Habari zenu waungwana.....
Huu ni waraka kwa vijana/wavulana wanaokaribia kuwa WANAUME. Kuwa MWANAUME si mchezo na si lelemama. Ushawahi kusikia Chama cha Wanaume, Umoja wa Wanaume, Umoja wa Wanasheria Wanaume, Umoja wa Madaktari wanaume etc?........ Hii inamaanisha MWANAUME ni Taasisi inayojitegemea.
Mwanaume kamili aliyekamilika si kama yule aliyozungumzia Bishanga kwenye sredi yake (kwa makusudi siweki link yake hapa)
Ili uwe MWANAUME yakupasa kwanza kabisa kumshukuru Mungu kwa kuumbwa jinsia ya kiume. Umepewa upendeleo lazima ushukuru. Halafu:
1. Uwe RIJALI na MMILIKI (hili halihitaji ufafanuzi) Ukishakuwa rijali unapaswa uwe na UMILIKI. Umiliki wa mwanaume rijali ni umiliki wa MWANAMKE/WANAWAKE. Iwe rasmi au vinginevyo. (Umiliki wa watoto pia ni muhimu japokuwa hili lategemea zaidi mapenzi ya Mungu). Ikumbukwe kuwa Mwanamke ni MALI ya mwanaume lakini watoto ni mali ya Mwanamke na Mwanamme.
2.Uwe na MAAMUZI. Usilegelege katika maamuzi yako. Mwanaume ndiyo kichwa cha familia, kichwa hakipaswi kuyumbishwa na mabega.....sawa? Kumbuka wewe ni taasisi!
3. MWAJIBIKAJI: Ni wajibu wako kuhakikisha Mwanamke UNAYEMMILIKI anatosheka na na kuridhika na huduma zako. Bioloji yake ipate habari yake sawa sawa, tumbo lake lipate chakula cha kutosha, mwili wake upate mavazi na miguu viatu. Mkipata watoto na mwanamke wako ni wajibu wako kuhakikisha wanapata mahitaji yote wanayostahili. Kama huna uwezo kwanini uzae kama kuku? Kulaaaleki!
4. Ukishafanikiwa kuyamudu yooote hayo hapo juu, usisahau kuwa duniani kuna wanaume wenzako. Tafuta muda wa kukutana na wanaume wenzako uongeze ujuzi na maarifa ya kuuishi uanaume. Hapo valuu, biya na nyama choma vinaruhusiwa kusikiliza maongezi yenu. Ukishapiga haya makitu rudi kwa mwanamke wako kampe haki yake kulaaleki. Ikumbukwe kuwahi kurudi nyumbani si sifa ya mwanaume. Mwache Mwanamke wako awe na muda wa kuwa huru na kulea watoto.
5. Inapotokea kwa namna yoyote na kwa sababu yoyote ile necha ikashika kasi ukajikuta unaenda nje ya MWANAMKE WAKO, hakikisha unaenda kwa uangalifu. MWANAMKE WAKO asijue! Kosa kubwa sana akijua, na hii si sifa ya mwanaume. Huo ni uvulana. Na huko ufanye kwa UANGALIFU. Usijemletea maradhi MWANAMKE wako.
Kuna wakongwe wenzangu, WANAUME wenzangu kibao wako hapa jamvini wanaweza kuendeleza huo mlolongo.
Au kama vipi, leo ni ijumaa, twaweza panga mkakati wa kukutana ili tuzungumzie uanaume wetu.
SISI NDIO WANAUME BANA! Wanaume ndio SISI.
Wanaume wengine hawa hapa wanaendeleza waraka.....
A REJOINDER:
Preamble:
Katika utangulizi wako Aspirini unadai eti mwanaume ni Taasisi,my foot,apparently hata Adam katika bustani ya Eden thought so,see where he ended!
Aidha unadai kuwa mwanaume kapendelewa kuumbwa,hivi aliyelaaniwa akaambiwa kwa jasho lako utakula ni nani sio kidume Adam? na alitenda kosa gani by the way?
Tuje kwenye mada sasa pweint kwa pweint:
1
.Urijali/umiliki:
Hivi wewe ukawazia kummiliki mwanamke amekuwa gari au nyumba.Is a woman a 'thing'?Hata katika lugha ya kijerumani mwanamke ni 'die' ,mwanaume ni 'der' na vitu vyote vilivyobaki ni 'das' au mwanamke unamuweka kundi la 'das'?
2.
Maamuzi:Maamuzi yapi unayaongelea hapa yale yanayotolewa na kichwa cha juu ya kuamua kujenga,kufungua duka ,kununua gari?au yale unayoamua kwa kukutumia kichwa cha chini ya kuamua kulala na hausgel,kuzaa nje ya ndoa,kumjengea hawara n.k?
3.
Uwajibikaji: Wangapi siku hizi wanalishwa na kuvishwa na wake zao? wanaume kibao wanatunzwa na wake zao na si kwamba hawataki kutunza kaya zao la hasha,ni circumnstances mme anajikuta ana kipato kidogo kuliko mkewe.Do you become less of a man kwa kuwa mke ana mshahara mkubwa kukuzidi? Learn to be humble.
Na hili la kudai mwanaume wa ukweli ni yule anayemridhisha mkewe kitandani,kama kigezo ni hicho basi duniani wanaume ni wa kuhesabu maana takwimu zinaonyesha ni wanawake wachache kwenye ndoa ambao huwa wanapata orgasm za kiukwelikweli.Wapo kinamama hadi wanapata vitukuu orgasm hawaijui.
4.
Muda wa kukutana na wanaume wenzio: Hivi huko vijiweni la kuongea ni nini hasa kama sio kupapasa makalio ya mabaamedi? Na sio hilo tu, vijiweni huko ndo centre ya kudanganyana...oh mwanamke asikubabaishe bana akikujibu tia makofi...kumbe anayekushauri hayo akifika nyumbani kwake ni magoti chini mke wangu samahani nimechelewa kurudi.
5.
Kwenda nje: Eti mradi mkeo asijue.Kumbe mnawaogopa? na kimada ukimpa mimba huo uso utauweka wapi,au ndo yale ya watoto kukutana makaburini kwenye msiba wa baba?
6.
Uangalifu: tungekuwa waangalifu tungezaa nje?
'Sisi ndio wanaume bana'.......hahahahahahaa...usijisifu subiri usifiwe otherwise tutasema:
DEBE TUPU HALIACHI KUSHINDA
mwisho nasema:
Mwanamke akiwezeshwa anaweza!
Big up kinamama,yes you can!!!!!!
Yours sincerely,
Bishanga Abashaija.