Sofia Simba na Sakata la Mafisadi na Wapiganaji!

Sofia Simba na Sakata la Mafisadi na Wapiganaji!

Kwa takribani siku nne au tano zilizopita nimekuwa nikisikiliza, kusoma, kuhusu Bibi Yetu, mama yetu, dada yetu, jirani, rafiki, adui etc Sohia binti Simba mtoto wenyewe wanasema wa mjini, mke wa aliye kuwa mstahiki meya nk.
lakini jambo lilonigua na matamshi yake ambayo nionavyo mimi hayaendani na elimu yake, labda iwe feki, wadhifa au nyadhifa tulizo nazo, mwisho nikajiuliza ndivyo waafrika tulivyo? au ndio watanzania walivyo? au ndio serikali yetu ilivyo na mwisho wa yote ndivyo ccm ilivyo au akinamama wengi walivyo.
Sasa ili kuondoa aibu hii ni vyema serikali yetu na vyama vyetu vikaachana na siasa au utendaji wa kupeana nchi au wadhifa kwa kigezo cha urafiki, maana wewe unaweza kufanya kwa nia nzuri, lakini unayemchagua akaona ukaribu wa kiongozi, urafiki nk ndio nguvu yake naye akaitumia vibaya, matokeo yake ndio haya malumbano, na kuharibu nchi na sifa za nchi licha ya sifa za viongozi wetu, matokeo yake watanzania wote tunaonekana ni watu wa havinitishi tishi (mipasho) mdundiko style.
Sasa imefika wakati sisi watanzania tujiulize sisi ndio watu wa design hiyo, hatuna watu wenye sifa na staha zifaazo ilituwakilisha na kutuongoza kwenye nyadhifa hizo, jamani akin dada zangu , akinamama. bibi, wachumba, wake hakuna moja wenu mwenye kufaa?
Serikali yetu hivi ndio picha mnayo tupa sisi watanzania? kweli tutakuwa salama na Wizara ya Usalama wa Taifa yenye kiongozi wa Namna hiyo?
 
Samahni lakini nilisikia elimu ya huyu mama ni certificate yani hana hata ka diploma duh kama ni kweli haya!!
 
Samahni lakini nilisikia elimu ya huyu mama ni certificate yani hana hata ka diploma duh kama ni kweli haya!!

Huyu mama ana masters yake tena halali wala sio feki. Hayo mambo ya certificate ni uzushi tu.
 
Huyu mama ana masters yake tena halali wala sio feki. Hayo mambo ya certificate ni uzushi tu.

hiyo masters yake halali imemsaidia nini? mbona anafikiria, kuongea na kutenda kama mmama ambaye hata form 4 hajafika?
 
hiyo masters yake halali imemsaidia nini? mbona anafikiria, kuongea na kutenda kama mmama ambaye hata form 4 hajafika?
Kumbuka Mama Sophy ni binadamu hivyo ana mapungufu yake, lakini sio kigezo cha watu kuongopa elimu yake.Na vile vile unaweza kupata elimu lakini usielimike.
 
Unaweza ukamwambia Mzee Melecela atoe majina ya watu waliomchangia ktk hiyo harusi yake, ili tujue ukweli.
 
Usidanganyike hata akiwa anasaidia Chadema hawezi sema kwa siasa mbuzi za Bongo kama hizi za kuuana kibiashara na visasi !
 
Watanzania muda si mrefu natoka kuongea na mzee wetu nikajaribu kumwelekeza watu walivyochukulia kwa niaba ya familia ameomba tusishindane na vichaa na yawezekana kichaa hayuko pekee SOPHIA SIMBA WAO VICHAA WENGI NYUMA YAKE NA HATA HUMU JF...SO AMEOMBA TUWE WAVUMILIVU KATIKA WAKATI HUU WA MPITO MAFISADI WAKIJITAHIDI KUJISAFICHA


simba hawezi kukurupuka tu na kutowa kauli kama zile ,kuna ukweli ndani yake kazee hiki kina kaujanja mwingi.
 
hata mimi naanza ku-doubt umakini wa huyu baba! Haihitaji kulumbana namna hiyo
 
Watanzania muda si mrefu natoka kuongea na mzee wetu nikajaribu kumwelekeza watu walivyochukulia kwa niaba ya familia ameomba tusishindane na vichaa na yawezekana kichaa hayuko pekee SOPHIA SIMBA WAO VICHAA WENGI NYUMA YAKE NA HATA HUMU JF...SO AMEOMBA TUWE WAVUMILIVU KATIKA WAKATI HUU WA MPITO MAFISADI WAKIJITAHIDI KUJISAFICHA

Sasa wewe unamtetea Malecela? Malecela yupo CCM, na CCM ni Chama Cha Majambazi. Kama hizi habari hazina ukweli; kwanini hamjibu kwa hoja? toeni majina ya watu waliotoa misaada na gharama za hiyo harusi ili tujue nani mkweli.
 
simba hawezi kukurupuka tu na kutowa kauli kama zile ,kuna ukweli ndani yake kazee hiki kina kaujanja mwingi.

Lakini si kila mtu hapa Tanzania anapokea michango ya Arusi, wewe mwenzetu ulirudisha mchango wa mtu kwenye arusi yako? Mimi mbona hili la kuchangiwa kwenye Arusi sioni kama ni issue, watu hata hapa nadani wamechangiwa mamilioni na watu kwenye arusi na hawakuuliza zimetoka wapi, leo Malecela imekuwa issue khaaa!
 
kuwa na vitabu haimaanishi unaweza kuvisoma, sofia simba yuko juu ya usalama wa taifa lakini haimaanishi kuwa anaelewa kitu, sofia simba ni garasa.

Mengi alivyomuambia sofia simba awe anapata ushauri kwa usalama wa taifa ni sawa sawa, kwa ajili sofia simba anaongea kama mtu ambaye hajapata ushauri kabisa na, kama amepata ushauri wamemchuza.
Je unamaanisha maneno anayoongea sofia simba ni ushauri wa ro??? Ro is better than that..

mengi kutoa statement ni sahii, kwa ajili kila kwenye vikao vya ccm jina lake linatoka mara hivi mara vile.

pia uzushi kwamba yeye amejiunga/atajiunga ccm - watu ambao wako kwenye siasa wanajua mengi ni mwana ccm lakini wananchi wa kawaida wanalishwa yanayoandikwa kwenye magazeti, kwa hyio kutoa statement sio kwa ajili ya wanasiasa bali ni kwa ajili ya wananchi wakawaida waliokuwa wanalishwa uongo wa magazeti.
 
You are are not so sure Muungwana hatowi matusi...kama hawezi kujibu hoja hukubali yaishe...siyo kutukuna ndo aonekaneje...so he is stupid.
kama ni hoja watazijibu wenyewe ..kwanza kilango anaandaa mashambulizi..ala cha msingi anatakiwa atoe na maeleze kuwa huo mshiko walipewa kweli au?
 
Malecela toka clean, vipi ulitumia pesa za mafisadi kuendesha harusi yako?

Tuache Unafiki ni Bush tu alirudisha pesa za rambi rambi za prince wa saudi arabia baada ya september 11, nyie watanzania wenzangu nani kwenye historia aliwahi kurudisha michango ya arusi au kipaimara kwa sababu hajui mtoaji amezipata wapi aua anajua mtoaji kuwa ni mwizi??? Mbona hata makanisani na misikitini tunapokea pesa za wezi sembuse malecela kupokea pesa kwa ajili ya arusi. Hapo hakuna hoja, ilikuwa arusi na kamati ya arusi ndio inakusanya michango. nani alikuwa m/kiti wa kamati na wajumbe waulizeni wawape nani walitoa na break down

Hawa akina Simba siku zote watatutoa kwenye ukweli tujadili yasiyo na tija kwa watanzania, Arusi ya Malecela huwezi fananisha na deal la Richmond, Meremeta, Kagoda, IPTL, TRL, Deep Green, Mwananchi et al, Jamani nchi imeuzwa rudini kwenye mstari, anza kwanza kulipua ndege, then teketeza vifaru vya adui ndio uje kwenye hao askari wa miguu.

Nyie mnaanza kujadili namna ya kulipua mahema yao kwanza ha ha ha Khaaa!
 
Unaweza ukamwambia Mzee Melecela atoe majina ya watu waliomchangia ktk hiyo harusi yake, ili tujue ukweli.
Hapa ndo kidonda kilipopata makali ya ndimu...asigeuze maneno,aende kwenye dai la msingi, na Mwkyembe naye aje aseme, sakata la Richmond na msimamo wake katika ununuzi wa mitambo ya Dowans,pana uhusiano gani na kampuni yake ya umeme wa upepo...asijidaijidai kutaka kuwacheza shere watanzania.
ILANI KWA WANA JF.
CCM haina mpiganaji wa ufisadi, nasisitiza tena wote ni mafisadi,wanaopiga makelele na kujiita ni vinara wa vita vya ufisadi wana ajenda zao mifukoni na maslahi yao binafis pembeni,wanawazubaisha watanzania tu,kujidai kuwa wao ni vinara wa ufisadi wakati sasa dhahiri ya mambo inakuja wanafichuana wenyewe kwa wenyewe, na humu JF nimeshaona dalili za kuwaonea huruma na kuwaamini eti kweli ni vinara wa kupambana na ufisadi...huu ni undumilakuwili wa kisiasa, haiwezekani 'wapambanaji wa ufisadi wawe na waamini na waumini wa chama hicho hicho kinacholea matajiri na mafisadi,kinachong'ang'ania sera ya kulindana lindana, kinachochochea mgawanyiko wa kijamii kati ya wenye nacho na wasiokuwa nacho, kinacholea system mbovu ya kuendesha nchi,kinacholazimisha kukaa madarakani japo wanachi hawakitaki(zanzibar).Ili niamini kuwa hao wanaojitapa na mapambano ya ufisadi ni wapiganani wa kweli na wazalendao na wapo tayari kuwa upande wananchi wanyonge na si kwa matumbo yao binafsi kama wanavyoonekana sasa basi watoke CCM na wajiunge au waanzishe vuguvugu lao huru kuendeleza mapambano...hivyo ndivyo alivyofanya Odinga alipoiondoa DP kutoka KANU...Bingu wa Mutharika alipoanzisha chama chake akiwa ikulu Malawi, kuepusha kuwa mnafiki...na matokeo tumeona.
 
Hapa ndo kidonda kilipopata makali ya ndimu...asigeuze maneno,aende kwenye dai la msingi, na Mwkyembe naye aje aseme, sakata la Richmond na msimamo wake katika ununuzi wa mitambo ya Dowans,pana uhusiano gani na kampuni yake ya umeme wa upepo...asijidaijidai kutaka kuwacheza shere watanzania.
ILANI KWA WANA JF.
CCM haina mpiganaji wa ufisadi, nasisitiza tena wote ni mafisadi,wanaopiga makelele na kujiita ni vinara wa vita vya ufisadi wana ajenda zao mifukoni na maslahi yao binafis pembeni,wanawazubaisha watanzania tu,kujidai kuwa wao ni vinara wa ufisadi wakati sasa dhahiri ya mambo inakuja wanafichuana wenyewe kwa wenyewe, na humu JF nimeshaona dalili za kuwaonea huruma na kuwaamini eti kweli ni vinara wa kupambana na ufisadi...huu ni undumilakuwili wa kisiasa, haiwezekani 'wapambanaji wa ufisadi wawe na waamini na waumini wa chama hicho hicho kinacholea matajiri na mafisadi,kinachong'ang'ania sera ya kulindana lindana, kinachochochea mgawanyiko wa kijamii kati ya wenye nacho na wasiokuwa nacho, kinacholea system mbovu ya kuendesha nchi,kinacholazimisha kukaa madarakani japo wanachi hawakitaki(zanzibar).Ili niamini kuwa hao wanaojitapa na mapambano ya ufisadi ni wapiganani wa kweli na wazalendao na wapo tayari kuwa upande wananchi wanyonge na si kwa matumbo yao binafsi kama wanavyoonekana sasa basi watoke CCM na wajiunge au waanzishe vuguvugu lao huru kuendeleza mapambano...hivyo ndivyo alivyofanya Odinga alipoiondoa DP kutoka KANU...Bingu wa Mutharika alipoanzisha chama chake akiwa ikulu Malawi, kuepusha kuwa mnafiki...na matokeo tumeona.
kwa hiyo nani anelekea kushinda na kukonga nyoyo za wapuuzi (watanzania) katika haya makundi mawili?
 
Tuache Unafiki ni Bush tu alirudisha pesa za rambi rambi za prince wa saudi arabia baada ya september 11, nyie watanzania wenzangu nani kwenye historia aliwahi kurudisha michango ya arusi au kipaimara kwa sababu hajui mtoaji amezipata wapi aua anajua mtoaji kuwa ni mwizi??? Mbona hata makanisani na misikitini tunapokea pesa za wezi sembuse malecela kupokea pesa kwa ajili ya arusi. Hapo hakuna hoja, ilikuwa arusi na kamati ya arusi ndio inakusanya michango. nani alikuwa m/kiti wa kamati na wajumbe waulizeni wawape nani walitoa na break down

Hawa akina Simba siku zote watatutoa kwenye ukweli tujadili yasiyo na tija kwa watanzania, Arusi ya Malecela huwezi fananisha na deal la Richmond, Meremeta, Kagoda, IPTL, TRL, Deep Green, Mwananchi et al, Jamani nchi imeuzwa rudini kwenye mstari, anza kwanza kulipua ndege, then teketeza vifaru vya adui ndio uje kwenye hao askari wa miguu.

Nyie mnaanza kujadili namna ya kulipua mahema yao kwanza ha ha ha Khaaa!
kula tano dada
 
Back
Top Bottom