Bishop Hiluka
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 7,140
- 14,678
Kizungumkuti!
Na Bishop Hiluka
“Hii ni trela tu, picha kamili keshokutwa! Hakyamungu keshokutwa hakai mtu hapa… mi naapa! Nitakunywa na nitatembea uchi ukumbi mzima kama mademu wakinimaindi poa tu, au vipi kichaa wangu?” Kabwe alipiga kelele kilevi, wakati huo huo Liston alikuwa analazimisha kumshika matiti dada mmoja aliyepita karibu yake…
Fuatilia stori hii hadi mwisho ya kusisimua kuyajua yote yanayoleta kizungumkuti...
KATIKATI ya jiji la Dar es Salaam hali ya hewa ilikuwa ya joto sana kama kawaida, hata katika majira yale ya saa tano za asubuhi. Asubuhi ile pilika pilika za watu zilikuwa zimeshamiri katikati ya jiji hilo kubwa zaidi Tanzania, na hivyo kulifanya kuchangamka sana kama ilivyokuwa kawaida yake.
Katika eneo la Mnazi Mmoja, barabara ya Lumumba kulionekana msululu mrefu wa magari, zikiwemo daladala zilizokuwa zikizunguka kutokea mtaa wa Uhuru katika kituo cha daladala cha Mnazi Mmoja na kupita barabara ya Bibi Titi kabla hazijaingia katika mtaa wa Mkunguni na kisha kutokea barabara ya Lumumba.
Katika barabara ile ya Lumumba, gari dogo la kifahari aina ya BMW X6 xDrive 50i la rangi ya samawati lililotokea katika barabara ya Morogoro kwa mwendo wa taratibu na kujiunga katika msululu ule, kisha lilichepuka na kwenda kusimama chini ya miti ya kivuli iliyokuwa imepandwa kando ya ile barabara.
Hata hivyo, dereva wa gari lile alionekana kutoridhika na eneo lile, akaanza kutafuta sehemu nzuri zaidi na baadaye alikwenda kuliegesha gari lake kwenye eneo lililokuwa na magari mengine mawili matatu yaliyokuwa yameegeshwa pale, na vijana kadhaa walionekana wakiosha magari.
Vijana wawili waosha magari walimfuata haraka yule dereva wa lile gari na kuonekana kumzonga, kila mmoja alionekana akitaka apewe tenda ya kuosha lile gari lakini yule dereva hakuonekana kuwajali. Alibaki ametulia kimya akiusikilizia muungurumo laini wa lile gari kwa kitambo kirefu.
Ndani ya gari lile kulikuwa na watu wawili tu, mwanamume mmoja ambaye ndiye aliyekuwa akiendesha lile gari na mwanadada mrembo sana ambaye alikuwa ameketi pembeni yake kwenye siti ya abiria.
Yule mwanamume alikadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka arobaini na arobaini na tano. Alikuwa mrefu wa futi sita na ushee, mweusi na shababi kwelikweli aliyekuwa na mwenye mwili uliojengeka kwa misuli.
Macho yake yalikuwa makali na alikuwa amevaa kofia ya rangi ya bluu aina ya kapelo, t-shirt ya pundamilia iliyokuwa na miraba ya bluu na myeupe aina ya form six na suruali ya jeans ya rangi ya bluu. Miguuni alikuwa amevaa buti ngumu za ngozi zilizokuwa na rangi nyeusi.
Mwanamume yule aliitwa Carlos Mwamba na aliendelea kutulia kwenye siti yake nyuma ya usukani akiwa ameibana njiti moja ya kiberiti kwenye pembe ya mdomo wake, huku akiendelea kuusikilizia muungurumo laini wa lile gari.
Kushoto kwa Carlos Mwamba, kwenye ile siti ya mbele ya abiria yule mrembo aliyekuwa ameketi aliitwa Jackline Mgaya na alikuwa mke wa ndoa wa Carlos, wakiwa wameoana takriban miaka mwili iliyokuwa imepita.
Jackline au kama alivyopenda kujulikana kwa kifupi kwa jina la Jacky alikuwa na umri usiozidi miaka therathini, alikuwa mrefu na mweupe mwenye haiba nzuri ya kuvutia sana.
Alikuwa na nywele nyeusi za kibantu alizokuwa amezikata vizuri na kubaki ndogo ndogo na hivyo kumfanya aonekane mzuri wa asili. Alikuwa na sura yake ya duara na macho makubwa ya kike na legevu yaliyokuwa yamezungukwa na kope ndefu na nyeusi.
Pua yake ilikuwa ndogo na iliyochongoka mfano wa pua ya kihabeshi na mdomo yake ilikuwa laini yenye maki na kingo pana kiasi zilizokuwa zimekolezwa kwa lipstick ya rangi ya chocolate pamoja na vishimo vidogo mashavuni mwake vilimfanya azidi kuonekana mrembo zaidi.
Jacky alikuwa na masikio madogo yasiyochusha aliyokuwa ameyatoga na kuyavalisha hereni kubwa za kitamaduni zilizokuwa na umbo la mviringo. Alikuwa amevaa blauzi nyepesi ya arangi ya pinki iliyoyaficha vyema matiti yake imara yenye ukubwa wa wastani yaliyokuwa na chuchu nyeusi imara zilizosimama kikamilifu ndani ya blauzi ile.
Shingoni alikuwa kavaa mkufu mwembamba wa dhahabu uliokuwa umeizunguka ile shingo nyembamba na kidani cha dhahabu kilichokuwa na herufi ya “J” kilikuwa kimepotelea katikati ya uchochoro mdogo wa yale matiti.
Kwenye mkono wake wa kushoto alikuwa amevaa bangili kadhaa za pembe na vidole vyake viwili vya mkono huo alikuwa amevaa pete ndogo za madini ghali ya tanzanite na green tourmaline.
Mkono wake wa kulia alivaa saa ndogo ghali na nzuri ya kike aina ya Cartier La Dona, ambayo bei yake ilikuwa si haba kama angeamua kuibadili kwa pesa za madafu, kwani ilikuwa imemgharimu kiasi cha dola za Marekani 137,000.
Cartier La Dona Watch ilikuwa ni saa ghali sana iliyotengenezwa kwa madini ya dhahabu nyeupe ya Karati 18 ikiwa na kesi imara iliyokuwa na milimita 27 kwa 29 na mkanda wake pia ulikuwa umetengenezwa kwa dhahabu nyeupe, ikiwa na gerentii ya miaka hamsini.
Alikuwa ameinunua nchini Switzerland walipokwenda kwenye fungate muda mfupi tu baada ya ndoa yao iliyoacha gumzo jijini Arusha na kwenye viunga vyake.
Gari ikiwa bado inaunguruma taratibu Jacky alishusha pumzi za ndani kwa ndani na kutazama nje kwa kitambo fulani huku macho yake yakielekea moja kwa moja kwenye jengo la ghorofa la Benki ya Biashara.
Alilitazama lile jengo kwa makini akionekana kama aliyekuwa akijiuliza jambo kuhusiana na lile jengo, kisha aliyashusha macho yake kuutazama mkoba wake mzuri wa kike wa rangi ya pinki uliokuwa umelala juu ya mapaja yake mazuri.
Aliufungua ule mkoba na kutoa humo mkebe mdogo wa duara wa rangi nyekundu kisha aliinua macho yake kujitazama kwa kitambo kifupi kwenye kioo cha lile gari cha katikati kinachotumika kuangalia nyuma huku akigeuza geuza uso wake pembe zote.
Alikunja uso wake huku akiminya midomo yake mizuri yenye maki, na hapo mashavu yake yakapiga misingi, pembe za midomo yake zikafinya, akashusha pumzi ndefu za ndani kwa ndani huku akigeuka kumtazama Carlos aliyekuwa ametulia tuli kama maji mtungini na kuachia tabasamu bashasha.
Carlos aliendelea kutulia pale nyuma ya usukani akionekana kuwaza mbali sana, alimtupia jicho Jacky mara moja tu, kisha akayahamisha macho yake na kutazama kwenye lile jengo la Benki ya Biashara huku sura yake ikiwa haioneshi tashwishwi yoyote.
Jacky alimtazama Carlos kwa makini kisha akaufungua ule mkebe akatoa vipodozi na kuanza kujiremba akiongezea urembo kwenye sura yake huku akijitazama kwenye kile kioo cha gari cha katikati kinachoonesha nyuma.
Itaendelea...
Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY
Na Bishop Hiluka
“Hii ni trela tu, picha kamili keshokutwa! Hakyamungu keshokutwa hakai mtu hapa… mi naapa! Nitakunywa na nitatembea uchi ukumbi mzima kama mademu wakinimaindi poa tu, au vipi kichaa wangu?” Kabwe alipiga kelele kilevi, wakati huo huo Liston alikuwa analazimisha kumshika matiti dada mmoja aliyepita karibu yake…
Fuatilia stori hii hadi mwisho ya kusisimua kuyajua yote yanayoleta kizungumkuti...
KATIKATI ya jiji la Dar es Salaam hali ya hewa ilikuwa ya joto sana kama kawaida, hata katika majira yale ya saa tano za asubuhi. Asubuhi ile pilika pilika za watu zilikuwa zimeshamiri katikati ya jiji hilo kubwa zaidi Tanzania, na hivyo kulifanya kuchangamka sana kama ilivyokuwa kawaida yake.
Katika eneo la Mnazi Mmoja, barabara ya Lumumba kulionekana msululu mrefu wa magari, zikiwemo daladala zilizokuwa zikizunguka kutokea mtaa wa Uhuru katika kituo cha daladala cha Mnazi Mmoja na kupita barabara ya Bibi Titi kabla hazijaingia katika mtaa wa Mkunguni na kisha kutokea barabara ya Lumumba.
Katika barabara ile ya Lumumba, gari dogo la kifahari aina ya BMW X6 xDrive 50i la rangi ya samawati lililotokea katika barabara ya Morogoro kwa mwendo wa taratibu na kujiunga katika msululu ule, kisha lilichepuka na kwenda kusimama chini ya miti ya kivuli iliyokuwa imepandwa kando ya ile barabara.
Hata hivyo, dereva wa gari lile alionekana kutoridhika na eneo lile, akaanza kutafuta sehemu nzuri zaidi na baadaye alikwenda kuliegesha gari lake kwenye eneo lililokuwa na magari mengine mawili matatu yaliyokuwa yameegeshwa pale, na vijana kadhaa walionekana wakiosha magari.
Vijana wawili waosha magari walimfuata haraka yule dereva wa lile gari na kuonekana kumzonga, kila mmoja alionekana akitaka apewe tenda ya kuosha lile gari lakini yule dereva hakuonekana kuwajali. Alibaki ametulia kimya akiusikilizia muungurumo laini wa lile gari kwa kitambo kirefu.
Ndani ya gari lile kulikuwa na watu wawili tu, mwanamume mmoja ambaye ndiye aliyekuwa akiendesha lile gari na mwanadada mrembo sana ambaye alikuwa ameketi pembeni yake kwenye siti ya abiria.
Yule mwanamume alikadiriwa kuwa na umri wa kati ya miaka arobaini na arobaini na tano. Alikuwa mrefu wa futi sita na ushee, mweusi na shababi kwelikweli aliyekuwa na mwenye mwili uliojengeka kwa misuli.
Macho yake yalikuwa makali na alikuwa amevaa kofia ya rangi ya bluu aina ya kapelo, t-shirt ya pundamilia iliyokuwa na miraba ya bluu na myeupe aina ya form six na suruali ya jeans ya rangi ya bluu. Miguuni alikuwa amevaa buti ngumu za ngozi zilizokuwa na rangi nyeusi.
Mwanamume yule aliitwa Carlos Mwamba na aliendelea kutulia kwenye siti yake nyuma ya usukani akiwa ameibana njiti moja ya kiberiti kwenye pembe ya mdomo wake, huku akiendelea kuusikilizia muungurumo laini wa lile gari.
Kushoto kwa Carlos Mwamba, kwenye ile siti ya mbele ya abiria yule mrembo aliyekuwa ameketi aliitwa Jackline Mgaya na alikuwa mke wa ndoa wa Carlos, wakiwa wameoana takriban miaka mwili iliyokuwa imepita.
Jackline au kama alivyopenda kujulikana kwa kifupi kwa jina la Jacky alikuwa na umri usiozidi miaka therathini, alikuwa mrefu na mweupe mwenye haiba nzuri ya kuvutia sana.
Alikuwa na nywele nyeusi za kibantu alizokuwa amezikata vizuri na kubaki ndogo ndogo na hivyo kumfanya aonekane mzuri wa asili. Alikuwa na sura yake ya duara na macho makubwa ya kike na legevu yaliyokuwa yamezungukwa na kope ndefu na nyeusi.
Pua yake ilikuwa ndogo na iliyochongoka mfano wa pua ya kihabeshi na mdomo yake ilikuwa laini yenye maki na kingo pana kiasi zilizokuwa zimekolezwa kwa lipstick ya rangi ya chocolate pamoja na vishimo vidogo mashavuni mwake vilimfanya azidi kuonekana mrembo zaidi.
Jacky alikuwa na masikio madogo yasiyochusha aliyokuwa ameyatoga na kuyavalisha hereni kubwa za kitamaduni zilizokuwa na umbo la mviringo. Alikuwa amevaa blauzi nyepesi ya arangi ya pinki iliyoyaficha vyema matiti yake imara yenye ukubwa wa wastani yaliyokuwa na chuchu nyeusi imara zilizosimama kikamilifu ndani ya blauzi ile.
Shingoni alikuwa kavaa mkufu mwembamba wa dhahabu uliokuwa umeizunguka ile shingo nyembamba na kidani cha dhahabu kilichokuwa na herufi ya “J” kilikuwa kimepotelea katikati ya uchochoro mdogo wa yale matiti.
Kwenye mkono wake wa kushoto alikuwa amevaa bangili kadhaa za pembe na vidole vyake viwili vya mkono huo alikuwa amevaa pete ndogo za madini ghali ya tanzanite na green tourmaline.
Mkono wake wa kulia alivaa saa ndogo ghali na nzuri ya kike aina ya Cartier La Dona, ambayo bei yake ilikuwa si haba kama angeamua kuibadili kwa pesa za madafu, kwani ilikuwa imemgharimu kiasi cha dola za Marekani 137,000.
Cartier La Dona Watch ilikuwa ni saa ghali sana iliyotengenezwa kwa madini ya dhahabu nyeupe ya Karati 18 ikiwa na kesi imara iliyokuwa na milimita 27 kwa 29 na mkanda wake pia ulikuwa umetengenezwa kwa dhahabu nyeupe, ikiwa na gerentii ya miaka hamsini.
Alikuwa ameinunua nchini Switzerland walipokwenda kwenye fungate muda mfupi tu baada ya ndoa yao iliyoacha gumzo jijini Arusha na kwenye viunga vyake.
Gari ikiwa bado inaunguruma taratibu Jacky alishusha pumzi za ndani kwa ndani na kutazama nje kwa kitambo fulani huku macho yake yakielekea moja kwa moja kwenye jengo la ghorofa la Benki ya Biashara.
Alilitazama lile jengo kwa makini akionekana kama aliyekuwa akijiuliza jambo kuhusiana na lile jengo, kisha aliyashusha macho yake kuutazama mkoba wake mzuri wa kike wa rangi ya pinki uliokuwa umelala juu ya mapaja yake mazuri.
Aliufungua ule mkoba na kutoa humo mkebe mdogo wa duara wa rangi nyekundu kisha aliinua macho yake kujitazama kwa kitambo kifupi kwenye kioo cha lile gari cha katikati kinachotumika kuangalia nyuma huku akigeuza geuza uso wake pembe zote.
Alikunja uso wake huku akiminya midomo yake mizuri yenye maki, na hapo mashavu yake yakapiga misingi, pembe za midomo yake zikafinya, akashusha pumzi ndefu za ndani kwa ndani huku akigeuka kumtazama Carlos aliyekuwa ametulia tuli kama maji mtungini na kuachia tabasamu bashasha.
Carlos aliendelea kutulia pale nyuma ya usukani akionekana kuwaza mbali sana, alimtupia jicho Jacky mara moja tu, kisha akayahamisha macho yake na kutazama kwenye lile jengo la Benki ya Biashara huku sura yake ikiwa haioneshi tashwishwi yoyote.
Jacky alimtazama Carlos kwa makini kisha akaufungua ule mkebe akatoa vipodozi na kuanza kujiremba akiongezea urembo kwenye sura yake huku akijitazama kwenye kile kioo cha gari cha katikati kinachoonesha nyuma.
Itaendelea...
Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY