Hebu tuwe realistic, tusijaribu kubadilisha ukweli wa kilichosemwa na Mzee Makamba, hapo hakuna siasa wala chochote kingine.
Kwa hiyo video uliyoiweka hapo juu, nimemsikia kwa kinywa chake akitamka; "watu wazuri hawafi" huyu amekosea, aambiwe ukweli, asitetewe akazidi kuharibika, mnamponza.
Ndio maana Samia ameomba radhi kwa hiyo kauli yake, kuonesha mzee alikosea.
..mimi nimesikiliza kwa kirefu zaidi kabla na baada ya hayo maneno yanayokukwaza.
..Ni kweli Mzee Makamba amekosea.
..Lakini ni makosa na nia mbaya kwa baadhi yetu kudai Mzee Makamba alimlenga Magufuli.
..Jambo lingine ni kwamba Rais Ssh aliomba radhi na kuliweka sawa suala hili.