Suzy Elias
JF-Expert Member
- Nov 9, 2021
- 1,067
- 6,193
Je, Majaliwa wa 2015-2021 ndiye huyo wa sasa!?
Ukweli ni kwamba, siye Majaliwa tuliye mzoea. Siye PM Majaliwa aliye wahi kuwa na uwezo wa kuchukua uamuzi mgumu kwa Watumishi wazembe wa Serikali. Na siye Kassim aliye ogopewa na Watendaji wazembe wa Serikali.
Kwa hakika, Majaliwa kapoa kawa wa baridi na mwenye wingi wa hofu wa kuamua jambo! Majaliwa wa leo ni Kassim wa kusubiri ishara ya Samia ya kutopendezwa na jambo fulani ndipo naye huanza kuchukua hatua.
Siyo siri tena Taifa la Tanzania linamhitaji PM Majaliwa wa 2015-2021 ili likomboke na mafisadi na wazembe kazini!
Ni wakati sahihi sasa wapenda haki tumlazimishe Kassim awe yule na si huyo wa sasa.
Eti, kwa mshangao wa haja kuhusu madudu yanayoendelea pale Tanesco kwa mfano Majaliwa yule angekuwa msinyaa kama tete kwalo!?
Ukweli ni kwamba, siye Majaliwa tuliye mzoea. Siye PM Majaliwa aliye wahi kuwa na uwezo wa kuchukua uamuzi mgumu kwa Watumishi wazembe wa Serikali. Na siye Kassim aliye ogopewa na Watendaji wazembe wa Serikali.
Kwa hakika, Majaliwa kapoa kawa wa baridi na mwenye wingi wa hofu wa kuamua jambo! Majaliwa wa leo ni Kassim wa kusubiri ishara ya Samia ya kutopendezwa na jambo fulani ndipo naye huanza kuchukua hatua.
Siyo siri tena Taifa la Tanzania linamhitaji PM Majaliwa wa 2015-2021 ili likomboke na mafisadi na wazembe kazini!
Ni wakati sahihi sasa wapenda haki tumlazimishe Kassim awe yule na si huyo wa sasa.
Eti, kwa mshangao wa haja kuhusu madudu yanayoendelea pale Tanesco kwa mfano Majaliwa yule angekuwa msinyaa kama tete kwalo!?