Mtu wa Asali
Senior Member
- May 9, 2022
- 152
- 291
Siyo siri tena ndani ya CCM kuna kundi linaitwa “Matokeo Chanya”
Ambalo linaundwa na viongozi waandamizi wa awamu ya tano wa Serikali na chama, Kiongozi wao Mkuu ni Kitila Mkumbo, Katibu ni Mwita Waitara akisaidiwa na Mpina na Lusinde.
Hawa wanasema ndiyo wenye Kulinda Legacy ya Mwendazake kwa maslahi ya Biashara ambazo zilikuwa uncompleted. Kifupi wametengeneza kundi litakaloingia kwenye uchaguzi 2025 kama ikishindikana iwe 2030. Wengine ndani ya kundi hilo ni William Lukuvi, Aluko Kabudi, Bashiru Ally pamoja na Kassim Majaliwa.
Mfumo huo umewekwa Nakshi na aliyewahi kuwa mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa Dk. Rafael Chegeni.
Hivi Karibuni Dk. Chegeni aliteuliwa katika teuzi za moja ya nafasi kuwa mkuu wa mkoa wa Mara na baadaye jina lake kuondolewa.
Dk. Chegeni ameamua kucheza kamari ndani ya CCM kujaribu kwa mara nyingi kama alivyofanya kwa Lowassa na kushindwa wanaimani safari hii wataweza kwa kuwa wana uzoefu.
Mara kadhaa Dk Chegeni amekuwa akinukuliwa kuwa “Watafanya kila wawezalo kuleta Utata kuwe na maridhiano kwa kuhakikisha mgombea wanayemtaka katika uchaguzi wa 2025”
Katika Nukuu nyingi Chegeni ametoa hoja kwa Mpina na Lusinde kabla ya uchaguzi mkuu kuna maelekezo wanapaswa kusimamia yaingizwe kwenye katiba kufanyika kwa mabadiliko kwa kuruhusu mgombea binafsi.
Luhaga Mpina
Mbunge wa Kisesa amenukuliwa kwa kinywa chake akisema kuwa atatumia nguvu zake zote kuhakikisha kuwa kundi lake linapata ushindi, lengo la sasa ni kuhakikisha wanatengeneza kundi kubwa lenye ushawishwi wa Wananchi kupitia mgombea binafsi.
Kitila Mkumbo
Katibu wa kundi la matokeo chanya”. Ameeleza msimamo wake wa kumuunga mkono Kassimu Majaliwa na kueleza ni kitendo cha kiungwana na ni suala la kikatiba ni Uhuru wa mawazo kwa kila mtu kusema chochote na ndiyo msingi wa demokrasia.
Kuna taarifa kuwa tayari kuna Vijana wa “matokeo chanya” wametumwa katika maeneo mbalimbali ya nchi ni pamoja na Meatu, Makete, Karatu, Bariadi, Busega, Karagwe, Bunda, Kasulu, Mpanda, Masasi, Ruangwa, Kibondo, Kilolo na Rungwe.
Mshauri wa Timu ya matokeo chanya mwenyekiti wa kamati ya Amani ya madhehebu ya Dini, Mkoa wa Dar es salaam Sheikh Alhadi Juma Mussa ndiye anayetumika kuwashawishi viongozi wa dini kumuunga mkono “kassimu Majaliwa” katika harakati zake za kugombea.
Ambalo linaundwa na viongozi waandamizi wa awamu ya tano wa Serikali na chama, Kiongozi wao Mkuu ni Kitila Mkumbo, Katibu ni Mwita Waitara akisaidiwa na Mpina na Lusinde.
Hawa wanasema ndiyo wenye Kulinda Legacy ya Mwendazake kwa maslahi ya Biashara ambazo zilikuwa uncompleted. Kifupi wametengeneza kundi litakaloingia kwenye uchaguzi 2025 kama ikishindikana iwe 2030. Wengine ndani ya kundi hilo ni William Lukuvi, Aluko Kabudi, Bashiru Ally pamoja na Kassim Majaliwa.
Mfumo huo umewekwa Nakshi na aliyewahi kuwa mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa Dk. Rafael Chegeni.
Hivi Karibuni Dk. Chegeni aliteuliwa katika teuzi za moja ya nafasi kuwa mkuu wa mkoa wa Mara na baadaye jina lake kuondolewa.
Dk. Chegeni ameamua kucheza kamari ndani ya CCM kujaribu kwa mara nyingi kama alivyofanya kwa Lowassa na kushindwa wanaimani safari hii wataweza kwa kuwa wana uzoefu.
Mara kadhaa Dk Chegeni amekuwa akinukuliwa kuwa “Watafanya kila wawezalo kuleta Utata kuwe na maridhiano kwa kuhakikisha mgombea wanayemtaka katika uchaguzi wa 2025”
Katika Nukuu nyingi Chegeni ametoa hoja kwa Mpina na Lusinde kabla ya uchaguzi mkuu kuna maelekezo wanapaswa kusimamia yaingizwe kwenye katiba kufanyika kwa mabadiliko kwa kuruhusu mgombea binafsi.
Luhaga Mpina
Mbunge wa Kisesa amenukuliwa kwa kinywa chake akisema kuwa atatumia nguvu zake zote kuhakikisha kuwa kundi lake linapata ushindi, lengo la sasa ni kuhakikisha wanatengeneza kundi kubwa lenye ushawishwi wa Wananchi kupitia mgombea binafsi.
Kitila Mkumbo
Katibu wa kundi la matokeo chanya”. Ameeleza msimamo wake wa kumuunga mkono Kassimu Majaliwa na kueleza ni kitendo cha kiungwana na ni suala la kikatiba ni Uhuru wa mawazo kwa kila mtu kusema chochote na ndiyo msingi wa demokrasia.
Kuna taarifa kuwa tayari kuna Vijana wa “matokeo chanya” wametumwa katika maeneo mbalimbali ya nchi ni pamoja na Meatu, Makete, Karatu, Bariadi, Busega, Karagwe, Bunda, Kasulu, Mpanda, Masasi, Ruangwa, Kibondo, Kilolo na Rungwe.
Mshauri wa Timu ya matokeo chanya mwenyekiti wa kamati ya Amani ya madhehebu ya Dini, Mkoa wa Dar es salaam Sheikh Alhadi Juma Mussa ndiye anayetumika kuwashawishi viongozi wa dini kumuunga mkono “kassimu Majaliwa” katika harakati zake za kugombea.