Mkuu,
Watanzania si wapuuzi,tatizo wana kamba imewazonga vibaya, kila wakijaribu kutafakari wapi waanze kujizongowa na mazonge na mzongemzonge huo,kuna kitu kinakazia fundo la mwisho, kwa hiyo kamba haizongoki na kila siku watanzania wanaendelea kuwa katika mzonge huo. CCM ni kamba iliyowazonga vibaya watanzania, wakati CCM kama chama na sera na miongozo yake kimeshindwa kwa miaka 45 kuleta mabadiliko ya maana katika hali na maisha ya mwananchi wa kawaida,kuna viongozi ndani ya chama hicho wanajidai kuwadanganya watanzani kuwa eti hali si hiyo(kuwa CCM haina uwezo tena kuongoza),bali kuna kundi la mafisadi ndani ya CCM, bila kuwa wakweli kuwa mfumo na muundo wa chama ni wa kiwizi wizi,kuanzia namna ya kupata viongozi wa chama mpaka wa kitaifa ni mipango mipango tu ya kufungafunga na kupenyezanapenyezana.Watanzania wakielekezwa palipo kosewa na kuanza kuelewa, panazuka hoja na kundi la watu kutoka huko huko CCM wakijidai eti wao ni vinara wa kupambana na ufisadi, huku wakificha unafiki wao na undumilakuwili wao kwa watanzani,kwa alama zao utawajuwa, siku zote wanatafuta huruma za wananchi eti kama kweli vile kuwa kelele wanazopiga ni kwa ajili ya wananchi wananyonge,huku wakificha dhamira zoa chafu. Eti ni majemedari wa vita zidi ya ufisadi, kwa sera ipi,mfumo upi,utaratibu upi,ari ipi,maadili yepi ambayo ni kinyume na ubovu wa CCM katika hayo yote...wao wanaoutegemea?
Na kwa kuonyesha kuwa CCM haiishi katika imani hizo na misimamo hiyo ya hao wanaojinadi kupinga ufisadi, tumeshuhudia sote jinsi walivyopata upinzani ndani ya chama chao na wao wenyewe kuanikwa uovu wao,unafiki wao na dhamira zao chafu kwa watanzania. Hali kama hii waliishi nayo ndugu zetu wa Kenya, wakiamini kuwa KANU si tatizo,tatizo eti ni viongozi baadhi tu wanaokichafua...kumbe hata hao waliokuwa wakipiga makelele ndani ya KANU kuwa kuna ufisadi na wakakosana na Mzee Moi,wenyewe hawakuwa wasafi na maovu yao yakaanikwa kwa staili hiyo hiyo mama Simba na wengine walivyoanika ndani ya CCM,wananchi wakabaki wasiamini nani anasema kweli, nani anatetea kwa niaba yao. Baade,kipindi tena wakajuwa kuwa tatizo si nani wala nani. Tatizo ni KANU imechoka na haina jipya la kuwafanyia Wakenya...kilichofuatia unakijuwa.
Sasa hapa tatizo si nani anasema kweli kati ya Mama sophia na hao majemedari wanafiki wa vita vya ufisadi, kwakuwa wote wanalinda kama si nyongo basi maini ya matumbo yao tu na si ya watanzania.Tatizo ni CCM yote,kama KANU, kuwa imeshachoka na inahitaji kupumzika, na wanaoweza kuipumzisha ni watanzania wenyewe,hawezi kuja malaika kuleta mabadiliko, wakati umefika kusahau kuwa CCM hii ndo TANU ile iliyoleta uhuru, CCM ndo chama kile alichokiacha Nyerere,CCM hii ndo chama kile kinachongojea tu miaka 47 kuondoa maradhi,njaa na ujinga wa watanzania. CCM hii si ile tena...watanzania wataendelea kupigwa danadana ya kutafuta nani mkweli nani muongo katika kundi la watu waongo wanaoishi kuwachanganya akili watanzani kila kukicha.
CCM IMECHOKA WATANZANIA IPUMZISHENI...HAKUNA ATAKAKE LALA NJAA KAMA KESHO CCM ITAKUWA BENCH,IKITAZAMA MECHI...
WAZAMBIA wanaendelea na maisha bila ya UNIP, wa Kenya wanaendelea na maisha bila ya KANU...Waghana,Wasenegal,Malawi n.k wote hawa wanaendelea na maisha yao bila ya vyama hivi vilovyoleta ukombozi,watanzania wanasubiri nini...au VICHWA VYAO HAVIFIKIRI na matumbo yao (wanyonge si mafisadi) hayana njaa ya mabadiliko?