Sofia Simba na Sakata la Mafisadi na Wapiganaji!

Sofia Simba na Sakata la Mafisadi na Wapiganaji!

time for commercial break

mengi%2B(2).jpg

Huyo dada kakumaliza sana kwa vile hajavaa hijab nini?!
 
uliyoyasema kwenye kamati ya mzee mwinyi ni ya aibu kwa aliyekuteua na wale uliojaribu kuwatetea. Sitaki niyarudie lakini kwa heshima yote uliyobakia nayo your time is up ma'am. Thank you for your unforgetable diservice to our country. Tukiamka tusikie umejiuzulu na kuwa mfano wa utawala bora. Usisubiri uundiwe kamati.
aondoke kwa lipi? Kwanini wewe ni nani? Mwanaccm?
 
Hivi alishamalizana na waziri mambo ya ndani katika lile bifu lao?? Au hili ni jingine, just in case lile likimalizwa kiutu uzima?

Swali muhimu sana hili, waziri wa mambo ya ndani aliamua kutofuata sheria za nchi kwenye issue yake dhidi ya Mengi?
 
Wewe ndio mkurupukaji hapa. Sasa hiki ni nini umeandika? Hata hueleweki. Rudia tena kusoma ulichoandika uone ulivyochemsha.

HAWA SIO KOSA LAO NDIO WALE WALE WAKINA DK-""NCHIMBI""...MAHANGA-A.K.A"DK"
 
Daniel Mjema, Dodoma na Ramadhan Semtawa

WAZIRI mkuu wa zamani, John Malecela jana alimshukia Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Sophia Simba akisema kuwa tuhuma alizozitoa dhidi yake zinatokana na waziri huyo kuwa mgonjwa wa akili, huku mkewe ana Kilango, akimshangaa kwa kukalia tuhuma hizo kwa kipindi kirefu.


Mbali na wanandoa hao, mwenyekiti wa IPP, Reginald Mengi naye alipuuza tuhuma alizorushiwa na Waziri Simba akisema kuwa hawezi kubishana na mjinga.


Malecela, Kilango na Mengi ni miongoni mwa watu kadhaa walioshambuliwa na Waziri Simba Jumatano, akiwatuhumu wanandoa hao kuwa walichukua fedha za kifisadi wakati walipofanya harusi yao mjini Dodoma na katika kampeni za urais za mwaka 2005, huku akimtuhumu Mengi kuwa anatumia vyombo vyake vya habari kuichafua CCM na serikali yake kwa maslahi binafsi.


Wote watatu hawakuingia ndani kukanusha madai hayo ya Simba wala kutoa ufafanuzi, na badala yake Mengi na Malecela walimrushia maneno makali wakimwita kuwa ni mgonjwa wa akili, asiye na maadili, mropokaji na ambaye si msafi huku Kilango akisema kuwa bado anatafakari.


Malecela, ambaye alikuwa waziri mkuu na makamu wa kwanza wa rais (1990 hadi 1994), alidai kuwa Simba ni mgonjwa wa kichwa na akili hivyo anapaswa kupelekwa Hospitali ya Mirembe kabla ya kurudi Dar es Salaam baada ya bunge kuisha.


Hospitali ya Mirembe iliyo mjini Dodoma hujishughulisha zaidi na tiba ya watu wenye matatizo ya akili.


Kama ilivyokuwa kwa Kilango ambaye alidai juzi kuwa mashambulizi dhidi yake yanatokana na mumewe, Malecela naye jana alidai kushambuliwa kwake ni kutokana na mkewe Kilango kwamba ameona azungumze kwa kifupi kuhusu hali halisi ya akili ya Simba.


"Najua chanzo kikubwa ni mama (Kilango), yeye leo ametoa taarifa yake, lakini na mimi ninalo moja dogo la kusema kijana ambalo ni ushauri kwa Waziri Simba," alisema Malecela.


"Simba ni mgonjwa, ana matatizo ya akili kichwani, namshauri apelekwe au aende Mirembe akapimwe akili na kupata matibabu kabla hajarudi Dares Salaam."


Mzee Malecela ambaye ni mjumbe wa kudumu wa Kamati Kuu na makamu mwenyekiti mstaafu wa CCM, alisema Simba atafanya kosa kama atarudi Dar es Salaam bila kwenda Mirembe kupima akili na kupata matibabu.


"Asirudi Dar es Salaam bila kupita Mirembe kupima akili, kwa maana atakuwa amepoteza fursa ya kujua matatizo aliyonayo kichwani kwake," alisisitiza.


Kwa sasa Waziri Simba yuko Dodoma kuhudhuria vikao vya Bunge na alitoa kauli za kumshambulia Malecela, Kilango, Mengi na Mwakyembe kwenye mikutano inayoendelea baina ya wabunge wa CCM na Kamati ya Mwinyi ya kutafuta chanzo cha kutoelewana ndani ya chama hicho.


Malecela, ambaye aliwahi kuteuliwa kuwa mmoja wa watu sita wenye busara katika nchi za Umoja wa Madola mwaka 1985, hakueleza kama ana ushahidi wa madai yake.


Hata hivyo, Simba aliwahi kuugua akiwa Afrika Kusini na baadaye Hindul Mandal akiwa anasumbuliwa na kizunguzungu na kutapika, ugonjwa ambao waziri huyo aliwakariri madaktari wakisema utapona taratibu.


Hata hivyo, alipoulizwa iwapo tuhuma za yeye kufadhiliwa na Patel katika harusi yake na kupewa kiasi hicho cha fedha Sh200 milioni za kampeni za Urais mwaka 2005, Malecela alisema tuhuma hizo zimetolewa na mgonjwa.


Naye mbunge wa Same Mashariki, Kilango alionyesha kushangazwa na tuhuma hizo na kumshangaa waziri huyo kukalia tuhuma nzito alizozitoa kwa muda mrefu bila kuzifikisha kwenye vyombo vya sheria.


Kilango na Malecela walituhumiwa na Simba Jumatano kuwa nao walichukua fedha za ufisadi, akidai kuwa harusi yao ilifadhiliwa na Jeetu Patel, ambaye ni mtuhumiwa wa ufisadi na hali kadhalika kampeni za urais za Malecela za mwaka 2005.


Katika tuhuma zake, Waziri Simba alidai kuwa Kilango ni mnafiki na si msafi kiasi cha kuwanyooshea wenzake vidole na kwamba kelele zake zote zimetokana na kukosa kuwa mke wa rais baada ya Malecela kuenguliwa mapema na CCM kwenye mchakato wa kumpaya mgombea wake.


Lakini jana, Kilango alisema hatakatishwa tamaa na tuhuma hizo nzito, ambazo alisema bado anazitafakari, ili kubaini kiini chake na sababu za kutolewa sasa katika kipindi ambacho vita dhidi ya ufisadi imepamba moto.


Kilango, ambaye mwaka huu alitunukiwa Tuzo ya Mwanamke Jasiri na serikali ya Marekani, alimshangaa Simba kukaa kimya na tuhuma hizo tangu 2005 wakati vyombo vya dola vipo.


"Kama Mheshimiwa Simba alikuwa na ushahidi wa tuhuma nzito kama hizo tangu mwaka 2005 kama ambavyo anataka Watanzania waamini, bado haiingii akilini ni kitu gani kilichomfanya asitoe taarifa hizo katika vyombo vya dola,” alihoji Kilango.


Kilango alifafanua kwamba Simba ni waziri mwenye dhamana ya utawala bora ambaye ana vyombo vya uchunguzi chini yake kama Takukuru, lakini akashangaa kutovitumia.


“Ni imani yangu kwamba, mheshimiwa Simba ambaye ni waziri katika Ofisi ya Rais atapimwa na wananchi kama malumbano anayoyaanzisha sasa yana chembe ya ukweli kiasi gani au ni kujaribu kuwahamisha Watanzania katika vita nzito dhidi ya ufisadi,” alisema.


Katika taarifa yake ya maandishi, Kilango alisema asingependa kuingia katika malumbano na waziri huyo kwa kuwa itawapa taabu Watanzania kutofautisha pumba na mchele.


Kauli ya Simba inaonekana kuibua mjadala mpya katika vita dhidi ya ufisadi katika kipindi hiki ambacho kimetawaliwa na malumbano makali baina ya wabunge wanaojinadi kuwa ni makamanda wa vita ya ufisadi na wale wanaodai kuchukulia vita hiyo kuwa ni ya kukichafua chama na serikali.


Malumbano hayo yamefikia kipindi ambacho wabunge wenyewe wameanza kuhoji maamuzi yao ya kukubaliana na ripoti ya kamati teule iliyochunguza kashfa ya mchakato wa utoaji wa zabuni ya uzalishaji umeme wa dharura kwa kampuni ya Richmond Development na kutaka uchunguzi mpya ufanyike ukihusisha tume huru.


Tayari mawaziri wawili, Dk Makongoro Mahanga na Simba wamejitokeza kumtetea Edward Lowassa ambaye aliachia wadhifa wake wa waziri mkuu kutokana na kutakiwa na ripoti hiyo kufanya maamuzi kwa kutumia busara yake kutokana na kashfa hiyo.


Hata mbunge wa Bariadi, Andrew Chenge, ambaye alijiuzulu uwaziri baada ya kutajwa kwenye kashfa ya ununuzi wa rada, naye amejikuta akipata watetezi, akiwemo Waziri Simba ambaye alielezea kuwa uchunguzi umeonyesha kuwa mwanasheria huyo mkuu wa zamani wa serikali hana hatia.


Nje ya Bunge, Mengi ndiye aliyeguswa zaidi na Waziri Simba na jana aliongea na waandishi wa habari kuhusu tuhuma hizo akisema: "Dont argue with a fool because people may not know the difference between you and the fool (usibishane na mjinga kwa sababu watu wanaweza kushindwa kufahamu tofauti yako na huyo mjinga)."


Hata hivyo, Mengi alisema wakati mwingine unalazimika kujibu hoja "unapoona mtu anapotosha mambo kwa makusudi" na akaeleza kuwa Waziri Simba si mtu msafi hivyo ni vema katika vita ya ufisadi inayoendelea akakaa kimya kuliko kujitokeza na kuropoka.


Mengi, ambaye amekuwa akionekana kuunga mkono kundi linalopambana na ufisadi, alimtaka Waziri Simba kutafuta ushauri kutoka taasisi za serikali, ikiwemo Idara ya Usalama wa Taifa, kabla hajazungumza.


Hata hivyo, Mengi hakutoa maelezo ya tuhuma kwamba amekuwa akitumia vyombo vyake vya habari kuendesha kampeni zinazoichafua CCM na serikali yake kwa maslahi yake binafsi na badala yake alielezea uanachama wake kwenye chama hicho tawala.


"Kwa muda mrefu sasa nimekuwa nikituhumiwa na baadhi ya viongozi wa CCM kwamba, mimi si mwanachama wa chama hicho na kwamba sitoi misaada ya hali na mali kwa chama," alisema Mengi katika mkutano wake na waandishi.


"Kwanza, kuhusu kuropoka kwamba sitoi misaada kwa CCM, hilo ni jambo linalozushwa na watu binafsi na kwa malengo binafsi. Viongozi wakuu wa CCM ambao ni waadilifu na wanaosimamia ukweli wanajua undani wa jambo hili. Siwezi kusema nasaidia nini CCM, kwa kuwa itakuwa ni kukidhalilisha chama changu.


"Pili, kuhusu uanachama wangu wa CCM, napenda kuwaambia kwamba mimi ni mwanachama wa CCM tangu tarehe 18 Aprili,1977 na kadi yangu ni na. B124595, iliyotolewa na tawi la Kisutu, wilaya ya Ilala, mkoa wa Dar es Salaam."


Katika mkutano huo, Mengi alitumia vielelezo kujibu tuhuma kwamba amejiunga na CCM hivi karibuni.


Mengi alisema anashangaa kauli za Waziri Simba na katibu wa CCM mkoani Dares Salaam, Shaaban Kilumbe kwamba, alipita matawi yote na kubaini hakuna sehemu ambako aliwahi kuwa mwanachama.


"Lakini wakati mwingine inawezekana hakuona kweli kwa sababu labda hajui kusoma... ni kitu kibaya sana kujaribu kuzungumzia mambo yanayohusu kusoma wakati hujui kusoma, labda Reginald kasoma John," alituhumu.


Aliongeza kwamba wanaosema CCM hakuna kiongozi msafi ni dhahiri wao ndiyo wameingia katika chama hicho hivi karibuni na kusisitiza: "Ningetoa ushauri waondoke na watuachie chama chetu kwa kuwa hawafahamu misingi imara ya CCM."


Tangu Kamati ya Mwinyi ianze kazi ya kuwahoji wabunge mjini Dodoma, kumekuwepo na kurushiana maneno ya kudhalilishana baina ya wabunge hao wa chama tawala, kwa ufisadi na kupokea fedha zinazotokana na ufisadi.


Source - Mwananchi
 
Daniel Mjema, Dodoma na Ramadhan Semtawa

WAZIRI mkuu wa zamani, John Malecela jana alimshukia Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Sophia Simba akisema kuwa tuhuma alizozitoa dhidi yake zinatokana na waziri huyo kuwa mgonjwa wa akili, huku mkewe ana Kilango, akimshangaa kwa kukalia tuhuma hizo kwa kipindi kirefu.



Source - Mwananchi

Hii ni kali kweli kweli.
 
Ngoma inogile, nasubiri kusikia Mwakyembe na wengine walioguswa watasemaje!
 
MALUMBANO makali yameendelea kuitikisa Kamati ya rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi baada ya makombora ya juzi kuelekezwa kwa Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango na mumewe, mzee John Malecela.

Kamati hiyo imekuwa ikipokea mashambulizi makali baina ya wabunge ambao wanaonekana kuwa vinara wa vita dhidi ya ufisadi na wale ambao wanaona kuwa vita hiyo inawalenga, kiasi cha kurushiana tuhuma nzito zilizo na mwelekeo wa kuchafuana.

Baada ya kulipuana Jumanne, juzi ilikuwa zamu ya Mama Kilango na mumewe Malecela wakati Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Sophia Simba alipotoa tuhuma nzito akidai kuwa wawili hao pia wamekula fedha za ufisadi.

Habari kutoka vyanzo vyetu zilieleza kuwa Simba alidiriki kudai kuwa hata harusi ya makamu huyo wa zamani wa CCM na Kilango ilifadhiliwa na mtuhumiwa wa ufisadi, Jeetu Patel.

Patel kwa sasa ana kesi katika Mahakama ya Kisutu akituhumiwa kuiibia Benki Kuu (BoT) kwa kuchota takribani Sh11 bilioni kutoka katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA).

Akijieleza kwenye kamati hiyo, Simba alimtuhumu Malecela, ambaye aliwahi kuwa waziri mkuu katika serikali ya awamu ya kwanza, kuwa wakati akiwania kuteuliwa kugombea urais kwa tiketi ya CCM mwaka 2005, Jeetu Patel alimpa Sh200 milioni kwa ajili ya kampeni zake.

Malecela, ambaye wakati huo alikuwa makamu mwenyekiti wa CCM, aliondolewa mapema kwenye mbio za urais, ikiwa ni mara ya pili baada ya kuenguliwa tena mapema mwaka 1995.

Waziri huyo mwenye dhamana ya utawala bora akiwa na taasisi nyeti kama Takukuru na Idara ya Usalama wa Taifa, alizidi kurusha makombora kwa wanandoa hao, akisema Mama Kilango ni mnafiki na sio msafi kiasi cha kuwanyooshea wengine vidole wakati harusi na kampeni zake za ubunge zilifadhiliwa na mtuhumiwa huyo wa ufisadi.

Habari zinasema kuwa Mama Simba alikuwa akizungumza kwa kujiamini na kwa ujasiri na kumtuhumu Mama Kilango kuwa kelele zake zote zinatokana na nongwa ya "kuukosa U-first lady (kuwa mke wa rais)."

Alieleza kuwa kelele zote za mbunge huyo wa Same Mashariki zinatokana na chuki na uchu wa madaraka na si kweli kwamba ni mpinga ufisadi, kwa mujibu wa mtoaji habari wetu.

Lakini Patel, alipoulizwa kuhusu tuhuma hizo za Waziri Simba kwamba alifadhili harusi ya Malecela na kampeni zake za urais, alionekana kustuka na kusema: "Haa...we nani kakwambia... Bwana ehee, mimi sijui lolote kuhusu hayo.

"Kwa sasa mimi najiangalia mwenyewe, nina matatizo yangu mengi nahangaika nayo."

Hata alipofafanuliwa kwamba, maneno hayo yalisemwa na Waziri Simba, alijibu: "Kama wao wamesema wenyewe huko, mimi sijui."

Naye Kilango alisema alishuhudia wakati wakati makombora hayo yakirushwa na kueleza kwamba anajiandaa kujibu mapigo.

Mbunge huyo machachari alisema anajua kwamba mambo yote yaliyosemwa, yanamlenga yeye na si mumewe Malecela.

"Mimi ni mwanasiasa... andikeni yote yaliyozungumzwa bila ya kuacha baadhi na siwezi kuwashtaki," alisema Kilango.

Mzee Malecela hakutaka kuzungumzia lolote kuhusu tuhuma hizo wakati alipoulizwa juu ya uhusiano wake na Patel na kama aliwahi kupokea kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya kampeni.

"Ahaa... kijana naomba uniache nipumzike," alisema Malecela.

Mbali na mzee Malecela na mkewe, Waziri Simba pia alimgeukia mwenyekiti mtendaji wa IPP, Reginald Mengi akimtuhumu kuwa anaendesha vyombo vya habari vinavyoichafua CCM na serikali yake kwa maslahi yake binafsi.

Pia alimshambulia mbunge wa Kyela, Dk Harrison Mwakyembe na mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka, akiwatuhumu kuwa ni watu wenye njaa na kwamba, wanalipwa fedha kufanya kazi hiyo.

Waziri Simba alisema kuwa hata tuhuma dhidi ya mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge na mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, zimetokana na chuki binafsi.

Simba alisema kuwa uchunguzi wa kashfa ya rada ulishamalizika na Chenge akasafishwa na kuongeza kwamba hata uchunguzi wa Richmond umebaini kulikuwa hakuna rushwa, kwa mujibu wa mtoaji habari wetu.

Suala la Richmond liliibuka tena mbele ya kamati hiyo ya Mwinyi wakati mbunge wa Bukoba Vijijini, Nazir Karamagi alipolalamika kuwa ripoti ya kamati teule ya Bunge iliyoozwa Dk Mwakyembe haikumtendea haki.

habari hizo toka ndani ya kikao hicho zinaeleza kuwa Karamagi alisema ripoti ya Richmond ilionea baadhi ya watu na akapendekeza iundwe tume huru kupitia mchakato huo kuona kama wana makosa ili haki itendeke.

Mbunge huyo ambaye alijiuzulu uwaziri baada ya Lowassa kuachia wadhifa wake wa waziri mkuu kutokana na kashfa hiyo, alisema maamuzi yake kuhusu Richmond yalitokana na mapendekezo ya Bodi ya Tanesco.

Naye Dk Mwakyembe alijibu hoja iliyotolewa Jumanne na mbunge wa Ukonga, Dk Makongoro Mahanga aliyedai kuwa ripoti ya Richmond ni 'feki', akisema tatizo la Dk Mahanga ni uelewa mdogo.

Kuhusu hoja ya Karamagi, Dk Mwakyembe alisema malalamiko yake si sahihi kwa sababu yapo maeneo mengi ambayo Karamagi alishiriki na yako bayana hayahitaji mjadala.

Aliwatahadharisha Wabunge kuacha kudodosa sana ripoti ya Richmond kwani watazidi kumchafua Lowassa na kwamba wanaweza kufungwa kwa sababu upo ushahidi dhahiri.

Dk Mwakyembe aliwataka viongozi wa CCM wenye tuhuma kuiga mfano wa Mzee Mwinyi aliyejiuzulu baada ya mauaji yaliyofanywa na vyombo vya dola mkoani Shinyanga.

Akizungumza mbele ya kamati hiyo, kwa mujibu wa vyanzo vyetu, alimshambulia spika wa Bunge, Samuel Sitta akidai kuwa kama si mizengwe, suala la Richmond lingemalizwa kwa taratibu za kichama.

Habari hizo zinadai kuwa Chenge, aliyewahi kuwa mwanasheria mkuu wa serikali, alisema Lowassa alizungukwa na kwamba kulikuwa na njama za kummaliza ingawa hakusema njama hizo zilifanywa na nani.

Chenge aliitetea serikali ya awamu ya tatu kuhusu kuingia mikataba mibovu na kusisitiza hakukuwa na uzembe kwani mikataba yote ilipitiwa na kukubaliwa na Baraza la Mawaziri.

Hata hivyo, mbunge wa Muleba Kusini, Wilson Masilingi alisimama na kuomba kutoa taarifa na kumwomba Mzee Mwinyi na kamati yake wawabane wabunge wanaodai wanasema ukweli.

Masilingi alipinga maelezo ya Chenge kuhusu mikataba na kusisitiza kuwa maelezo yake yalijaa ushabiki na kusema Baraza la Mawaziri liliridhia mikataba kutokana na ushauri wake (Chenge).

Mbunge wa Kwela, Dk Chrisant Mzindakaya, ambaye aliwahi kupata umaarufu kwa kulipua kashfa, aliwataka wabunge wakubali matokeo kuhusu Ripoti ya Richmond ili taifa lisonge mbele badala ya malumbano yasiyokwisha.

Kwa mujibu wa vyanzo vyetu, Mzindakaya aliwataka wabunge wafahamu kuwa ripoti hiyo ilishapitishwa na Bunge na haiwezi kurejeshwa ianze tena upya.

Naye Dk Mlingwa (Shinyanga Mjini), alisema mpasuko unaoinyemelea CCM unatokana na chama hicho kuacha misingi yake ya kuwa chama cha wakulima na wafanyakazi na badala yake kinawakumbatia wafanyabiashara.

Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Emanuel Nchimbi alitumia nafasi yake kuomba maridhiano ya wabunge wa CCM, kujenga moyo wa kusameheana ili chama kisonge mbele.


Daniel Mjema,Dodoma
__________________
A wise man once told me, luck isn't some mystical
 
MALUMBANO makali yameendelea kuitikisa Kamati ya rais mstaafu, Ali Hassan Mwinyi baada ya makombora ya juzi kuelekezwa kwa Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango na mumewe, mzee John Malecela.

Kamati hiyo imekuwa ikipokea mashambulizi makali baina ya wabunge ambao wanaonekana kuwa vinara wa vita dhidi ya ufisadi na wale ambao wanaona kuwa vita hiyo inawalenga, kiasi cha kurushiana tuhuma nzito zilizo na mwelekeo wa kuchafuana.

Baada ya kulipuana Jumanne, juzi ilikuwa zamu ya Mama Kilango na mumewe Malecela wakati Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Sophia Simba alipotoa tuhuma nzito akidai kuwa wawili hao pia wamekula fedha za ufisadi.

Habari kutoka vyanzo vyetu zilieleza kuwa Simba alidiriki kudai kuwa hata harusi ya makamu huyo wa zamani wa CCM na Kilango ilifadhiliwa na mtuhumiwa wa ufisadi, Jeetu Patel.

Patel kwa sasa ana kesi katika Mahakama ya Kisutu akituhumiwa kuiibia Benki Kuu (BoT) kwa kuchota takribani Sh11 bilioni kutoka katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA).

Akijieleza kwenye kamati hiyo, Simba alimtuhumu Malecela, ambaye aliwahi kuwa waziri mkuu katika serikali ya awamu ya kwanza, kuwa wakati akiwania kuteuliwa kugombea urais kwa tiketi ya CCM mwaka 2005, Jeetu Patel alimpa Sh200 milioni kwa ajili ya kampeni zake.

Malecela, ambaye wakati huo alikuwa makamu mwenyekiti wa CCM, aliondolewa mapema kwenye mbio za urais, ikiwa ni mara ya pili baada ya kuenguliwa tena mapema mwaka 1995.

Waziri huyo mwenye dhamana ya utawala bora akiwa na taasisi nyeti kama Takukuru na Idara ya Usalama wa Taifa, alizidi kurusha makombora kwa wanandoa hao, akisema Mama Kilango ni mnafiki na sio msafi kiasi cha kuwanyooshea wengine vidole wakati harusi na kampeni zake za ubunge zilifadhiliwa na mtuhumiwa huyo wa ufisadi.

Habari zinasema kuwa Mama Simba alikuwa akizungumza kwa kujiamini na kwa ujasiri na kumtuhumu Mama Kilango kuwa kelele zake zote zinatokana na nongwa ya "kuukosa U-first lady (kuwa mke wa rais)."

Alieleza kuwa kelele zote za mbunge huyo wa Same Mashariki zinatokana na chuki na uchu wa madaraka na si kweli kwamba ni mpinga ufisadi, kwa mujibu wa mtoaji habari wetu.

Lakini Patel, alipoulizwa kuhusu tuhuma hizo za Waziri Simba kwamba alifadhili harusi ya Malecela na kampeni zake za urais, alionekana kustuka na kusema: "Haa...we nani kakwambia... Bwana ehee, mimi sijui lolote kuhusu hayo.

"Kwa sasa mimi najiangalia mwenyewe, nina matatizo yangu mengi nahangaika nayo."

Hata alipofafanuliwa kwamba, maneno hayo yalisemwa na Waziri Simba, alijibu: "Kama wao wamesema wenyewe huko, mimi sijui."

Naye Kilango alisema alishuhudia wakati wakati makombora hayo yakirushwa na kueleza kwamba anajiandaa kujibu mapigo.

Mbunge huyo machachari alisema anajua kwamba mambo yote yaliyosemwa, yanamlenga yeye na si mumewe Malecela.

"Mimi ni mwanasiasa... andikeni yote yaliyozungumzwa bila ya kuacha baadhi na siwezi kuwashtaki," alisema Kilango.

Mzee Malecela hakutaka kuzungumzia lolote kuhusu tuhuma hizo wakati alipoulizwa juu ya uhusiano wake na Patel na kama aliwahi kupokea kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya kampeni.

"Ahaa... kijana naomba uniache nipumzike," alisema Malecela.

Mbali na mzee Malecela na mkewe, Waziri Simba pia alimgeukia mwenyekiti mtendaji wa IPP, Reginald Mengi akimtuhumu kuwa anaendesha vyombo vya habari vinavyoichafua CCM na serikali yake kwa maslahi yake binafsi.

Pia alimshambulia mbunge wa Kyela, Dk Harrison Mwakyembe na mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka, akiwatuhumu kuwa ni watu wenye njaa na kwamba, wanalipwa fedha kufanya kazi hiyo.

Waziri Simba alisema kuwa hata tuhuma dhidi ya mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge na mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, zimetokana na chuki binafsi.

Simba alisema kuwa uchunguzi wa kashfa ya rada ulishamalizika na Chenge akasafishwa na kuongeza kwamba hata uchunguzi wa Richmond umebaini kulikuwa hakuna rushwa, kwa mujibu wa mtoaji habari wetu.

Suala la Richmond liliibuka tena mbele ya kamati hiyo ya Mwinyi wakati mbunge wa Bukoba Vijijini, Nazir Karamagi alipolalamika kuwa ripoti ya kamati teule ya Bunge iliyoozwa Dk Mwakyembe haikumtendea haki.

habari hizo toka ndani ya kikao hicho zinaeleza kuwa Karamagi alisema ripoti ya Richmond ilionea baadhi ya watu na akapendekeza iundwe tume huru kupitia mchakato huo kuona kama wana makosa ili haki itendeke.

Mbunge huyo ambaye alijiuzulu uwaziri baada ya Lowassa kuachia wadhifa wake wa waziri mkuu kutokana na kashfa hiyo, alisema maamuzi yake kuhusu Richmond yalitokana na mapendekezo ya Bodi ya Tanesco.

Naye Dk Mwakyembe alijibu hoja iliyotolewa Jumanne na mbunge wa Ukonga, Dk Makongoro Mahanga aliyedai kuwa ripoti ya Richmond ni 'feki', akisema tatizo la Dk Mahanga ni uelewa mdogo.

Kuhusu hoja ya Karamagi, Dk Mwakyembe alisema malalamiko yake si sahihi kwa sababu yapo maeneo mengi ambayo Karamagi alishiriki na yako bayana hayahitaji mjadala.

Aliwatahadharisha Wabunge kuacha kudodosa sana ripoti ya Richmond kwani watazidi kumchafua Lowassa na kwamba wanaweza kufungwa kwa sababu upo ushahidi dhahiri.

Dk Mwakyembe aliwataka viongozi wa CCM wenye tuhuma kuiga mfano wa Mzee Mwinyi aliyejiuzulu baada ya mauaji yaliyofanywa na vyombo vya dola mkoani Shinyanga.

Akizungumza mbele ya kamati hiyo, kwa mujibu wa vyanzo vyetu, alimshambulia spika wa Bunge, Samuel Sitta akidai kuwa kama si mizengwe, suala la Richmond lingemalizwa kwa taratibu za kichama.

Habari hizo zinadai kuwa Chenge, aliyewahi kuwa mwanasheria mkuu wa serikali, alisema Lowassa alizungukwa na kwamba kulikuwa na njama za kummaliza ingawa hakusema njama hizo zilifanywa na nani.

Chenge aliitetea serikali ya awamu ya tatu kuhusu kuingia mikataba mibovu na kusisitiza hakukuwa na uzembe kwani mikataba yote ilipitiwa na kukubaliwa na Baraza la Mawaziri.

Hata hivyo, mbunge wa Muleba Kusini, Wilson Masilingi alisimama na kuomba kutoa taarifa na kumwomba Mzee Mwinyi na kamati yake wawabane wabunge wanaodai wanasema ukweli.

Masilingi alipinga maelezo ya Chenge kuhusu mikataba na kusisitiza kuwa maelezo yake yalijaa ushabiki na kusema Baraza la Mawaziri liliridhia mikataba kutokana na ushauri wake (Chenge).

Mbunge wa Kwela, Dk Chrisant Mzindakaya, ambaye aliwahi kupata umaarufu kwa kulipua kashfa, aliwataka wabunge wakubali matokeo kuhusu Ripoti ya Richmond ili taifa lisonge mbele badala ya malumbano yasiyokwisha.

Kwa mujibu wa vyanzo vyetu, Mzindakaya aliwataka wabunge wafahamu kuwa ripoti hiyo ilishapitishwa na Bunge na haiwezi kurejeshwa ianze tena upya.

Naye Dk Mlingwa (Shinyanga Mjini), alisema mpasuko unaoinyemelea CCM unatokana na chama hicho kuacha misingi yake ya kuwa chama cha wakulima na wafanyakazi na badala yake kinawakumbatia wafanyabiashara.

Naibu Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Emanuel Nchimbi alitumia nafasi yake kuomba maridhiano ya wabunge wa CCM, kujenga moyo wa kusameheana ili chama kisonge mbele.


Daniel Mjema,Dodoma
__________________
A wise man once told me, luck isn't some mystical

KWA HUU UPUUZI JAMANI NAHISI HATA RAIS WAKE ALIEMTEUA LAZIMA AWE ANA MATATIZO KAMA SI AKILI YA KISAIKOLOJIA
VIVA CHAMA CHA MAJAMBAZI
 
Ushahidi wa kitumbo kitumbo na daily news?

Nilidhani ungefanya zaidi ya hili?

Alivyoumbuliwa na RA kwamba familia yake ilikwapua hela za wawekezaji mwenyewe alikiri kwamba wawekezaji walichotewa hela zao kinyume na urtaratibu wa kampuni na baada ya kugundua hilo alilala mbele (resign). hakusema alipiga kelele dhidi ya ufisadi kwa sababu beneficiaries walikuwa familia yake na marafiki. Sasa huyu ni mpiganaji?

Angalia video ya majibu yake dhidi ya mashambulizi ya RA.

Mzee mengi 'mpenda vita' kama daily News wangeoongopa kwamba hesabu zao (NICOL) zilikuwa chafu unadhani anagekaa kimya?
 
Sofia Simba ni zao la ufisadi pia ni zao la siasa na uongozi wa kubebana..ebu tujikumbushe alipofika hapo alipo...mwaka 2005 aligombea kula za maoni jimbo la Ilala ila kwa bahati mbaya alishidwa na mbunge wa sasa Mh Zungu..aliposhindwa akaenda UWT kutafuta viti maalumu na huko pia aliangukia pua ila kwa kuwa alikuwa karibu na watu walioshika nchi basi bwana mkubwa alivyopata urais akaona si mbaya akamteua kuwa mbunge na kumpa uwaziri kabisa...yani SOFIA SIMBA amebebwa kwa mbereko ya chuma......
 
Back
Top Bottom