi hufia kwenye kidonda…” Yusuf alitamka maneno yale na kujikuta akitabasamu huku akiwapita bila kuwasalimia wafanyakazi wenzake walioonekana kuongea na kutaniana wakiwa furaha asubuhi ile.

Wale wafanyakazi wakageuka kumtazama kwa mshangao, walimsalimia lakini alionekana yuko mbali sana kimawazo huku akionekana kuongea peke yake. Wale wafanyakazi wakapigwa na butwaa na kubaki wakitazamana bila kupata jibu.

* * * * *

Saa kumi na mbili jioni ya siku ile iliwakuta Carlos na Jacky wakiwa nyumbani kwa Jasmine katika mtaa wa Butiama eneo la Vingunguti. Jioni ya siku ile hali ya hewa ya jiji la Dar es Salaam ilikuwa imepoa zaidi kutokana na manyunyu hafifu ya mvua yaliyokuwa yakianguka kutoka angani kulikotanda wingu zito la mvua.

Lakini pamoja na hali ile ya manyunyu bado haikuwazuia watu kurandaranda mitaani huku kila mmoja akiwa kwenye pilika pilika zake.

Jasmine alikuwa akiishi katika nyumba ya kawaida aliyokuwa ameachiwa na baba yake, nyumba ile ilikuwa ya vyumba vinne, sebule, jiko, choo na bafu, na ilikuwa imezungushiwa ua mkubwa.

Alikuwa msichana wa umri wa miaka ishirini na tano, alikuwa mrefu kiasi na mwenye weusi wa kung’aa usiochusha, kichwani alikuwa na nywele nyingi mfano wa mmanga, zilizosukwa kwa mtindo wa yeboyebo na kumwagika mgongoni.

Jioni ile Jasmine alikuwa amevaa gauni fupi la kitenge lililoshonwa kwa mtindo wa pencil dress na lilionekana kumkaa vizuri sana mwilini huku likiuchora vyema mwili wake matata wenye umbo la kuvutia. Miguuni alikuwa amevaa sandals ngumu za ngozi zilizokuwa zimeshikilia kwenye miguu yake mizuri kwa kamba.

Jasmine alikuwa na uso wa mviringo na sura ya kitoto isiyoishiwa tabasamu muda wote huku macho yake makubwa na legevu ya kike yakiongezea mvuto wa sura yake. Pua yake ilikuwa ndefu na midomo yake ilikuwa laini yenye kingo pana kiasi zilizopakwa rangi nzuri ya mdomo.

Muda ule Jasmine alikuwa kaketi sebuleni kwake akiwasikiliza wageni wake Jacky na Carlos waliofika kumtembelea katika ugeni ule wa ghafla ambao hakuwa ameutarajia kabisa.

Je, Carlos na Jacky wanataka kumwambia nini Jasmine, na kwa nini wamfuate yeye? Endelea kufuatilia simulizi hii ya aina yake ya kusisimua...
 
Kizungumkuti! - 10

Na Bishop Hiluka

Carlos aliigundua hofu aliyokuwa nayo Jacky, hivyo aliamua kumsogelea na hapo hapo mikono yake yote miwili ikaanza kufanya ziara ya kwenye mwili wa Jacky, huku mkono wa kulia ukienda moja kwa moja kwenye kifua cha Jacky.

Please forgive me, my love, I did not intend to scare you, you know precisely how much I love you so much and I do not want to see another man navigating to this body,” (Tafadhali nisamehe, mpenzi wangu, sikukusudia kukutisha, unajua kiasi gani nakupenda sana na nisingependa kuona mwanaume mwingine akijivinjari kwenye mwili huu) Carlos alisema kwa namna ya kumbembeleza Jacky.

Endelea...

Kisha aliupeleka mkono wake kwenye chuchu laini za Jacky zilizosimama kwa utulivu juu ya milima miwili isiyofahamu adha yoyote ya volkano.

But since we need money, I have to let you go to another man, I hope you know precisely what I mean, my darling,” (Lakini kwa kuwa tunahitaji pesa, nalazimika kukuruhusu kwenda kuonana na mwanamume mwingine, natumaini unajua hasa namaanisha nini, mpenzi wangu) Carlos alizidi kusisitiza huku akiachia tabasamu pana.

Jacky hakusema neno bali alibaki kimya huku akimtazama Carlos kwa makini. Hata hivyo, Carlos hakusubiri jibu la Jacky, alipeleka mkono wake kwenye tumbo la Jacky na kuanza kukipapasa kitovu chake laini chenye kishimo kidogo kilichotengeneza ziada nyingine ya uzuri wake.

Kisha mkono wa pili ulikwenda moja kwa moja kiunoni na aliigusa nyonga yake laini iliyokuwa na mifupa miteke iliyopakana na mzigo imara wa makalio yaliyotuama vyema. Wakati akiendelea kumpapasa, Jacky akaamua kuvunja ukimya huku akimtazama Carlos usoni.

“Carlos!” Jacky aliita kwa sauti laini ya mahaba.

Yes, my love,” Carlos aliitikia kwa sauti yake nzito iliyokuwa na kila aina ya kiashiria cha kuhemkwa na tamaa za kimwili.

I’m tired with this life and I need to live a normal life, you don’t know what I’m going through right now…” (Nimechoshwa na maisha haya na ninahitaji kuishi maisha ya kawaida, hujui napitia magumu gani hivi sasa…) Jacky alisema kwa huzuni na kuongeza.

“Hivi kwa nini tusiachane na maisha haya na tuishi maisha huru ya mke na mume? Tuna shida gani, kama ni pesa tayari tunazo nyingi tu…” Jacky alianza kusema kwa utulivu huku akiipitisha mikono yake nyuma ya shingo ya Carlos na kuzifanya chuchu za matiti yake kukitekenya kifua cha Carlos.

Kitendo kile kikafanya joto kali la mwili wa Jacky limfanye Carlos ajisikie faraja ya aina yake. Carlos alimtazama Jacky machoni na kuyaona machozi yakianza kumlenga machoni.

I understand, my love, but nobody ever felt satisfied with money. We still have many things to do so we need money…” (Naelewa, mpenzi, lakini hakuna aliyewahi kutosheka na pesa. Bado tuna mambo mengi ya kufanya hivyo tunahitaji pesa…) alisema Carlos huku kwa kutumia kiganja chake taratibu alianza kumfuta Jacky machozi.

“…so we don’t have time to rest. We need to work day and night to make sure we have more money,” (…hivyo hatuna muda wa kupumzika. Tunahitaji kufanya kazi mchana na usiku kuhakikisha tunapata pesa zaidi) aliongeza Carlos huku akiendelea kuyafuta machozi kwenye macho ya Jacky.

Jacky aliusukuma mkono wa Carlos kutoka machoni mwake kisha akajisogeza nyuma kidogo huku akimtazama Carlos kwa makini.

You depend on me to complete this mission, so you’ll have to listen to me. This is the last mission and after this you’ll never ask me again, promise?” (Unanitegemea kukamilisha mpango huu, kwa hiyo unapaswa kunisikiliza. Huu mpango ni wa mwisho na baada ya hapo hutaniambia tena, unaniahidi hivyo?) Jacky alisema huku machozi yakianza kumtiririka kwenye mashavu yake, hakujua kwa nini alikuwa akisita sana kuifanya ile kazi.

Promise!” (Nakuahidi) Carlos alisema.

“Baada ya mpango huu kukamilika nataka tuachane na hizi kazi. Nataka tuanze aina mpya ya maisha, I’m dreaming to have a good family and be happy,” (Nina ndoto ya kuwa na familia nzuri na maisha ya furaha) Jacky alisema na hapo Jacky akamsogelea na kuvuta karibu zaidi, kisha ndimi zao zikakutana. Kilichofuata baada ya pale ilikuwa ni sauti ya pumzi zao sambamba na miguno isiyoeleweka ya mahaba.

Kama mtu aliyepandwa na wazimu wa mapenzi, Jacky akaanza kumvua Carlos singleti yake na kuitupilia mbali kisha akapeleka mikono yake kifuani kwa Carlos na kuanza kumpapasa kwa pupa. Carlos alitaka kumzuia lakini Jacky akamng’ata mkono.

Don’t stop me, please make my night beautiful,” (Usinizuie, tafadhali ufanye usiku wangu kuwa wa kupendeza) Jacky aliongea kwa hasira kama mwehu huku akiivuta chini bukta ya Carlos kwa pupa.

I thought we still need to talk and plan our things well,” (Nilidhani bado tunahitaji kuongea na kupanga mambo yetu vizuri) Carlos alinong’ona.

No, we’re done. Now I want to spend time with you, I need you so badly,” (Hapana, tumekwisha maliza, sasa nahitaji kujivinjari na wewe, nakuhitaji vibaya sana) Jacky alisema huku akihema kwa nguvu, muda ule ule alimvuta Carlos na ndimi zao zikaingia tena kazini zikitekenyana taratibu mdomoni.

Japokuwa Carlos alikuwa mtu hatari wa kuogopwa aliyekubuhu katika umafia lakini mbele ya mlimbwende yule, hasa wakati kama ule, alikuwa kama mbwa muoga mbele ya chatu mwenye njaa kali.

Jacky aliinuka na kuvua haraka gauni lake na kulitupa kando na hivyo kubakiwa na nguo yake nzuri ya ndani huku harufu nzuri ya manukato yake ikimshawishi Carlos kuendelea na hatua iliyofuata.

Carlos hakuwa na ujasiri tena wa kupingana zaidi na hisia zake, hivyo taratibu aliupeleka mkono wake ndani ya nguo ya ndani ya Jacky na kuanza kuyatomasa makalio yake laini yaliyoshiba minofu.

Jacky aliachia mguno hafifu wakati mkono mwingine wa Carlos ulipokuwa ukiyatomasa matiti yake taratibu. Kisha Carlos alianza kutembeza taratibu ulimi wake shingoni kwa Jacky na hatimaye sikioni na hapo ikasikika sauti hafifu ya Jacky ya mguno wa mahaba.

Jacky hakuweza kuvumilia tena hivyo haraka akaishusha chini nguo yake ya ndani na kuupeleka mkono wake akiichezea ikulu ya Carlos na kumfanya aanze kuhema ovyo.

Muda mfupi uliofuata walikuwa kwenye kochi kubwa la sofa pale pale sebuleni huku kila mmoja akiwa amepandwa na wazimu wa mapenzi. Mara wakajikuta wakiwa kwenye sayari nyingine ya mahaba mazito iliyokuwa kama kisiwa cha raha kwa ajili yao.

Sebule ile ikajazwa na vilio vya mahaba toka kwa Jacky vilivyoashiria raha ya aina yake aliyokuwa akiipata. Jacky alikuwa msichana mtundu sana aliyemudu vyema mitindo mbalimbali kiasi cha kumfanya Carlos ajihisi kama mvulana wa shule ya msingi.

Hiki kweli ni kizungumkuti, je, nini kitaendelea? Fuatana nami katika safari hii ya kusisimua...
X-rated kabisa hii Aisee Kuna watoto wa shule wanapitia humu lakini....🤔🤔
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom