Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,774
Nimetafakari sana kauli ya Waziri wa mambo ya ndani, Nchimbi, alipoulizwa na waandishi wa habari iweje mikutano ya CCM haikuingiliwa na polisi siku hiyo hiyo Chadema walipopigwa Iringa na mwandishi kuuwawa, akasema alimuuliza Mukama akaambiwa ile ya CCM ilikuwa mikutano ya ndani. (Angalia picha uone mkutano mmojawapo "wa ndani" wa CCM ulivyokuwa, na watu wengi zaidi ya ule wa CHADEMA Iringa)
Ukiangalia picha za tukio la Iringa (angalia picha nimeambatanisha), utaona waziwazi kwamba CHADEMA wamepigwa na mwandishi kuuwawa katika eneo la ofisi ya CHADEMA, na bendera ya CHADEMA ikipepea katika mojawapo ya majengo ya hilo eneo. Taarifa zinasema polisi walikuwa wanatupa mambomu ndani ya ofisi ya CHADEMA, dhidi ya watu waliokuwa ofisini.
Sasa je, hili suala la kuzuia "maandamano ya CHADEMA", na kuruhusu "mikutano ya ndani ya CCM" siku hiyo hiyo moja linakujaje?
Na iweje Waziri Nchimbi anamuuliza Mukama badala ya kuwauliza polisi kwa nini hawakuzuia mkutano wa CCM? Alitegemea jibu gani toka kwa Mukama?
Mie si mwanachama wa CCM wala CHADEMA, lakini nasema wazi, SIO SIRI, POLISI WANAWAONEA CHADEMA, WANAWAPENDELEA
CCM
Ukiangalia picha za tukio la Iringa (angalia picha nimeambatanisha), utaona waziwazi kwamba CHADEMA wamepigwa na mwandishi kuuwawa katika eneo la ofisi ya CHADEMA, na bendera ya CHADEMA ikipepea katika mojawapo ya majengo ya hilo eneo. Taarifa zinasema polisi walikuwa wanatupa mambomu ndani ya ofisi ya CHADEMA, dhidi ya watu waliokuwa ofisini.
Sasa je, hili suala la kuzuia "maandamano ya CHADEMA", na kuruhusu "mikutano ya ndani ya CCM" siku hiyo hiyo moja linakujaje?
Na iweje Waziri Nchimbi anamuuliza Mukama badala ya kuwauliza polisi kwa nini hawakuzuia mkutano wa CCM? Alitegemea jibu gani toka kwa Mukama?
Mie si mwanachama wa CCM wala CHADEMA, lakini nasema wazi, SIO SIRI, POLISI WANAWAONEA CHADEMA, WANAWAPENDELEA
CCM