Single mums and dads come this way

Single mums and dads come this way

Hakuna sehemu kafundishwa matusi,tena kilaza kamsifu mamaake kwa kumlea kwenye maadili,kuna watu humu wamelelewa na wazazi wawili lakini wana matusi ajabu,kilaza katukana hapo kwanza?!hayo ni majina tu kayatoa kwa mtu asiyejali familia yake hasa watoto,mi nasema mwanaume kama huyo ni Fisi Maji.Alaa!

sio fisi maji mbwa mwitu,nguruwe pori,dudu lisilouma
wanakera sana hao wakataa watoto
tena asa hv waweza kuta wazazi wastaarabu ila hao watoto majanga
 
Ndio maana Kongosho ame suggest tuwe objective...
Ukute na mkeo ni kati ya hao wanaolia kuwa ni victims...
Ukweli hauwezi patikana kwa kusikia story za upande mmoja...
Kila mtu anaona mwenzie ndio mkosaji...

Sasa mwenye access na mtoto anatafuta support ya mtoto against mzazi mwenzie...

Ndio maana tukipima maelezo ya mtu tunajaribu kumsaidia aone na mapungufu yake pia...
Kitu ambacho watu wake wa karibu wanaweza wakawa wanaogopa kumwambia japo wanakiona...
Labda ndiye anayetegemewa kwenye ukoo ...hivyo anaambiwa anachotaka kusikia...
Mke wangu tumeish nae kwa miaka kumi na kupata watoto wawil wa kiume,aliamua kuondoka na watoto wote na kurudi kwao.Baada ya mda mfup alipata kaz na kupanga chumba.Alipopanga ni karibu namm ninapoishi.Watoto wangu walikua wanaishi maisha magumu kwan walikua wanakuja kwangu na kunieleza.Baada ya takriban miez sita niligundua kuwa rafiki yangu wa karibu na kama ndg yangu ndie alie mpangashia chumba,kumtafutia kaz napia anawalisha adi wazaz wa mke wangu.Ilinibidi nikashtaki ofsin icho kitendo il jamaa ahamishwe,cha ajabu familia ya mke wangu na mke wangu wote wakanifungulia kes kuwa nawatishia.Mtoto wangu mkubwa aliekua ananipa siri wakamfukuza.Mpaka sasa naish nae.Napata changamoto nyingi sana kumlea kwan ni mdogo yupo darasa la nne na mimi kaz zinanibana.Akimaliza mtihan wa taifa tampeleka akaish na wazaz wangu.Mwanamke kaniudh na jamaa yangu ameniuzi sana.
 
yaani roho inaniuma sana.mimi umri mdogonilio nao nalea watoto wawili wa marehemu dada yangu(mungu ampunzishe kwa amani) baada ya kuzalishwa na wanaume tofauti.isitoshe baba zao wapo mitaani wanazurura tu yaani roho inaniuma sana.hao watoto niwajue kwa lote kuhusu malazi,maradhi,chakula,matibabu na shule. yaani mi nafikiria nitajipanga lini.kwani nafikiria nikio huyo mwanamke ataweza kukaa na hawa watoto na wanawake wenyewe wa siku hizi.lakini ok mungu atanilipia tu.
 
Uko sahihi ndugu yangu hata mimi ilinitokea hivyo aliniambia nitoe but nilikataa na mapenzi yakaisha tangu mimba mpaka sasa mtoto ana miaka mitano hajui anachokula anachovaa wala matibabu na anajua kama ana mtoto natamani nicngemwambia kama ni mtoto wake hataki hata kumuona nimemuongopea mpaka sasa nimeamua kumwambia ukweli baba yako hakutaki

pole kwa maumivu lakini kama umeamua kumweleza mtoto ukweli kuhusiana na babake basi tafuta maneno kulingana na umri. Kama ni mdogo si umwambie baba yupo lakini ana kazi nyingi.... akikua kua mwambie baba yako hakupendi lakini msamehe, wanaume wengi ni watu wazuri isipokuwa baba alighafilika tu. Pamoja na machungu yetu sisi ni wazazi (naongea kama single mama kwa hiyo msiseme sijapitia hayo mliyopitia). Kama mzazi una wajibu wa kumfundisha mtoto wako values kama kupenda na kusamehe. Unavyomwambia mtoto baba yako hakutaki katika umri mdogo unamfanya aoanishe jinsi ya kiume na kumkataa. hapo unatengeneza mwanamke atakayechukia wanaume au atakayekuja kupenda wanaume waharibifu kama baba yake, au atakayekuja kutenda wanaume kama njia ya kumuadhibu baba yake (sijui kwa nini nime-assume mtoto wako ni wa kike). We hata kama unamchukia huyo mwanaume jikaze uanze kumwambia mtoto wako amsamehe babake na ampende baba yake hata kama baba hampendi. Kwa mtoto mdogo hili linatekelezeka kwa urahisi sana. Hata ukifa leo umuache mtoto ukiwa umepanda mbegu nzuri moyoni mwake.

Mimi mtoto wangu anamfahamu babake ila kuna kipindi alikuwa ananiandama sana kwa nini hatukai pamoja. Nikawa nampa majibu yanayoibua maswali mapya kila siku. Siku moja nikamuuliza baba mmoja hivi nimjibu nini mtoto anielewe? Maana ni kama amenizidi akili. Kila ninachomwambia anakihoji. Yule baba akanijibu, hilo tu? njoo hapa tuombe. baadhi ya maneno ni kuwa roho mtakatifu anipe cha kuongea na kumfunulia mtoto kuelewa. Nikafika nyumbani nikiwa nimejaa confidence lakini nataka kuongea confo likashuka. Nikaanza kucheza nae kisha nikaanza kujieleza maneno meeeeengi. mtoto alinijibu maneno machache sana. "...Mungu ndo alipenda unizae hivyo ... I know god loves me....and i love you and dad." Macho yakanitoka, hata sikuamini kama naongea na mtoto wa miaka mitano. Kesho yake akaniropokea. "...mama umshukuru baba maana bila yeye usingenizaa...". huko moyoni nikasema hili litoto limetumwaa nini. nikamjibu sawa. Kuanzia siku hiyo sijaskia tena maswali kuhusu hiyo mada, na akisali anatuombea wazazi wote wawili na familia ya baba yake. By the way mimi na babake tuliachana, baada ya muachano ndo nagundua nimeondoka na kiinua mgongo-mimba baada ya miaka 5 ya uchumba sugu.
 
Wewe unajua maana ya mshenga kweli? And by the way just so you know, you are a very CLOSED MINDED PERSON. For one those type of people need not and in fact do not have to pronounce themselves as such. But you wouldn't understand this stuff coz it is way above your level of the so called "open mindedness"!!!

ha ha ha lol we mshari kweli tangia jana unapayuka tu! NB:nawakilisha nilichoandika!Accept other peoples choices and stop judging them period!TAKE IT OR LEAVE IT!
 
Ukiwa objective humu unaweza kupigwa hata mawe.

aisee kuna haja ya mimi kurudi chuo. Kumbe mtu anakuwa objective anapotoa mtazamo wa tofauti na wenzie, na mwingine anakuwa subjective mtazamo wake unapofanana na wa yule anayezungumziwa! objectivity=non-conformity. Ingekuwa hoja hapa ni jua linachomoza magharibi na kuchwea mashariki labda ningewaelewa wanaojiita objective, lakini kuongelea hali ambayo haifanani hata kwa watu wenye nayo ukweli ni kuwa unakuwa objective kwenye subjectivity yako tu na si vinginevyo. na ndo unakuta mtu anadai single mom anajinyanyapaa na anamfananisha na gay anayepaza sauti yake apewe uhuru wake na straights wanaojiona wana haki zaidi. Anadai gay anajinyanyapaa wakati akijikubali anatungiwa sheria ili anyongwe au afungwe. Objectivity in deed!!
 
duu! umeongea saaana kwa uchungu. Sasa kama mamako alikuficha kuhusu babako na ulivyomkomalia akakwambia na wewe mwenyewe ukachukua hatua kumfata babako akakutolea nje huoni kama mama yako alikuwa na sababu ya kutokwambia toka mwanzo? Unajuaje kama baba yako alimwambia amkome tangu ukiwa tumboni na ndo maana ulivyomkabili akakutimua? unajitwisha mzigo wa kujionea huruma bure tu eti huna mashangazi sijui ndugu zako ni wachache. Hebu kamuulize prof masalakulangwa pale hubert kairuki anaishije maana yeye aliokotwa akakulia mission - hakuna cha baba, mama wala shangazi. Sijawahi kumhoji lakini huwa nahisi anashukuru kwa yote maana asingetupwa uprofesa wake na baraka zingine alizopewa angezisikia redioni tu. Na sisi wengine tungeikosa huduma yake. Nimesikikitka hata ulivyosema unahangaika upate hela labda babako atakukubali. We kaka wewe! hebu acha kujinyanyapaa bwana. Wasamehe hao wazazi wako, tafuta hela ikusaidie wewe na familia yako. Huna upungufu wowote. Watu tumekulia mazingira kama hayo hayo na tumetoka huko tukiwa washindi. Huku nje ya jf tuna-inspire watu wanaona kuna tumaini kwenye maisha. Haijalishi umetokea wapi. Cha msingi uko hapo ulipo, amua kuishi kwa furaha au kwenye kifungo cha vitimbi vya wazazi. Usijidanganye kuwa ungejikuta ndoani hali ingekuwa tofauti. Kuna wenzio wana baba na mama tena wenye uwezo lakini wameharibikiwa kabisa. Sasa kama mamako aligoma kukwambia kuhusu babako na ulivyomjua babako ukaambulia kutimuliwa, hawa watu wangeoana ungekuwa mtoto wa aina gani? Kawaulize watoto/watu wazima walioishi kwenye paa lenye ndoa aina ya kosovo! Usipoteze muda kwenye kuota maisha uliyotaka yawe. Maisha yashakuleta mpaka hapo chukua hatua kuyaboresha.

Halafu ushauri kuwa wamama/wababa wasizae mtoto zaidi ya mmoja na watu tofauti ni mzuri lakini uzoefu wa aina yako haufanani dunia nzima. Kuna mama namjua ana watoto watatu kila mmoja na babake lakini wanae wanapendana sana na wa kwanza ameshaanza maisha yake ya ndoa, wengine bado wanasoma. Kwa hiyo uzoefu wako si wa wengine.

Halafu naamini kina mama huwa na sababu nzuri tu za kutowaambia watoto kuhusu baba zao mpaka wakati wanapoona mtoto amefikia uwezo wa kuujua ukweli hasa kama ni mzito. Sasa imaggine mamako angekwambia ukiwa mdogo kuwa baba yako alikukataa, si ungeathirika sana? Hapo umemfata babako ukiwa mtu mzima umeishia kulia na kuazimia kutafuta hela ili akukubali. Maadam babako ameshajua kuwa hata we umefata, we muache, endelea na mambo yako. Kwani waliofiwa na baba zao wakiwa tumboni wanaishije? Kwa nini wewe unalikuza sana hili jambo?

Kuna wamama wengine ukiwauliza kuhusu baba unawaumiza tu. Huu mfano ninautoa hapa ni wa kweli, ni wa mtu wa karibu kwangu. Huyu alipewa mimba na baba yake mzazi akiwa na miaka 14. Enzi za zamani na sasa kwa wachache mama akavumilia, mtoto akazaliwa mama akamchukua akamlea kama mtoto wake wa mwisho. Yule mtoto aliyenajisiwa na baba akaondolewa pale nyumbani akaenda kuishi mkoani na ndugu. Yule mtoto aliyezaliwa akawa anamwita mama yake dada, na bibi yake sijui mama mkubwa akawa anamwita mama. Baba tu ndo alipatia. Miaka ikaenda, kwa kuwa lile jambo kimila lilikuwa ni laana, tambiko lilifanyika kwa hiyo kuna wajumbe wa tambiko walishindwa kutunza siri. Kwa hiyo binti akiwa kwenye miaka ya 20 akapata nyuuz kuwa yule mamake si mamake, ila hawakumwambia mama yake ni nani. Mtoto akaenda kuanzisha timbwili nyumbani. Mama wa watu kaishia kupoteza tu fahamu na kulazwa. Ikabidi siri iwekwe hadharani ila wakamsihi binti akienda kwa mama yake mzazi aendelee tu kumwita dada maana ile siri hata mume wa dada yake haijui (wakati huo yule dada-mama alikuwa ameshakaa kwenye zaidi ya miaka 10 na watoto watatu.

Hili jambo lilikuwa zito sana kwa binti. Akaanza kujichukia, akawa kahaba na haikupita miaka mitano akawa ameshaambukizwa VVU akafa. Wakati wa msiba wake ndo shemeji yake ambaye ni babake wa kambo wa kambo anajua ukweli kuwa mkewe alizaa na babake. Ile ndoa mpaka leo ipo inakaribia miaka 30. Nia yangu ni kuonyesha tu kuwa mioyo ya watu ina mengi.

kaka hukunielewa vizuri,nimesema ktk kufatilia nilijikuta nina baba wawili,moja niliye ambiwa na ndugu zangu na mwangine niliye ambiwa na mama yangu wote niliwasiliana nao kwa simu na sio ana kwa ana na wote walikubali.hapo ndipo nilipo pata tatizo tena pia sijaomba msaada kutoka kwa yoyote hata siku moja nilichosema ni kuwa siku nikiwa na pesa nisafiri nikawacheki labda nitagundua ni yupi kati yao.
 
Una-enjoy eeh? Basi kama vipi hao watoto wangu uwalee vizuri, ila nikija tena najua utanipa halafu utakuja humu kulialia au ukishajaa kwa mara nyingine au sio?

objectivity ishaingiliwa haki ya nani
 
Hakuna sehemu kafundishwa matusi,tena kilaza kamsifu mamaake kwa kumlea kwenye maadili,kuna watu humu wamelelewa na wazazi wawili lakini wana matusi ajabu,kilaza katukana hapo kwanza?!hayo ni majina tu kayatoa kwa mtu asiyejali familia yake hasa watoto,mi nasema mwanaume kama huyo ni Fisi Maji.Alaa!

Usimfundishe mwanao kumuita Baba yake fisi Maji, no matter how frustrated you are kwa aliyokutendea. Mfundishe kumpenda kila mtu, kuheshimu hata huyo Baba kwa kuwa hatapungukiwa na kitu.
 
duu! umeongea saaana kwa uchungu. Sasa kama mamako alikuficha kuhusu babako na ulivyomkomalia akakwambia na wewe mwenyewe ukachukua hatua kumfata babako akakutolea nje huoni kama mama yako alikuwa na sababu ya kutokwambia toka mwanzo? Unajuaje kama baba yako alimwambia amkome tangu ukiwa tumboni na ndo maana ulivyomkabili akakutimua? unajitwisha mzigo wa kujionea huruma bure tu eti huna mashangazi sijui ndugu zako ni wachache. Hebu kamuulize prof masalakulangwa pale hubert kairuki anaishije maana yeye aliokotwa akakulia mission - hakuna cha baba, mama wala shangazi. Sijawahi kumhoji lakini huwa nahisi anashukuru kwa yote maana asingetupwa uprofesa wake na baraka zingine alizopewa angezisikia redioni tu. Na sisi wengine tungeikosa huduma yake. Nimesikikitka hata ulivyosema unahangaika upate hela labda babako atakukubali. We kaka wewe! hebu acha kujinyanyapaa bwana. Wasamehe hao wazazi wako, tafuta hela ikusaidie wewe na familia yako. Huna upungufu wowote. Watu tumekulia mazingira kama hayo hayo na tumetoka huko tukiwa washindi. Huku nje ya jf tuna-inspire watu wanaona kuna tumaini kwenye maisha. Haijalishi umetokea wapi. Cha msingi uko hapo ulipo, amua kuishi kwa furaha au kwenye kifungo cha vitimbi vya wazazi. Usijidanganye kuwa ungejikuta ndoani hali ingekuwa tofauti. Kuna wenzio wana baba na mama tena wenye uwezo lakini wameharibikiwa kabisa. Sasa kama mamako aligoma kukwambia kuhusu babako na ulivyomjua babako ukaambulia kutimuliwa, hawa watu wangeoana ungekuwa mtoto wa aina gani? Kawaulize watoto/watu wazima walioishi kwenye paa lenye ndoa aina ya kosovo! Usipoteze muda kwenye kuota maisha uliyotaka yawe. Maisha yashakuleta mpaka hapo chukua hatua kuyaboresha.

Halafu ushauri kuwa wamama/wababa wasizae mtoto zaidi ya mmoja na watu tofauti ni mzuri lakini uzoefu wa aina yako haufanani dunia nzima. Kuna mama namjua ana watoto watatu kila mmoja na babake lakini wanae wanapendana sana na wa kwanza ameshaanza maisha yake ya ndoa, wengine bado wanasoma. Kwa hiyo uzoefu wako si wa wengine.

Halafu naamini kina mama huwa na sababu nzuri tu za kutowaambia watoto kuhusu baba zao mpaka wakati wanapoona mtoto amefikia uwezo wa kuujua ukweli hasa kama ni mzito. Sasa imaggine mamako angekwambia ukiwa mdogo kuwa baba yako alikukataa, si ungeathirika sana? Hapo umemfata babako ukiwa mtu mzima umeishia kulia na kuazimia kutafuta hela ili akukubali. Maadam babako ameshajua kuwa hata we umefata, we muache, endelea na mambo yako. Kwani waliofiwa na baba zao wakiwa tumboni wanaishije? Kwa nini wewe unalikuza sana hili jambo?

Kuna wamama wengine ukiwauliza kuhusu baba unawaumiza tu. Huu mfano ninautoa hapa ni wa kweli, ni wa mtu wa karibu kwangu. Huyu alipewa mimba na baba yake mzazi akiwa na miaka 14. Enzi za zamani na sasa kwa wachache mama akavumilia, mtoto akazaliwa mama akamchukua akamlea kama mtoto wake wa mwisho. Yule mtoto aliyenajisiwa na baba akaondolewa pale nyumbani akaenda kuishi mkoani na ndugu. Yule mtoto aliyezaliwa akawa anamwita mama yake dada, na bibi yake sijui mama mkubwa akawa anamwita mama. Baba tu ndo alipatia. Miaka ikaenda, kwa kuwa lile jambo kimila lilikuwa ni laana, tambiko lilifanyika kwa hiyo kuna wajumbe wa tambiko walishindwa kutunza siri. Kwa hiyo binti akiwa kwenye miaka ya 20 akapata nyuuz kuwa yule mamake si mamake, ila hawakumwambia mama yake ni nani. Mtoto akaenda kuanzisha timbwili nyumbani. Mama wa watu kaishia kupoteza tu fahamu na kulazwa. Ikabidi siri iwekwe hadharani ila wakamsihi binti akienda kwa mama yake mzazi aendelee tu kumwita dada maana ile siri hata mume wa dada yake haijui (wakati huo yule dada-mama alikuwa ameshakaa kwenye zaidi ya miaka 10 na watoto watatu.

Hili jambo lilikuwa zito sana kwa binti. Akaanza kujichukia, akawa kahaba na haikupita miaka mitano akawa ameshaambukizwa VVU akafa. Wakati wa msiba wake ndo shemeji yake ambaye ni babake wa kambo wa kambo anajua ukweli kuwa mkewe alizaa na babake. Ile ndoa mpaka leo ipo inakaribia miaka 30. Nia yangu ni kuonyesha tu kuwa mioyo ya watu ina mengi.

mkaka fula hv rafki yangu alikua baba ake hamjui
yule mama akaanza kuumwa akamwita mwanawe akamwambia niahidi hutamtafuta baba ako ht nikifa
yule mama amekufa mkaka hana jinsi yupo tu
 
inakuondolea kuwa objective.

sympathy ya nini? Empathy ya nini? Sijamlazimisha mtu kuwa na self pity, sio tatizo langu.

Haimaanishi kwasababu its anyonymous basi you can behave like a rackless bitch,there is someone behind the screen that you are delivering your msg to.
Una lack communication skills mkuu lazima ujue jinsi ya kudeliver message kwa mtu kama kweli unataka kusikilizwa,hata kama unamcritisize kuna jinsi ya kumwambia mtu na asijisikie vibaya!Na lazima ujue huo ujumbe unaopeleka una uzito gani na utamuathiri vipi mtu na ndio maana tukapewa emotions,sympathy and empathy.
 
yaani roho inaniuma sana.mimi umri mdogonilio nao nalea watoto wawili wa marehemu dada yangu(mungu ampunzishe kwa amani) baada ya kuzalishwa na wanaume tofauti.isitoshe baba zao wapo mitaani wanazurura tu yaani roho inaniuma sana.hao watoto niwajue kwa lote kuhusu malazi,maradhi,chakula,matibabu na shule. yaani mi nafikiria nitajipanga lini.kwani nafikiria nikio huyo mwanamke ataweza kukaa na hawa watoto na wanawake wenyewe wa siku hizi.lakini ok mungu atanilipia tu.

Pole sana Shekau.Mungu ni mwema sana atakufanyia wepesi na uombe na kufunga ili upate mke atakaelea hao watoto vizuri na kwa upendo ili wasijione wakiwa,maana wanawake sisi ni wabaya afadhali ya chui.Mungu akutie nguvu usikate tamaa maisha yako yatanyooka kwa namna ya pekee.
 
kaka hukunielewa vizuri,nimesema ktk kufatilia nilijikuta nina baba wawili,moja niliye ambiwa na ndugu zangu na mwangine niliye ambiwa na mama yangu wote niliwasiliana nao kwa simu na sio ana kwa ana na wote walikubali.hapo ndipo nilipo pata tatizo tena pia sijaomba msaada kutoka kwa yoyote hata siku moja nilichosema ni kuwa siku nikiwa na pesa nisafiri nikawacheki labda nitagundua ni yupi kati yao.

aaaa... Kumbe!! huyo aliyekwambia mama yako ndiye. Basi hilo liache, hayo mengine zingatia. Huna UPUNGUFU kama unavyoonyesha kwenye hadithi yako.
 
Mmmhhh...isije kuwa amezaa na baba yake...
Si unajua kuna wababa wanabaka au kulaghai mabinti zao...
Otherwise why????

mkaka fula hv rafki yangu alikua baba ake
yule mama akaanza kuumwa akamwita mwanawe akamwambia niahidi hutamtafuta baba ako ht nikifa
yule mama amekufa mkaka hana jinsi yupo tu
 
aisee kuna haja ya mimi kurudi chuo. Kumbe mtu anakuwa objective anapotoa mtazamo wa tofauti na wenzie, na mwingine anakuwa subjective mtazamo wake unapofanana na wa yule anayezungumziwa! objectivity=non-conformity. Ingekuwa hoja hapa ni jua linachomoza magharibi na kuchwea mashariki labda ningewaelewa wanaojiita objective, lakini kuongelea hali ambayo haifanani hata kwa watu wenye nayo ukweli ni kuwa unakuwa objective kwenye subjectivity yako tu na si vinginevyo. na ndo unakuta mtu anadai single mom anajinyanyapaa na anamfananisha na gay anayepaza sauti yake apewe uhuru wake na straights wanaojiona wana haki zaidi. Anadai gay anajinyanyapaa wakati akijikubali anatungiwa sheria ili anyongwe au afungwe. Objectivity in deed!!
Nimependa sana ulivyofafanua chukua like!
 
We are not in a battle field nor are we arguing. I respect your line of thinking & believe that you are entitled to your opinions.
Cool. I do respect yours too, I understand there is a lot you are not disclosing but I still feel there is something you are doing wrong. Besides I have nothing to gain or lose for whatever decision you take. Just think about it.
 
ha ha ha lol we mshari kweli tangia jana unapayuka tu! NB:nawakilisha nilichoandika!Accept other peoples choices and stop judging them period!TAKE IT OR LEAVE IT!
Exactly!!! Nilijua usingeelewa. Anyway its alright.
 
Sijamzi maneno mabaya ila namweleza ukweli wa kilichotokea. Na wala sijali hata akimuuliza baba ake kwan ndicho alichokifanya. Simsingizii ila namweleza ukweli binti yake wa kile baba yake alikifanya.
Unahitaji darasa zito la saikolojia ya watoto. Huyo mtoto unamuharibu wala humsaidii kama unavyodhani.
 
Inashangaza kwa kweli, nitaelewa kwa mtu aliyebakwa na kupata ujauzito lakini umeiachia kwa hiari?

Sielewi kabisa hizi 'solidarity foreva' zinakujaje. Na tangu enzi na enzi wapo tu watu wanaolelewa na mzazi mmoja.
Kuna wengine ni kweli inabidi wahurumiwe sana ila kuna baadhi unakuta chupi wanavua wenyewe, na wanajua kabisa wanaweza kupata mimba, huyo mwanaume mwenyewe hawajaongea lolote kuhusu uwezekano wa mimba na nini kinafuata, wanapigwa mimba wanatoswa halafu wanalialia wahurumiwe. Mbaya zaidi hawataki kukubali kuwa hata wao wana makosa. Mimi nimewauliza kwenye moja ya comment zangu, unamwamini mwanaume umezaliwa naye?!! Kingine kumbukeni hata kama wanaume pia wana makosa lakini anayebeba mimba ni mwanamke. Sasa endeleeni kuhurumiana na hizi "I am proud" kinda of statements.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom