Special message to Mama Janeth Magufuli

Special message to Mama Janeth Magufuli

Mh. Makamba baba yake January kasema kuwa Kinana na Kikwete hawajafa maana watu wabaya huwa wanakufa akimaanisha Dkt Magufuli alikuwa mtu mbaya ndiyo maana alikufa, Mkapa alikufa kwa sababu alikuwa mtu mbaya, Mwl Nyerere alikufa kwa sbabau alikuwa mtu mbaya, Mzee Karume alikufa kwa sababu alikuwa mtu Mbaya, Horace Kolimba alikufa kwa sababu alikuwa mtu Mbaya …..
Umesema uwongo.

Alisema watu wazuri hawafi mapema, ndiyo maana Kikwete na Kinana bado wapo.
 
Umesema uwongo.

Alisema watu wazuri hawafi mapema, ndiyo maana Kikwete na Kinana bado wapo.
Si ndiyo maana yake watu wabaya wanakufa kama alivyokufa Dkt Magufuli, wale watu wema kama yeye Makamba hawatakuja kufa
 
Kwa hali ilivyo ya kisiasa hapa nchini na mahusiano ya marehemu na hawa walioshika hatamu kwa Sasa....na ukizingatia matamshi yaliyopita ya watu hao au waliokaribu na watu hao juu ya marehemu ni rahisi kuleta tafsiri hiyo katika lugha ya picha na mafumbo........Kwa kifupi mzee Makamba amewehuka kwa kauli haijalishi wajihi wa marehemu
Ma-rope kaongea maneno tu. Aliyesemwa yeye alifanya kwa vitendo.
 
Hivi tunaelewana kweli? Nakwambia hali ya uchaguzi ilivyo ni kwamba piga uwa lazima ccm ndio atangazwe mshindi wa nafasi ya urais kwa njia yeyote ile, na miaka yote kumekuwa na malalamiko hayo.
Prof. Assad alisema "watanzania wanashiriki kupiga kura ila hawashiriki uchaguzi" ila wewe bado ulikuwa unaamini kuna uwezekano wa siku kutangazwa mshindi wa urais asiye mgombea wa ccm, ndio nimekuuliza atatangazwa na nani huyo mshindi? Mpaka watu wanataka tume huru wanajua tatizo lilipo ila wewe mwezetu kumbe ulikuwa unaona ipo siku matokeo yatabadilika kwa mfumo huo huo wa uchaguzi jinsi ulivyo.

Usichanganye kuelewana na kukubaliana na utakacho. Kutangazwa mshindi ni jambo tofauti na matokeo ya jumla ya uchaguzi. Kadiri miaka ilivyokuwa inasonga wagombea wa upinzani kura zao zilikuwa zinazidi kupanda. Na hiyo ni kuanzia udiwani, ubunge hadi kura urais kwani huo ndio uhalisia.

Labda uchaguzi chini ya Magufuli ulikuwa tofauti na uhalisia, wakati wa Magufuli malalamiko hayakuwa wizi wa kura bali kunajisi uchaguzi. Jitahidi uelewa hapo. Naona umejikita kwenye wizi, wakati kipindi cha wizi, kura za wapinzani zilikuwa zinazidi kupanda maana ndio uhalisia, lakini wakati wa Magufuli matokeo yakawa kinyume na uhalisia.
 
Mbona mama kaeleza vizuri kuwa hakuwa na nia mbaya alikuwa anajaribu kusahihisha aliposema Mama asipoweza asifike mwaka 2015 Mungu ataleta mwingine mzuri, ndipo akachomekea wazuri huwa hawafi.
Mama aliingia kwenye mind ya huyu ding ? Tafsiri inaconnect direct kutokana na phycho analysis watu waliyonayo juu ya kundi hili.ndani ya ccm .kwani nani.hawajui hawa ?
 
Usichanganye kuelewana na kukubaliana na utakacho. Kutangazwa mshindi ni jambo tofauti na matokeo ya jumla ya uchaguzi. Kadiri miaka ilivyokuwa inasonga wagombea wa upinzani kura zao zilikuwa zinazidi kupanda. Na hiyo ni kuanzia udiwani, ubunge hadi kura urais kwani huo ndio uhalisia.

Labda uchaguzi chini ya Magufuli ulikuwa tofauti na uhalisia, wakati wa Magufuli malalamiko hayakuwa wizi wa kura bali kunajisi uchaguzi. Jitahidi uelewa hapo. Naona umejikita kwenye wizi, wakati kipindi cha wizi, kura za wapinzani zilikuwa zinazidi kupanda maana ndio uhalisia, lakini wakati wa Magufuli matokeo yakawa kinyume na uhalisia.
Kwenye kutangazwa mshindi ndio penye tatizo, hapo ndio ccm panapo wafanya waendelee kubaki madarakani, sasa wewe ambaye ulikuwa unasubiria kumzidi ccm kwa kura nyingi kwenye uchaguzi ndio nakuuliza nani atakutangaza wewe kuwa ndio mshindi au ndio yale ya marehemu Maalim Seif ya kujitangaza mwenyewe?

Ndiyo maana nakwambia kuwa ccm wamejimilikisha hiyo nafasi ya urais kuwa ni yao tu kivyovyote vile, watu wanasema ccm wanategemea dola kubaki madarakani watu wanataka tume huru ya uchaguzi yote hayo kwa sababu wameona tatizo lilipo. Ila wewe unaniambia mie napotosha na kwamba et upinzani kura zao zilikuwa zinaongezeka hivyo unaamini ingekuja kutokea upinzani kupata kura nyingi za urais na kupata urais!

Elewa kwamba tatizo sio ccm kuiba kura tu bali ni kwamba ccm wanatumia njia zozote zile ili kubaki madarakani, we kubali tu ukweli wa kwamba ccm wanawaanchia ubunge na udiwani ndio mgawane ili kubalance ila sio urais.
 
Si ndiyo maana yake watu wabaya wanakufa kama alivyokufa Dkt Magufuli, wale watu wema kama yeye Makamba hawatakuja kufa
Na kwanini iwe kama alivyokufa Magufuli na isiwe kama alivyokufa Mkapa au Nyerere?! Kwanini mumlishe maneno ambayo hajayasema na kuleta tafsiri mnazotaka nyinyi?!
 
Na kwanini iwe kama alivyokufa Magufuli na isiwe kama alivyokufa Mkapa au Nyerere?! Kwanini mumlishe maneno ambayo hajayasema na kuleta tafsiri mnazotaka nyinyi?!
Nyerere na Mkapa hawakufa katikati ya uongozi wao, walimaliza muda wao na wakastaafu. Lakini pia inajulikana hakukuwa na mahusiano mazuri kati ya Mzee Makamba na Magufuli, kwahiyo ipo wazi kwamba Mzee makamba kamkusudia Magufuli ambaye hakufika 2025 kumalizia awamu yake hivyo kwa sababu Samia ni mtu mzuri hivyo hutokufa kabla ya hiyo 2025 atakuwa hai kama JK na Kinana ambao bado wako hai.
 
Nyerere na Mkapa hawakufa katikati ya uongozi wao, walimaliza muda wao na wakastaafu. Lakini pia inajulikana hakukuwa na mahusiano mazuri kati ya Mzee Makamba na Magufuli, kwahiyo ipo wazi kwamba Mzee makamba kamkusudia Magufuli ambaye hakufika 2025 kumalizia awamu yake hivyo kwa sababu Samia ni mtu mzuri hivyo hutokufa kabla ya hiyo 2025 atakuwa hai kama JK na Kinana ambao bado wako hai.
Kuna mahali popote palisemwa kuhusu yeyote kufa katikati ya uongozi wake?! Maelezo yako yote ni ya kufanya assumptions.
 
Acha uchochezi na uchongqnishi mleta mada. Hakuna aliyemnanga jiwe leo. Hayo ni mawazo yako tu.

Hebu mtaje mtu aliyemtaja jiwe kwa jina lake. Vinginevyo ni uzushi na uzandiki tu unaojaribu kuueneza.
Ulitaka ataje jina? Kwahiyo yale maneno alikuwa amemulenga nani? Tena nusu aropoke ila kwakuwa nana alikuwepo akasita.
Mtu akifanya ubaya hawezi nyamaza lazima aropoke tu maana nafsi inamuuma.
 
Nyerere na Mkapa hawakufa katikati ya uongozi wao, walimaliza muda wao na wakastaafu. Lakini pia inajulikana hakukuwa na mahusiano mazuri kati ya Mzee Makamba na Magufuli, kwahiyo ipo wazi kwamba Mzee makamba kamkusudia Magufuli ambaye hakufika 2025 kumalizia awamu yake hivyo kwa sababu Samia ni mtu mzuri hivyo hutokufa kabla ya hiyo 2025 atakuwa hai kama JK na Kinana ambao bado wako hai.
Kitendo cha kusema eti mtu mzuri hafi kasoro tu ataje jina. Hivi unafikiri wanaweza nyamaza milele? Ndo wanajisema hivyo, subiri kwenye kampain tutaona mengi.

Rip jpm wetu mzuri
 
Kuna mahali popote palisemwa kuhusu yeyote kufa katikati ya uongozi wake?! Maelezo yako yote ni ya kufanya assumptions.
Kasema Samia wanamchagua hiyo 2025 na kama akifa wataweka mwengine ila akasema Samia hawezi kufa kwa sababu wazuri hawafi, sasa hapo unashindwa kuelewa nini kwamba kakusudiwa Magufuli ambaye wanamtambua kuwa ni mbaya na ndio aliyekufa kabla kufika 2025? Kwanza jiulize suala la wazuri na wabaya limekujaje na hao wabaya ni akina nani?
 
Kwani kiongozi aliyekufa ni jiwe peke yake? Mkapa, Nyerere, Kawawa, Karume, n.k hawakuwa viongozi?

Acheni kusambaza uzushi na uzandiki. Lkn bahati nzuri hamna cha kumfanya
😏😏😏😏😏😏😏😏😏😏😏😏😏😏
 
Kwani kiongozi aliyekufa ni jiwe peke yake? Mkapa, Nyerere, Kawawa, Karume, n.k hawakuwa viongozi?

Acheni kusambaza uzushi na uzandiki. Lkn bahati nzuri hamna cha kumfanya
Hao uliyowataja ni watu wabaya kwa Mzee makamba? Tunajua Magufuli (aliye mrekodi Mzee Makamba) ndio mtu mbaya kwa Mzee makamba na ndio rais ambaye kafia madarakani hakumaliza muda wake wa uongozi hadi hiyo 2025, ndio maana Mzee makamba anamwambia Samia kuwa yeye atafika 2025 hatokufa kwa sababu ni mtu mzuri.
 
Back
Top Bottom