Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,175
Bishop Hiluka leo utakua umetingwa sana jamani pole Askofu Jacky wako nipo nakusubiri mm
Bibie ujue nakuelewa sana comments zako zipo vizuri na zina tija keep it upBishop Hiluka leo utakua umetingwa sana jamani pole Askofu Jacky wako nipo nakusubiri mm
HahahhahaBibie ujue nakuelewa sana comments zako zipo vizuri na zina tija keep it up
Hahahahaa, bora umesema wewe mkuu. Mi na Tater tukisemaga tunaonekana wapambeBibie ujue nakuelewa sana comments zako zipo vizuri na zina tija keep it up
Hahahahaa, najua unajua cha kufanya. #tunakutegemeaHahahhaha
Askofu wangu sio kawaida yake hii ujue
Bishop Hiluka leo utakua umetingwa sana jamani pole Askofu Jacky wako nipo nakusubiri mm
Shunie mwenzio nimekuja mbio baada ya kusikia unaniita. Usikonde Jacky, wangu japo umenisababishia balaa nyumbani, lakini nzi kufia kwenye kidonda ni halali. Ngoja nizimwage halafu niendelee na job...
Heshima yako mkuu. Ngoja sasa nianze kupitia kizungumkuti mdogo mdogo😀😀😀...
Poa...Heshima yako mkuu. Ngoja sasa nianze kupitia kizungumkuti mdogo mdogo
the Legend☆
Shukrani sana mkuu Bishop. Mambo ni motoMzigo ndiyo huo nimeubwaga hivyo mshindwe wenyewe tu. Kila hatua tunayopiga kwenda mbele ndivyo tunavyokutana na kizungumkuti... Tukutane tena kesho panapo majaaliwa...
Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY HALELUYA MOSHI Clkey
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Hahahahaha Asante Bishop wangu Yusuph na pole mno na kaziShunie mwenzio nimekuja mbio baada ya kusikia unaniita. Usikonde Jacky, wangu japo umenisababishia balaa nyumbani, lakini nzi kufia kwenye kidonda ni halali. Ngoja nizimwage halafu niendelee na job...
Kizungumkuti! - 25
Na Bishop Hiluka
Jioni ile Jasmine alikuwa amevaa gauni fupi la kitenge lililoshonwa kwa mtindo wa pencil dress na lilionekana kumkaa vizuri sana mwilini huku likiuchora vyema mwili wake matata wenye umbo la kuvutia. Miguuni alikuwa amevaa sandals ngumu za ngozi zilizokuwa zimeshikilia kwenye miguu yake mizuri kwa kamba.
Jasmine alikuwa na uso wa mviringo na sura ya kitoto isiyoishiwa tabasamu muda wote huku macho yake makubwa na legevu ya kike yakiongezea mvuto wa sura yake. Pua yake ilikuwa ndefu na midomo yake ilikuwa laini yenye kingo pana kiasi zilizopakwa rangi nzuri ya mdomo.
Muda ule Jasmine alikuwa kaketi sebuleni kwake akiwasikiliza wageni wake Jacky na Carlos waliofika kumtembelea katika ugeni ule wa ghafla ambao hakuwa ameutarajia kabisa.
Endelea...
Sebule yake ilikuwa ndogo yenye samani za kawaida zikiwemo seti moja ya makochi yaliyoanza kuchoka foronya na meza ndogo ya chakula iliyozungukwa na viti vinne iliyokuwa upande wa kushoto kwenye sebule ile.
Katikati ya sebule ile kulikuwa na meza nyingine fupi na nzuri ya mbao ya mti wa msonobari iliyokuwa imefunikwa kwa kitambaa cha rangi ya samawati kizuri chenye maua mekundu na kijani ya kufuma kwa mkono.
Upande wa kulia wa ile sebule kulikuwa na kabati dogo lililokuwa na vitabu, DVD mbalimbali za filamu, kisimbuzi cha StarTimes na seti ya televisheni aina ya Hitachi ya inchi 21. Pia kulikuwa na deki ya DVD iliyokuwa na vumbi ikiashiria kuwa haikuwa imetumika kwa muda mrefu.
Sakafu ya mle ndani ilikuwa imefunikwa kwa zulia kuukuu la plastiki lililokuwa na rangi ya bluu na maua yenye rangi nyekundu na njano na kuta za sebule ya nyumba ile zilikuwa nyeupe zikiwa zimetundikwa picha mbili kubwa, moja ilikuwa picha ya Jasmine na picha nyingine ilikuwa ya wazazi wake.
Pia kulikuwa na picha kubwa ya kuchorwa ya wanyama wa mwituni maarufu kama Tingatinga na kalenda ya mwaka huo iliyokuwa imetundikwa ukutani upande mwingine wa ukuta.
Jasmine alikuwa akiishi na dada yake, Zaituni Mungi, mtoto wa mama yake mkubwa, ambaye kwa wakati ule hakuwepo pale nyumbani. Aliishi na zaituni baada ya kufiwa na baba yake mwaka mmoja tu uliokuwa umepita, wakati mama yake alikufa wakati Jasmine alipokuwa na miaka kumi, akiwa darasa la nne.
Katika nyumba ile yenye vyumba vinne Jasmine aliishi kwenye chumba kimoja na dada yake pia alikuwa na chumba kimoja na vyumba vingine viwili vilivyobakia alikuwa amevipangisha na hivyo kila mwezi aliingiza shilingi laki moja kama kodi ya vyumba viwili, na alipoongezea na shilingi laki mbili alizokuwa akilipwa kama mshahara kazini kwake, zilitosha kabisa kumfanya asiukimbie mji.
Jasmine aliwatazama Jacky na Carlos kwa zamu na kushusha pumzi ndefu za ndani kwa ndani akionekana kutafakari sana. Ilionekana kuwa alikuwa njia panda na alishindwa aamue nini kutokana na maneno aliyoelezwa na wale wageni wake.
Carlos na Jacky walikuwa wametumia zaidi ya dakika ishirini wakijaribu kumshawishi akubaliane na kile walichomweleza katika mpango wao wa kupata mabilioni ya pesa lakini yeye alionekana kutokubaliana kabisa na wazo lile.
Baada ya kuonekana kuwa ameshindwa kushawishika ilimbidi Carlos atafute njia nyingine ya kumfanya akubali, alimtazama kwa makini kisha alimtupia jicho Jacky na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.
“Jasmine, hivi unajua kuwa marehemu baba yako alikuwa rafiki yangu mkubwa na si tu tulisaidiana kwa mambo mengi bali alikuacha mikononi mwangu, kweli si kweli?” aliuliza Carlos akiwa amemkazia macho Jasmine.
“Ni kweli, baba, lakini…” alijibu Jasmine kwa sauti yenye mashaka huku akiangalia chini.
“Aah nisikilize kwanza, Jasmine… najua kuwa baba yako hakukuachia rasilimali yoyote zaidi ya hii nyumba ambayo ni ya kawaida sana. Je, unadhani kwa nyumba hii tu bila mipango mingine utaishi vipi katika karne hii? Kumbuka wewe ni mtoto wa kike na kwa umri wako unahitaji kujirusha, unahitaji kuishi maisha mazuri na pia unahitaji kuvaa vizuri… unadhani vitu vyote hivyo utavipataje?” Carlos alisema huku akizidi kumkazia macho Jasmine.
Jasmin alitaka kusema neno lakini alisita na kubaki kimya akimtumbulia macho Carlos. Carlos alitoa kibunda cha fedha kiasi cha shilingi milioni moja na kumshikisha Jasmine mkononi huku akimlainisha na tabasamu kabambe.
“Sikiliza, fedha hizi si hongo bali ni kwa ajili ya kukusaidia chakula na matatizo madogo madogo tu ya hapa nyumbani kwa hizi siku mbili tatu utakazokuwa unatafakari proposal yangu,” Carlos alisema huku akizidi kuachia tabasamu la kumlainisha.
“Lakini naogopa…” Jasmine alisema kwa wasiwasi huku akitamani kuzikataa zile fedha.
“Jasmin, hivi nikueleze mara ngapi? Hundi moja tu ya katikati itakupa shilingi milioni mia moja ya kuchunga maisha yako ya baadaye!” Carlos alimwambia Jasmine huku sura yake ikiendelea kupambwa na tabasamu.
Jasmin alimtazama Carlos kwa wasiwasi, akaziangalia zile fedha kisha akainua tena sura yake kumtazama Carlos, akataka kusema lakini maneno yakawa hayatoki na hivyo kuishia kufumbua mdomo tu, kisha alivuta pumzi ndefu na kuzishusha taratibu huku akigeuza tena shingo yake kumtazama Jacky.
Jacky aliachia tabasamu maridhawa ili kumlainisha Jasmine huku akimuonesha ishara ya kumsisitiza akubaliane na proposal ya Carlos. Jasmine alijikuta akichanganyikiwa, aliinamisha kichwa chake na kuanza kutafakari.
Kikatokea kitambo kifupi cha ukimya wakati Jasmine akiwa amezama kwenye tafakari, muda wote Carlos na Jacky walikuwa wakimwangalia kwa makini huku wakisubiria kusikia jibu lake. Mara Jasmine akainua uso wake kumtazama Carlos huku akilazimisha tabasamu.
“Sawa, nitajaribu,” alisema huku akishusha pumzi ndefu kana kwamba alikuwa ametoka kwenye mashindano ya mbio ndefu.
“Usiseme utajaribu, tunachotaka ufanye kweli,” Carlos alimsisitiza kwa sauti tulivu lakini yenye kuamuru.
“Sawa, nitafanya,” Jasmine alisema na kuwafanya Jacky na Carlos watazamane na kutabasamu, kisha wakapeana ishara ya kuondoka. Walisimama wakamuaga Jasmine na kuondoka wakimwacha bado yupo katika hali ya sintofahamu.
Walipotoka nje ya ile nyumba ya Jasmine, Carlos na Jacky waliingia kwenye gari lao la kifahari aina ya Range Rover Sport L494 la rangi nyeupe.
Jacky ndiye aliyekuwa akiendesha lile gari, aliliondoa kwa utulivu na mara tu baada ya kuyaacha maskani ya Jasmine walishika uelekeo wa barabara ya lami iliyokuwa ikielekea kwenye machinjio ya ng’ombe ya Vingunguti.
Katika barabara ile kulikuwa na magari mengi katika muda ule wa jioni yaliyotokea katikati ya mji, hivyo Jacky alilazimika kuendesha gari lake kwa mwendo wa kawaida, japo alikuwa na haraka.
Wakati wakiwa katika barabara ile macho ya Carlos yalikuwa makini sana kutazama kila mahali katika namna ya kuchunguza kama kulikuwa na gari lolote au pikipiki iliyoonesha ishara ya kuwafuatilia nyendo zao. Walivuka daraja la Mto Msimbazi na baada ya mwendo wa dakika chache walifika katika eneo la Barakuda.
Kisha walishika barabara ya kuelekea Segerea na baada ya mwendo mrefu hatimaye safari yao iliwafikisha katika makazi yao ya kisasa katika eneo la watu wenye ukwasi. Lile gari likafunga breki mbele ya geti kubwa jeusi la jumba moja kubwa la ghorofa mbili lililozungukwa na miti mirefu ya kivuli na ukuta mrefu wenye usalama wa uhakika.
Muda ule mvua ya wastani ilikuwa inanyesha, hata hivyo haikuwazuia kuingia ndani ya jumba lao la kifahari.
Jacky alibonyeza remote na mara lile geti jeusi likaanza kufunguka taratibu, kisha gari akaliingiza lile ndani ya uzio mrefu wa lile jumba uliokuwa umefungwa mfumo maalumu ya umeme wa kuzuia wezi juu yake.
Itaendelea...
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]