Bishop Hiluka
R I P
- Aug 12, 2011
- 7,150
- 14,724
- Thread starter
- #61
Kizungumkuti! - 16
Na Bishop Hiluka
“Kwa nyinyi wenzetu mnaochezea fedha kila siku wala si ghali sana. Ni shilingi laki tatu na elfu hamsini tu kwa usiku mmoja, unapata bia mbili bure na chai ya asubuhi. Unaonaje?” Jacky alisema huku akiachia kicheko hafifu.
Yusuf alitaka kusema neno lakini akasita na kushusha pumzi za ndani kwa ndani huku akitingisha kichwa chake taratibu na kumtupia jicho yule mhudumu wa ile hoteli, ambaye muda wote alikuwa amesimama akiwatazama kwa zamu huku akitabasamu.
Jacky aligundua kuhusu hilo na kubetua mabega yake juu huku akiendelea kutabasamu.
Endelea...
“Anyway, what will you drink?” (Hata hivyo, sijui utakunywa nini?) Jacky alimuuliza Yusuf akiwa bado amemkazia macho.
“Castle baridi itapendeza,” Yusuf alijibu huku akiketi juu ya kochi mojawapo la sofa.
“Tuletee chupa mbili za castle baridi na chupa kubwa ya whisky,” Jacky alimwambia yule mhudumu aliyekuwa bado amesimama kimya akingoja kupewa oda.
“Vinywaji hivyo vyote vimo ndani ya hilo jokofu, labda kama mnahitaji huduma nyingine kama chakula,” alisema yule mhudumu huku akielekeza kidole chake kwenye lile jokofu dogo.
“Okay, basi tukihitaji chochote nitakupigia simu,” alisema Jacky huku akiachia tabasamu kisha akainuka na kwenda kufungua lile jokofu akatoa chupa mbili za Castle, bilauri mbili na chupa kubwa ya whisky.
Yule mhudumu aliachia tabasamu pana la kirafiki na kuondoka, Yusuf alimtazama Jacky kwa makini na kushusha pumzi zaa ndani kwa ndani. “Niliona nibahatishe kukupigia simu ingalau nisikie sauti yako,” alivunja ukimya.
“Yaani ulitaka usikie sauti tu, basi!” Jacky aliuliza huku akiangua kicheko hafifu kisha akaviweka vile vinywaji juu ya ile meza ndogo fupi ya mbao. Yusuf alitabasamu tu bila kujibu kisha akainamisha kichwa chake akionekana kufikiria mbali, huku akionekana kumtupia jicho la wizi Jacky kwa matamanio.
“Haya sauti yangu tayari umeshaisikia na mimi mwenyewe ndiyo niko hapa hapa mbele yako, tena tukiwa peke yetu, unasemaje?” Jacky alisema na kuangua tena kicheko hafifu.
“Kwani ninalo tena!” lilikuwa jibu fupi la Yusuf lililomaanisha kuwa alikuwa amesalimu amri huku akiinamisha sura yake kutazama chini kwa aibu.
Hata hivyo, Yusuf alikuwa akihisi joto kali la mwili lililosababisha kijasho jembamba kianze kumtoka licha ya kuwa mle ndani kulikuwa na kiyoyozi kilichokuwa kikitoa ubaridi mkali. Alianza kuhisi mapigo ya moyo wake yakibadili mwendo wake na kwenda mbio isivyo kawaida!
Aliilamba midomo yake iliyoanza kukauka huku akianza kuhisi pumzi zake zikimpaa na kuanza kuhema kwa nguvu kama mtu aliyekosa hewa safi ya oksijeni, alifungua vifungo vya shati lake na kubaki kifua wazi. Muda wote huo Jacky alikuwa akimtazama kwa makini kisha akaachia tabasamu.
“Kama unahisi jasho livue kabisa halafu njoo uketi hapa kitandani,” Jacky alimwambia Yusuf huku akimuonesha kwa mkono sehemu ya kukaa karibu yake.
Yusuf hakupinga alilivua lile shati na kulitupia juu ya kochi jingine la sofa kisha akainuka na kwenda kuketi pale kitandani sehemu aliyooneshwa na Jacky.
Jacky alifungua zile chupa za bia, akamimina pombe kwenye bilauri zote mbili, kisha bilauri moja alimpa Yusuf na nyingine aliishika mkononi. Akanyoosha mkono wake kumwelekea Yusuf, wakagongesha zile bilauri.
“Cheers!” walisema kwa pamoja wakitakiana heri na kuangua kicheko hafifu.
Yusuf aliinua ile bilauri akapiga funda moja kubwa la bia na kusisimkwa mwili wake. Alipoishusha ile bilauri alimtazama Jacky kwa tabasamu.
“Hivi una muda gani wa kazi pale benki?” Jacky alimuuliza Yusuf huku akipiga funda la bia na kuiweka ile bilauri juu ya meza.
“Nina miaka minne,” Yusuf alisema huku akiinua tena bilauri ya bia. Jacky alimtazama kwa makini kwa kitambo kifupi kisha akaitazama pete ya harusi iliyokuwa kidoleni kwake na kuachia tabasamu.
“Are you married? I can see you have a wedding ring,” (Umeoa? Naona una pete ya harusi) Jacky alisema huku akiangua kicheko hafifu.
“To be honest… I have a wife and a kid. Kwani vipi?” (Kusema kweli… nina mke na mtoto) aliuliza Yusuf huku akimkazia macho Jacky.
“Aah, napenda tu kujua nipo na mwanamume wa aina gani, mbona wewe kwenye simu uliniuliza kama nimeolewa!” Jacky alijibu kwa madaha huku akijipinda kumtazama Yusuf kwa mahaba. Walibaki wametazamana kwa kitambo fulani na kujikuta wote wakiachia tabasamu lililozaa kicheko.
“Hivi umepanga au unaishi katika nyumba yako?” Jacky aliuliza tena baada ya kile kicheko kukoma huku akimkazia macho Yusuf.
“Sijafanikiwa kujenga, pesa ngumu sana siku hizi, si unajua tena awamu hii ya hapa kazi tu jinsi inavyokaba kila kona…” Yusuf alisema na kuangua kicheko hafifu.
“Najua, ila kila kitu kinataka mipangilio. Je, una gari?” Jacky aliuliza tena lakini kabla Yusuf hajajibu, simu yake ya mkononi ilianza kuita.
Yusuf alishtuka na kuitazama kwa makini, akaonesha kusita kidogo huku akimtupia jicho Jacky. Hata hivyo Jacky alimuashiria kuwa aipokee tu, Yusuf aliichukua na kubofya kitufe cha kupokelea na akuiweka kwenye sikio.
“Eh mama Jasmine!” Yusuf alisema mara tu alipoiweka ile simu kwenye sikio.
“Uko wapi, baba Jasmine? Huku Jasmine ananisumbua sana!” sauti ya mke wake ilisikika ikilalamika kutoka upande wa pili wa simu.
“Kwani homa imemrudia tena?” Yusuf aliuliza kwa wasiwasi huku akimtupia jicho Jacky.
“Wala hana homa, ila hataki kulala mpaka akuone,” sauti ya mke wake ilisikika tena ikilalamika.
“Okay, nipo sehemu nina kikao kidogo na rafiki zangu, nitarudi mara tu nikishamaliza kikao, kama nusu saa hivi inayokuja,” Yusuf alisema na kukata simu kisha alimtupia jicho Jacky huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.
“Is that your wife?” (Ni mkeo huyo?) Jacky alimuuliza Yusuf huku akionekana kutabasamu.
Yusuf alikubali kwa kubetua kichwa kisha akanyanyua bilauri yake ya bia na kuinywa bia yote iliyokuwemo kwenye ile bilauri huku akishusha pumzi ndefu. Jacky alimtazama kwa madaha na kummiminia bia nyingine.
“But you have not yet answered my question…” (Lakini bado hujajibu swali langu…) Jacky alimwambia Yusuf huku akimkazia macho.
“What question?” (Swali gani?) Yusuf aliuliza huku akimtazama Jacky kwa mshangao.
“I asked if you had a car.” (Niliuliza kama una gari).
“I do not have a car,” (Sina gari) Yusuf alisema huku akiweka msisitizo kwa kutingisha kichwa chake kukataa.
“Hata kagari kadogo dogo tu?” Jacky aliuliza tena huku akiachia tabasamu.
Itaendelea...
Na Bishop Hiluka
“Kwa nyinyi wenzetu mnaochezea fedha kila siku wala si ghali sana. Ni shilingi laki tatu na elfu hamsini tu kwa usiku mmoja, unapata bia mbili bure na chai ya asubuhi. Unaonaje?” Jacky alisema huku akiachia kicheko hafifu.
Yusuf alitaka kusema neno lakini akasita na kushusha pumzi za ndani kwa ndani huku akitingisha kichwa chake taratibu na kumtupia jicho yule mhudumu wa ile hoteli, ambaye muda wote alikuwa amesimama akiwatazama kwa zamu huku akitabasamu.
Jacky aligundua kuhusu hilo na kubetua mabega yake juu huku akiendelea kutabasamu.
Endelea...
“Anyway, what will you drink?” (Hata hivyo, sijui utakunywa nini?) Jacky alimuuliza Yusuf akiwa bado amemkazia macho.
“Castle baridi itapendeza,” Yusuf alijibu huku akiketi juu ya kochi mojawapo la sofa.
“Tuletee chupa mbili za castle baridi na chupa kubwa ya whisky,” Jacky alimwambia yule mhudumu aliyekuwa bado amesimama kimya akingoja kupewa oda.
“Vinywaji hivyo vyote vimo ndani ya hilo jokofu, labda kama mnahitaji huduma nyingine kama chakula,” alisema yule mhudumu huku akielekeza kidole chake kwenye lile jokofu dogo.
“Okay, basi tukihitaji chochote nitakupigia simu,” alisema Jacky huku akiachia tabasamu kisha akainuka na kwenda kufungua lile jokofu akatoa chupa mbili za Castle, bilauri mbili na chupa kubwa ya whisky.
Yule mhudumu aliachia tabasamu pana la kirafiki na kuondoka, Yusuf alimtazama Jacky kwa makini na kushusha pumzi zaa ndani kwa ndani. “Niliona nibahatishe kukupigia simu ingalau nisikie sauti yako,” alivunja ukimya.
“Yaani ulitaka usikie sauti tu, basi!” Jacky aliuliza huku akiangua kicheko hafifu kisha akaviweka vile vinywaji juu ya ile meza ndogo fupi ya mbao. Yusuf alitabasamu tu bila kujibu kisha akainamisha kichwa chake akionekana kufikiria mbali, huku akionekana kumtupia jicho la wizi Jacky kwa matamanio.
“Haya sauti yangu tayari umeshaisikia na mimi mwenyewe ndiyo niko hapa hapa mbele yako, tena tukiwa peke yetu, unasemaje?” Jacky alisema na kuangua tena kicheko hafifu.
“Kwani ninalo tena!” lilikuwa jibu fupi la Yusuf lililomaanisha kuwa alikuwa amesalimu amri huku akiinamisha sura yake kutazama chini kwa aibu.
Hata hivyo, Yusuf alikuwa akihisi joto kali la mwili lililosababisha kijasho jembamba kianze kumtoka licha ya kuwa mle ndani kulikuwa na kiyoyozi kilichokuwa kikitoa ubaridi mkali. Alianza kuhisi mapigo ya moyo wake yakibadili mwendo wake na kwenda mbio isivyo kawaida!
Aliilamba midomo yake iliyoanza kukauka huku akianza kuhisi pumzi zake zikimpaa na kuanza kuhema kwa nguvu kama mtu aliyekosa hewa safi ya oksijeni, alifungua vifungo vya shati lake na kubaki kifua wazi. Muda wote huo Jacky alikuwa akimtazama kwa makini kisha akaachia tabasamu.
“Kama unahisi jasho livue kabisa halafu njoo uketi hapa kitandani,” Jacky alimwambia Yusuf huku akimuonesha kwa mkono sehemu ya kukaa karibu yake.
Yusuf hakupinga alilivua lile shati na kulitupia juu ya kochi jingine la sofa kisha akainuka na kwenda kuketi pale kitandani sehemu aliyooneshwa na Jacky.
Jacky alifungua zile chupa za bia, akamimina pombe kwenye bilauri zote mbili, kisha bilauri moja alimpa Yusuf na nyingine aliishika mkononi. Akanyoosha mkono wake kumwelekea Yusuf, wakagongesha zile bilauri.
“Cheers!” walisema kwa pamoja wakitakiana heri na kuangua kicheko hafifu.
Yusuf aliinua ile bilauri akapiga funda moja kubwa la bia na kusisimkwa mwili wake. Alipoishusha ile bilauri alimtazama Jacky kwa tabasamu.
“Hivi una muda gani wa kazi pale benki?” Jacky alimuuliza Yusuf huku akipiga funda la bia na kuiweka ile bilauri juu ya meza.
“Nina miaka minne,” Yusuf alisema huku akiinua tena bilauri ya bia. Jacky alimtazama kwa makini kwa kitambo kifupi kisha akaitazama pete ya harusi iliyokuwa kidoleni kwake na kuachia tabasamu.
“Are you married? I can see you have a wedding ring,” (Umeoa? Naona una pete ya harusi) Jacky alisema huku akiangua kicheko hafifu.
“To be honest… I have a wife and a kid. Kwani vipi?” (Kusema kweli… nina mke na mtoto) aliuliza Yusuf huku akimkazia macho Jacky.
“Aah, napenda tu kujua nipo na mwanamume wa aina gani, mbona wewe kwenye simu uliniuliza kama nimeolewa!” Jacky alijibu kwa madaha huku akijipinda kumtazama Yusuf kwa mahaba. Walibaki wametazamana kwa kitambo fulani na kujikuta wote wakiachia tabasamu lililozaa kicheko.
“Hivi umepanga au unaishi katika nyumba yako?” Jacky aliuliza tena baada ya kile kicheko kukoma huku akimkazia macho Yusuf.
“Sijafanikiwa kujenga, pesa ngumu sana siku hizi, si unajua tena awamu hii ya hapa kazi tu jinsi inavyokaba kila kona…” Yusuf alisema na kuangua kicheko hafifu.
“Najua, ila kila kitu kinataka mipangilio. Je, una gari?” Jacky aliuliza tena lakini kabla Yusuf hajajibu, simu yake ya mkononi ilianza kuita.
Yusuf alishtuka na kuitazama kwa makini, akaonesha kusita kidogo huku akimtupia jicho Jacky. Hata hivyo Jacky alimuashiria kuwa aipokee tu, Yusuf aliichukua na kubofya kitufe cha kupokelea na akuiweka kwenye sikio.
“Eh mama Jasmine!” Yusuf alisema mara tu alipoiweka ile simu kwenye sikio.
“Uko wapi, baba Jasmine? Huku Jasmine ananisumbua sana!” sauti ya mke wake ilisikika ikilalamika kutoka upande wa pili wa simu.
“Kwani homa imemrudia tena?” Yusuf aliuliza kwa wasiwasi huku akimtupia jicho Jacky.
“Wala hana homa, ila hataki kulala mpaka akuone,” sauti ya mke wake ilisikika tena ikilalamika.
“Okay, nipo sehemu nina kikao kidogo na rafiki zangu, nitarudi mara tu nikishamaliza kikao, kama nusu saa hivi inayokuja,” Yusuf alisema na kukata simu kisha alimtupia jicho Jacky huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.
“Is that your wife?” (Ni mkeo huyo?) Jacky alimuuliza Yusuf huku akionekana kutabasamu.
Yusuf alikubali kwa kubetua kichwa kisha akanyanyua bilauri yake ya bia na kuinywa bia yote iliyokuwemo kwenye ile bilauri huku akishusha pumzi ndefu. Jacky alimtazama kwa madaha na kummiminia bia nyingine.
“But you have not yet answered my question…” (Lakini bado hujajibu swali langu…) Jacky alimwambia Yusuf huku akimkazia macho.
“What question?” (Swali gani?) Yusuf aliuliza huku akimtazama Jacky kwa mshangao.
“I asked if you had a car.” (Niliuliza kama una gari).
“I do not have a car,” (Sina gari) Yusuf alisema huku akiweka msisitizo kwa kutingisha kichwa chake kukataa.
“Hata kagari kadogo dogo tu?” Jacky aliuliza tena huku akiachia tabasamu.
Itaendelea...