Stori ya kusisimua - Kizungumkuti!

Bishop Hiluka

JF-Expert Member
Aug 12, 2011
7,140
14,678
Kizungumkuti!

Na Bishop Hiluka

“Hii ni trela tu, picha kamili keshokutwa! Hakyamungu keshokutwa hakai mtu hapa… mi naapa! Nitakunywa na nitatembea uchi ukumbi mzima kama mademu wakinimaindi poa tu, au vipi kichaa wangu?” Kabwe alipiga kelele kilevi, wakati huo huo Liston alikuwa analazimisha kumshika matiti dada mmoja aliyepita karibu yake…

Fuatilia stori hii hadi mwisho ya kusisimua kuyajua yote yanayoleta kizungumkuti...

KATIKATI ya jiji la Dar es Salaam hali ya hewa ilikuwa ya joto sana kama kawaida, hata katika majira yale ya saa tano za asubuhi. Asubuhi ile pilika pilika za watu zilikuwa zimeshamiri katikati ya jiji hilo kubwa zaidi Tanzania, na hivyo kulifanya kuchangamka sana kama ilivyokuwa kawaida yake.

Katika eneo la Mnazi Mmoja, barabara ya Lumumba kulionekana msululu mrefu wa magari, zikiwemo daladala zilizokuwa zikizunguka kutokea mtaa wa Uhuru katika kituo cha daladala cha Mnazi Mmoja na kupita barabara ya Bibi Titi kabla hazijaingia katika mtaa wa Mkunguni na kisha kutokea barabara ya Lumumba.

Katika barabara ile ya Lumumba, gari dogo la kifahari aina ya BMW X6 xDrive 50i la rangi ya samawati lililotokea katika barabara ya Morogoro kwa mwendo wa taratibu na kujiunga katika msululu ule, kisha lilichepuka na kwenda kusimama chini ya miti ya kivuli iliyokuwa imepandwa kando ya ile barabara.

Hata hivyo, dereva wa gari lile alionekana kutoridhika na eneo lile, akaanza kutafuta sehemu nzuri zaidi na baadaye alikwenda kuliegesha gari lake kwenye eneo lililokuwa na magari mengine mawili matatu yaliyokuwa yameegeshwa pale, na vijana kadhaa walionekana wakiosha magari.

Vijana wawili waosha magari walimfuata haraka yule dereva wa lile gari na kuonekana kumzonga, kila mmoja alionekana akitaka apewe tenda ya kuosha lile gari lakini yule dereva hakuonekana kuwajali. Alibaki ametulia kimya akiusikilizia muungurumo laini wa lile gari kwa kitambo kirefu.

Ndani ya gari lile kulikuwa na watu wawili tu, mwanamume mmoja ambaye ndiye aliyekuwa akiendesha lile gari na mwanadada mrembo sana ambaye alikuwa ameketi pembeni yake kwenye siti ya abiria.

Yule mwanamume alikadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka arobaini na arobaini na tano. Alikuwa mrefu wa futi sita na ushee, mweusi na shababi kwelikweli aliyekuwa na mwenye mwili uliojengeka kwa misuli.

Macho yake yalikuwa makali na alikuwa amevaa kofia ya rangi ya bluu aina ya kapelo, t-shirt ya pundamilia iliyokuwa na miraba ya bluu na myeupe aina ya form six na suruali ya jeans ya rangi ya bluu. Miguuni alikuwa amevaa buti ngumu za ngozi zilizokuwa na rangi nyeusi.

Mwanamume yule aliitwa Carlos Mwamba na aliendelea kutulia kwenye siti yake nyuma ya usukani akiwa ameibana njiti moja ya kiberiti kwenye pembe ya mdomo wake, huku akiendelea kuusikilizia muungurumo laini wa lile gari.

Kushoto kwa Carlos Mwamba, kwenye ile siti ya mbele ya abiria yule mrembo aliyekuwa ameketi aliitwa Jackline Mgaya na alikuwa mke wa ndoa wa Carlos, wakiwa wameoana takriban miaka mwili iliyokuwa imepita.

Jackline au kama alivyopenda kujulikana kwa kifupi kwa jina la Jacky alikuwa na umri usiozidi miaka therathini, alikuwa mrefu na mweupe mwenye haiba nzuri ya kuvutia sana.

Alikuwa na nywele nyeusi za kibantu alizokuwa amezikata vizuri na kubaki ndogo ndogo na hivyo kumfanya aonekane mzuri wa asili. Alikuwa na sura yake ya duara na macho makubwa ya kike na legevu yaliyokuwa yamezungukwa na kope ndefu na nyeusi.

Pua yake ilikuwa ndogo na iliyochongoka mfano wa pua ya kihabeshi na mdomo yake ilikuwa laini yenye maki na kingo pana kiasi zilizokuwa zimekolezwa kwa lipstick ya rangi ya chocolate pamoja na vishimo vidogo mashavuni mwake vilimfanya azidi kuonekana mrembo zaidi.

Jacky alikuwa na masikio madogo yasiyochusha aliyokuwa ameyatoga na kuyavalisha hereni kubwa za kitamaduni zilizokuwa na umbo la mviringo. Alikuwa amevaa blauzi nyepesi ya arangi ya pinki iliyoyaficha vyema matiti yake imara yenye ukubwa wa wastani yaliyokuwa na chuchu nyeusi imara zilizosimama kikamilifu ndani ya blauzi ile.

Shingoni alikuwa kavaa mkufu mwembamba wa dhahabu uliokuwa umeizunguka ile shingo nyembamba na kidani cha dhahabu kilichokuwa na herufi ya “J” kilikuwa kimepotelea katikati ya uchochoro mdogo wa yale matiti.

Kwenye mkono wake wa kushoto alikuwa amevaa bangili kadhaa za pembe na vidole vyake viwili vya mkono huo alikuwa amevaa pete ndogo za madini ghali ya tanzanite na green tourmaline.

Mkono wake wa kulia alivaa saa ndogo ghali na nzuri ya kike aina ya Cartier La Dona, ambayo bei yake ilikuwa si haba kama angeamua kuibadili kwa pesa za madafu, kwani ilikuwa imemgharimu kiasi cha dola za Marekani 137,000.

Cartier La Dona Watch ilikuwa ni saa ghali sana iliyotengenezwa kwa madini ya dhahabu nyeupe ya Karati 18 ikiwa na kesi imara iliyokuwa na milimita 27 kwa 29 na mkanda wake pia ulikuwa umetengenezwa kwa dhahabu nyeupe, ikiwa na gerentii ya miaka hamsini.

Alikuwa ameinunua nchini Switzerland walipokwenda kwenye fungate muda mfupi tu baada ya ndoa yao iliyoacha gumzo jijini Arusha na kwenye viunga vyake.

Gari ikiwa bado inaunguruma taratibu Jacky alishusha pumzi za ndani kwa ndani na kutazama nje kwa kitambo fulani huku macho yake yakielekea moja kwa moja kwenye jengo la ghorofa la Benki ya Biashara.

Alilitazama lile jengo kwa makini akionekana kama aliyekuwa akijiuliza jambo kuhusiana na lile jengo, kisha aliyashusha macho yake kuutazama mkoba wake mzuri wa kike wa rangi ya pinki uliokuwa umelala juu ya mapaja yake mazuri.

Aliufungua ule mkoba na kutoa humo mkebe mdogo wa duara wa rangi nyekundu kisha aliinua macho yake kujitazama kwa kitambo kifupi kwenye kioo cha lile gari cha katikati kinachotumika kuangalia nyuma huku akigeuza geuza uso wake pembe zote.

Alikunja uso wake huku akiminya midomo yake mizuri yenye maki, na hapo mashavu yake yakapiga misingi, pembe za midomo yake zikafinya, akashusha pumzi ndefu za ndani kwa ndani huku akigeuka kumtazama Carlos aliyekuwa ametulia tuli kama maji mtungini na kuachia tabasamu bashasha.

Carlos aliendelea kutulia pale nyuma ya usukani akionekana kuwaza mbali sana, alimtupia jicho Jacky mara moja tu, kisha akayahamisha macho yake na kutazama kwenye lile jengo la Benki ya Biashara huku sura yake ikiwa haioneshi tashwishwi yoyote.

Jacky alimtazama Carlos kwa makini kisha akaufungua ule mkebe akatoa vipodozi na kuanza kujiremba akiongezea urembo kwenye sura yake huku akijitazama kwenye kile kioo cha gari cha katikati kinachoonesha nyuma.

Itaendelea...

Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY
 
Kizungumkuti! - 2

Na Bishop Hiluka

Jacky alimtazama Carlos kwa makini kisha akaufungua ule mkebe akatoa vipodozi na kuanza kujiremba akiongezea urembo kwenye sura yake huku akijitazama kwenye kile kioo cha gari cha katikati kinachoonesha nyuma.

Aliporidhishwa na urembo wake alishusha tena pumzi za ndani kwa ndani na kuufunga ule mkebe, akarudisha kwenye mkoba wake na kuufunga, kisha akageuza tena shingo yake kumtazama Carlos aliyekuwa bado ametulia tuli kwenye siti yake nyuma ya usukani.

Hapo Carlos akaachia tabasamu jepesi usoni mwake lililoyafanya meno yake yaliyokuwa yamepoteza mng’ao wake kwa sababu ya ukungu wa moshi wa sigara na pombe kali kuonekana vizuri.

Are you nervous, my love?” (Vipi, una wasiwasi, mpenzi?) Carlos alimuuliza Jacky huku akiendelea kutabasamu.

No, I’m not,” (Hapana, sina) alijibu Jacky huku akijiinua kidogo akapeleka shingo yake karibu na Carlos.

Na hapo akasogeza midomo yake karibu zaidi na midomo ya Carlos, midomo yao ilipokutana Jacky akambusu Carlos kisha akashika vyema mkoba wake na kuteremka kutoka kwenye lile gari huku akimwacha Carlos ndani ya gari akiwa bado katulia akisubiri.

Take care, my love, and try in anyway you can to make him go crazy about you,” (Kuwa makini, mpenzi, na jaribu kila uwezavyo kumchanganya atakapokuona) Carlos alisema kwa sauti tulivu.

Don’t worry, honey,” (Usihofu, mpenzi) Jacky alijibu huku akipiga hatua zake taratibu na kwa madaha kuivuka ile barabara ya Lumumba kisha akaelekea upande wa pili akilifuata moja kwa moja lile jengo la Benki ya Biashara.

Alipokuwa akitembea ndipo umbile lake lilipoonekana vizuri, alikuwa mrefu na mwenye umbo zuri sana, kiuno chake kilikuwa chembamba kiasi chenye misuli imara kilichokuwa kimeizuia suruali yake ya rangi nyeusi ya jeans iliyolichora vyema umbo lake matata lenye kuzitaabisha vibaya nafsi za mwanaume wakware.

Miguuni alikuwa amevaa buti ngumu za kike za ngozi na kwa kweli alikuwa kapendeza sana, alitembea akiangalia huku na kule huku akiwa amening’iniza mkoba wake wa kike begani uliomfanya kuvutia zaidi. Itoshe tu kusema kuwa Jacky alikuwa mwanadada mrembo kwelikweli aliyestahili hata kutwaa taji la urembo la dunia!

She’s so gorgeous… I’m very lucky because this is exactly the type of woman I was always dreaming for,” (Ni mrembo hasa… nina bahati sana kwa sababu huyu ndio aina ya mwanamke ambaye siku zote nilikuwa naota kumpata) Carlos aliwaza huku akimsindikiza Jacky kwa macho.

Alishusha pumzi za ndani kwa ndani huku akijiegemeza kwenye kiti chake na mara akaanza kukumbuka alivyokutana na Jacky kwa mara ya kwanza kabla hawajaangukia kwenye mapenzi mazito ambayo baadaye yalikuja kuzaa ndoa…

______

Ilikuwa siku ya Jumatano, Carlos alikuwa amechelewa sana kutoka hotelini kwake baada ya kukurupuka kitandani saa tatu na nusu za asubuhi akiwa chumba namba 204 cha Arusha Crown Hotel jijini Arusha!

Arusha Crown Hotel ilikuwa hoteli nzuri ya kisasa iliyokuwa katikati ya jiji la Arusha, katika barabara ya Makongoro jirani kabisa na Uwanja wa Mpira wa Sheikh Amri Abeid Kaluta.

Baada ya kuamka Carlos hakuzubaa, alifahamu nini maana ya kuzingatia muda, alielekea haraka bafuni na kujimwagia maji. Ilimchukua muda mfupi sana kuoga na muda mfupi baadaye alikuwa amemaliza kujiandaa huku akiwa katika mwonekano bomba wa suti nzuri ya gharama iliyokuwa na rangi ya kijivu, shati la rangi ya samawati, tai ya rangi ya bluu na viatu vyeusi vya ngozi.

Alipotoka hotelini aliendesha gari lake kama kichaa katika barabara ya Makongoro, akavuka Uhuru Roundabout na kusonga mbele hadi alipoipata AICC Roundabout, akakunja kuingia kushoto akilipita jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa hadi katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Arusha (AICC).

Alipoteremka kwenye gari lake alitembea kama mtu aliyekuwa anakimbia akiwahi kwenye mkutano wa wafanyabiashara na wadau wa madini uliokuwa ukifanyika AICC na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndiye alikuwa mgeni rasmi.

Mkutano ule ulikuwa umeandaliwa na Shirikisho la Wafanyabiashara wa Madini Tanzania kujadili kero na tozo mbalimbali, na yeye alikuwa mmoja wa wafanyabiashara wa madini walioalikwa kwenye mkutano ule.

Katika jengo lile la AICC Carlos aliendelea kutembea kwa kasi ile ile na kama ingetokea angejikwaa basi angeweza kupata ajali mbaya sana. Alipokuwa akikata kona kuingia kwenye korido iliyokuwa ikielekea kwenye ukumbi ule wa mikutano, akiwa katika mwendo ule ule ghafla alishtukia anagongana na mwanadada mmoja aliyekuwa akija mbele yake na kila mmoja aliangusha vitu alivyokuwa amebeba mkononi.

Yule mwanadada aliangusha simu yake aina ya Samsung Galaxy S8 na Carlos aliangusha simu yake aina ya Iphone X na briefcase yake ndogo nyeusi iliyokuwa na nyaraka zake muhimu.

Carlos alimtazama yule mwanadada na hapo macho yake hayakuamini kile alichokuwa amekiona, alikuwa akitazamana na msichana mrefu mrembo sana aliyekuwa amevalia suti nadhifu ya kike ya rangi ya bluu iliyokolea ya ‘single button’ iliyokuwa imemkaa vyema na kumpendeza sana na viatu vyenye vikanyagio virefu vya mchuchumio.

Yule mrembo alimtazama Carlos kwa hasira na kuduwaa kisha aliyapeleka macho yake kuiangalia simu yake ya Samsung Galaxy S8 iliyoanguka pale sakafuni. Wakati huo huo Carlos aliinamisha mgongo wake na kuiokota ile simu kisha akamkabidhi yule mrembo huku naye akiendelea kuokota simu na briefcase yake.

“Samahani sana, bibie, sikukusudia…” Carlos alijaribu kujitetea baada ya kumuona yule mrembo akimtazama pasipo kuonesha tashwishwi yoyote. Yule mrembo alibaki kimya akionekana kuduwaa huku akimtazama Carlos.

“Sijui simu imeumia, anti?” aliuliza huku akimtazama kwa makini. Yule mrembo alishusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Usijali, ipo sawa,” hatimaye yule mrembo alisema huku akiiwasha ile simu yake iliyokuwa imezima.

Carlos alistaajabishwa na sauti laini ya yule mrembo iliyovunjika ilipenya sawia kwenye ngoma za masikio yake, ukichanganya na macho yake yaliyolegea, vyote kwa pamoja vilitoa haiba ya kike ndani mwa yule mrembo na kummwaia Carlos.

Macho ya Carlos yaliganda kwenye sura ya yule mrembo huku akionekana kusahau kabisa kuwa alikuwa amechelewa kwake kwenye mkutano wa wafanyabiashara na wadau wa madini. Yule mrembo alipohakikisha kuwa simu yake haikuwa na tatizo, aliminya midomo yake na kumtupia jicho Carlos na kuanza kupiga hatua kwa madaha kuondoka eneo lile.

Itaendelea...
 
Kizungumkuti! - 3

Na Bishop Hiluka

Macho ya Carlos yaliganda kwenye sura ya yule mrembo huku akionekana kusahau kabisa kuwa alikuwa amechelewa kwake kwenye mkutano wa wafanyabiashara na wadau wa madini. Yule mrembo alipohakikisha kuwa simu yake haikuwa na tatizo, aliminya midomo yake na kumtupia jicho Carlos na kuanza kupiga hatua kwa madaha kuondoka eneo lile.

Ile suti aliyokuwa amevaa ilikuwa imembana kidogo mwili wake na hivyo kusababisha mistari ya chupi iweze kujichora kwenye ule mzigo wa makalio, na utembeaji wake uliwafanya wanaume waliopishana naye kumtazama kwa matamanio na wala hakuna aliyejuta kumwangalia.

Mwondoko wake na mwili wake ulivyokuwa ukitingishika ulizidi kumfanya azidi kuvutia na ilikuwa kama vile alikuwa anaamua vile kwani mwendo wake na sauti ya vile viatu vye visigino virefu alivyokuwa amevaa vilikuwa vinaendana hasa. Na ilikuwa ni bahati sana kwa macho ya mwanamume yeyote kuona kiumbe kama yule wa shani akipita mbele yake.

Carlos aliduwaa akabaki mdomo wazi akimsindikiza kwa macho hadi alipomuona akiiingia kwenye mlango mmoja uliokuwa na maneno ‘Staff Only’ juu yake na kuacha gumzo kule nyuma. Kila mwanamume aliyepishana naye alitamani angalau angeisikia hata sauti yake tu.

Carlos alizinduka na kuanza kutembea kwa kasi ile ile ili kuwahi kwenye ule ukumbi wa mikutano kwa ajili ya mkutano. Baada ya mkutano ule kumalizika Carlos alirejea hotelini alikofikia lakini akiwa na mawazo mengi kuhusu yule mrembo aliyegongana naye asubuhi.

Walipotoka kwenye mkutano alimtafuta rafiki yake, Godlove Kimaro aliyekuwa akiishi hapo jijini Arusha, alimweleza kuhusu yule mrembo na kumpa kazi ya kufuatilia taarifa zote za yule mrembo na ikibidi amlete hotelini kwake huku akimuahidi kumpa fedha nyingi kuliko ambazo amekuwa akimpa endapo angefanikiwa.

Aliazimia kutoondoka jijini Arusha pasipo kuonana na yule mrembo hata kama ingemchukua wiki mbili. Hata hivyo, jioni ya saa kumi na mbili ya siku ya pili Kimaro alimpigia simu na kumpa habari njema kuwa kila kitu kilikuwa safi.

Alimweleza yote aliyotaka kuyafahamu kuwa yule mrembo aliitwa Jackline Mgaya, alikuwa msomi aliyefanya kazi pale AICC na hakuwa ameolewa. Alimweleza mengi kumhusu Jacky ambayo yalizidi kumsisimua Carlos na kwamba baada ya kumwimbisha sana Jacky hatimaye alikuwa amekubali kuonana naye siku iliyofuata saa kumi na mbili jioni pale pale hotelini.

Kwa habari zile Carlos alijikuta akitokwa na kijasho chembamba sehemu mbalimbali za mwili wake, huku akihisi ubaridi fulani wa woga wa aina yake ukimtambaa mwilini na mapigo ya moyo wake yakibadili mwendo wake na kwenda mbio isivyo kawaida!

Siku iliyofuata saa kumi na mbili jioni Carlos alikuwa chumbani kwake amejipumzisha, akitazama runinga na pembeni yake kwenye meza ndogo ya kioo kulikuwa na chupa kubwa ya Whisky na bilauri.

Chumba chake kilikuwa kikubwa na kizuri cha kifahari, kilikuwa na kitanda kikubwa cha samadari cha futi sita kwa sita, cha mbao ngumu za mninga, chenye droo mbili kila upande kilichokuwa katikati ya chumba.

Juu ya zile droo kulikuwa na taa mbili za rangi nyekundu na mbele ya kitanda hicho kulikuwa na seti nzuri ya runinga pana aina ya LG ya inchi hamsini na mbili na chini yake kulikuwa na meza nzuri nyeusi ya kioo. Juu ya ile meza kulikuwa na simu yake ya kisasa ya Iphone X na kando ya ile meza kulikuwa na briefcase yake nyeusi.

Upande wa kulia wa kile chumba kulikuwa na jokofu dogo la vinywaji lililokuwa kwenye kona ya chumba, na hatua chache kutoka kwenye lile jokofu hilo kulikuwa na dirisha pana la kioo lililokuwa limefunikwa kwa pazia zito na refu lenye nakshi za michoro ya maua yaliyodariziwa vizuri na kuyafanya yapendeze.

Pia kulikuwa na kabati kubwa la kisasa la nguo ambalo lilikuwa limefungwa muda huo na pembeni ya lile kabati hilo kulikuwa na kochi moja kubwa la sofa na meza ya kioo mbele yake iliyokuwa na chupa kubwa ya Whisky na bilauri moja.

Kando ya lile sofa kulikuwa na meza fupi ya mbao iliyokuwa simu ya mezani na kitabu kidogo chenye orodha ya majina ya watu na kampuni zilizotumia huduma ya simu ile ya mezani na kwenye kona ya chumba hicho upande wa kushoto kabisa kulikuwa na mlango wa kuelekea kwenye chumba kidogo cha maliwato na bafu.

Chini sakafuni kulikuwa na zulia nene lililokuwa na mchanganyiko wa maua ya rangi mbalimbali yaliyolifanya kuvutia. Akiwa ameketi alisikia mlango wa chumba chake ukigongwa taratibu, Carlos aligeuza shingo yake kuutazama ule mlango kwa shauku.

Aliinuka haraka na kuufungua kidogo huku akichungulia nje, macho yake yakagongana na macho ya kimaro ambaye alimfanyia ishara kuwa alikuwa na mgeni, Carlos aliufungua mlango huku akirudi nyuma kuwapisha waingie.

Kimaro aliingia na kufuatiwa na Jacky aliyeingia mle ndani akiwa na wasiwasi kidogo. Kwa sekunde kadhaa Carlos alibaki ameduwaa akimtazama Jacky aliyekuwa amesimama huku akitazama chini kwa aibu.

Jacky alikuwa amevaa amevaa sketi fupi nyekundu iliyokuwa na miraba myeupe na bluu iliyoyashika vyema mapaja yake yaliyonona yaliyokuwa yameshikiliwa na hipsi pana na huko nyuma kukiwa na mzigo wa haja wa makalio.

Juu alivaa blauzi ya nyeupe ya mikono mirefu na viatu vyenye vikanyagio virefu vya mchuchumio na begani alikuwa ametundika mkoba mzuri wa ngozi ya pundamilia ambao ulionekana kumgharimu fedha nyingi.

Oh my Gosh! What a beautifull angel…” (Mungu wangu! Urembo wa kimalaika…) Carlos alijikuta akiwaza huku akiendelea kumkazia macho Jacky. Alizidi kuchanganywa na uzuri wa Jacky na alikiri kuwa asubuhi hakuwa amemchanganyia vizuri macho.

Kimaro was right. Jacky ana uzuri wa kipekee mno. Katika wasichana wote ambao amewahi kuniletea kila ninapokuja hapa jijini Arusha hajawahi kumleta msichana mrembo kama huyu,” Carlos aliendelea kuwaza huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.

“Boss, kutana na Jackline Mgaya,” Kimaro alimzindua Carlos kutoka kwenye mawazo.

“Jacky, huyu ndiye Boss wangu anaitwa Carlos Mwamba, nadhani mlishakutana asubuhi pale AICC,” Kimaro akaendelea na utambulisho.

Itaendelea...
 
Kizungumkuti! - 4

Na Bishop Hiluka

“Boss, kutana na Jackline Mgaya,” Kimaro alimzindua Carlos kutoka kwenye mawazo.

“Jacky, huyu ndiye Boss wangu anaitwa Carlos Mwamba, nadhani mlishakutana asubuhi pale AICC,” Kimaro akaendelea na utambulisho.

Jacky aliinua uso wake kumtazama Carlos usoni kisha akanyoosha mkono wake kumsalimia Carlos kwa adabu huku akiyakwepesha macho yake yalijaa aibu.

“Hello, Mr Mwamba,” Jacky alisema kwa sauti tulivu na nyororo iliyotosha kabisa kumtoa nyoka pangoni huku akiachia tabasamu bashasha.

“Hello! Karibu sana Jacky, nimefurahi kukuona tena,” Carlos alisema huku akilamba midomo yake iliyoanza kukauka.

“Hata mimi nimefurahi kukutana tena na wewe, Mr Mwamba,” alisema Jacky huku akiangalia chini kwa aibu, alionekana kuwa hawezi kumtazama mwanamume usoni kwa sekunde tatu mfululizo bila kukwepesha macho yake na kutazama kando kwa jinsi alivyojaa haiba na aibu. Carlos akamtazama Kimaro na kumpiga ukope.

“Kimaro, asante kwa kumfikisha mgeni wangu, sasa nenda kamuone yule binti wa mapokezi ana ujumbe wako,” Carlos alisema na Kimaro akaondoka bila kusubiri kwani alikwisha elewa kuwa fedha yake ilikuwa imeachwa pale mapokezi.

Carlos akamkaribisha Jacky kwenye sofa lililokuwa mle chumbani huku yeye akienda moja kwa moja kwenye jokofu dogo lililokuwemo mle ndani aambalo lilisheheni vinywaji mbalimbali.

“Jacky, sijui unatumia kinywaji gani?” aligeuza shingo yake akamuuliza Jacky.

Anything that you can choose for me, Mr Mwamba,” (Chochote unachoweza kunichagulia) Jacky aliasema kwa sauti laini iliyozidi kumpagawisha Carlos na kuachia tabasamu pana.

Carlos alilamba midomo yake na kuchukua bilauri, kisha akarudi pale kwenye meza ndogo na kuchukua ile chupa kubwa ya Whisky na kumimina katika bilauri akampatia Jacky.

“Karibu sana Jacky, Nina furaha kubwa mno kuwa nawe kwa usiku huu,” Carlos alisema huku akipiga funda kubwa la mvinyo na kuonesha kusisimkwa.

“Hata hivyo, ninatamani sana kukufahamu zaidi, Jacky,” alisema tena Carlos baada ya kuikita juu ya meza ile bilauri.

“Unahitaji kufahamu kitu gani kuhusu mimi, Mr Mwamba?” Jacky aliuliza huku akikwepesha macho yake na kutazama kando kwa aibu.

Just call me Carlos. I need to know everything about you… your life, relationship, everything,” (Niite Carlos tu. Nahitaji kujua kila kitu kukuhusu… maisha yako, uhusiano, kila kitu) Carlos alisema huku akimkazia macho Jacky.

Why do you want to know about my life and everything? Is this an interrogation,” (Kwa nini unataka kujua kuhusu maisha yangu na kila kitu? haya ni mahojiano?) Jacky alisema huku akimtupia jicho Carlos akionesha kuwa na aibu.

Not an interrogation… (Siyo mahojiano…) ni kwamba nina sababu zangu binafsi za kutaka kukufahamu kiundani,” Carlos alisema huku akinywa funda kubwa la mvinyo.

Can you tell me what the reasons are?” (Unaweza kuniambia ni sababu zipi) Jacky aliuliza huku akimtazama Carlos kwa macho yake yaliyolegea.

The only reason is that, I’m looking for a wife, (Sababu pekee ni kwamba, natafuta mke) na umebeba sifa zote za mwanamke anayefaa kuwa mke wangu,”

Wife?” (Mke?) Jacky aliuliza kwa mshtuko.

Yes a wife,” (Ndiyo, mke) Carlos alijibu kwa sauti tulivu huku akimtazama Jacky kwa makini.

A handsome guy like you, you are still single up to now, or you want me to be your second wife?” (Mwanamume mtanashati kama wewe bado hujaoa hadi sasa, au unataka kunifanya mke wa pili?)” Jacky aliuliza tena huku akiendelea kumkazia macho Carlos.

Trust me, I'm not married, and if you’re ready I’ll make you the most beautifull woman in the world. I’ll give you all luxuries,” (Niamini, sijaoa, na kama uko tayari nitakufanya mrembo kuliko wanawake wote duniani. Nitakupa starehe zote) Carlos alisema kwa kujigamba na kumfanya Jacky aangue kicheko hafifu.

Jacky, I’m serious about this. It’s not a joke,” (Jacky, niko siriazi. Huu siyo utani) Carlos alisisitiza baada ya kuona Jacky anacheka.

You don’t have to tell me, I can see it in your eyes…” (Wala huhitaji kuniambia, macho yako tu yanaongea…) alisema Jacky.

But, are you sure that you love me and you want to marry me?” (Lakini una hakika unanipenda na unataka kunioa?) Jacky aliuliza.

Yes, I’m ready anytime and any day,” (Ndiyo, tena niko tayari muda wowote na siku yoyote) carlos aliongea kwa kujiamini huku akimtulizia macho Jacky bila kupepesa macho.

Jacky alimtazama kwa makini sana kwa kitambo kirefu, ilikuwa ni kama vile alikuwa akiyasoma mawazo yake.

What you need from me is a difficult thing, it’s about my life and yours…” (Jambo unalohitaji kwangu ni jambo gumu linalohusu maisha yangu na yako vilevile…) Jacky alisema kwa sauti ya tulivu huku akimtazama Carlos kwa makini.

“Kwa hiyo, halihitaji uamuzi wa papara, tunahitaji muda wa kufahamiana zaidi,” aaliongeza na kunyanyua bilauri ya mvinyo, akapiga funda kubwa na kuusikilizia wakati ulipokuwa ukiteremka tumboni.

So what do you say?” (Kwa hiyo unasemaje?) Carlos aliuliza kwa sauti ya chini.

Say what?” (Kusema nini?) Jacky akauliza huku akimtazama Carlos kwa mshangao.

About tonight, will you spend this night with me? I need you so badly!” (Kuhusu usiku wa leo, tutakuwa wote usiku wa leo? Nakuhitaji vibaya sana!).

It’s okay, but if you need love and comfort from me I’m ready to give you but not in exchange for money,” (Sawa, lakini kama unahitaji penzi na faraja kutoka kwangu niko tayari lakini si kwa kwa fedha) akasema Jacky.

Waliendelea na maongezi na mwishowe wakajikuta wakiwa kitandani, muda ule taa mbili za rangi nyekundu zilikuwa zinatoa mwanga hafifu wenye mg’ao na kufanya nusu ya chumba kuwa kizani.

Muda huo Carlos alikuwa amefumba macho yake huku akisikia raha ya aina yake wakati mikono ya Jacky ikichezea ikulu.

Ooh Jacky… ooh… aah...” Carlos alilalama lakini Jacky hakumjali, aliendeleza utundu wake kwa kutumia mikono halafu taratibu akapiga magoti na kuanza manjonjo kwa kutumia mdomo wake, jambo lililomfanya Carlos atamani kupiga kelele kwa raha aliyoipata.

Haukupita muda Carlos alijikuta akiwa katika hali mbaya na hakuweza tena kuvumilia, hivyo wakaingia ulingoni. Ulikuwa ni mpambano mkali kila mmoja akionesha ufundi na kutaka kuutawala mchezo.

Walibadili kila aina ya mfumo wa uchezaji ili mradi kujihakikishia ushindi mnono mwisho wa mchezo, Jacky alijitahidi kumwonesha Carlos mautundu aliyokuwa nayo na kumfanya kutoa miguno kwa raha aliyojisikia huku akimimina ahadi nyingi ambazo aliapa kuwa angezitekeleza. Hadi dakika tisini wote walikuwa hoi wakitweta kama wakimbiaji wa mbio ndefu.

Itaendelea...
 
Kizungumkuti! - 5

Na Bishop Hiluka

Walibadili kila aina ya mfumo wa uchezaji ili mradi kujihakikishia ushindi mnono mwisho wa mchezo, Jacky alijitahidi kumwonesha Carlos mautundu aliyokuwa nayo na kumfanya kutoa miguno kwa raha aliyojisikia huku akimimina ahadi nyingi ambazo aliapa kuwa angezitekeleza. Hadi dakika tisini wote walikuwa hoi wakitweta kama wakimbiaji wa mbio ndefu.

Thank you, Carlos, you said you wanted me so badly,” (Asante, Carlos, ulisema unanihitaji vibaya sana) alisema Jacky huku akitweta kwa nguvu.

“Jacky…” Carlos alitaka kusema neno lakini Jacky akamwekea kidole mdomoni akimzuia kusema.

You don’t have to say anything, Carlos,” (Huhitaji kusema chochote, Carlos) alisema Jacky huku akirembua macho yake.

Yeah, but spend this night with me, Jacky. I still need you so badly, you are wonderfull woman,” (Ni kweli, lakini kesha nami usiku huu, Jacky. Bado nakuhitaji vibaya sana, hakika wewe ni mwanamke wa ajabu) alisema Carlos kwa sauti nzito ya chini iliyokuwa na kitetemeshi.

Tangu siku ile mapenzi yao yalinoga, hasa baada ya kugundua kuwa walikuwa na vitu vingi walivyofanana, ikiwemo wote kupata mafunzo ya kujihami, wote walikuwa wasomi wenye ujasiri katika kuyakabili mambo, wote walikuwa na kiu ya kutafuta pesa kwa hali yoyote na wote walikuwa na utaalamu wa masuala ya teknolojia.

Carlos alikuwa amehitimu Shahada ya System Analysis na Jacky alikuwa amehitimu Shahada ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Information Technology).

Kila mwisho wa wiki Carlos aliruka kwa ndege kutoka jijini Dar es Salaam na kwenda jijini Arusha, na baadaye Jacky alikuwa akija jijini Dar es Salaam na kukaa siku mbili kisha aliruka na ndege kurudi Arusha, na baada ya miezi kadhaa ya kuchunguzana hatimaye walikubaliana kuoana huku Jacky akiacha kazi pale AICC…

______

Carlos alizinduliwa kutoka kwenye yale mawazo na dada mmoja wa kampuni ya maegesho ya magari aliyekuwa akiweka karatasi ya madai kwenye kioo kikubwa cha mbele cha gari lake.

* * * * *

Jacky alikuwa ameingia ndani ya jengo lile la benki na kusimama, akazungusha macho yake kutazama huku na kule kisha alikwenda moja kwa moja hadi kwenye dirisha namba tatu la kaunta ya ile benki. Alifika pale kaunta na kusimama nyuma ya mteja mmoja mwanamume mtu mzima aliyekuwa ameegemea kaunta ile.

Nyuma ya ile kaunta kulikuwa na kijana mmoja mtanashati sana, mrefu na mwembamba aliyekadiriwa kuwa na miaka therathini. Kijana yule alikuwa amevaa sare za kazi: suruali ya rangi ya bluu, shati jeupe lenye kola ya rangi ya bluu bahari na nembo ya benki ile upande wa kushoto wa kifua chake.

Pia alikuwa amevaa koti la suti ya rangi ya bluu na shingoni alikuwa amevaa tai ndogo ya bluu iliyokuwa na nembo ya ile benki. Yule kijana aliitwa Yusuf na alikuwa ‘busy’ akimhudumia yule mteja wa benki mtu mzima aliyekuwa ameegemea kaunta.

Yusuf alimtupia jicho Jacky na kwa nukta kadhaa na kupata mshtuko, alijikuta akiuajabia uzuri wa Jacky uliokuwa mbele ya macho yake na kusahau kidogo kumhudumia yule mteja huku akiduwaa, aliendelea kukodoa macho yake kwa kitambo fulani.

Yule mteja mtu mzima aliyekuwa akihudumiwa na Yusuf baada ya kumuona Yusuf kaduwaa, aligeuza shingo yake kutazama kule ambako macho ya Yusuf yalikuwa yakitazama na kukutana na uso wa Jacky uliokuwa umepambwa na tabasamu bashasha.

Yule mzee akajikuta akiachia tabasamu zuri la kirafiki huku akishusha pumzi ndefu za ndani kwa ndani.

Jacky aliinamisha uso wake kuangalia sakafuni kwa aibu baada ya kuona macho ya wanaume wawili yakimtazama kwa mshangao, kisha aliufungua mkoba wake na kutoa kadi ndogo, akaishika kwa uficho mkononi mwake huku akiufunga ule mkoba, akaendelea kusubiri zamu yake ifike.

Yusuf alishusha pumzi za ndani kwa ndani na kuendelea kumhudumia yule mzee, muda huo huo Jacky aliamua kugeuza shingo yake kuwatazama wateja waliokuwemo ndani ya ile benki na kuhisi kijasho chembamba kikimtoka licha ya kuwa mle ndani ya ile benki kulikuwa na viyoyozi vilivyokuwa vikitoa ubaridi mkali uliowafanya baadhi ya wateja kujikunyata kwa baridi.

Moyo wake ulikuwa umeanza kupoteza utulivu kabisa huku kijasho chepesi kikizidi kumtoka sehemu mbalimbali za mwili wake, alianza kushangaa kukutwa na hali ile wakati alikuwa amekwisha fanya mambo makubwa na ya hatari kuliko lile alilokuwa anatarajia kulifanya.

C’mon, Jacky, just relax,” alijipa moyo akijiambia atulie na asiwe na wasiwasi, alivuta pumzi ndefu za ndani kwa ndani kisha akazishusha taratibu huku akiminya midomo yake yenye maki, na kutoa kitambaa chake laini kilichokunjwa kwa umaridadi kutoka kwenye mkoba wake, akajifuta jasho.

Aliporudisha kitambaa kwenye mkoba akaitupia jicho saa yake ya mkononi aina ya Cartier La Dona na kushusha tena pumzi ndefu za ndani kwa ndani.

“Habari yako, dada?” Jacky alishtuliwa na salamu kutoka kwa yule mfanyakazi wa benki baada ya yule mteja mtu mzima kuondoka, yule mfanyakazi alikuwa akimtazama Jacky kwa hamu na kwa tabasamu.

“Nzuri tu, kaka Yusuf, hujambo?” alisema Jacky huku akiachia tabasamu na pembe za midomo yake zikafinya, kisha tabasamu lake likageuka kuwa kicheko hafifu.

Yusuf alionekana kushituka kidogo, akamtazama Jacky kwa makini huku akijitahidi kuwa mtulivu. Jacky aliendelea kutabasamu.

“Umelijuaje jina langu?” hatimaye Yusuf aliuliza kwa udadisi huku akizidi kumkazia macho Jacky.

Jacky aliangua tena kicheko hafifu na kunyoosha kidole chake kuonesha beji maalumu iliyokuwa imechomekwa kwenye shati la Yusuf katika kifua chake ikiwa imeandikwa jina lake.

"Si hiyo beji uliyovaa kwenye shati lako. Au wewe siyo Yusuf?" alisema Jacky huku akiwatupia jicho wateja wengine waliokuwa wakihudumiwa kwenye kaunta zingine.

"Hmm, mimi ndiye. Karibu sana, sijui nikusaidie nini, dada…?" alisema Yusuf na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

Jacky alitoa tena kitambaa chake na kufuta jasho jepesi lililokuwa likimtoka, akageuza shingo yake kuwatazama wateja waliokuwemo ndani ya ile benki kisha akampenyezea Yusuf ile kadi kwa uficho akihakikisha hakuna mtu mwingine zaidi ya Yusuf aliyeona kitendo kile.

Itaendelea...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom