Stori ya kusisimua - Kizungumkuti!

Stori ya kusisimua - Kizungumkuti!

Kizungumkuti! - 68

Na Bishop Hiluka

ILIPOISHIA

“Nzuri tu, karibuni,” Dk Masha aliitikia huku akimpa ASP Komba mkono, kisha akamsalimia Sajenti Mapambano na wote wakaketi kwenye viti. Walipoketi tu Dk Masha alivuta droo ndogo ya meza yake na kutoa humo kitabu kidogo cha kumbukumbu.

“Kitu pekee nilichokipata kutoka kwenye mfuko wa suruali ya marehemu ni hiki kitabu chake cha kumbukumbu,” Dk Masha alisema huku akinyoosha mkono wake kumpa ASP Komba kile kitabu.

ASP Komba alikipokea kile kitabu cha kumbukumbu, maarufu kama Diary na kukigeuza geuza huku akikiangalia kwa umakini. Kilikuwa kitabu kidogo cha rangi ya bluu.

“Pia kuna karatasi zingine mbili tatu, labda zitaweza kuwasaidia,” Dk Masha alisema tena huku akichukua zile karatasi na kunyoosha mkono wake kumpa ASP Komba.

Endelea...

ASP Komba alizipokea zile karatasi na kuzitupia jicho mara moja kisha akayarudisha macho yake kwenye kile kitabu cha kumbukumbu. Akakifungua na macho yake yakatua kwenye ukurasa wa kwanza tu ambapo alikutana na jina la mmiliki wa kile kitabu, “Carlos Mwamba” likiambatana na taarifa zingine binafsi ikiwemo mawasiliano yake.
ASP Komba akaonesha kushtuka kidogo kwa kuwa alimfahamu vyema Carlos Mwamba, ni wiki chache tu zilizokuwa zimepita walikutana wakaongea na Carlos Mwamba alimuahidi kuwa alitaka kulisaidia Jeshi la Polisi kiasi cha shilingi milioni 100 katika operesheni zake mbalimbali.
ASP Komba alishusha pumzi kisha akaanza kuangalia kurasa mbili tatu na hapo macho yake yakatua kwenye karatasi mbili zilizokuwa zimepachikwa kwenye ukurasa mmoja wa kile kitabu cha kumbukumbu.
ASP Komba alizitoa zile karatasi na kuzitazama kwa umakini, karatasi moja ilikuwa ni nakala kivuli (photocopy) ya hundi ya The Jacarandah Group iliyokuwa na saini na karatasi nyingine ilikuwa imeandikwa namba kadhaa za simu.
ASP Komba alizitazama zile namba kwa umakini mkubwa na kugundua kuwa namba mbili kati ya zile zilikuwa ni namba alizokuwa ameziona kwenye simu ya Yusuf, moja ikiwa ni namba ya Joram Mbezi, ambayo pale ilipewa jina la Kisu na namba ya Belinda Jackson, ambayo pale ilipewa jina la beloved coordinator.
Pia katika orodha ile kulikuwa na namba aliyoifahamu kuwa ni ya Yusuf na namba nyingine mbili ambazo hakuweza kuzifahamu. ASP Komba alijikuta akiachia tabasamu pana ambalo baadaye lilitengeneza kicheko hafifu na hivyo kuwafanya Dk Masha na Sajenti Mapambano wapate shauku ya kutaka kujua kilichokuwa kimeandikwa kwenye zile karatasi.
“Vipi, afande, kuna lolote umegundua?” Dk Masha alimuuliza ASP Komba kwa shauku huku akijitahidi kurefusha shingo yake ili ajionee kilichokuwemo kwenye zile karatasi.
“Huwezi kuamini, umenisaidia sana, dokta… nilikuwa nina hamu kubwa sana ya kukutana na huyu mtu,” ASP Komba alisema huku akiendelea kutabasamu.
“Nani, huyu marehemu?” Dk Masha alimuuliza ASP Komba kwa mshangao.
“Naam! Lakini tayari kajihukumu mwenyewe…” ASP Komba alisema na kusita kidogo, kisha kama aliyegutuka akauliza, “Na hali ya yule binti aliyekuwa na marehemu ikoje?”
“Yule binti kama atavuka kesho jioni basi ataweza kuongea,” Dk Masha alisema huku akishusha pumzi za ndani kwa ndani.
ASP Komba aliinuka kutoka kwenye kiti chake huku akiendelea kutabasamu kisha akampa ishara fulani Sajenti Mapambano ambaye pia aliinuka, wakamuaga Dk Masha.
“Nakushukuru sana, dokta, huwezi kujua ni kwa kiasi gani umeifanya kazi yangu kuwa rahisi mno, nitakutembelea kesho au keshokutwa kutegemea na hali ya yule binti itakavyokuwa, maana nina hamu kubwa ya kutaka kuongea naye.”
“Karibuni sana,” Dk Masha alijibu huku akiinuka kutoka kwenye kiti chake na kuwasindikiza ASP Komba na Sajenti Mapambano. Wakatoka nje na kuelekea walikokuwa wameegesha gari lao.
Waliingia kwenye gari lao na dereva akaliondoa, waliamua kurudi ofisini. Walipofika ofisini ASP Komba aliketi kwenye kiti chake, akaanza kupitia maandishi yaliyokuwa yameandikwa kwenye kile kitabu cha kumbukumbu cha Carlos Mwamba, ukurasa mmoja baada ya mwingine.
Kuna wakati alijikuta akisisimkwa mwili wake kutokana na kusoma mipango ya hatari iliyokuwa imeandikwa kwenye kile kitabu cha kumbukumbu ikionesha tarehe ya kutekeleza mipango ile na aina ya watu ambao wangetumika kufanikisha mipango ile.
ASP Komba hakuamini kabisa kile alichokuwa akikisoma kwenye kile kitabu cha kumbukumbu cha Carlos Mwamba, mtu aliyekuwa rafiki yake, yeye na mkewe Jackline Mgaya Mwamba. Siku zote ASP Komba aliamini kuwa Carlos ni mfanyabiashara mwenye mafanikio na raia mwema aliyependa kusaidia wengine kwa hali na mali, kumbe ni mbwa mwitu ndani ya ngozi ya kondoo!
Hadi wakati ule ASP Komba alikuwa bado akikkikodolea macho kile kitabu cha kumbukumbu akiwa haamini kama ni kweli Carlos Mwamba alikuwa nyuma ya uhalifu ule, akaamua kuingiza jina la Carlos Mwamba kwenye ile kompyuta maalumu ya Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai ya Kanda Maalumu iliyokuwa pale ofisini ili kutafuta taarifa zake.
Alipoingiza tu lile jina zilikuja taarifa nyingi zilizoonesha kuwa Carlos Mwamba alikuwa mfanyabiashara wa madini mwenye mafanikio makubwa akimiliki kampuni mbili, Mwamba Mines iliyojihusisha na biashara ya madini na Jaco Investment (ikiwa ni kifupi cha Jackline na Carlos) iliyokuwa ikihusika na ujenzi wa majumba (estates), na hakuwa na rekodi yoyote ya uhalifu.
Taarifa zile zilibainisha kuwa jina lake kamili aliitwa Carlos Michael Mwamba, mzaliwa wa jijni Mwanza, umri wake ulikuwa miaka arobaini na mbili, alikuwa na mke Jackline Mgaya Mwamba na aliwahi kupata mafunzo na kuhitimu Shahada ya Kwanza ya System Analysis and Design katika Chuo Kikuu cha Oxford Uingereza na baadaye alifanya mafunzo ya shahada ya uzamili katika masuala ya takwimu (Statistics) huku huko Oxford nchini Uingereza…
ASP Komba alishusha pumzi ndefu huku akimtazama msaidizi wake, Sajenti Mapambano, kisha akakohoa kidogo kusafisha koo lake huku akizitazama kwa makini picha kadhaa za Carlos zilizokuwa zimeambatana na taarifa ile.
“Niseme wazi, taarifa hizi zimenishtua sana, sikutegemea kama Carlos Mwamba anaweza kuwa ndiye Master Planner aliye nyuma ya uhalifu huu!” ASP Komba alisema huku akishusha pumzi.
Kisha alitoa paketi ya sigara na kuiweka kwenye pembe ya mdomo wake na kuchukua kiberiti kutoka mfukoni, akawasha ile sigara kwenye pembe ya mdomo wake na kusimama, akaelekea dirishani.
Alisimama pale dirishani na kutazama nje kupitia ukuta msafi wa kioo cha dirisha akiyatazama mandhari ya jiji la Dar es Salaam yaliyokuwa yakipendeza katika muda ule wa alasiri. Hata hivyo, hakuwa na tashwishwi yoyote katika sura yake.
Alivuta sigara yake kwa utulivu huku akiutoa moshi mwingi na kuutazama kwa makini kisha akapiga mkupuo mwingine mkubwa wa moshi na alipoitoa sigara mdomoni akapuliza moshi wake pembeni huku akiutazama kabla ya macho yake kuweka kituo kwenye magari machache yaliyokuwa yameegeshwa katika sehemu maalumu ya kuegesha magari yaliyokuwa na kesi au matatizo katika lile jengo la polisi.
Alilitazama gari la Carlos Mwamba aina ya BMW X6 xDrive 50i la rangi ya samawati lililokuwa limeharibika vibaya baada ya kupata ajali kule kwenye daraja la Mto Msimbazi katika eneo la Vingunguti.
Wakati akiwa bado amesimama pale dirishani akitazama chini mara mlango wa kile chumba ukagongwa na kufunguliwa, ASP Komba na Sajenti Mapambano wakageuza shingo zao kutazama kule mlangoni na kumuona askari mmoja aliyekuwa na cheo cha Koplo akiingia na kutembea kwa ukakamavu hadi pale dirishani kisha akasimama karibu na ASP Komba na kupiga saluti ya ukakamavu.
“Afande, kuna mtu mmoja amepiga simu akijitambulisha kama raia mwema anayeishi Tabata Segerea, amesema kuwa amesikia mzozo mkali kwenye nyumba ya jirani yake anayeitwa Carlos Mwamba kuhusiana na mgao wa fedha,” yule askari mwenye cheo cha Koplo alisema.
Maneno yale yakawafanya ASP Komba na Sajenti Mapambano waangaliane kwa makini. Kikatokea kitambo kifupi cha ukimya, kisha ASP Komba akashusha pumzi za ndani kwa ndani.

Itaendelea...

Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY
Shukrani Mr Bishop.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ingawa alikuwa mafia ila kifo cha Carlos kimenikitisha naona kama kafa mapema. Nilimuhisi kama main character
Hahahaa, mimi alinikera kumuua Kisu, na kutowapa chao waliomsaidia kwenye ile dili. Mtu kama yusuf ka-risk career yake akiamini hiyo dili ingemtoa mazima, matokeo yake hajapata hata mia, na ndio kwanza kajiongezea majanga.
Ndio maana watu makini kwenye dili kama zile wanachukua 'advance' mapemaaa

the Legend☆
 
Hahahaa, mimi alinikera kumuua Kisu, na kutowapa chao waliomsaidia kwenye ile dili. Mtu kama yusuf ka-risk career yake akiamini hiyo dili ingemtoa mazima, matokeo yake hajapata hata mia, na ndio kwanza kajiongezea majanga.
Ndio maana watu makini kwenye dili kama zile wanachukua 'advance' mapemaaa

the Legend☆
Ngoma droo.... Carlos nae hajapata hata mia badala yake "kafwarikiii"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ngoma droo.... Carlos nae hajapata hata mia badala yake "kafwarikiii"

Sent using Jamii Forums mobile app
Hahahaha. Ila ni uzembe wake, mtu kapiga dili ya 1b+ imetiki fresh afu bado akaendelea kukaa kuskilizia upepo pale pale alipokua anakaa. Ningemuona mjanja kabla hata ya dili kutiki awe kashaandaa mazingira ya kupotea kabisa na Jacky, ili ngoma ilivyotiki tu amalizane na jamaa kuwapa chao afu yeye apotee chap

the Legend☆
 
Hahahaha. Ila ni uzembe wake, mtu kapiga dili ya 1b+ imetiki fresh afu bado akaendelea kukaa kuskilizia upepo pale pale alipokua anakaa. Ningemuona mjanja kabla hata ya dili kutiki awe kashaandaa mazingira ya kupotea kabisa na Jacky, ili ngoma ilivyotiki tu amalizane na jamaa kuwapa chao afu yeye apotee chap

the Legend☆
Hiki ndo kizunzungu
 
Asante kwa somo
Hahahaaaa, mkuu the_legend moja ya sifa kubwa za mwandishi yeyote mzuri ni kufanya utafiti kabla hajaandika kuhusu kitu chochote, kama nilivyowahi kueleza mwandishi anatakiwa kuiona hadithi yake kama vile anaona sinema, asikie na sauti za wahusika, jambo linaloitwa visualization”.

Ngoja nikudokeze kidogo, zipo sifa kubwa tisa anazotakiwa kuwa nazo mwandishi, na kama utaweza kufit kwenye sifa hizi lazima utakuwa mwandishi mzuri sana unayeandika stori zinazogusa miyo ya watu:

1. Organizational skill: mwandishi mzuri wa hadithi anapaswa kuwa na uwezo mkubwa wa kuandaa na kupangilia taarifa zake kuhusiana na kisa anachokusudia kukiandika.

2. Analytical ability: mwandishi mzuri wa hadithi lazima awe na uwezo wa kuchambua taarifa na kujua kama zitagusa mahitaji halisi ya wasomaji wake, na awe na uwezo wa kutofautisha mambo muhimu na yasiyo muhimu kabla ya kuyaweka kwenye kurasa.

3. Interest in diverse topics: hadithi nzuri inahitaji kufanyiwa utafiti wa kina. Mwandishi mzuri anapaswa kufanya utafiti kwa kila jambo analoliandikia bila kujali ukubwa au udogo wa jambo lenyewe.

4. Empathy for your audience: mwandishi lazima awe na uwezo wa kuzama ndani ya mitazamo ya wasomaji wake na kuyaelewa mambo wanayoyapenda, mitindo yao, tabia zao, matamanio yao n.k. ili kuhakikisha kuwa wanashiriki kwenye hadithi yake na kuwa sehemu ya hadithi kwa kuamini kuwa ni sehemu ya maisha yao, pia awe na uwezo wa kuwafanya wasichoke kuifuatilia.

5. Writing skills: mwandishi anapaswa kuwa na uwezo wa kuandika kwa ufasaha kwa lugha iliyobebwa na msingi imara wenye kumvutia yeyote atakayesoma, lugha ambayo inapaswa kuwa ya uwazi na lazima awe na uwezo mzuri katika matumizi ya sarufi.

6. Ability to think visually: mwandishi anapaswa kuwa na uwezo wa kuyabeba mawazo yake sambamba na picha (visualization), awe na uwezo wa kuiona taswira kupitia maandishi yake na awaoneshe wasomaji wake kile kinachoendelea kwenye hadithi yake.

7. Creativity: Ubunifu ni jambo muhimu sana kwa mwandishi, ubunifu unahitajika sana kwa ajili ya kuweza kuandika hadithi nzuri itakayogusa mioyo na hisia za wasomaji. Hata hivyo, huwezi kuwa mbunifu kama husomi kazi za waandishi wengine.

8. Presentation and selling skills: mwandishi lazima awe na uwezo mkubwa wa kuwasilisha mawazo yake kwa ufanisi na kuiuza kazi yake kwa wateja.

9. Ability to work on a team: kiutendaji wakati mwingine mwandishi hujikuta akilazimika kufanya kazi na watu wengine wenye mahitaji na mitazamo tofauti, hivyo, anapaswa awe na uwezo wa kufanya kazi kwenye kundi…

Nimeona nitoe somo kidogo kwa faida ya wengine. sasa tuendelee na KIZUNGUMKUTI...

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom