Stori ya kusisimua - Kizungumkuti!

Stori ya kusisimua - Kizungumkuti!

Shukrani sana Bishop...much blessing to you ndugu.

Still tupo pamoja.
Kizungumkuti! - 6

Na Bishop Hiluka

“Umelijuaje jina langu?” hatimaye Yusuf aliuliza kwa udadisi huku akizidi kumkazia macho Jacky.

Jacky aliangua tena kicheko hafifu na kunyoosha kidole chake kuonesha beji maalumu iliyokuwa imechomekwa kwenye shati la Yusuf katika kifua chake ikiwa imeandikwa jina lake.

"Si hiyo beji uliyovaa kwenye shati lako. Au wewe siyo Yusuf?" alisema Jacky huku akiwatupia jicho wateja wengine waliokuwa wakihudumiwa kwenye kaunta zingine.

"Hmm, mimi ndiye. Karibu sana, sijui nikusaidie nini, dada…?" alisema Yusuf na kushusha pumzi za ndani kwa ndani.

Jacky alitoa tena kitambaa chake na kufuta jasho jepesi lililokuwa likimtoka, akageuza shingo yake kuwatazama wateja waliokuwemo ndani ya ile benki kisha akampenyezea Yusuf ile kadi kwa uficho akihakikisha hakuna mtu mwingine zaidi ya Yusuf aliyeona kitendo kile.

Endelea...

Yusuf alimtazama Jacky kwa mshangao na kuipokea ile kadi, aliiangalia kwa makini kwa kitambo kifupi kisha akainua uso wake kumtazama Jacky akiwa na uso wenye maswali.

Jacky aliachia tabasamu kabambe na kujilegeza. "Dont worry, call me anytime when you get chance, there’s something important we need to talk," (Usihofu, nipigie wakati wowote utakapopata nafasi, kuna kitu muhimu tunahitaji kuongea) alisema Jacky kisha akageuka na kuanza kuondoka eneo lile haraka kabla Yusuf hajasema lolote.

Yusuf alitaka kusema neno lakini alisita na kubaki akimkodolea macho Jacky wakati alipokuwa akitembea kwa madaha huku akili ya Yusuf ikijikuta ikipumbazika mno na mtikisiko maridhawa wa mwili wa Jacky.

Yusuf aliendelea kumsindikiza Jacky kwa macho na kwa utulivu hadi pale alipofungua mlango na kutoka nje ya lile jengo la benki, kisha aliitupia tena jicho la haraka ile kadi na kuitumbukiza mfukoni. Akaendelea kupokea hundi za wateja wengine.

Jacky alipotoka nje ya lile jengo la benki alitembea kwa madaha, tembea yake ilikuwa adimu kuipata kwa wasichana wengi ambao pamoja na kujikwatua, bado walishindwa kupata miondoko kama yake. Tembea ya Jacky iliwafanya watu wageuze shingo zao kumtazama alipokuwa akipita huku macho yao yakishindwa kuamini kile walichokuwa wamekiona, ni kama walikuwa wamemuona malaika.

Kila alikopita, wazee kwa vijana walikuwa wakibabaika, na hawakuisha kugeuza vichwa vyao ili kuustaajabia mwili wake jinsi ulivyoumbika! Alikuwa tofauti sana na wasichana wengine wengi ambao walijiona na kujikweza juu ya kila kiumbe duniani, wasiridhike hata kukanyaga ardhi.

Wakati Jacky alipokuwa akivuka barabara ya Lumumba kuelekea lilipokuwa limeegeshwa gari lao, kuna gari moja dogo lilimpita na muda ule dereva alijikuta akimshangaa na kuivamia pikipiki ya magurudumu matatu aina ya Bajaj iliyokuwa imeegeshwa pembezoni mwa barabara, akairusha kule.

Kidogo lizuke vurumai kubwa katika ya yule dereva na wananchi wenye hasira, akiwemo dereva wa Bajaj, vurumai ambalo lingeweza kuigeuza sehemu ile kuwa Mogadishu, badala yake watu wote walisahau kuhusu ile ajali na kujikuta wakigeuza vichwa vyao kuangalia kazi ya Mungu ilivyotendeka vyema katika mwili wa Jacky huku wengine wakipiga mbinja.

“Dah, tuacheni utani jamani, ilikuwa haki ya dereva kupotea njia!” mwanamume mmoja wa makamo alisema kwa sauti ya juu na kuwafanya watu waliokuwa na hasira kuanguka kicheko.

Hata hivyo, Jacky hakujishughulisha nao, aliendelea na safari yake kwani hali kama ile alikwishaizoea, alifika lilipo gari lao na kufungua mlango wa abiria, akaurusha mkoba wake kwenye siti ya nyuma.

Aliminya midomo yake yenye maki na kuachia tabasamu wakati alipokuwa anaingia kwenye gari na kuufunga mlango kisha alifunga mkanda wa siti na kumtazama Carlos kwa tabasamu.

"Let’s go, my love," (Twende, mpenzi) alisema huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.

Carlos alimtazama Jacky kwa makini na kuliondoa gari taratibu bila kusema neno. Kisha aliiacha barabara ya Lumumba na kushika uelekeo wa upande wa kulia akiufuata mtaa wa Mkunguni.

Baada ya mwendo mfupi wa safari yao aliyafikia makutano ya mtaa ule wa Mkunguni na barabara ya Bibi Titi Mohammed, mbele ya Soko la Kisutu. Carlos alichepuka na kuingia upande wa kulia akiifuata barabara ya Bibi Titi Mohammed.

Katika barabara ile ya Bibi Titi Mohammed Carlos alilazimika kupunguza mwendo kutokana na msongamano mkubwa wa magari, alitazama nyuma kupitia kioo cha katikati cha gari kinachoruhusu kuona nyuma ili kuchunguza kama kulikuwa na chochote alichokitilia mashaka au lah!

Alishtuka sana baada ya kuhisi kulikuwa na jambo lisilo la kawaida, alitazama kwa makini na aliweza kuliona gari aina ya Toyota Land Cruiser Pick-up la rangi nyeusi likiwa katika foleni nyuma yao, alikumbuka kuliona gari lile tangu alipotoka barabara ya Lumumba na kuingia katika mtaa wa Mkunguni.

Hata hivyo, hakutaka kumshtua Jacky, aliendesha kimya kimya hadi walipozifikia taa za kuongozea magari barabarani katika makutano ya barabara za Uhuru na Bibi Titi Mohammed. Pale kwenye makutano Carlos walishindwa kuvuka kwa kuzuiwa na taa nyekundu za kuongozea magari barabarani.

Aliitupia macho saa yake ya mkononi na kuminya midomo yake huku akitazama tena nyuma yake kupitia kile kioo cha katikati cha gari kinachoruhusu kuona nyuma, hakuliona lile gari.

Alipogeuza shingo yake kutazama kando akaliona lile gari Toyota Land Cruiser Pick-up jeusi likiwa limesimama sambamba na gari lake upande wao wa kushoto, na sasa aliweza kusoma maandishi makubwa ya POLISI yaliyokuwa yameandikwa ubavuni.

Mbele ya lile gari kulikuwa na dereva na ofisa mmoja wa polisi na nyuma ya lile gari kulikuwa na maofisa watano wa polisi waliokuwa wameketi na walishika bunduki aina ya SMG zilizotundikwa begani na kulalia vifuani.

Wale askari walikuwa wakilitazama lile kwa makini sana. Hapo akili ya Carlos ilianza kupoteza utulivu taratibu kadiri lile gari lilivyoendelea kusimama pale. Jacky alishtuka na kugeuza shingo yake kutazama kule lilikokuwa lile gari la Polisi baada ya kumuona Carlos akioneshwa kubabaika kidogo.

Carlos alikuwa akihisi kijasho chepesi kikimtoka usoni, alitoa kitambaa na kufuta jasho usoni huku akiendelea kuwachunguza wale askari wenye mitutu ya bunduki kwa makini sana huku akijaribu kuyasoma mawazo yao.

Mara taa ya kijani ya kuongozea magari ikawaruhusu kupita, Carlos akashusha pumzi za ndani kwa ndani na kuingiza gia huku akiliondoa gari lake, alizivuka zile taa na kushuhudia lile gari la Polisi likifuatia nyuma yake, alipokwenda mbele kidogo akapunguza mwendo na kukata kona kuingia mtaa wa Sofia Kawawa upande wake wa kushoto ili kuona kama alikuwa anafuatiliwa.

Lile gari la Polisi nalo lilipunguza mwendo na kuingia kufuata uelekeo ule ule japokuwa lilikawia kidogo kuingia. Tukio lile lilimfanya Carlos ahisi kuishiwa nguvu ingawa hakuwa na uhakika kama wale Polisi walikuwa wakimfuata yeye, hata hivyo kwa namna nyingine ile ilikuwa ni ishara mojawapo ya kumtahadharisha kuwa alipaswa kuwa makini.

Itaendelea...

Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Kizungumkuti! - 11

Na Bishop Hiluka

Jacky hakuweza kuvumilia tena hivyo haraka akaishusha chini nguo yake ya ndani na kuupeleka mkono wake akiichezea ikulu ya Carlos na kumfanya aanze kuhema ovyo.

Muda mfupi uliofuata walikuwa kwenye kochi kubwa la sofa pale pale sebuleni huku kila mmoja akiwa amepandwa na wazimu wa mapenzi. Mara wakajikuta wakiwa kwenye sayari nyingine ya mahaba mazito iliyokuwa kama kisiwa cha raha kwa ajili yao.

Sebule ile ikajazwa na vilio vya mahaba toka kwa Jacky vilivyoashiria raha ya aina yake aliyokuwa akiipata. Jacky alikuwa msichana mtundu sana aliyemudu vyema mitindo mbalimbali kiasi cha kumfanya Carlos ajihisi kama mvulana wa shule ya msingi.

Endelea...

Alikuwa amezitendea vyema hisia za Carlos na raha aliyoipata Carlos iliyafanya macho yake yashindwe tena kumtazama Jacky usoni. Hata hivyo, Carlos naye hakuachwa nyuma, kwani alikuwa akimchezesha Jacky gwaride la ukweli.

Ooh Carlos, you’re a real man!” (Carlos, wewe ni mwanamume kwelikweli!) Jacky alisema huku akitweta baada ya kumaliza mzunguko mmoja, aligeuza shingo yake kumtazama Carlos aliyekuwa amejilaza kwenye sofa akitiririkwa na jasho kutokana na shughuli ile ambayo haikuwa ndogo.

Kisha Jacky alijiinua kutoka pale sakafuni alipojikuta akiwa amelala, akachukua chupa ya whisky na kumimina katika bilauri kisha akapiga funda kubwa huku akisisimkwa mwili na kushusha pumzi ndefu.

You’re so wonderful, my love. I swear in heaven and earth, I’ve never met a man who knows love like you!” (Wewe ni mwanamume wa aina yake, mpenzi wangu, naapa sijawahi kukutana na mwanaume anayeyajua mapenzi kama wewe!) Jacky alisema huku akitweta na kujipweteka kwenye sofa.

“Dah! Jacky mtundu sana na ana sifa zote, ni mwanamke mrembo sijapata kuona na mambo anayonifanyia kila siku yananipagawisha, ninashukuru kuwa na mwanamke huyu maishani mwangu. Ana kila kitu ninachokihitaji kwa mwanamke. Halafu yuko tofauti sana na wanawake wengine,” Carlos aliwaza huku akimtupia jicho Jacky.

“Mwili wote unaniuma kwa gwaride alilonichezesha Carlos, huyu ni kidume kweli kweli kwani muziki wake si mdogo utadhani ana mapafu ya farasi!” Jacky naye aliwaza huku akijiinua kutoka pale kwenye sofa na kuelekea maliwato.

“Dah! Mwili wote hauna nguvu hata kidogo, Carlos huwa ananikimbiza mchaka mchaka kwelikweli,” alijiambia wakati akijimwagia maji mwilini ili kurejesha nguvu mwilini.

“Lakini, ni kweli huyu mwanamume ananipenda au kanioa ili anitumie kama project yake ya kujipatia fedha? Kwa nini aniruhusu nikalale na mwanamume mwingine sababu ya fedha? Hivi nitaendelea na maisha haya ya kuutumia mwili wangu kwa ajili ya fedha hadi lini? I’m tired with this kind of life,” (Nimechoka na aina hii ya maisha) Jacky aliwaza wakati akitoka kule maliwato na kurudi sebuleni alipokuwa ameketi Carlos.

* * * * *
Ilikuwa tayari imetimia saa mbili na nusu ya usiku wakati Jacky na Carlos walikuwa wamelala usingizi kwenye kochi kubwa la sofa pale pale sebuleni na kupitiwa na usingizi mtamu wa uchovu. Walipitiwa usingizi baada ya kwenda mzunguko wa pili uliowafanya washindwe hata kuinuka na kuamua kuangusha gari pale pale.

Wote walikuwa watupu huku Jacky akiwa amekilaza kichwa chake kifuani kwa Carlos. Mguu wake mmoja ulikuwa katikati ya mapaja ya Carlos huku mkono wake mmoja akiwa ameuzungusha shingoni kwa Carlos na alikuwa akikoroma kwa sauti hafifu ya uchovu.

Mara simu ya Jacky ilianza kuita kwa fujo na kumshtua Carlos, ambaye aliinua kichwa chake kuitazama kwa makini. Hii ilikuwa simu nyingine aina ya Nexus 6P ambayo ni tofauti na ile ya IPhone X, na aliitumia kwenye dili za hatari tu.

Ile simu ilifanyia utundu kwa kumfanya mtu yeyote ambaye angejaribu kuifuatilia mahali alipo asiweze kubaini, kuna wakati ingesoma kuwa yupo Australia au Uingereza, alifanya vile ili hata kama lingetokea jambo lolote ingekuwa vigumu kumhusisha kwani hata namba iliyotumika katika simu ile ilisajiliwa kwa jina bandia la Belinda Jackson.

Ile simu ilikuwa juu ya ile meza ya duara na iliendelea kuita kwa fujo na kugeuka kero kubwa masikioni mwake. Carlos aliinua mkono wake wa kulia ambao aliutumia kuvaa saa na kuitazama saa yake ya mkononi aina ya Ferrari King Gold hublot aliyoinunua Dubai kwa dola za Marekani 43,600.

Ooh shit! It is quarter past eight!” (Ooh! Ni saa mbili na robo!) Carlos aling’aka kwa mshangao huku akiikodolea macho kwa makini ile saa yake kisha alimtazama Jacky ambaye alikuwa anakoroma na kuanza kumpigapiga mgongoni ili kumwamsha.

Jacky alifumbua macho yake kivivuvivu na kumtazama Carlos usoni kisha alinyanyua kichwa chake na kugeuza shingo yake kuitazama ile simu iliyokuwa bado inaita huku akipiga miayo ya uchovu.

Alijaribu kuipuuza ile simu na kukilaza tena kichwa chake kifuani kwa Carlos lakini iliendelea kuita kwa fujo na kusababisha kero masikioni mwake. Aliinuka akaichukua na kuitazama namba ya mpigaji kwa makini, kisha akaipokea na kuiweka sikioni.

Hello!” Jacky alizungumza kwa sauti laini huku akipiga mwayo mrefu kutokana na uchovu wa usingizi.

Hello, I think I’m talking to Belinda Jackson, right?” (Halo, nadhani nazungumza na Belinda Kizito, au siyo?) sauti ya upande wa pili wa simu ilipenya kwenye sikio la Jacky na kumfanya ashtuke kidogo. Alikunja sura yake huku akijaribu kutafakari haraka haraka jibu ambalo angetoa.

Yes, who is this?” (Ndiyo, nani mwenzangu?) Jacky aliuliza kwa mashaka kidogo.

My name is Yusuf Akida,” (Jina langu ni Yusuf Akida) sauti ile ilizungumza kwa utulivu.

“Which Yusuf?” (Yusuf gani?) Jacky aliuliza tena huku akikunja sura yake kujaribu kukumbuka kama aliwahi kukutana na mtu mwenye jina hilo.

You came to the bank this morning and gave me your business card…” (Ulikuja pale benki leo asubuhi na ukanipa kadi yako…) ile sauti iliongea kwa utulivu na kushusha pumzi ndefu.

Ooh… Yusuf! How are you, my love?” (Ooh… Yusuf! Habari yako, mpenzi?) Jacky alisema kwa sauti nyororo huku akiachia kicheko hafifu kilichopenya vyema kwenye sikio la Yusuf.

I’m fine…” (Sijambo…) ile sauti ilijibu kisha kimya kifupi kikapita.

“Samahani sana kwa kukukera kwa simu saa hizi, nilitaka tu kukusalimia nisikie sauti yako,” sauti ile ilisema.

Jacky aliachia tabasamu pana huku akigeuza shingo yake kumtazama Carlos kisha akamkonyeza. Carlos alijiweka sawa pale kwenye sofa na kusogeza sikio lake akiwa na hamu ya kutaka kusikiliza maongezi.

“Wala usijali, Yusuf, hujanikera kabisa! We nipigie muda wowote tu, ndiyo maana nimekupa namba yangu,” Jacky alisema kwa sauti laini yenye kusihi.

“Asante sana, Belinda…” Yusuf alisema na kunyamaza tena. Kitambo kingine kifupi cha ukimya kikapita huku kila mmoja akionekana kuzama kwenye tafakuri, na wakati hali ile ikiendelea mara Yusuf akavunja ukimya. “Bila shaka saa hizi uko nyumbani!”

Jacky aliachia kicheko cha mahaba huku akigeuza tena shingo yake kumtazama Carlos ambaye muda wote alikuwa ametega sikio lake kwa shauku ya kutaka kusikia kilichokuwa kinaongewa.

“Ndiyo, niko nyumbani,” Jacky alijibu huku akibana midomo yake yenye maki.

Itaendelea...

Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY HALELUYA MOSHI
 
Kizungumkuti! - 12

Na Bishop Hiluka

“Asante sana, Belinda…” Yusuf alisema na kunyamaza tena. Kitambo kingine kifupi cha ukimya kikapita huku kila mmoja akionekana kuzama kwenye tafakuri, na wakati hali ile ikiendelea mara Yusuf akavunja ukimya. “Bila shaka saa hizi uko nyumbani!”

Jacky aliachia kicheko cha mahaba huku akigeuza tena shingo yake kumtazama Carlos ambaye muda wote alikuwa ametega sikio lake kwa shauku ya kutaka kusikia kilichokuwa kinaongewa.

“Ndiyo, niko nyumbani,” Jacky alijibu huku akibana midomo yake yenye maki.

Endelea...

You are in bed?” (Upo kitandani?) Yusuf aliuliza tena kwa shauku.

Nope… I'm just sitting in the living room,” (Wala… nimeketi tu sebuleni) Jacky alisema huku aking’onga.

Are you alone or you are with someone?” (Uko peke yako au una mtu?) Yusuf aliuliza tena kwa shauku huku sauti yake ikiashiria wivu fulani.

Jacky aliangua kicheko kingine cha mahaba, kicheko cha safari hiyo kilikuwa kicheko hafifu lakini kilichopenya vyema kwenye sikio la Yusuf na kumfanya akunje sura yake.

Why are you laughing, Belinda, or have I asked a question that is unusual?” (Mbona unacheka, Belinda, au nimeuliza swali ambalo si la kawaida?) Yusuf aliuliza kwa sauti tulivu iliyopenya haswa kwenye sikio la Jacky.

Jacky alilamba midomo yake kwa madaha huku akijiegemeza kifuani kwa Carlos. Carlos akamkumbatia huku akizishika chuchu zake na kumfanya Jacky asisimkwe.

“No, it's a very common question,” (Hapana, ni swali la kawaida kabisa) Jacky alijibu kisha akageuza shingo yake kumwangalia Carlos na kusogeza mdomo wake kwenye mdomo wa Carlos, kisha akambusu.

I’m all alone. Do you want to come and give me a company?” (Nipo peke yangu tu. Vipi unataka kuja kunipa kampani?) Jacky alimuuliza Yusuf swali la uchokozi huku akitoa ulimi wake na kulamba midomo.

Where are you living?” (Kwani unaishi wapi?) Yusuf aliuliza kwa shauku.

“Naishi Masaki…”

“Aah, Masaki! Kwani ubavu wa kuja huko ninao basi! Kuja huko kwenu si mpaka nipewe Viza!” Yusuf alisema kwa utani huku akiangua kicheko hafifu.

“Viza?” Jacky aliuliza kwa mshangao.

“Ndiyo, nitaingiaje maeneo ya watu wazito kama naingia sokoni?” Yusuf alisema huku akichia kicheko kingine hafifu na kumfanya Jacky naye aangue kicheko.

“Acha mzaha bwana…” Jacky alisema baada ya kile kicheko huku akimpapasa Carlos kwenye kidevu.

But, I’m just curious, Belinda. Be honest with me, living at Masaki all alone! I guess whoever your husband he is, he is sure a big or rich guy…” (Lakini, najaribu kujiuliza, Belinda. Kuwa mkweli tu, unaishi Masaki peke yako! Nahisi huyo mumeo, bila shaka atakuwa mtu mkubwa au tajiri sana…) Yusuf aliuliza kwa wasiwasi.

Trust me, Yusuf, I’m not married. I’m all alone… ” (Niamini, Yusuf, wala sijaolewa. Naishi peke yangu…)

“Or maybe you're related to a very rich family?” (Au pengine unatoka katika familia tajiri sana?) Yusuf akauliza kwa sauti yenye wasiwasi

Hmm…” Jacky aliguna.

And they are taking good care of you…” (Na wanakuhudumia vizuri sana…) Yusuf akasema tena kabla Jacky hajasema lolote.

Oh, Yusuf my dear, why can’t we skip this conversation and talk about our matters?” (Oh Yusuf mpendwa wangu, kwa nini tusiyaache maongezi haya na kuzungumzia mambo yetu?) Jacky alimkatisha Yusuf huku akionekana kuanza kukereka.

Okay, I’m very sorry for…” (Sawa, samahani kwa…)

Don’t worry, my love. Niambie uko wapi saa hizi?” Jacky alisema na kumkata kauli Yusuf.

“Nipo hapa Malapa La Promise Hotel, sijui unapajua?”

“Napafahamu sana,” alisema Jacky na kushusha pumzi za ndani kwa ndani, kisha kikazuka kitambo kifupi cha ukimya.

Do you want me to come there?” (Kwani unataka nije hapo?) hatimaye Jacky aliuliza huku akimkonyeza Carlos.

“Njoo kama unaweza,” Yusuf alisema huku akishusha pumzi ndefu.

Okay, give me just forty-five minutes I’ll be there,” (Sawa, nipe kama dakika arobaini na tano tu nitakuwa hapo)

I’m patiently waiting, but I’m sorry for troubling you,” (Nakusubiri kwa hamu, lakini samahani kwa usumbufu) Yusuf alisema kwa sauti ya kusihi.

Don’t worry,” Jacky alisema na kukata simu huku akishusha pumzi ndefu za ndani kwa ndani. Alipeleka mkono wake wa kulia kwenye kifua cha Carlos na kuanza kumpapasa, kisha alimbusu kwenye paji la uso kwa furaha.

The first step towards billions,” (Hatua ya kwanza kuelekea kwenye mabilioni) Jacky alisema huku akimbusu Carlos mfululizo kwenye mashavu na mdomo wake. Muda wote Carlos alibaki kimya akimtazama bila kusema neno, uso wake haukuonesha tashwishwi yoyote.

The way is clear, my love,” (Njia iko wazi, mpenzi wangu) Jacky alisema huku akizidi kujiegemeza kwenye kifua cha Carlos.

But, be very careful, my love, I hope you don’t see the way to jail,” (Lakini, kuwa mwangalifu sana Jacky, nina imani huioni njia ya kwenda gerezani) Carlos alimtahadharisha Jacky kwa sauti tulivu.

Do not worry, I'm very careful,” (Ondoa shaka, nipo makini sana) Jacky huku alisema akimtoa wasiwasi Carlos.

Kitambo kifupi cha ukimya kikapita huku kila mmoja akionekana kuzama kwenye tafakuri na wakati hali ile ikiendelea mara Jacky akakumbuka jambo na kumtazama Carlos.

So what do you say, nikaoge niondoke?” Jacky alimuuliza Carlos huku akimtazama usoni.

“Nakutakia kila la heri,” Carlos alijibu na muda ule ule Jack alijiinua kutoka pale kwenye sofa na kuelekea maliwatoni.

Itaendelea...
 
Kizungumkuti! - 13

Na Bishop Hiluka

Kitambo kifupi cha ukimya kikapita huku kila mmoja akionekana kuzama kwenye tafakuri na wakati hali ile ikiendelea mara Jacky akakumbuka jambo na kumtazama Carlos.

So what do you say, nikaoge niondoke?” Jacky alimuuliza Carlos huku akimtazama usoni.

“Nakutakia kila la heri,” Carlos alijibu na muda ule ule Jack alijiinua kutoka pale kwenye sofa na kuelekea maliwatoni.

Endelea...

Alioga chap chap na baada ya dakika kadhaa alitoka bafuni na kuingia chumbani, akafungua kabati maalumu ambalo lilitumika kuhifadhi nguo maalumu kwa matukio maalumu, akajichagulia gauni maalumu kwa siku ile iliyoendana na umbo lake.

Lilikuwa gauni jepesi la rangi nyekundu la mikono mirefu lililolichora vyema umbo lake na kuishia juu ya magoti yake huku likiwa na mpasuo kwa mbele ulioacha paja lake nusu wazi na kuifichua vizuri hazina ya kupendeza yenye mvuto wa ajabu ya miguu na mapaja yake maangavu yenye misuli imara ya rangi maridhawa ya mng’ao.

Miguuni alivaa viatu vizuri vyekundu vya ngozi ya mamba vilivyokuwa na vikanyagio virefu vya mchuchumio.

Kisha alisimama mbele ya meza iliyokuwa imesheheni vipodozi vya kila aina akajipodoa na kuuremba uso wake. Midomo yake ya kike yenye kingo pana kiasi aliikoleza vizuri rangi ya mdomo na masikio yake madogo yasiyochusha aliyavalisha hereni maalumu za madini ghali ya tanzanite na kujipulizia manukato ghali aina ya Clive yenye harufu nzuri ya kuhamasisha ngono.

Alipomaliza akajitazama tena katika kioo kikubwa na kutabasamu, kwa kweli usiku ule alipendeza mno kuliko kawaida na uzuri wake uliongezeka mara dufu. Kisha akakumbuka kuchukua mkufu wake mwembamba wa dhahabu safi uliokuwa na kidani cha madini ya tanzanite, na kuuvaa.

Ule mkufu ulionekana kuizunguka vyema shingo yake nyembamba huku kile kidani kikipotelea katikati ya mfereji wa matiti yake mazuri.

I’m so pretty. Thank you God for giving me this beauty…” (Mimi ni mrembo. Asante Mungu kwa kunipa uzuri huu…) aliwaza huku akijigeuza geuza kujitazama kwa makini.

Aliporidhika alichukua mkoba wake mzuri wa kike wa rangi nyekundu akautundika begani, kisha akatoka chumbani na kuelekea sebuleni, pale sebuleni alisimama na kumtazama Carlos kwa makini kisha alimpungia mkono na kuanza kuondoka.

“Mpaka asubuhi?” Carlos aliuliza kwa sauti yake nzito iliyokuwa imebeba wivu mkubwa.

Jacky aligeuza shingo yake kumtazama Carlos na kuachia tabasamu. “Ikibidi nitalala mpaka asubuhi, na kama kiroho kinakuuma niahirishe,” alisema huku akiangua kicheko hafifu.

“Aah, nenda…” Carlos alisema huku akijiinua kutoka pale kwenye sofa alipokuwa ameketi na kuanza kuelekea maliwatoni lakini akasita kidogo na kugeuka kumtazama Jacky. “Lakini isiwe kavukavu, sawa?” alisema huku akimkazia macho.

Jacky aliachia tabasamu na kufungua mkoba wake akatoa kondomu kadhaa na kumuonesha Carlos, kisha akazirudisha kwenye mkoba wake na kutoka huku akiangua kicheko hafifu.

Alipotoka alielekea moja kwa moja kwenye banda la magari na kuchagua gari aina ya Toyota Landcruiser GX V8 jeusi, akabonyeza rimoti maalumu iliyokuwa kwenye ufunguo wa gari, kitasa cha mlango wa lile gari kikafunguka.

Jacky aliufungua mlango wa lile gari na kufungua mkoba wake kisha akatoa simu yake ya mkononi aina ya Nexus 6P na kuurusha ule mkoba kwenye siti ya pili.

Aliingia kwenye gari na kuwasha injini ya lile gari kisha akabonyeza rimoti maalumu kwa ajili ya kufungua geti na mara lile geti likaanza kujifungua taratibu. Jacky akaliondoa lile gari na kugeuka kubonyeza tena rimoti na mara lile geti likajifunga tena. Akaingiza gia na kupotelea mtaani.

Katika muda ule wa usiku jiji la Dar es Salaam lilikuwa limetawaliwa na pilika pilika za aina yake za watu, pikipiki na magari yaliyoonekana kukatisha barabarani, hasa katika barabara kuu za jiji.

Jacky aliendesha gari lake kwa umakini lakini akiwa katika mwendo wa kasi huku akipishana na pikipiki na magari mengine na alipofika katika eneo la Barakuda aliifuata barabara iliyokuwa ikipitia eneo la Vingunguti na baadaye kwa Mnyamani.

Kwa kupita barabra ile ilimsaidia kukwepa foleni ndefu ya magari katika barabara ya Mandela, na hivyo baada ya dakika arobaini alikuwa amefika Buguruni Malapa.

Alifika katika hoteli ya La Promise wakati Yusuf akionekana kuchoka kusubiri, maana alikuwa anaitazama saa yake ya mkononi mara kwa mara na kutingisha kichwa huku akionekana kuishiwa uvumilivu.

Jacky alitafuta sehemu nzuri na kuliegesha gari lake kwenye eneo la maegesho ya magari katika ile hoteli ya La Promise, kisha aliteremka na kuingia ndani, akapandisha ngazi chapchap kuelekea ghorofa ya kwanza kwenye eneo la baa kwa mwendo wa madaha huku akitoa simu yake na kupiga zile namba za Yusuf huku akiangaza macho yake kutazama huku na kule.

Yusuf akiwa amekata tamaa aliona simu yake ikiita na kabla hajaipokea aliweza kumuona Jacky akiingia na kusimama huku akiendelea kuangaza macho yake huku na kule. Yusuf alisimama na kupunga mkono wake hewani kumwita. Jacky alimuona na kukata simu kisha akamfuata huku akiachia tabasamu.

Jacky alimkumbatia Yusuf kwa bashasha kwa namna ya kumsalimia, kisha aliketi kwenye kiti kitupu huku akimtazama kwa tabasamu kabambe.

“Pole sana, Yusuf, naona umesubiri muda mrefu, eh?” aliuliza Jacky huku akiitazama saa yake ya mkononi.

“Siyo sana. Hata hivyo jambo la muhimu ni kwamba umefika, sijui utakunywa nini?” alisema Yusuf huku akinyoosha mkono wake kumwita mhudumu wa ile baa kwa ishara.

“Hapana, twende mahali pengine pazuri zaidi ambako tutakunywa kwa raha na kuongea mambo yetu kwa nafasi zaidi,” Jacky alisema huku akiinuka kutoka kwenye kile kiti.

“Wapi?” Yusuf aliuliza huku akimtazama Jacky kwa mshangao akionekana kushtuka kidogo.

“Kuna sehemu nzuri sana nimeibuku mara tu baada ya kunipigia simu, hiyo sehemu ni maalumu kwa ajili yetu,” Jacky alisema huku akimshika Yusuf mkono wake kumuinua.

Yusuf aliinuka bila kupinga, akaanza kumfuata Jacky nyuma kama vile mbwa aliyemuona chatu.

“Umekuja na gari?” Jacky alimuuliza Yusuf mara tu walipofika chini.

“Hapana, nimekuja kwa miguu maana sikai mbali na hapa,” Yusuf alijibu lakini akasita baada ya kumuona Jacky akimfungulia mlango wa abiria wa gari la kifahari aina ya Toyota Landcruiser GX V8 jeusi. Akataka kuuliza lakini akasita na kuingia kimya kimya.

Je, Jacky amepanga kumpeleka wapi Yusuf? Fuatilia hatua kwa hatua mkasa huu wa kusisimua...
 
Kizungumkuti! - 14

Na Bishop Hiluka

“Kuna sehemu nzuri sana nimeibuku mara tu baada ya kunipigia simu, hiyo sehemu ni maalumu kwa ajili yetu,” Jacky alisema huku akimshika Yusuf mkono wake kumuinua.

Yusuf aliinuka bila kupinga, akaanza kumfuata Jacky nyuma kama vile mbwa aliyemuona chatu.

“Umekuja na gari?” Jacky alimuuliza Yusuf mara tu walipofika chini.

“Hapana, nimekuja kwa miguu maana sikai mbali na hapa,” Yusuf alijibu lakini akasita baada ya kumuona Jacky akimfungulia mlango wa abiria wa gari la kifahari aina ya Toyota Landcruiser GX V8 jeusi. Akataka kuuliza lakini akasita na kuingia kimya kimya.

Endelea...

Jacky aliliondoa lile gari kutoka pale La Promise hadi kwenye jengo la ofisi za kampuni ya visimbuzi ya StarTimes akakata kushoto na kuingia katika barabara ya Uhuru akiungana na magari yaliyokuwa yakitokea Buguruni.

Hapo alipunguza mwendo kutokana na msongamano wa magari katika barabara ile finyu, akaendesha hadi walipofika katika eneo la Bungoni akakata na kuingia upande wa kulia akiifuata barabara iliyokuwa na magari machache, hasa daladala akijaribu kuikwepa foleni ndefu ya magari katika barabara ile ya Uhuru.

Aliongeza mwendo na baada ya kitambo fulani cha safari walijikuta wamefika kwenye majengo ya wafanyabiashara wadogo, maarufu kama Machinga Complex.

Hapo alikata tena na kuingia upande wa kulia akiifuata barabara ya Kawawa hadi alipokwenda kuungana na barabara ya Nyerere katika eneo la Veta. Kisha alikata kuingia upande wa kushoto akiifuata barabara ile ya Nyerere.

Muda wote Yusuf alikuwa ametulia kimya akimtazama Jacky kwa jicho la wizi huku akiwa hajui wanaelekea wapi.

Baada ya kuendesha gari kwa umakini wakipita barabara hii na ile hatimaye walitokea katika eneo la Posta na kuifuata barabara ya Garden, kisha Jacky alikwenda hadi kwenye hoteli ya Southern Sun iliyopo katika eneo tulivu zaidi.

Aliliegesha gari lake katika viunga vya maegesho ya magari vya jengo la hoteli ile yenye hadhi ya nyota nne ambayo ilikuwa imejengwa katikati kabisa ya jiji la Dar es Salaam.

Mahali ilipokuwepo ile hoteli ilikuwa ni mwendo wa dakika 6 tu kwa kutembea kutoka kwenye ufukwe wa Bahari ya Hindi na ilikuwa jirani na hospitali ya rufaa ya wagonjwa wa saratani ya Ocean Road.

Jacky aliichagua hoteli ile kwa kuwa ilikuwa katika eneo tulivu mno lisilo na bughudha ikiwa jirani na ofisi mbalimbali za kibalozi katika jiji la Dar es Salaam, ilikuwa na eneo maalumu la mazoezi [gym], bwawa la kuogelea na kituo cha biashara.

Eneo la mbele la maegesho ya magari ya ile hoteli ambalo lilikuwa ng’ambo ya pili ya barabara lilipandwa miti mizuri aina ya coconut palms pamoja na miti mingine mirefu ya kivuli.

Pia kulikuwa na bustani nzuri ya maua ndani ya uzio wa ile hoteli na taa hafifu za ardhini zilizokuwa zikimulika eneo lile na hivyo kulifanya eneo lote lipendeze zaidi.

Jacky alishusha pumzi za ndani kwa ndani na kugeuza shingo yake kumtazama Yusuf ambaye muda wote alikuwa kimya, aliachia tabasamu pana huku akifungua mlango wa gari na kushuka.

“Tumefika,” Jacky alimwambia Yusuf baada ya kumuona akiwa bado ameketi kwa utulivu akiwa anashangaa.

Yusuf alishuka haraka kutoka kwenye lile gari, wakaanza kukatisha kwenye viunga vile vya maegesho ya magari taratibu na kuelekea mbele ya lile jengo, sehemu kulipokuwa na mlango mkubwa wa kioo na varanda pana yenye ngazi iliyofunikwa kwa kofia nzuri ya zege.

Walipoingia ndani walipokelewa kwa bashasha zote na wahudumu wa ile hoteli ambao sura zao zilikuwa zimepambwa na tabasamu la kirafiki muda wote.

Walipita moja kwa moja wakiuvuka ule ukumbi wa mapokezi na kuelekea upande wa kushoto wakashuka ngazi chache chini wakiuvuka mgahawa wa Baraza Grill ambao ulikuwa kwa ajili ya chakula cha kitanzania na cha kimataifa.

Ule ulikuwa ukumbi mkubwa kiasi wenye meza nyingi za kulia chakula zenye umbo mstatili zilizozungukwa kwa viti nadhifu vyenye foronya laini.

Meza zile zilikuwa zikimefunikwa kwa vitambaa visafi vya rangi nyeupe na juu yake kuliwekwa kadi ngumu za kupendeza zenye orodha ya vyakula na vinywaji vinavyopatika katika hoteli ile.

Pia kulikuwa na karatasi laini nyeupe za tishu za kufutia mikono na vifaa vyote muhimu vya kujipatia maakuli kama uma, visu na vijiko, na bila kusahau vikasha wiwili vidogo; kimoja cha kuwekea chumvi ya mezani na kingine cha vijiti vya kuchokolea meno.

Pembeni ya meza zile kulikuwa na makochi mazuri ya sofa yaliyopangwa kuzizunguka meza fupi za vioo katika mpangilio mmoja uliovutia. Pia mwisho wa ukumbi ule kulikuwa na kaunta kubwa ya vinywaji.

Madirisha makubwa ya vioo ya ukumbi ule yalikuwa yamefunikwa kwa mapazia marefu yenye rangi nzuri za kupendeza. Ukutani kulikuwa na runinga pana za bapa maarufu kama ‘flat screen’ zilizokuwa zikiendelea kurusha vipindi mbalimbali vya burudani.

Katika ule ukumbi kulikuwa na watu wachache waliokuwa wameketi wakijipatia mlo na vinywaji huku wakiendelea na maongezi yao.

Ukumbi haukuwa mkubwa na ulikuwa umetenganishwa na ile sehemu ya mapokezi kwa ukuta mdogo uliokuwa unamruhusu mtu yeyote kuweza kuona mle ndani bila usumbufu wowote.

Walipovuka eneo lile walitokea upande wa nyuma wa lile jengo kulikokuwa na mgahawa mwingine wa Kivulini ambako mara nyingi palitumika kwa ajili ya chakula cha kimataifa na ulikuwa unatazama eneo kubwa lenye bustani nzuri yenye miti mbalimbali na swimming pool.

Katika mgahawa ule wa Kivulini kulikuwa na watu wachache, Wazungu kwa Waafrika waliokuwa wakiendelea na maongezi yao ya hapa na pale katika viti vizuri na meza fupi za mbao.

Watu wale walikuwa wakijipatia vinywaji, wengine wakiwa katika maongezi ya kibiashara huku wakivuta sigara na kutazama mechi ya mpira wa miguu ya ligi ya Ulaya kati ya Manchester United na Juventus iliyokuwa ikioneshwa ‘mbashara’ kwenye runinga kubwa iliyotundikwa ukutani.

Wakati wakitafuta eneo tulivu la kuketi mara mhudumu mmoja wa kike wa baa ile aliyevalia nadhifu aliwaona na kuwafuata akiwa tayari kuwahudumia. Alipowafikia aliwasalimia kwa adabu kubwa na kwa bashasha zote.

Kabla yule mhudumu hajauliza Jacky alimnong’oneza jambo na kumfanya yule mhudumu amtupie jicho Yusuf na kuachia tabasamu. Hata hivyo, Yusuf aliyaona yote yaliyokuwa yakiendelea pale lakini alijifanya kama hajaona na kubaki mtulivu.

Itaendelea...

Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY HALELUYA MOSHI Clkey
 
Kizungumkuti! - 15

Na Bishop Hiluka

Wakati wakitafuta eneo tulivu la kuketi mara mhudumu mmoja wa kike wa baa ile aliyevalia nadhifu aliwaona na kuwafuata akiwa tayari kuwahudumia. Alipowafikia aliwasalimia kwa adabu kubwa na kwa bashasha zote.

Kabla yule mhudumu hajauliza Jacky alimnong’oneza jambo na kumfanya yule mhudumu amtupie jicho Yusuf na kuachia tabasamu. Hata hivyo, Yusuf aliyaona yote yaliyokuwa yakiendelea pale lakini alijifanya kama hajaona na kubaki mtulivu.

Endelea...

Kisha yule mwanadada aliwachukua Jacky na Yusuf hadi sehemu ya mapokezi ambako aliwakabidhiwa kwa mwanadada mwingine, ambaye alivuta droo na kuchukua kadi maalumu ya kielektroniki iliyotumika kufungua mlango wa chumba.

Kisha alimuashiria Jacky kwa mkono kuwa wamfuate, alitangulia akawaongoza kuelekea sehemu kulipokuwa na lifti ya lile jengo la hoteli ya kuelekea juu, walitembea taratibu wakiliacha lile eneo la mapokezi na kushika uelekeo wa upande wa kulia hadi kwenye mlango wa lifti za lile jengo.

Walipofika pale yule dada mhudumu alibonyeza kitufe fulani ukutani na mlango wa ile lifti ukafunguka kisha wakaingia ndani ya kile chumba cha lifti, na alipohakikisha wote wameingi yule mhudumu alibonyeza kitufe ukutani akiiamuru ile lifti iwafikishe kwenye ghorofa ya tano ya lile jengo.

Mlango ulipojifunga ile lifti ilianza kupanda juu hadi ilipofika katika ghorofa ya tano ya lile jengo, ikagota na mlango wa kile chumba cha lifti ukafunguka kuwaruhusu waliomo ndani watoke nje.

Yule mhudumu alitangulia kutoka, Jacky na Yusuf wakamfuata, walijikuta wametokezea kwenye korido pana iliyomezwa na utulivu wa aina yake. Korido ile ilikuwa ikipakana na milango kadhaa ya vyumba kwa upande wa kushoto na kulia.

Katikati ya ile korido kulikuwa na kitufe kikubwa chekundu cha kengele ya hatari pembeni ya mtungi mkubwa wa gesi ya kuzimia moto wa dharura.

Kwenye dari ya korido ile kulikuwa na taa ndefu za tubelight za mtindo wa kupendeza zilizokuwa zikiangaza mwanga wa wastani na hivyo kuyafanya mandhari ya ile korido yawe tulivu na ya kupendeza.

Katika korido yote kulikuwa na hewa safi iliyokuwa ikisambazwa taratibu na viyoyozi viwili, kimoja kikiwa mwanzo wa ile korido na kingine mwisho wa korido. Sakafu ya korido ile ilikuwa na tarazo maridadi zilizokuwa na nakshi za kupendeza na hapakuwa na kitu kingine cha ziada zaidi ya utulivu mkubwa.

Jacky na Yusuf walitembea taratibu katikati ya ile korido wakimfuata yule dada mhudumu aliyekuwa ametangulia mbele, waliipita milango kadhaa mikubwa na imara ya mbao ngumu iliyokuwa ikitazamana na ile korido, ambayo juu yake kulikuwa na vibao vidogo vya rangi nyeusi vilivyokuwa na utambulisho wa namba ya chumba husika.

Wakati wakipita Yusuf alikuwa akiyatembeza macho yake upande huu na ule kusoma namba zilizokuwa juu ya milango ya vyumba vilivyokuwa vikitazamana na ile korido.

Yule dada mhudumu aliwaongoza hadi kwenye mlango wa mwisho kabisa ambao pia ulikuwa mlango mkubwa na imara wa mbao ngumu. Yule mhudumu aliichukua ile kadi ya kielektroniki na kuipitisha juu ya kile kitasa cha mlango kisha akakishika na kukinyonga, ule mlango ukafunguka na hapo akausukuma taratibu na kuingia mle ndani.

Jacky na Yusuf walimfuata taratibu na kuingia ndani ya kile chumba, wakajikuta wametokea kwenye chumba kikubwa sana cha kisasa. Yusuf alisimama katikati ya kile chumba akikitazama kwa namna ya kukitathmini vizuri mandhari yake.

Kilikuwa chumba kikubwa sana chenye nafasi ya kutosha. Upande wa kushoto kulikuwa na kitanda kikubwa cha mbao chenye godoro la foronya laini lililokuwa limefunikwa kwa shuka safi za rangi ya pinki.

Kando ya kile kitanda kulikuwa na mlango wa kuelekea kwenye chumba cha maliwato.

Kulikuwa na makochi mawili ya sofa nyuma ya meza ndogo fupi ya mbao yenye kibakuli kidogo cha majivu ya sigara juu yake na pembeni yake kulikuwa na kabati zuri la nguo la ukutani lililokuwa pembeni ya dirisha kubwa la kile chumba. Lile dirisha lilifunikwa kwa mapazia marefu na mepesi yaliyoruhusu hewa safi kupenya mle ndani.

Makochi yale yalikuwa yakitazamana na seti moja kubwa ya runinga pana aina ya Sumsung iliyokuwa imefungwa vizuri ukutani na kuunganishwa na king’amuzi cha kilichokuwa na chaneli nyingi za kimataifa.

Chini ya ile runinga kulikuwa na meza ndogo ambayo juu yake ilikuwa na simu ya mezani. Pembeni ya simu ile kulikuwa na kitabu kikubwa cha rangi ya njano chenye orodha ya majina na namba za simu za watu na kampuni mbalimbali.

Pia ndani ya kile chumba kulikuwa na jokofu dogo lililokuwa limesheheni vinywaji mbalimbali ndani yake.

Yule mhudumu aliziendea swichi zilizokuwa ukutani na kubonyeza swichi moja ili kuwasha kiyoyozi kilichokuwa sehemu fulani kwenye kona ya kile chumba, na hapo hewa safi ya ubaridi ilianza kusambaa mle ndani.

Jacky aligeuka akamtazama Yusuf kwa namna iliyomweleza kuwa walikuwa wamefika sehemu tulivu kama alivyomuahidi, huku akiutupia mkoba wake kitandani.

Welcome to Southern Sun, here is a quiet place and nice to enjoy. Have you ever been here before?” (Karibu Souther Sun, hii ni sehemu tulivu na nzuri ya kufurahia. Sijui umeshawahi kuja hapa kabla?) Jacky alimuuliza Yusuf huku akimtazama kwa madaha.

Nope, I've never come here even once. It's my first time today. It’s a nice place,” (Wala, sijawahi kufika hapa hata mara moja. Ni mara yangu ya kwanza leo kufika hapa. Ni sehemu nzuri) Yusuf alisema huku akizungusha macho yake kuyashangaa mandhari ya kile chumba.

“Unapaonaje hapa, pako poa au siyo?” Jacky alimuuliza Yusuf ambaye muda wote alikuwa amesimama akiwa anayashangaa mandhari ya kile chumba.

Yusuf aliitikia kwa kubetua kichwa huku macho yake yakizidi kuvinjali ndani ya kile chumba. Jacky alijitupia kitandani huku akimtazama Yusuf kwa tabasamu.

“Hivi chumba kama hiki kwa siku ni bei gani?” hatimaye Yusuf aliuliza huku akishindwa kuficha mshangao wake.

“Kwa nyinyi wenzetu mnaochezea fedha kila siku wala si ghali sana. Ni shilingi laki tatu na elfu hamsini tu kwa usiku mmoja, unapata bia mbili bure na chai ya asubuhi. Unaonaje?” Jacky alisema huku akiachia kicheko hafifu.

Yusuf alitaka kusema neno lakini akasita na kushusha pumzi za ndani kwa ndani huku akitingisha kichwa chake taratibu na kumtupia jicho yule mhudumu wa ile hoteli, ambaye muda wote alikuwa amesimama akiwatazama kwa zamu huku akitabasamu.

Jacky aligundua kuhusu hilo na kubetua mabega yake juu huku akiendelea kutabasamu.

Itaendelea...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom