Mine eyes
JF-Expert Member
- Apr 11, 2016
- 6,581
- 7,232
kabisa yaani!Wewe weka story na ww huwezi kuwa mume mwenza kirahisi rahisi hivi
Sent using Jamii Forums mobile app
kabisa yaani!Wewe weka story na ww huwezi kuwa mume mwenza kirahisi rahisi hivi
Na wewe umo mkuu?Hivi Shunie tupo wangapi babe?
Naona kama unafuata nyayo za Jacky kimya kimya!!
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Heshima yako mkuu Bishop[emoji114][emoji114][emoji114] Hakika hiyo tasnia ya uandishi unaimudu ipasavyoHahahaaaa, mkuu the_legend moja ya sifa kubwa za mwandishi yeyote mzuri ni kufanya utafiti kabla hajaandika kuhusu kitu chochote, kama nilivyowahi kueleza mwandishi anatakiwa kuiona hadithi yake kama vile anaona sinema, asikie na sauti za wahusika, jambo linaloitwa “visualization”.
Ngoja nikudokeze kidogo, zipo sifa kubwa tisa anazotakiwa kuwa nazo mwandishi, na kama utaweza kufit kwenye sifa hizi lazima utakuwa mwandishi mzuri sana unayeandika stori zinazogusa miyo ya watu:
1. Organizational skill: mwandishi mzuri wa hadithi anapaswa kuwa na uwezo mkubwa wa kuandaa na kupangilia taarifa zake kuhusiana na kisa anachokusudia kukiandika.
2. Analytical ability: mwandishi mzuri wa hadithi lazima awe na uwezo wa kuchambua taarifa na kujua kama zitagusa mahitaji halisi ya wasomaji wake, na awe na uwezo wa kutofautisha mambo muhimu na yasiyo muhimu kabla ya kuyaweka kwenye kurasa.
3. Interest in diverse topics: hadithi nzuri inahitaji kufanyiwa utafiti wa kina. Mwandishi mzuri anapaswa kufanya utafiti kwa kila jambo analoliandikia bila kujali ukubwa au udogo wa jambo lenyewe.
4. Empathy for your audience: mwandishi lazima awe na uwezo wa kuzama ndani ya mitazamo ya wasomaji wake na kuyaelewa mambo wanayoyapenda, mitindo yao, tabia zao, matamanio yao n.k. ili kuhakikisha kuwa wanashiriki kwenye hadithi yake na kuwa sehemu ya hadithi kwa kuamini kuwa ni sehemu ya maisha yao, pia awe na uwezo wa kuwafanya wasichoke kuifuatilia.
5. Writing skills: mwandishi anapaswa kuwa na uwezo wa kuandika kwa ufasaha kwa lugha iliyobebwa na msingi imara wenye kumvutia yeyote atakayesoma, lugha ambayo inapaswa kuwa ya uwazi na lazima awe na uwezo mzuri katika matumizi ya sarufi.
6. Ability to think visually: mwandishi anapaswa kuwa na uwezo wa kuyabeba mawazo yake sambamba na picha (visualization), awe na uwezo wa kuiona taswira kupitia maandishi yake na awaoneshe wasomaji wake kile kinachoendelea kwenye hadithi yake.
7. Creativity: Ubunifu ni jambo muhimu sana kwa mwandishi, ubunifu unahitajika sana kwa ajili ya kuweza kuandika hadithi nzuri itakayogusa mioyo na hisia za wasomaji. Hata hivyo, huwezi kuwa mbunifu kama husomi kazi za waandishi wengine.
8. Presentation and selling skills: mwandishi lazima awe na uwezo mkubwa wa kuwasilisha mawazo yake kwa ufanisi na kuiuza kazi yake kwa wateja.
9. Ability to work on a team: kiutendaji wakati mwingine mwandishi hujikuta akilazimika kufanya kazi na watu wengine wenye mahitaji na mitazamo tofauti, hivyo, anapaswa awe na uwezo wa kufanya kazi kwenye kundi…
Nimeona nitoe somo kidogo kwa faida ya wengine. sasa tuendelee na KIZUNGUMKUTI...
Nimesoma Creative Writing... hasa uandishi wa filamu na michezo ya kuigiza...Heshima yako mkuu Bishop[emoji114][emoji114][emoji114] Hakika hiyo tasnia ya uandishi unaimudu ipasavyo
the Legend☆
Nimooooooo
Akili kubwaaaa [emoji8]Hahahaaaa, mkuu the_legend moja ya sifa kubwa za mwandishi yeyote mzuri ni kufanya utafiti kabla hajaandika kuhusu kitu chochote, kama nilivyowahi kueleza mwandishi anatakiwa kuiona hadithi yake kama vile anaona sinema, asikie na sauti za wahusika, jambo linaloitwa “visualization”.
Ngoja nikudokeze kidogo, zipo sifa kubwa tisa anazotakiwa kuwa nazo mwandishi, na kama utaweza kufit kwenye sifa hizi lazima utakuwa mwandishi mzuri sana unayeandika stori zinazogusa miyo ya watu:
1. Organizational skill: mwandishi mzuri wa hadithi anapaswa kuwa na uwezo mkubwa wa kuandaa na kupangilia taarifa zake kuhusiana na kisa anachokusudia kukiandika.
2. Analytical ability: mwandishi mzuri wa hadithi lazima awe na uwezo wa kuchambua taarifa na kujua kama zitagusa mahitaji halisi ya wasomaji wake, na awe na uwezo wa kutofautisha mambo muhimu na yasiyo muhimu kabla ya kuyaweka kwenye kurasa.
3. Interest in diverse topics: hadithi nzuri inahitaji kufanyiwa utafiti wa kina. Mwandishi mzuri anapaswa kufanya utafiti kwa kila jambo analoliandikia bila kujali ukubwa au udogo wa jambo lenyewe.
4. Empathy for your audience: mwandishi lazima awe na uwezo wa kuzama ndani ya mitazamo ya wasomaji wake na kuyaelewa mambo wanayoyapenda, mitindo yao, tabia zao, matamanio yao n.k. ili kuhakikisha kuwa wanashiriki kwenye hadithi yake na kuwa sehemu ya hadithi kwa kuamini kuwa ni sehemu ya maisha yao, pia awe na uwezo wa kuwafanya wasichoke kuifuatilia.
5. Writing skills: mwandishi anapaswa kuwa na uwezo wa kuandika kwa ufasaha kwa lugha iliyobebwa na msingi imara wenye kumvutia yeyote atakayesoma, lugha ambayo inapaswa kuwa ya uwazi na lazima awe na uwezo mzuri katika matumizi ya sarufi.
6. Ability to think visually: mwandishi anapaswa kuwa na uwezo wa kuyabeba mawazo yake sambamba na picha (visualization), awe na uwezo wa kuiona taswira kupitia maandishi yake na awaoneshe wasomaji wake kile kinachoendelea kwenye hadithi yake.
7. Creativity: Ubunifu ni jambo muhimu sana kwa mwandishi, ubunifu unahitajika sana kwa ajili ya kuweza kuandika hadithi nzuri itakayogusa mioyo na hisia za wasomaji. Hata hivyo, huwezi kuwa mbunifu kama husomi kazi za waandishi wengine.
8. Presentation and selling skills: mwandishi lazima awe na uwezo mkubwa wa kuwasilisha mawazo yake kwa ufanisi na kuiuza kazi yake kwa wateja.
9. Ability to work on a team: kiutendaji wakati mwingine mwandishi hujikuta akilazimika kufanya kazi na watu wengine wenye mahitaji na mitazamo tofauti, hivyo, anapaswa awe na uwezo wa kufanya kazi kwenye kundi…
Nimeona nitoe somo kidogo kwa faida ya wengine. sasa tuendelee na KIZUNGUMKUTI...
Dah Carlos masikiniKizungumkuti! - 67
Na Bishop Hiluka
“Karibuni,” Jacky alisema baada ya kuwafungulia lile geti na na kusimama kando huku akiwatazama kwa umakini, hata hivyo, uso wake ulishindwa kuficha mshangao aliokuwa nao wakati akiwakaribisha ndani. Kabwe alimtazama kwa makini na kuachia tabasamu huku akiingia ndani na kufuatwa nyuma na Liston.
“Vipi hapa?” Kabwe alimuuliza Jacky huku akimkazia macho mara baada ya kuketi kwenye sofa pale sebuleni.
Endelea...
“Ah, ndo’ kama mlivyosikia!” Jacky aliongea kwa sauti ya unyonge huku akiwa amesimama akiwatazama wote wawili kwa makini.
“Kusikia nini, mbona sikuelewi, shem?” Kabwe alimuuliza Jacky huku akimkazia macho kwa mshangao.
“Kwani hamsomi magazeti, jamani au hamperuzi hata mitandao kujua yanayoendelea duniani?” Jacky aliwauliza huku akiwatazama kwa mshangao.
“Tunasoma lakini habari za magazetini hazituhusu…” Kabwe alijibu huku akionekana kupuuza kile alichokuwa akiambiwa na Jacky. Jacky alitaka kusema neno lakini Kabwe alimkatisha kwa ishara.
“Sikiliza shem, watu wa magazeti wanafanya biashara yao, watu wa mitandao wanaingiza fedha zao na sisi tunayafanya ya kwetu. Ndiyo nchi ya viwanda inavyokwenda, kila mtu na mambo yake, au siyo?” Kabwe alisema huku akicheua, na muda huo huo ile sebule ikaenea harufu ya pombe.
“Lakini habari zilizotoka leo kwenye magazeti zinatuhusu, ni kwamba mambo yetu ndiyo yamekwama…” Jacky alisema kwa huzuni na kukatishwa na sauti ya Liston aliyepiga ngumi juu ya meza huku akifoka.
“Haiwezekani! Kwani ile fedha mmeirudisha benki?” Liston alimuuliza Jacky huku macho yake yakiwaka kwa ghadhabu.
“Fedha yote ipo!” Jacky alisema huku akimtazama Liston kwa wasiwasi.
“Sasa kilichokwama ni nini? Unajua shem, usituchanganye hapa… kwanza niambie ukweli, ni kweli Kisu ameuawa maana tumesikia habari juu juu?” Kabwe alidakia huku akimkazia macho Jacky kisha akaendelea bila hata kusubiri jibu lake, “Mmemuua Kisu na sisi hatujui hatma yetu ni ipi! Naomba usituchanganye kabisa…” Kabwe alifoka.
Jacky alimtazama Kabwe kwa makini huku akijaribu kutafakari namna ya kukabiliana na hasira za wale wanaume endapo wangeamua kuanzisha vurugu.
“Kwanza mzee yuko wapi? Tunataka kuongea naye kama wanaume,” kabwe alimuuliza Jacky huku aakimkazia macho.
“Katoka kidogo lakini atarudi muda wowote kuanzia sasa.”
“Kama kakuachia mzigo wetu, tupe tusepe ili kila mtu afe na chake, maana sasa naona mnaanza uswahili,” Kabwe alimwambia Jacky huku akionekana kuanza kupandwa na jazba.
“Hajaniachia mzigo wowote wa kuwapeni leo, ninachojua kesho ndiyo mnatakiwa mje kuchukua mzigo wenu… labda nimpigie simu kumjulisha kuwa mmekuja leo,” Jacky alisema huku akiichukua simu yake iliyokuwa juu ya meza, kisha alibofya namba ya Carlos, akapiga na kusikiliza. Simu ya Carlos ilikuwa haipatikani!
Jacky alishtuka sana na kuitazama ile simu kwa mshangao kisha alipiga tena lakini bado simu ya Carlos ilikuwa haipatikani! Akashusha pumzi za ndani kwa ndani huku akiwatazama Kabwe na Liston katika hali ya kukata tamaa. “Simu yake haipatikani,” Jacky alisema kwa wasiwasi.
“Naona sasa mnatuchanganya, Kisu ameshakufa na sijui kama mlishamkatia chake, na sisi mnaanza kutuletea ngonjera… sikiliza tunachotaka ni hela yetu ama sivyo nyumba hii itawaka moto,” Kabwe alisema kwa ghadhabu.
“Msiwe hivyo jamani, hebu jaribuni kuwa na subira kama ni hela yenu ipo…” Jacky alisema kwa sauti laini huku akiachia tabasamu na kulegeza macho yake akijaribu kuwalainisha.
“Bwana ee, usitulegeze macho yako hapa ukadhani utamrusha mtu roho. Harushwi mtu roho hata kwa nini! Tunachotaka ni mzigo wetu tu, au kama vipi tutalianzisha!” Kabwe alifoka kwa sauti kubwa huku akiinuka kutoka kwenye lile sofa alilokuwa amekalia.
Jacky alimtazama Kabwe kwa makini huku akijiandaa kwa lolote endapo wangetaka kuleta vurugu kisha akayahamishia macho yake kwa Liston ambaye muda wote alikuwa ametulia kwenye kochi akimtazama huku macho yake yakiwaka kwa ghadhabu.
“Basi naomba mvute subira tu jamani, hakawii kurudi,” Jacky alisihi huku akiupima upepo.
Liston na Kabwe wakaangaliana. “Unasemaje kamanda wangu, tumsubiri au tukautwike halafu tuwajie jioni?” Kabwe alimuuliza Liston.
“Jioni ya saa ngapi? Wanaweza kutukimbia hawa,” Liston aliuliza huku naye akiinuka kutoka kwenye sofa.
“Tuwazukie mapema tu…”
“Poa, twen’zetu!” Liston alisema na hapo hapo wakaondoka wakimwacha Jacky amepigwa butwaa.
* * * * *
Saa tisa alasiri, gari lenye maandishi ya POLISI ubavuni aina ya Nissan Patrol la rangi nyeusi liliingia kwenye lango kuu la kuingilia katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ilala ya Amana, katika eneo la Amana Ilala jijini Dar es Salaam.
Walinzi wa hospitali ile ya Amana waliokuwa nadhifu kwa sare zao za ulinzi walimwelekeza Sajenti Mapambano aliyekuwa akiendesha lile gari sehemu maalumu ya kuliegesha gari lake katika maegesho maalumu ya magari.
Baada ya lile gari kuegeshwa katika eneo lile la maegesho ya magari, ASP Komba, ambaye muda ule alikuwa amevalia sare rasmi za polisi na cheo chake cha nyota tatu kikionekana vyema kwenye mabega yake, alishuka kutoka katika lile gari.
Sajenti Mapambano naye aliteremka na hapo wakaanza kupiga hatua kikakamavu wakielekea kwenye jengo la ofisi za madaktari wa hospitali ile. Walifika na kusimama mbele ya mlango mmoja na hapo ASP Komba akagonga mlango ule mara moja kisha akakishika kitasa, akakinyonga na kuusukuma mlango.
Mlango ulisalimu amri na kumruhusu ASP Komba kuingia ndani ya ile ofisi, Dk Fadhili Masha ambaye alikuwa ameinamisha uso wake akisoma taarifa fulani za mgonjwa kwenye faili alilokuwa amelishika mkononi aliinua uso wake na macho yake yakakutana na yale ya ASP Komba, akaachia tabasamu huku akiinuka kuwalaki ASP Komba na Sajenti Mapambano.
Dk Masha alikuwa mwanamume mrefu mnene na alikuwa mweupe kama chotara, akiwa na umri wa miaka takriban hamsini alionekana mwenye nguvu na misuli imara ya mikononi iliyotuna kikamilifu. Alikuwa na upara mpana uliokuwa unawaka na uso wake ulikuwa mpana huku miwani yake mikubwa ikiwa imeyahifadhi macho yake makubwa.
Alikuwa amevaa suruali ya bluu yenye mistari myeupe, shati la rangi ya samawati lililokuwa na mistari ya bluu ya pundamilia na juu ya lile shati alivaa koti refu jeupe la kidaktari na kuning’iniza shingoni kwake kifaa cha kupimia mapigo ya moyo ambacho kitaalamu kiliitwa stethoscope. Miguuni yule daktari alikuwa amevaa viatu vizuri vyeusi vya ngozi.
“Naona mmeniwahi, sasa hivi nilikuwa namalizia kuisoma hii taarifa kisha niondoke!” Dk Masha alisema baada ya kuwakaribisha wale maofisa wa polisi.
“Majukumu yametubana, dokta… vipi habari za muda?” ASP Komba alisema huku akinyoosha mkono wake kumsalimia Dk Masha.
“Nzuri tu, karibuni,” Dk Masha aliitikia huku akimpa ASP Komba mkono, kisha akamsalimia Sajenti Mapambano na wote wakaketi kwenye viti. Walipoketi tu Dk Masha alivuta droo ndogo ya meza yake na kutoa humo kitabu kidogo cha kumbukumbu.
“Kitu pekee nilichokipata kutoka kwenye mfuko wa suruali ya marehemu ni hiki kitabu chake cha kumbukumbu,” Dk Masha alisema huku akinyoosha mkono wake kumpa ASP Komba kile kitabu.
ASP Komba alikipokea kile kitabu cha kumbukumbu, maarufu kama Diary na kukigeuza geuza huku akikiangalia kwa umakini. Kilikuwa kitabu kidogo cha rangi ya bluu.
“Pia kuna karatasi zingine mbili tatu, labda zitaweza kuwasaidia,” Dk Masha alisema tena huku akichukua zile karatasi na kunyoosha mkono wake kumpa ASP Komba.
Itaendelea...
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] mine bwana
Mwehu ww I wish nikuone aisee kwa vituko vyako usikute mbabu ww na wajukuu
Hahahah
Khaaaaa makubwa hayaNimooooooo