Mhesh. Lema unafahamu suala hili limekuwa mjadala kutokana na mambo mawili; 1. Kwa bahati nzuri wakati kijana yule anatiwa hatiani kwa kosa la "kumwita Rais kuwa ni bwege" kule Arusha, kule Dodoma naibu spika wa Bunge alikuwa ametoka kumdhalilisha mbunge wa upinzani kwa kumwambia kuwa "aache ubwege wake". 2. Sheria ya mtandao imeibua maswali mengi mno mno!
Ni sawa, hata mimi siungi mkono Rais kuitwa "bwege", lakini tujiulize pia je, tunaunga mkono nani aitwe "bwege"? Kwamba rais wetu asiitwe bwege lakini wengine wana deserve kuitwa mabwege, siyo? Hivi tunawezaje kumwambia yule kijana kuwa alikosea, wakati inaonekana ni halali kwa ninyi wabunge wa upinzani kuitwa "mabwege"?
Tunalo tatizo kubwa katika jamii yetu, kwanza ya kuona kama vile viongozi hawakosei wakati ukweli viongozi hao ndio wamekuwa sehemu au bomba la kutiririsha ukiukwaji wa maadili katika jamii yetu. Huyu kijana ambaye leo mnamwambia alikosea, ndiye alishuhudia watanzania wenzake pale Jangwani wakitukanwa na mtu wa hadhi ya Rais kwamba ni wapumbavu kabisa kwa sababu tu wanaunga mkono siasa za upinzani.
Nakubaliana na wewe Mhesh. Lema tumwambie huyo kijana kwamba kumwita Rais kuwa ni "bwege" ni kosa kimaadili (ya hapa kwetu maana kwa wengine sio shida) achilia mbalia sheria hiyo ya hovyo ya makosa ya mtandao. Lakini viongozi wetu nao wafahamu kuwa wao pia wananayoyatenda na kuyatamka yanachochea vijana "kuwaita mabwege"!