pierre tall
JF-Expert Member
- Nov 5, 2013
- 4,245
- 3,728
Hakuna dhambi mbaya kama kujidanganya mwenyewe,HUWEZI KAMWE kuwa na furaha yakulea mtoto peke yako hata uwe na mali na utajiri mkubwa kiasi gani,kitu kinaitwa FURAHA huwa hakilinganishwi na mali hata kidogo,kinalinganishwa na usawa,haki na amani katika mazingira uliyopo,kuwa na mtoto unamlea peke yako kila ukimuangalia na yeye akikuuliza mzazi mwenzako(baba/mama) yupo wapi kisha ukakosa majibu SAHIHI naya kweli hapo ni LAZIMA tu amekunyima AMANI na hapo HUWEZI kusema kamwe una maisha ya furaha na amani eti kwa sababu una mali,ni UPUMBAVU ulioje uliochanganyikana na fikra mfu sanjali na ubinafsi wa hali ya juu kusema kuwa una Furaha na amani ya wewe/mimi wakati kuna kiumbe anayetupa kero ya moyoni kwa kila kumuona au atapotuuliza,HESHIMA na UBINADAMU wetu haupimwi kwa kiwango cha mali,kinapimwa kwa jinsi unavyojali furaha ya mwingine,kwa sababu furaha yako/yangu inakuja pale unapompa furaha mwingine,hii ni toka misingi ya dunia hadi milele..DAMU ya MTU haipotei kamwe,itachukua miaka mingi ijayo ila ipo siku tu itajulikana na hii ni kawaida,haijawahi kuwa kinyume,tutawaficha watoto wetu kuhusu mzazi wake halisi ila siku atakuja mtafuta tu..Watu wataandika hapa kujifariji ila moyoni tunajua jinsi gani tunavyojikaanga na haya mafuta,sisi siyo wanyama kuwa ulibeba tu mimba au kubebesha mtu mimba halafu tusiwe na uchungu wakupata uungwaji mkono upande wa pili katika malezi...kimsingi tunahitajika kuwaeleza ukweli hawa watoto wetu na siyo kuwaficha maana bado haitusaidii hata kidogo,unampa mtoto uongo mkubwa halafu bado moyoni unaumia...Kama ulimpa mimba binti wa watu na ukamkimbia,mtoto akija kwako mueleze ukweli uwe huru hata kama atakuchukia ila kwa MUNGU wako umenawa mikono,kama ULIOLEWA/KUWA KATIKA MAHUSIANO kisha ukaachika katika mazingira yakutokuwa muaminifu(kuchepuka) wakati huo ukiwa na mimba muambie ukweli mtoto kuliko kuendelea kumlisha maneno ya sumu kuwa baba alikutelekeza..UKWELI HUKUWEKA HURU TUSIJIFARIJI KINAFKI(tusijipake mafuta kwa mgongo wa chupa).