A REJOINDER:
Preamble:
Katika utangulizi wako Aspirini unadai eti mwanaume ni Taasisi,my foot,apparently hata Adam katika bustani ya Eden thought so,see where he ended!
Aidha unadai kuwa mwanaume kapendelewa kuumbwa,hivi aliyelaaniwa akaambiwa kwa jasho lako utakula ni nani sio kidume Adam? na alitenda kosa gani by the way?
Tuje kwenye mada sasa pweint kwa pweint:
1.Urijali/umiliki:
Hivi wewe ukawazia kummiliki mwanamke amekuwa gari au nyumba.Is a woman a 'thing'?Hata katika lugha ya kijerumani mwanamke ni 'die' ,mwanaume ni 'der' na vitu vyote vilivyobaki ni 'das' au mwanamke unamuweka kundi la 'das'?
2.Maamuzi:Maamuzi yapi unayaongelea hapa yale yanayotolewa na kichwa cha juu ya kuamua kujenga,kufungua duka ,kununua gari?au yale unayoamua kwa kukutumia kichwa cha chini ya kuamua kulala na hausgel,kuzaa nje ya ndoa,kumjengea hawara n.k?
3.Uwajibikaji: Wangapi siku hizi wanalishwa na kuvishwa na wake zao? wanaume kibao wanatunzwa na wake zao na si kwamba hawataki kutunza kaya zao la hasha,ni circumnstances mme anajikuta ana kipato kidogo kuliko mkewe.Do you become less of a man kwa kuwa mke ana mshahara mkubwa kukuzidi? Learn to be humble.
Na hili la kudai mwanaume wa ukweli ni yule anayemridhisha mkewe kitandani,kama kigezo ni hicho basi duniani wanaume ni wa kuhesabu maana takwimu zinaonyesha ni wanawake wachache kwenye ndoa ambao huwa wanapata orgasm za kiukwelikweli.Wapo kinamama hadi wanapata vitukuu orgasm hawaijui.
4.Muda wa kukutana na wanaume wenzio: Hivi huko vijiweni la kuongea ni nini hasa kama sio kupapasa makalio ya mabaamedi? Na sio hilo tu, vijiweni huko ndo centre ya kudanganyana...oh mwanamke asikubabaishe bana akikujibu tia makofi...kumbe anayekushauri hayo akifika nyumbani kwake ni magoti chini mke wangu samahani nimechelewa kurudi.
5.Kwenda nje: Eti mradi mkeo asijue.Kumbe mnawaogopa? na kimada ukimpa mimba huo uso utauweka wapi,au ndo yale ya watoto kukutana makaburini kwenye msiba wa baba?
6. Uangalifu: tungekuwa waangalifu tungezaa nje?
'Sisi ndio wanaume bana'.......hahahahahahaa...usijisifu subiri usifiwe otherwise tutasema:
DEBE TUPU HALIACHI KUSHINDA
mwisho nasema:
Mwanamke akiwezeshwa anaweza!
Big up kinamama,yes you can!!!!!!
Yours sincerely,
Bishanga Abashaija.