Sinagogi hili la Siloam Ministries

Sinagogi hili la Siloam Ministries

Dini ya leo ni biashara inayolipa sana na kila mwenye uelewa kidogo wa theolojia hutaka kuanzisha kanisa lake
Kuna baadhi licha ya pesa Kuna mambo ya siri wanafanya au wana taratibu zao zenye kuacha maswali mengi
Hivi karibuni nilikutana na mwamimi aliyekimbia kanisa la Sialom mkoani pwani akanihadithia mengi ya kushangaza
-kwao majina si kama haya yetu bali majina yao ni kama haya..Siku yake!Ahadi!Agano! Kimbilio! Jaribu nk nk
-Chakula kwao wanaita karamu
-Maji yanaitwa damu yake
-wakipigiwa simu hawataji eneo husika bali wanasema wako mlima wa moto ili adui asijue uko wapi
-Wanaamini makombo ni tiba (makombo ya Chakula wanakula makuhani wao )
-viongozi wao wanajulikana kwa jina la makuhani
-ibada zao huanza saa sita alfajiri kwa kughani maneno ya kujirudiarudia tena kwa sauti ya juu (kupayuka)
-nguo zao ni suruari fupi nyeupe na kanzu
Maisha yao kwa sehemu kubwa wanategemea malipo kwa wale wanaokuja kuponywa kanisani
Hii ni imani lakini ni vema ukaamini kitu kisicho na ukakasi...muumini huyu amefanikiwa kukimbia na sasa yuko huru
Yote haya yanaletwa na stress za maisha, kabla ya awamu ya tano kukaba kila kona ulisikia watu wanakula makombo kanisani?
 
HHAHAHHAHHAHHAAHAHH ni hatariiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
Kuna jamaa yangu kakimbilia huko alikuwa mlutheli,sasa ukimpigia simu ukitaja jina lake anakata simu then anakutumia sms anakwambia mimi naitwa nuru huyo unayemtaja ni mdudu gani simfahamu!
iiiiiii Yesu nipe macho mimi uwiiiii sio kwa kusombwa hivi
 
Wanaamini kuwa wao ndio wako kwenye imani iliyo sahihi kuliko watu wengine, Mungu wao ni Mungu wa Elijah.
 
  • Thanks
Reactions: dtj
Nabii wao Elia hakufa alipaa walimuona
Nasikia eti mke wa Elia anataka mali za kanisa ziwe zake kuna ka ugomvi na viongozi wa kanisa
ila nimesikia tu s
 
Nabii wao Elia hakufa alipaa walimuona
Nasikia eti mke wa Elia anataka mali za kanisa ziwe zake kuna ka ugomvi na viongozi wa kanisa
ila nimesikia tu s
Na pia inawezekana ulisikia ukiwa kwenye njozi, wasikuulize mengi. Tumekuelewa mkuu.
 
Nabii wao Elia hakufa alipaa walimuona
Nasikia eti mke wa Elia anataka mali za kanisa ziwe zake kuna ka ugomvi na viongozi wa kanisa
ila nimesikia tu s
Na kanisa limesha gawanyika Mara mbili kunawafuasi wa mke wa Eliya na wale wasiokuwa wafuasi wake
 
Pool of Siloam!

Hili kanisa ni moja kati ya makanisa ya kiroho lililo tofauti na makanisa yote ya kikristo. Ngoja nikupe story kidogo juu ya hili kanisa,
Mosi.... Hakuna popote penye ishara/alama ya msalaba kama ilivyo makanisa mengine ya kikristo, ndani ya majengo ya makanisa yao.

Pili... Kila mkoa Tanzania una jina lake, Kwa mfano Moshi panaitwa Ararati, Singida panaitwa Sayuni, Mwanza - Yericko,

Hata hapa DSM kila kitongoji kina jina lake, Mfano TABATA inaitwa, .... wanajua wenyewe

Tatu: Kiongozi wao anaitwa MUNGU WA MAJESHI- MIAKA 1000 , wanamwabudu kama mungu, wanaamini hata huwezi kumuona

Nne: Mwanzilishi wa hilo kanisa , alikuwa anaitwa Munuo (Mmachame), alifariki mwaka juzi bila kukosea, akazikwa huko Bagamoyo, wanasema alipaa mbinguni kama Yesu, hata vyombo vya habari ya CNN , BBC vilionyesha. Ajab hakuna local media hata moja iliyoripoti tukio kubwa kama hilo.

wachungaji wengi wa hilo kanisa ni Wamachame

Tano: Biblia yao haina kava la juu, wameweka lakwao, kila siku wanabadili na kupunguza mistari kwenye biblia, MUNGU WA MAJESHI anasemu MUNGU wetu aliye hai ndie kamwaguza kufanya hivyo. Kwa kifupi biblia yao ina viaraka

Sita: wanaposali /wakiwa kwenye maombi wanatingisha vichwa , na kubana sauti inakuwa kavu hatari. Kama ni mara ya kwanza kwenda hapo, huwezi kusikia chochote.

Saba: waumini wao wana hali mbaya sana kiuchumi.

Nane:
Hawatumii miezi yetu, sijui February, Janurary au March , wao miezi yao ni Zifa, n.k

Ukienda hapo utastaajabu....

Pole yao ,kila mtu aamini chake .Haya makanisa ni wizi wa mchana kwa watanzania wajinga waliojiunga nayo.
 
Maisha yamekua magumu sana kudanganya mtu imekua pia rahisi ili aungane na wewe wote mzame kwenye ujinga...huu ulokole naamini utapita baada ya miaka kadhaa watu watajitambua..kwasasa ukweli hakuna mshika dini...
 
Shika neno tenda neno ndio salamu yao
Muumini akifariki kwao ni sherehe hipika vyakula vya kila aina na hakuna kulia
 
  • Thanks
Reactions: dtj
Achana na imani za watu fateni zenu, nadhani ndo nyinyi hata Bible mwaichukia bila sababu usomaji wenu ka msaishaji paper,
 
Back
Top Bottom