Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote hayupo.
Angekuwepo, dunia hii isingekuwa na baya lolote.
Uwepo wa mabaya katikadunia hii, kifo, matetemeko, tsunamis etc, unathibitisha Mungu huyo hayupo.
Angekuwepo, asingeuumba ulimwengu huu kwa ukatili hivyo ukawa na mabaya hayo yote.
Mungu huyo katungwa tu na watu katikakupambana na mazingira yao duniani.
Kipi kigumu kuelewa hapo?
Nikikwambia sijui square root ya 2 ni nini, lakini najua si 10, kwa sababu square root ya 2 ni lazima iwe ndogo kuliko 2, utakubalihilo jibu kama likosawa?
Mungu mjuzi wa yote na mwenye upendo wote yupo.
Asingekuwepo, ulimwengu usingekuwepo.
Haiwezekani, mtu awe alivyo kama hakuumbwa na Mungu, Haiwezekani kuwe hakuna Mungu akisha mtu kwa bahati mbaya ahitaji macho kuona, masikio kusikia, miguu kutembea, mikono kushika, ngozi kuhisi n.k, bila Mungu hivi vitu haviwezekani kuwepo.
Mungu anaupendo, na ndio maana akaweka guidelines watu wazifuate, kutozifuata haimaanishi kuwa Mungu hayupo, kuwepo kwa division Zero mashuleni haimaanishi kuwa hakuna elimu.
Uwepo wa kifo, ni ushahidi wa uwepo wa Mungu, kwa sababu katika Quran amesema kuwa yeye ndio wa milele, hivo mtu hawezi kuwa wa milele, LAZIMA AFE! kuwepo kwa matetemeko, nayo ni ushahidi wa uwepo, kwani bila ya hizi events, dunia isingetosha, ( FYI: Hata wanasayansi wanatambua kuwa hizi events ni essential for life cycle of the earth) uwepo wa mabaya nayo ni ushahidi wa uwepo wake, kwa sababu amesema kuwa Muovu ataadhibiwa na mwema atazawadiwa mazuri. Na pia hoja yako hii ni dhaifu, kama unaamini uwepo wa mazuri basi ndio uwepo wake, bila shaka mazuri yapo mengi duniani!
🙂
Fikra ya uwepo wa muumbaji ni fikra ambayo ni halisi na hikutungwa. Anything complex must have a creator, na kama hakuna creator, then nothing can exist. Ushahidi wa hili upo mbele ya macho yako, nikikwambia simu unayotumia haina mtengenezaji utanibishia, tena vipi ukatae ulimwengu uliopo perfect ukose muumbaji?
Tambua kuwa, Mungu amabe sio kiumbe, hafananishwi na Square root, wala pembe tatu, katika kuthibitisha uwepo wake, mifano yako hii marufu ni batil.
Mungu mwenye upendo wote - Mungu ambae anakupa hewa ya Oxygen uvute bure ili uishi, hospitali unalipia. Mungu amekujaalia wanyama na miti kwa ajili ya uwepo wa mtu, je huu sio upendo? Mungu anaeleta Neema duniani, Mvua, chuma na madini mengine ambayo leo hii unayatumia kujinufaisha akisha unasema kuwa mungu hayupo?
Ingekuwa Mungu hayupo, tena what is the purpose of life? Hivi wewe inaingia akili kuwa hapa dunia mtu anakudhulumu, anakuibiwa na kukutesa, unataka kunambia kuwa ukifa basi ndio hamna kitu kwako uldhulumiwa na kuteswa?
Unaweza kuelezea ulimwengu umewezaje kuwa in a perfect order kupitia coincidence?
Ikiwa Unaamini kuwa sisi tulikuwa vijidudu tu hapo mwanzo, hivo vijidudu vilianzaje kujitengeza kwenye mme na mke? vilijuaje kuwa vitahitaji mdomo kula na ass kunya? vilijuaje hivo whatever you call them kuwa vitahitaji miguu, kwanini viligeuka kuwa mtu na sio nyoka? au kwanini sote hatukuwa one animal ila tumetofautiana?
Kama hakuna Muumbaji kwanini basi hatuoni mtu akitokea nje ya njia za uzazi, kama vile umekaa maskani tu, out of nowhere unamuona mtu anaanza kuform?
Mungu ndio Mjuzi wa yote, yeye kama Muumbaji, basi yeye ndio mwenye kujua kila kitu, hakuna kilichojificha kwake. Mtu uwezo wake wa kufikiri au kuchambua mambo unakikomo, na before Bing Bang hawezi kujua chochote kile, lakini Mungu mjuzi wa yote ndio mwenye kujua.
Kiufupi;
- ANYTHING COMPLEX MUST HAVE A CREATOR. Ukipinga Hili basi thibitisha vipi hicho kitu complex kitakuwa hakina muumbaji and how it came to being.