Naelewa mfano wako wa pembe tatu.Nikisema Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote hayupo kwa sababu kimantiki dhana ya kuwepo kwake inajipinga yenyewe, unaelewa nasema nini?
Dhana ya kuwepo kwake haijwahi kujipinga. Wewe unatumia mfano wa pembe tatu, vipi unamfananisha Mungu na pembe tatu ulioitengeza wewe? kiumbe ambae ukikosa oxygen tu umekwisha
Abaa, lini utatuthibitishia kuwa ulimwengu ulikuja wenyewe bila Muumbaji? hebu nipe exact date nijue hilo jibu utalileta lini? maana naona unalikimbia tu... Kwani unaogopa nini hasa? Wewe si ushasema kuwa hakuna Mungu wala Muumbaji? Sasa sie tunataka ututhibitishie tu kuwa ulimwengu ulikuja wenyewe!