Siungi mkono Rais kutukanwa!

Siungi mkono Rais kutukanwa!

Sawa, lakini hata mimi sidhani kabisa kama hilo kosa linaendana na adhabu aliyopewa huyo kijana.

Angeniita mimi 'bwege' unadhani hata angekamatwa?

Au hata ningeenda kumfungulia mashitaka unadhani angepewa hiyo adhabu aliyopewa?
Kwani hadhi yako ni sawa na rais kikatiba?
 
"Ninafikiri ni vyema na muhimu tukaendelea kukosoana kwa njia mbali mbali, lakini kwa hakika kabisa siungi mkono rais kutukanwa kwa kejeli ambazo zina sura ya mizaha na sio mabadiliko, Rais kuitwa BWEGE ni kosa na utovu wa nidhamu.

Kosa hili halipaswi kutiwa moyo wala kuungwa mkono, lakini kumwambia Kijana huyu kuwa alikosea ni jambo muhimu zaidi na la busara"

Godbless Lema (Mp)
Mhesh. Lema unafahamu suala hili limekuwa mjadala kutokana na mambo mawili; 1. Kwa bahati nzuri wakati kijana yule anatiwa hatiani kwa kosa la "kumwita Rais kuwa ni bwege" kule Arusha, kule Dodoma naibu spika wa Bunge alikuwa ametoka kumdhalilisha mbunge wa upinzani kwa kumwambia kuwa "aache ubwege wake". 2. Sheria ya mtandao imeibua maswali mengi mno mno!

Ni sawa, hata mimi siungi mkono Rais kuitwa "bwege", lakini tujiulize pia je, tunaunga mkono nani aitwe "bwege"? Kwamba rais wetu asiitwe bwege lakini wengine wana deserve kuitwa mabwege, siyo? Hivi tunawezaje kumwambia yule kijana kuwa alikosea, wakati inaonekana ni halali kwa ninyi wabunge wa upinzani kuitwa "mabwege"?

Tunalo tatizo kubwa katika jamii yetu, kwanza ya kuona kama vile viongozi hawakosei wakati ukweli viongozi hao ndio wamekuwa sehemu au bomba la kutiririsha ukiukwaji wa maadili katika jamii yetu. Huyu kijana ambaye leo mnamwambia alikosea, ndiye alishuhudia watanzania wenzake pale Jangwani wakitukanwa na mtu wa hadhi ya Rais kwamba ni wapumbavu kabisa kwa sababu tu wanaunga mkono siasa za upinzani.

Nakubaliana na wewe Mhesh. Lema tumwambie huyo kijana kwamba kumwita Rais kuwa ni "bwege" ni kosa kimaadili (ya hapa kwetu maana kwa wengine sio shida) achilia mbalia sheria hiyo ya hovyo ya makosa ya mtandao. Lakini viongozi wetu nao wafahamu kuwa wao pia wananayoyatenda na kuyatamka yanachochea vijana "kuwaita mabwege"!
 
Huo ndio ukomavu wa kisiasa wa Lema ambao wabunge na wengine wa upinzani waige siyo kupinga kila kitu kizuri ambacho serikali inafanya.
 
Naona msaliti mwingine huyu anajitegeneza taratibu.
 
Watu tunachokiongelea hapa ni double standards.. Matusi si mazuri kwa pande zote sio upande mmoja tu.. Kwahiyo na sisi tulioitwa malofa na wapumbavu tukiamua kujikusanya kupeleka shauri mahakamani Mr. Clean ataadhibiwa??

Wewe kama Mwanasheria naomba unijibu hilo..


Usichanganye mambo, kutukanwa wewe au fisadi Lowasa&Co. siyo sawa na kutukanwa Raisi wa JMTZ!
 
"Ninafikiri ni vyema na muhimu tukaendelea kukosoana kwa njia mbali mbali, lakini kwa hakika kabisa siungi mkono rais kutukanwa kwa kejeli ambazo zina sura ya mizaha na sio mabadiliko, Rais kuitwa BWEGE ni kosa na utovu wa nidhamu.

Kosa hili halipaswi kutiwa moyo wala kuungwa mkono, lakini kumwambia Kijana huyu kuwa alikosea ni jambo muhimu zaidi na la busara"

Godbless Lema (Mp)
Jamani juzi nkatika kipindi cha dakika 45, nilimsikia G Lema wa CDM akisema kuwa hana ID yoyote katika mtandao wa kijamii wowote. Sasa hii imetoka wapi?
 
Naye awe atumie busara. Si vyema mkuu wa kaya kuwaita watoto wa wenzie "vila.za" kama alivyowaita wale wanafunzi wa UDOM. Ajaribu kuzuia mizuka pale anapohutubia makundi ya watu, la sivyo vijana wataendelea kumtusi.
 
Rais wa Marekani anaitwa majina mengi mabaya kuliko hilo la bwege...
Sheria hizi lengo ni kuleta hofu kwa ujumla kwa watu
wasiwe free kumkosoa....

Kwani kukosoa lazima utukane au kutoa maneno ya kudhalilisha?? Kosoa kwa kutoa hoja sio VIOJA.
Na kama unaona hilo neno bwege ni sahihi basi jaribu kumuita mzazi wako hivyo ndiyo utaelewa uzito wake.
 
Nimeweka hoja ya ulinzi wa Rais kukuonyesha mantiki ya tofauti kati ya Rais wa nchi na wananchi mwingine.

Wewe unazungumzia istihaki. Unajua hata maana ya istihaki?

Kwangu kamwe istihaki haziwezi kumfanya binadamu mwingine awe na thamani kuliko binadamu wengine.

Yaani hapo unachosema ni sawa na kusema kuwa Diamond Platnumz ni tofauti na raia wengine kwa sababu kila hushangiliwa na mashabiki wake kila wamwonapo.

Unachekesha wewe.

Kusema wewe hauna tofauti na Rais wa nchi ni kuongea kwa kinadharia lakini kiuhalisia Rais wa nchi na wananchi wa kawaida wako tofauti.

Mimi ndo naongea kiuhalisia zaidi maana mahitaji yote yaliyo ya msingi kwa uhai wa binadamu hayatofautiani kisa tu huyu anafanya kazi hii na yule anafanya kazi ile.

Huyo Magu wako anaweza kuishi bila kula?

Hapana. Wewe unaongelea dhana ya kinadharia inayosema binadamu wote ni sawa lakini kiuhalisia binadamu wote siyo sawa.

Hapana. Wewe ndo nadhani hata hujaielewa vizuri hiyo dhana. Binadamu wote ni sawa haina maana ya kwamba kweli wote tuko sawa, la sivyo kusingekuwa na watu wafupi, warefu, wanene, weusi, wa kiume, wa kike, ma huntha, na kadhalika.

Hiyo dhana inahusiana na mambo ya kuheshimiana na kutendeana vyema pasipo kubagua wala kubaguana kwa kutumia vigezo bandia.

Rais kutokea miongoni mwa wananchi hakumfanyi awe ni sawa na wananchi wengine katika matendo na majukumu yake kama Rais.

Rais ni cheo tu. Cheo pamoja na istihaki zinazokuja na hicho cheo hakimfanyi awe tofauti na wananchi wengine. Naye ni mwananchi tu.

Matendo na majumu ya Rais ndiyo yanamfanya awe ni tofauti na wananchi wengine ndiyo maana hata Katiba ya Tanzania 1977 katika Sura ya Pili, Ibara ya 33(1-2) imebainisha ukweli kuhusu umuhimu wa Rais wa nchi.

Umuhimu wa cheo chake ama nafasi yake hakumfanyi awe tofauti. Naye ni mtu tu kama mimi na wewe.

Lazima uelewe kuwa kujiheshimu ni kuheshimiwa.

Huu ushauri nakushauri ungewapa huyo Magu wako na Mkapa.

Ninapoongelea Rais nina maana taasisi kwa ujumla wake.

Taasisi ni lidude au taasisi ni watu?

Rais Magufuli amevaa taasisi ya Urais na kutokana na taasisi hiyo, anatakiwa kisheria ajiheshimu.

Teh teh teh...sasa mbona hata hajiheshimu? Mtu anaropoka ropoka tu utadhani mlevi bana....

Hebu mtumie huo ushauri ajirudi bana.

Wewe mwananchi unaweza kuchagua kutojiheshimu na hakuna mtu au sheria inayokutaka kujiheshimu.

Kuna sheria inayotaka rais ajiheshimu?

Rais hawezi kuchagua kutojiheshimu na kama atataka kufanya hivyo basi inabidi aachie madaraka.

Kuna sheria inayomtaka hivyo?

Hii ndiyo tofauti ya msingi kati ya Rais wa nchi na mwananchi wingine.

Jaribu tena maana bado hujanionyesha tofauti aliyonayo Magufuli na wananchi wengine.
 
"Ninafikiri ni vyema na muhimu tukaendelea kukosoana kwa njia mbali mbali, lakini kwa hakika kabisa siungi mkono rais kutukanwa kwa kejeli ambazo zina sura ya mizaha na sio mabadiliko, Rais kuitwa BWEGE ni kosa na utovu wa nidhamu.

Kosa hili halipaswi kutiwa moyo wala kuungwa mkono, lakini kumwambia Kijana huyu kuwa alikosea ni jambo muhimu zaidi na la busara"

Godbless Lema (Mp)
The truth will always set you free. Your words are as informative, educative and liberating tool as a real politician
 
Kwa hiyo unataka kujilinganisha na Rais wa nchi?

Gharama za kukutunza unataka kuzilinganisha na gharama za kumtunza Rais?
Khee kilichovunjwa ni heshima ya mtu... na si uraisi wake... BINADAMU ANASTAHILI HESHIMA NA KUTHAMINIWA UTU WAKE.... nyie mnaodhani raisi nibmtu zaidi yako mnakosea... na ndo mnaoleta dhana ya umalaika..
 
Ukitukanwa mahakama ipo...
Ni jukumu lako kwenda mahakamani...
Akitukanwa Rais wapo wa kumwendea mahakamani sababu ni Rais...
Vyeo vinaenda na privileges ...huwezi kujilinganisha na mwenye cheo...ni kutafuta BP tu...
KWA sababu rais ni ndogo wa Mungu???
 
Rais wa Marekani anaitwa majina mengi mabaya kuliko hilo la bwege...
Sheria hizi lengo ni kuleta hofu kwa ujumla kwa watu
wasiwe free kumkosoa....
Mila, taratibu, kaninu za Marekeni tofauti na zetu na walipofikia wanatamani kubadikikakakini ni too late. NAdhani tujadili kwa context ya Tanzania na utamaduni wake!
 
Mkuu, kama umemsoma vema Lema amewakemea na hao wanaomchangia. Soma vizuri utaelewa
Yaani we ndio huja muelewa kabisa keywords ya Lema ni haya hapa "LAKI KUMWAMBIA HUYU KIJANA AMEKOSEA NI JAMBO LA BUSARA ZAIDI" Ana maanisha adhabu yote aliopewa haina maaana mpaka anaangaika kwenda kuchangisha watu na badala yake wangewezwa kumuonya kwa busara na akaelewa na kuwa balozi mzuri wa maadili.
 
Kemea kwanza tendo linalofanywa na vijana na madiwani wenu. Kitendo cha kumchangia fedha mtuhumiwa kinatoa taswira mbaya kwa chama chenu japo wengine wanaona ni kitendo cha kishujaa lakini huwezi kuenzi ushujaa katika mambo ya kijinga.

Ficha upumbavu wako.
 
Kwani kukosoa lazima utukane au kutoa maneno ya kudhalilisha?? Kosoa kwa kutoa hoja sio VIOJA.
Na kama unaona hilo neno bwege ni sahihi basi jaribu kumuita mzazi wako hivyo ndiyo utaelewa uzito wake.
Bwege sio sahihi hata kidogo Lakini kwa mtoto unamkanya sirudie tena. vile vile sio sahihi kuwaita watoto kama mzazi uliyezaa na una watoto V ,LAZA9. Mzazi hapo ameteleza vile vile- najua alikuwa labda kama anatania, lakini utani mwingine unaumiza roho! Ni sawasawa kumwambia mtu anayeanguka kifafa kuwa "ondoa kifafa chako hapa" ataumia sana hata kama ulilenga utani.,
 
Rais wa Marekani anaitwa majina mengi mabaya kuliko hilo la bwege...
Sheria hizi lengo ni kuleta hofu kwa ujumla kwa watu
wasiwe free kumkosoa....

Lakini ukumbuke hizi ni nchi mbili tofauti zenye sheria na mazingira tofauti
 
Heko Mh Lema. Kwa heko na hii wote tunge mwunga mkono na kufunga mjadala
 
Back
Top Bottom