Stori ya kusisimua - Kizungumkuti!

Stori ya kusisimua - Kizungumkuti!

Kizungumkuti! - 20

Na Bishop Hiluka

Jacky alifurahi sana na kummwagia Yusuf mabusu mfululizo, kisha kikafuata kitambo kirefu cha kupanga mipango kabambe ya namna ya kufanikisha mambo ya fedha, huku Jacky akitawala mazungumzo. Katikati ya maongezi yao Jacky alishtuka na kuangalia saa yake ya mkononi akapigwa na butwaa.

“Dah, saa tisa usiku!” Jacky alisema na kumshtua sana Yusuf.

“Oh my God, saa tisa! Sijui nitamwambia nini mke wangu! Sijawahi kulala nje hata siku moja na jana nimetoka nyumbani saa kumi na mbili jioni na sijarudi hadi saa hizi! Eeh Mungu nisamehe mja wako,” Yusuf aliwaza huku moyo wake ukijaa hofu…

Endelea...

* * * * *

Oh God, help me. What kind of life is this? Why do I live like this?” (Mungu wangu nisaidie. Haya ni maisha gani? Kwa nini ninaishi maisha kama haya?) Jacky alikuwa anawaza huku akilisikilizia tumbo lake lililokuwa dhaifu sana kwa vile usiku uliokuwa umetangulia alikuwa ametia kilevi tumboni na hakuwa amekula chakula.

Ukichanganya na mahaba mazito aliyoyapata kutoka kwa Yusuf usiku kucha yaliyochangiwa na kiu yake ya kutaka kupata taarifa sahihi za mabilioni ya pesa vilikuwa vimemchanganya sana Jacky na kumfanya asahau hata kula.

Kichwa chake kilikuwa kizito sana kutokana na mning’inio (hang over) uliotokana na uchovu wa pombe kali alizokuwa amekunywa usiku wa siku iliyotangulia. Wakati akiyawaza hayo ilikuwa tayari imeshatimia saa moja ya asubuhi, alikuwa amerudi nyumbani takriban nusu saa tu iliyokuwa imepita.

Alipofika nyumbani asubuhi ile jambo la kwanza alilofanya ilikuwa ni kukimbilia moja kwa moja bafuni kujimwangia maji ya uvuguvugu ili apate nguvu mpya, kwani mwili wote ulikuwa unamuuma kama kidonda kutokana na gwaride la usiku kucha alilokuwa amechezeshwa na Yusuf.

Kiukweli, mwanzoni alikuwa amemchukulia poa Yusuf kwa kudhani asingeweza kumudu dakika tisini za mchezo, kumbe alikosea sana kwani Yusuf aliweza kwenda hadi dakika mia moja na ishirini, na bado walipoingia kwenye matuta hakupatikana mshindi.

Jacky alikuwa amekutana na muziki wa Yusuf usio wa kitoto, kwani Yusuf alijua kucheza ngoma zote, msondo, ndekule, mdundiko, sindimba na nyinginezo pasipo kuomba poo na alikuwa hachoki utadhani alikuwa na mapafu kama ya farasi.

Asubuhi ile Jacky alipomaliza kujimwagia maji alijifunga khanga moja kifuani na taulo kiunoni na kuelekea jikoni ambako alianza kuandaa kifungua kinywa. Wakati alipokuwa mbioni kumaliza zoezi lile la kuandaa kifungua kinywa alishtushwa na mikono ya mtu iliyomshika kiunoni.

Aligeuka haraka nyuma huku moyo wake ukianza kupoteza utulivu, akamuona Carlos akiwa amesimama nyuma yake akitabasamu na hapo tabasamu jepesi likachomoza usoni kwake.

Kumbe muda ule alipokuwa akiandaa kifungua kinywa Carlos alikuwa amenyata taratibu kutoka chumbani alikokuwa amelala na kwenda kusimama nyuma yake bila yeye kujua.

Macho ya Carlos yalikuwa na kila dalili za uchovu na alisimama pale akimtazama Jacky kwa namna ambayo ilimshtua kidogo Jacky. Carlos alimtazama Jacky kwa kitambo kirefu bila kusema neno.

Alikuwa akiitazama hazina matata iliyokuwa imejificha katika umbo matata la Jacky na kujikuta akihisi donge la wivu likimkaba kooni kwake kwa kukubali kumruhusu Jacky kwenda kulala na mwanamume mwingine, eti sababu ya kutafuta pesa.

Kila alipozidi kuutazama kwa makini mwili wa Jacky jinsi ulivyoumbika vyema, ndivyo donge la wivu lilivyozidi kumkaba kooni na kuufanya moyo wake uanze kuumia sana.

“Mbona jana hukurudi nyumbani?” Carlos alijikuta akimuuliza Jacky kwa sauti nzito iliyojaa wivu na hasira. Jacky alimtazama kwa udadisi na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Kazi haikuwa rahisi kama unavyodhani, ilibidi nitumie mbinu ya ziada kumsomesha yule bwana ili anielewe,” Jacky aliongea kwa sauti nyororo yenye kusihi.

“Kwa hiyo baada ya kumaliza kumsomesha ndiyo mkaamua kukesha kabisa! Na usiniambie kuwa uliamua kwenda kavukavu!” Carlos alisema huku akimkazia macho Jacky kwa wasiwasi.

“Niende kavukavu kwani sijitakii mema!” Jacky aliongea kwa utulivu huku akiruhusu tabasamu lake kuchanua usoni kwake. Kisha alimsogelea Carlos karibu zaidi na kumkumbatia akiizungusha mikono yake kwenye kiuno cha Carlos, akambusu na kugeuka kuendelea na kazi yake ya kuandaa kifungua kinywa.

Carlos alisimama pale kwa kitambo kirefu akimtazama Jacky kwa makini, kisha alilazimisha tabasamu na kuondoka.

Dakika arobaini baadaye Jacky na Carlos walikuwa wameketi kwenye meza ya chakula wakipata kifungua kinywa. Jacky alikuwa mkimya mno wakati wote walipokuwa wakistafustahi asubuhi ile kitendo kilichomshangaza sana Carlos.

Alikuwa akila chakula lakini akili yake haikuonekana kuzama kwenye kile chakula pale mezani badala yake alikuwa akila taratibu kwa kupekua pekua chakula, huku mkono wake mmoja ukiwa shavuni, kuna wakati alikuwa akimtupia macho Carlos na kutabasamu.

Uzoefu wa Carlos kwa Jacky na wasichana warembo wa aina yake ukamwacha njia panda. Alijikuta akishindwa kula na kumtazama Jacky kwa udadisi lakini asielewe ni nini kilichokuwa katika mawazo ya Jacky, mwishowe akashindwa kuvumilia.

“Jacky, kwa nini jana usiku hukurudi, ni nini kilichokufanya ukaamua kukesha na yule bwana hadi asubuhi?” Carlos aliuliza kwa sauti iliyoonesha wazi kuwa sasa wivu kwa Jacky ulikuwa umemtawala.

“Hmm, si nimekwisha kujibu jamani, au kuna kingine? Kama hujapenda ungeniambia, ndiyo maana jana nilikuuliza kama ulikuwa unaona wivu nisiende. Sasa unaponiuliza swali lile lile mara mbili mbili nakuwa sielewi kwa nini ulinituma kufanya kazi ile kama hatuaminiani kiasi hiki!” Jacky alisema kwa utulivu lakini akionekana kukerwa sana na swali la Carlos.

“Siyo hivyo, mpenzi, wewe ni mke wangu tena wa ndoa, ni haki yangu kuhakikisha hupati madhara na unaendelea kuwa usalama, na kama ratiba ilibadilika nilitegemea ungenijulisha kwa simu kuwa hutorudi ili nijue cha kufanya…” Carlos alisema kwa sauti tulivu yenye kusihi.

“Cha kufanya kama kipi! Kwamba na wewe ungetafuta mwanamke mwingine wa kulala naye, siyo?” Jacky alimuuliza Carlos huku akiwa amemtulizia macho.

“Usinielewe vibaya, Jacky…”

“Labda nikwambie ukweli, yule bwana ni mwoga sana japo fedha anazitaka. Hivyo ilibidi nipoteze muda mwingi sana kumsomesha hadi anielewe, nimekuja kushtuka tayari ilikuwa imeshatimia saa tisa usiku, unadhani hapo ningefanyaje?” Jacky alimuuliza Carlos huku akiendelea kumtulizia macho yake.

“Okay nimekuelewa, hebu tuachane na hayo… sasa niambie umemuonaje kakuelewa?” Carlos aliuliza huku akijiegemeza kwenye kiti chake.

“Somo limemuingia sana! Tumeongea mambo mengi na kanipa data zote za kwenye tawi lao na akaunti ambayo tutaweza kuitumia kufanikisha mpango wetu. Kwa kifupi ameonesha ushirikiano mkubwa sana kwa kuwa hata yeye fedha anaitaka.”

“Ni akaunti ipi hiyo aliyokuwa data zake?”

The Jacarandah Group…

Wow!” Carlos alijikuta akiruka kwa furaha.

Muda ule Jacky aliinua kikombe chake cha chai ambayo tayari ilikuwa imepoa na kupiga funda kubwa akiimalizia chai yote iliyobaki, kisha alinawa mikono na kufuta midomo wake kwa kitambaa laini.

“Lakini kazi sasa ipo kwenye kuingia pale benki na kutoka na pesa yote hiyo bila kushitukiwa,” Jacky alisema huku akisukumia kando kikombe chake.

“Suala la kutoka na pesa benki wala si kazi, hilo niachie mimi. Mimi ndiye professional bank robber, nimefuzu mbinu zote za kihalifu na sijawahi kuacha rekodi yoyote ya kuwafanya polisi wanishtukie,” Carlos alisema huku akijipiga piga kifuani katika hali ya kujisifia, kisha akaendelea.

“Kwanza nimefurahi kwa kuwa ni habari muhimu sana kusikia The Jacarandah Group wanaweka pesa zao kwenye tawi lile, hapo itabidi twende kwa Jasmine tukaongee naye kwa kina sana,” Carlos alisema huku akiinuka kutoka pale kwenye kiti.

“Jasmine yupi?” Jacky aliuliza kwa shauku huku akimkazia macho Carlos.

“Mtoto wa marehemu Kombo, yule rafiki yangu tuliyemzika mwaka jana kule kwenye makaburi ya Vingunguti,” alisema Carlos.

Itaendelea...

Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY HALELUYA MOSHI Clkey
 
Kizungumkuti! - 20

Na Bishop Hiluka

Jacky alifurahi sana na kummwagia Yusuf mabusu mfululizo, kisha kikafuata kitambo kirefu cha kupanga mipango kabambe ya namna ya kufanikisha mambo ya fedha, huku Jacky akitawala mazungumzo. Katikati ya maongezi yao Jacky alishtuka na kuangalia saa yake ya mkononi akapigwa na butwaa.

“Dah, saa tisa usiku!” Jacky alisema na kumshtua sana Yusuf.

“Oh my God, saa tisa! Sijui nitamwambia nini mke wangu! Sijawahi kulala nje hata siku moja na jana nimetoka nyumbani saa kumi na mbili jioni na sijarudi hadi saa hizi! Eeh Mungu nisamehe mja wako,” Yusuf aliwaza huku moyo wake ukijaa hofu…

Endelea...

* * * * *

Oh God, help me. What kind of life is this? Why do I live like this?” (Mungu wangu nisaidie. Haya ni maisha gani? Kwa nini ninaishi maisha kama haya?) Jacky alikuwa anawaza huku akilisikilizia tumbo lake lililokuwa dhaifu sana kwa vile usiku uliokuwa umetangulia alikuwa ametia kilevi tumboni na hakuwa amekula chakula.

Ukichanganya na mahaba mazito aliyoyapata kutoka kwa Yusuf usiku kucha yaliyochangiwa na kiu yake ya kutaka kupata taarifa sahihi za mabilioni ya pesa vilikuwa vimemchanganya sana Jacky na kumfanya asahau hata kula.

Kichwa chake kilikuwa kizito sana kutokana na mning’inio (hang over) uliotokana na uchovu wa pombe kali alizokuwa amekunywa usiku wa siku iliyotangulia. Wakati akiyawaza hayo ilikuwa tayari imeshatimia saa moja ya asubuhi, alikuwa amerudi nyumbani takriban nusu saa tu iliyokuwa imepita.

Alipofika nyumbani asubuhi ile jambo la kwanza alilofanya ilikuwa ni kukimbilia moja kwa moja bafuni kujimwangia maji ya uvuguvugu ili apate nguvu mpya, kwani mwili wote ulikuwa unamuuma kama kidonda kutokana na gwaride la usiku kucha alilokuwa amechezeshwa na Yusuf.

Kiukweli, mwanzoni alikuwa amemchukulia poa Yusuf kwa kudhani asingeweza kumudu dakika tisini za mchezo, kumbe alikosea sana kwani Yusuf aliweza kwenda hadi dakika mia moja na ishirini, na bado walipoingia kwenye matuta hakupatikana mshindi.

Jacky alikuwa amekutana na muziki wa Yusuf usio wa kitoto, kwani Yusuf alijua kucheza ngoma zote, msondo, ndekule, mdundiko, sindimba na nyinginezo pasipo kuomba poo na alikuwa hachoki utadhani alikuwa na mapafu kama ya farasi.

Asubuhi ile Jacky alipomaliza kujimwagia maji alijifunga khanga moja kifuani na taulo kiunoni na kuelekea jikoni ambako alianza kuandaa kifungua kinywa. Wakati alipokuwa mbioni kumaliza zoezi lile la kuandaa kifungua kinywa alishtushwa na mikono ya mtu iliyomshika kiunoni.

Aligeuka haraka nyuma huku moyo wake ukianza kupoteza utulivu, akamuona Carlos akiwa amesimama nyuma yake akitabasamu na hapo tabasamu jepesi likachomoza usoni kwake.

Kumbe muda ule alipokuwa akiandaa kifungua kinywa Carlos alikuwa amenyata taratibu kutoka chumbani alikokuwa amelala na kwenda kusimama nyuma yake bila yeye kujua.

Macho ya Carlos yalikuwa na kila dalili za uchovu na alisimama pale akimtazama Jacky kwa namna ambayo ilimshtua kidogo Jacky. Carlos alimtazama Jacky kwa kitambo kirefu bila kusema neno.

Alikuwa akiitazama hazina matata iliyokuwa imejificha katika umbo matata la Jacky na kujikuta akihisi donge la wivu likimkaba kooni kwake kwa kukubali kumruhusu Jacky kwenda kulala na mwanamume mwingine, eti sababu ya kutafuta pesa.

Kila alipozidi kuutazama kwa makini mwili wa Jacky jinsi ulivyoumbika vyema, ndivyo donge la wivu lilivyozidi kumkaba kooni na kuufanya moyo wake uanze kuumia sana.

“Mbona jana hukurudi nyumbani?” Carlos alijikuta akimuuliza Jacky kwa sauti nzito iliyojaa wivu na hasira. Jacky alimtazama kwa udadisi na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Kazi haikuwa rahisi kama unavyodhani, ilibidi nitumie mbinu ya ziada kumsomesha yule bwana ili anielewe,” Jacky aliongea kwa sauti nyororo yenye kusihi.

“Kwa hiyo baada ya kumaliza kumsomesha ndiyo mkaamua kukesha kabisa! Na usiniambie kuwa uliamua kwenda kavukavu!” Carlos alisema huku akimkazia macho Jacky kwa wasiwasi.

“Niende kavukavu kwani sijitakii mema!” Jacky aliongea kwa utulivu huku akiruhusu tabasamu lake kuchanua usoni kwake. Kisha alimsogelea Carlos karibu zaidi na kumkumbatia akiizungusha mikono yake kwenye kiuno cha Carlos, akambusu na kugeuka kuendelea na kazi yake ya kuandaa kifungua kinywa.

Carlos alisimama pale kwa kitambo kirefu akimtazama Jacky kwa makini, kisha alilazimisha tabasamu na kuondoka.

Dakika arobaini baadaye Jacky na Carlos walikuwa wameketi kwenye meza ya chakula wakipata kifungua kinywa. Jacky alikuwa mkimya mno wakati wote walipokuwa wakistafustahi asubuhi ile kitendo kilichomshangaza sana Carlos.

Alikuwa akila chakula lakini akili yake haikuonekana kuzama kwenye kile chakula pale mezani badala yake alikuwa akila taratibu kwa kupekua pekua chakula, huku mkono wake mmoja ukiwa shavuni, kuna wakati alikuwa akimtupia macho Carlos na kutabasamu.

Uzoefu wa Carlos kwa Jacky na wasichana warembo wa aina yake ukamwacha njia panda. Alijikuta akishindwa kula na kumtazama Jacky kwa udadisi lakini asielewe ni nini kilichokuwa katika mawazo ya Jacky, mwishowe akashindwa kuvumilia.

“Jacky, kwa nini jana usiku hukurudi, ni nini kilichokufanya ukaamua kukesha na yule bwana hadi asubuhi?” Carlos aliuliza kwa sauti iliyoonesha wazi kuwa sasa wivu kwa Jacky ulikuwa umemtawala.

“Hmm, si nimekwisha kujibu jamani, au kuna kingine? Kama hujapenda ungeniambia, ndiyo maana jana nilikuuliza kama ulikuwa unaona wivu nisiende. Sasa unaponiuliza swali lile lile mara mbili mbili nakuwa sielewi kwa nini ulinituma kufanya kazi ile kama hatuaminiani kiasi hiki!” Jacky alisema kwa utulivu lakini akionekana kukerwa sana na swali la Carlos.

“Siyo hivyo, mpenzi, wewe ni mke wangu tena wa ndoa, ni haki yangu kuhakikisha hupati madhara na unaendelea kuwa usalama, na kama ratiba ilibadilika nilitegemea ungenijulisha kwa simu kuwa hutorudi ili nijue cha kufanya…” Carlos alisema kwa sauti tulivu yenye kusihi.

“Cha kufanya kama kipi! Kwamba na wewe ungetafuta mwanamke mwingine wa kulala naye, siyo?” Jacky alimuuliza Carlos huku akiwa amemtulizia macho.

“Usinielewe vibaya, Jacky…”

“Labda nikwambie ukweli, yule bwana ni mwoga sana japo fedha anazitaka. Hivyo ilibidi nipoteze muda mwingi sana kumsomesha hadi anielewe, nimekuja kushtuka tayari ilikuwa imeshatimia saa tisa usiku, unadhani hapo ningefanyaje?” Jacky alimuuliza Carlos huku akiendelea kumtulizia macho yake.

“Okay nimekuelewa, hebu tuachane na hayo… sasa niambie umemuonaje kakuelewa?” Carlos aliuliza huku akijiegemeza kwenye kiti chake.

“Somo limemuingia sana! Tumeongea mambo mengi na kanipa data zote za kwenye tawi lao na akaunti ambayo tutaweza kuitumia kufanikisha mpango wetu. Kwa kifupi ameonesha ushirikiano mkubwa sana kwa kuwa hata yeye fedha anaitaka.”

“Ni akaunti ipi hiyo aliyokuwa data zake?”

The Jacarandah Group…

Wow!” Carlos alijikuta akiruka kwa furaha.

Muda ule Jacky aliinua kikombe chake cha chai ambayo tayari ilikuwa imepoa na kupiga funda kubwa akiimalizia chai yote iliyobaki, kisha alinawa mikono na kufuta midomo wake kwa kitambaa laini.

“Lakini kazi sasa ipo kwenye kuingia pale benki na kutoka na pesa yote hiyo bila kushitukiwa,” Jacky alisema huku akisukumia kando kikombe chake.

“Suala la kutoka na pesa benki wala si kazi, hilo niachie mimi. Mimi ndiye professional bank robber, nimefuzu mbinu zote za kihalifu na sijawahi kuacha rekodi yoyote ya kuwafanya polisi wanishtukie,” Carlos alisema huku akijipiga piga kifuani katika hali ya kujisifia, kisha akaendelea.

“Kwanza nimefurahi kwa kuwa ni habari muhimu sana kusikia The Jacarandah Group wanaweka pesa zao kwenye tawi lile, hapo itabidi twende kwa Jasmine tukaongee naye kwa kina sana,” Carlos alisema huku akiinuka kutoka pale kwenye kiti.

“Jasmine yupi?” Jacky aliuliza kwa shauku huku akimkazia macho Carlos.

“Mtoto wa marehemu Kombo, yule rafiki yangu tuliyemzika mwaka jana kule kwenye makaburi ya Vingunguti,” alisema Carlos.

Itaendelea...

Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY@HALELUYA MOSHI Clkey
Asante Bishop

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kizungumkuti! - 21

Na Bishop Hiluka

“Suala la kutoka na pesa benki wala si kazi, hilo niachie mimi. Mimi ndiye professional bank robber, nimefuzu mbinu zote za kihalifu na sijawahi kuacha rekodi yoyote ya kuwafanya polisi wanishtukie,” Carlos alisema huku akijipiga piga kifuani katika hali ya kujisifia, kisha akaendelea.

“Kwanza nimefurahi kwa kuwa ni habari muhimu sana kusikia The Jacarandah Group wanaweka pesa zao kwenye tawi lile, hapo itabidi twende kwa Jasmine tukaongee naye kwa kina sana,” Carlos alisema huku akiinuka kutoka pale kwenye kiti.

“Jasmine yupi?” Jacky aliuliza kwa shauku huku akimkazia macho Carlos.

“Mtoto wa marehemu Kombo, yule rafiki yangu tuliyemzika mwaka jana kule kwenye makaburi ya Vingunguti,” alisema Carlos.

Endelea...

Jacky alikunja sura yake akijaribu kufikiria kwa kitambo kidogo kisha akabetua kichwa chake akionekana kukumbuka. “Okay… Kombo namkumbuka lakini Jasmine hata simkumbuki kabisa!” Jacky alisema huku akionekana kujaribu kuvuta taswira ya Jasmine bila mafanikio.

“Ukimuona utamkumbuka, tutaenda nyumbani kwake leo jioni tukamsomeshe, nina imani atatuelewa,” Carlos alisema huku akiliendea jokofu na kutoa chupa ya mvinyo aina ya Sauvignon Blanc.

Jacky aliinuka na kutoa vyombo kisha akavipeleka jikoni, aliporudi sebuleni alimkuta Carlos akiwa ameweka bilauri mbili mezani, hivyo wakashushia na mvinyo mtamu wa Sauvignon Blanc kama namna ya kujipongeza kwa kazi nzuri iliyofanyika.

Mvinyo ule ulionekana kuamsha ari mpya katika miili yao na hivyo kuwachangamsha vizuri kiasi cha kupunguza nishai machoni. Haikuchukua muda kila mmoja alijikuta mikono yake ikivinjari kwenye mwili wa mwenzake huku nguo zikitolewa na kutupwa huku na kule.

Japokuwa Jacky alipanga kupumzika asubuhi ile kutokana na mwili wake kukosa nguvu kwa kukimbizwa mchaka mchaka na Yusuf usiku kucha wa siku iliyotangulia, lakini hakuwa na namna, alijikuta akilazimika kukabiliana na gwaride jingine kutoka kwa mumewe Carlos.

“Hmm… sijui nitaendelea na maisha haya hadi lini? I’m sick and tired with this kind of life,” Jacky aliwaza wakati akipiga magoti na kuanza manjonjo yake akiisakama ikulu ya Carlos kwa kutumia mdomo wake… na muda mfupi uliofuata walikuwa wakielea angani kwenye sayari ya mbali sana isiyofikika kwa chombo chochote isipokuwa mahaba mazito.

* * * * *

Asubuhi ile nyumbani kwa Yusuf, kwenye nyumba ya kawaida ya kupanga iliyokuwa katika eneo la Ilala Bungoni, Yusuf alikuwa chumbani kwake amesimama mbele ya meza ya vipodozi yenye kioo kirefu cha kujitazama.

Alisimama pale kwa takriban dakika tano akiwa hajui afanye nini, na alipogutuka alichuku chanuo akaanza kuchana nywele zake taratibu huku akionekana kuwaza mbali.

Muda wote alionekana kuwa mtulivu sana na mwenye mawazo mengi. Asubuhi ile Yusuf alikuwa amevaa shati nzuri jeupe lililokuwa na mikono mirefu, suruali ya bluu na tai shingoni ya rangi ya bluu iliyokuwa na nembo ya benki aliyokuwa akiifanyia kazi.

Akiwa bado katika lindi la mawazo mara mlango wa chumba chake ukafunguliwa na mwanadada aliyekuwa na miaka kama ishirini na sita hivi akaingia, huyu alikuwa ni mkewe, Mama Jasmine.

Aliingia taratibu na kusimama huku akimtazama Yusuf kwa makini kuanzia kichwani hadi kwenye unyayo kisha akakisogelea kitanda na kujipwetekaa pale kitandani huku akiendelea kumtazama Yusuf.

Yusuf alionekana kushtuka sana, alimtupia jicho la wizi mkewe kupitia kile kioo cha kujitazama wakati akijifanya kuweka lile chanuo juu ya ile meza ya vipodozi.

Yule mwanamke alikuwa ni mdada mrembo sana aliyejaaliwa kuwa na uzuri wa asili, alikuwa na umbo kubwa kiasi lililovutia sana na sura ya kitoto. Alikuwa mrefu wa wastani na mweupe kwa rangi ya ngozi. Rangi ambayo ilikuwa na mng’aro wa aina yake na mvuto wa kipekee na wala hakuhitaji vikorombwezo vya aina yoyote kuinakshi ngozi ile.

Alikuwa na nywele nyingi alizokuwa amezifunika kwa kofia maalumu ya kulalia na mwilini alivaa nguo nyepesi ya kulalia ya rangi ya samawati iliyolichora vyema umbo lake zuri na juu ya ile nguo alijifunga khanga. Asubuhi ile alionekana mchovu sana kwa sababu ya kukesha usiku akimsubiri mumewe na usoni alionekana ni mwenye hasira.

Yusuf alijifanya kuitengeneza vizuri tai yake shingoni huku akimtupia tena jicho la wizi kupitia kile kioo cha kujitazama, kwa kuwa alikuwa hana ujasiri wa kumtazama moja kwa moja. Hata hivyo, aliamua kujipa ujasiri ili kuzikabili hasira za mkewe, maana kama maji yalikwisha mwagika na yasingeweza kuzoleka.

“Baba Jasmine, naomba unieleze ukweli vinginevyo leo patachimbika, jana ulilala wapi?” Yusuf alishtushwa na sauti ya mkewe.

“Jamani, si tumekwisha yazungumza! Nimekwambia nilikokuwa na sababu iliyonifanya nikashindwa kurudi nyumbani usiku, nikadhani labda tumeelewana kumbe mwenzangu bado hayajaisha?” Yusuf alijibu kwa sauti tulivu.

“Kwa nini hukunitaarifu jana hiyo hiyo kama ungechelewa kurudi ili nisiwe na wasiwasi kuhusu usalama wako?”

“Ni bahati mbaya tu nilijisahau, nimeomba samahani, nakuomba tena nisamehe yaishe ili tu…”

“Hayawezi kuisha kirahisi namna hiyo, yaani ulale nje, urudi hapa asubuhi ukiwa unanukia manukato ambayo sijawahi kuyasikia humu ndani halafu eti yaishe hivi hivi tu, haiwezekani! Mimi ni mkeo na ni lazima nijue kila kitu unachokifanya… Naomba uniambie jana ulilala wapi na ulikuwa na nani?” mkewe alimkata kauli huku akiongea kwa msisitizo, alikuwa amekasirika kweli kweli.

I need to know everything, you are my husband and you are important to me,” (Ninahitaji kujua kila kitu, wewe ni mume wangu na wewe ni muhimu kwangu) Mama Jasmine aliendelea kuongea kwa hasira, na kila alivyozidi kuongea ndivyo sauti yake ilivyozidi kupanda na kuwa kali zaidi.

I know that I’m important to you, and you are also very important to me…” (Najua mimi ni muhimu kwako, na wewe pia ni muhimu sana kwangu…) Yusuf alijaribu kujitetea huku akimsogelea mkewe taratibu.

Liar! I’m not important to you at all. I’m very disappointed,” (Muongo! Mimi si muhimu kwako kabisa. Nimefadhaika sana.) Mama Jasmine alilalamika huku hasira zake zikizidi kupanda.

Remember I'm not a little kid and not as foolish as you think,” (Kumbuka mimi si mtoto mdogo kabisa na wala si mpumbavu kama unavyofikiria) Mama Jasmine alizidi kulalamika kwa huzuni.

Yusuf alilazimisha tabasamu kisha akamsogelea na kupeleka mkono wake wa kulia kwenye uso wa mkewe kwa uangalifu huku uso wake ukizidi kuchanua kwa tabasamu, japo kwa kulazimisha.

Don’t touch me!” (Usiniguse!) Mama Jasmine aliusukuma mkono wa Yusuf kwa hasira na kurudi nyuma.

“Kama unadhani natania basi subiri uone, yaani ulale na malaya wako usiku kucha kisha unarudi asubuhi, halafu naongea unaniona kama katuni. Au naongea upuuzi?” Mama Jasmine alisema kwa hasira na kusonya. Kitendo cha kusonya kikamkasirisha sana Yusuf.

Itaendelea...
 
Kizungumkuti! - 22

Na Bishop Hiluka

Yusuf alilazimisha tabasamu kisha akamsogelea na kupeleka mkono wake wa kulia kwenye uso wa mkewe kwa uangalifu huku uso wake ukizidi kuchanua kwa tabasamu, japo kwa kulazimisha.

Don’t touch me!” (Usiniguse!) Mama Jasmine aliusukuma mkono wa Yusuf kwa hasira na kurudi nyuma.

“Kama unadhani natania basi subiri uone, yaani ulale na malaya wako usiku kucha kisha unarudi asubuhi, halafu naongea unaniona kama katuni. Au naongea upuuzi?” Mama Jasmine alisema kwa hasira na kusonya. Kitendo cha kusonya kikamkasirisha sana Yusuf.

Endelea...

“Unanisonya? Yaani Mama Jasmine umefikia hatua ya kunisonya! Naona sasa unaanza kuvuka mipaka,” Yusuf alisema huku akimtazama mkewe kwa hasira.

“Mipaka ya kwenda wapi?” Mama Jasmine aliuliza kwa hasira huku naye akimtazama Yusuf kwa hasira. Kwa kitambo walibaki wakiwa wametazama kwa hasira kama majogoo yaliyotaka kupigana.

“Hivi unataka tuoneshane jeuri ya kusema, au nini? Kwa kuwa unajua nakupenda ndiyo maana unaleta jeuri siyo, lakini siwezi kukaa kimya kwa madai yako kuwa eti nimekesha na malaya wakati si kweli, una ushahidi gani kuhusu madai yako?” Yusuf aliuliza huku akimkazia macho mkewe.

“Ushahidi uliopo machoni kwa Mungu unanitosha, na ninaamini atanilipia,” alisema mkewe huku akishusha pumzi ndefu kama aliyetoka kukimbia mbio ndefu. Yusuf alitaka kusema neno lakini hatia ikamkaba koo, akabaki kushangaa tu akimtumbulia macho mkewe. Kikapita tena kitambo kirefu cha ukimya.

“Yaani hata sielewi, nimekwambia ukweli wangu hutaki kuamini, nimeomba msamaha pia hutaki kukubali, sijui wewe ni mwanamke wa aina gani? Sasa sikiliza, mimi ndiye mwanamume humu ndani, nataka mambo haya yaishe na sitaki tena kuyasikia…” Yusuf alisema kwa hasira.

“Huwezi kunizuia kuongea, Yusuf…”

“He, mara hii nimeshakuwa Yusuf na si Baba Jasmine tena?” Yusuf aliuliza kwa mshangao huku akimkazia macho mkewe.

“Kwani siyo jina lako? Usitake kutafuta sababu ya kunifunga mdomo nisiongee, nitaongea na huwezi kunifanya kitu, kwa taarifa yako ni kwamba lazima niwafikishie taarifa hizi wazee,” mkewe alifoka kwa hasira. Maneno yale yalionekana kumuumiza sana Yusuf, hivyo akamsogelea mkewe.

“Mama Jasmine, this is the last warning. Tafadhali usithubutu tena kunijibu namna hiyo,” Yusuf alisema kwa sauti tulivu huku akimnyooshea kidole mkewe kwa hasira.

I’m not a coward to be scared, tena naomba usinitishe kabisa, Yusuf. Huwezi kunifanya lolote,” yule mwanamke alizidi kupandisha kwa kujiamini. Yusuf akamkaba shingoni kwa hasira na kumtingisha.

I married you because I love you very much, so don’t dare disrespect me again,” (Nilikuoa kwa sababu nakupenda sana, kwa hiyo usijaribu kunidharau tena) Yusuf aliongea kwa hasira na kutoka mle chumbani huku akiubamiza mlango nyuma yake.

Japo Yusuf alikuwa amemtisha mkewe na kuondoka kwa hasira lakini ukweli ni kwamba moyoni hakuwa na ujasiri kabisa wa kusimama mbele ya mkewe na kukanusha kilichokuwa kikisemwa. Kwa mara ya kwanza katika maisha yake ya ndoa alijikuta akiogopa sana, kwani katika miaka sita ya ndoa yao hakuwahi kabisa kumuona mkewe akiwa amekasirika kiasi ile.

Baada ya Yusuf kuondoka Mama Jasmine aliketi pale kitandani taratibu, macho yake yalijenga malengelenge ya machozi kiasi kwamba kila alichokitazama mle chumbani alikiona katika hali ya ukungu. Aliinamisha kichwa chake na kutafakari sana.

Aliendelea kuganda vile kwa muda mrefu akiwaza yaliyomjia akilini na katika kutafakari akakumbuka yaliyotokea usiku uliotangulia baada ya mumewe kuchelewa kurudi nyumbani.

Ilikuwa saa nne usiku, alikuwa kasimama barazani nje ya nyumba waliyokuwa wakiishi akionekana kutokuwa katika hali nzuri, japo alijitahidi sana kuwa mtulivu. Muda ule mtoto wake Jasmine wa miaka mitatu alikuwa kamng'ang'ania mama yake khanga.

Mama Jasmine na mwanawe walisimama pale nje wakitazama barabarani labda pengine wangeweza kumuona Yusuf akirudi nyumbani na mfuko wenye zawadi kama ilivyokuwa kawaida yake pindi alipotoka kwenda kutazama mpira au kukutana na rafiki zake baa na kupata bia mbili.

Baada ya Jasmine kuzidi kumsumbua alichukua simu yake na kubofya namba za Yusuf kisha akapiga na kuongea naye, Yusuf alimwambia kuwa alikuwa anamalizia kikao na angerejea nyumbani haraka mara baada ya kumaliza.

Mama Jasmine pia akakumbuka jinsi alivyokesha sebuleni kwenye kochi akiwa na wasiwasi akimsubiri Yusuf baada ya kutorudi, aliendelea kuketi pale kwenye kochi hadi ilipotimia saa kumi usiku akashindwa kuvumilia na kujikuta akipitiwa na usingizi pale pale sebuleni kwenye kochi.

Alikuja kushtuka alfajiri ya saa kumi na mbili baada ya kusikia mlango ukigongwa taratibu, aliinuka na kuufungua akamuona Yusuf akiingia huku akionekana kuchoka sana, pia hakuwa akimwangalia machoni mkewe.

Mama Jasmine alimtazama Yusuf kwa makini lakini Yusuf alionesha kuyakwepa macho ya mkewe, jambo hilo likamfanya Mama Jasmine ashtuke na kuona kuwa huenda kulikuwa na jambo ambalo Yusuf alikuwa akilificha.

“Mbona leo umechelewa sana kurudi?” Mama Jasmine alimuuliza Yusuf huku akimkazia macho.

“Nimechelewa? Hivi mtu huwa anachelewa nyumbani kwake?” Yusuf aliongea kwa mzaha huku akijichekesha.

Mama Jasmine akamuonesha saa iliyokuwa imetundikwa ukutani. “Hebu angalia saa, ni saa ngapi sasa?”

Yusuf aliiangalia ile saa ya ukutani, kisha akaiangalia na ile ya mkononi aliyokuwa ameivaa na kushusha pumzi za ndani kwa ndani. “Saa kumi na mbili na robo, lakini…” alisema lakini Mama Jasmine akamkatisha.

“Hivi huu ndiyo muda muafaka wa wewe kurudi nyumbani kwako?” Mama Jasmine aliuliza kwa utulivu huku akionekana kuzuia hasira zake.

“Samahani, mke wangu, kikao chetu kilikuwa kirefu sana na ukichanganya na pombe tulizokuwa tunakunywa si nikajisahau, nilipokuja kushtuka it was too late,” Yusuf alisema kwa utulivu huku akiyakwepa macho ya mkewe na kutazama pembeni na alionekana kuwa na wasiwasi.

“Hujanishawishi bado, kila nikiitazama sura yako na kile unachokiongea naona hata haviendani, How could you do this to me? How could you betray me?” (Unawezaje kunifanyia hivi? Unawezaje kunisaliti?) Mama Jasmine aliongea kwa uchungu huku akizidi kumkazia macho Yusuf.

“Labda nikwambie, unaweza kuongopa chochote, lakini ujue kuwa nafsi yako ndiyo inayojua ukweli na sasa inakusuta.”

Dont you trust me? I’ve told you the truth, I didnt do anything wrong,” (Huniamini? Nimeshakwambia ukweli, sijafanya chochote kibaya) Yusuf alijaribu kujitetea.

Mama Jasmine alimsogelea karibu zaidi na kusimama mbele yake huku akimkazia macho. “Baba Jasmine, hebu niangalie machoni halafu uniambie kuwa hujanisaliti.”

Yusuf alimtazama mkewe machoni na kushindwa kuongea, akayakwepesha macho yake na kutazama pembeni. “Kama huniamini basi, lakini ukweli utabaki pale pale kuwa siwezi kuisaliti ndoa yangu hata siku moja,” Yusuf alisema huku akiingia chumbani…

Itaendelea...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom