Ume elevate mjadala, kwa namna ambayo nafikiri ni ya juu zaidi kwenye uzi huu.
Hayo mambo ya majini na watu kuongea lugha tofauti ni mambo ambayo hatujayajua vizuri, kwa sababu hatujui vizuri ubongo unavyofanya kazi, na inawezekana babu alikuwa sehemu fulani miaka ya nyuma akapata kujua hizo kugha, sisi hatujui, na akiwa katika haki fulani anaongea, kurahisisha majibu, tunaaema hayo ni majini yanaongea.
Inawezekana ni majini kweli. Hapo itabidi tujue namna ya kutenganisha majini na habari nyingine za kisaikolonia na zinazoelezeka vizuri kibaiolojia tu. Kuna chunguzi zinazotakiwa kuwa logical, non self contradicting, provable etc. Sio hqbari za kuamini kabla ya uchunguzi.
Inawezekana jibu si manini wala magonjwa ya kisaikolojia. Inawezekana babu anawachezea tu watu akili (I hooe not).
Kuna jamaa wawili wakikamatwa Mombasa wanacheza ngoma uchi kama vichaa. Wametelekeza gari waliloliiba. Ikasemwa kwamba wameiba gari lenye alarm ya uchawi, unewawehusha. Watu wanaoamini mambo bika kutaka uthibitisho wala uchunguzi wakakimbikia jibu rahisi. Uchawi huu. Kama kuna mtu anabisha uchawi jibu ni hili. Itakuwaje watu wazima wacheze uchi vike katika mazingira yale ya kuiba gari? Watu wakasema huu ni uthibitisho wa uchawi.
Nikawaambia nit so fast. Tuchunguze zaidi jamani. Mbona tunakuwa rahisi kusema uchawi?
Na kweli. Baada ya siku chache, polisi wa Mombasa wakawakamata wale watu. Kumbe walikiowa wafanye vike ili kumtangaza "fundi" aliyeiwekea alarm ile gari apate wateja zaidi.
Kwa hiyo unaweza kuanza uchunguzi ukifikiri jibu kitakuwa ama ugonjwa wa akiki au jini, ukakuta hakuna ugonjwa wa akiki wala jini, jibu tofauti kabisa.
Zaidi, mimi kama mtu ninayekubali kwamba imani haziji bila misingi, nakubali haki za kikatiba na za Universal Declaration of Human Rights za kuanzia December 10 1948, kwamba kila mtu ana haki ya kuamini anavyotaka.
Lakini habari za imani zikiletwa JF kufanyiwa mijadala huru, zinafanyiwa mijadala huru.
Mijadala huru ni kaulimbiu ya JF.
Sent using
Jamii Forums mobile app