Sinagogi hili la Siloam Ministries

Sinagogi hili la Siloam Ministries

Kuna jamaa yangu kakimbilia huko alikuwa mlutheli,sasa ukimpigia simu ukitaja jina lake anakata simu then anakutumia sms anakwambia mimi naitwa nuru huyo unayemtaja ni mdudu gani simfahamu!
Hahahahah dah, jamaa yako imani yake ni kiwango cha mbingu aise
 
Hahahahah dah, jamaa yako imani yake ni kiwango cha mbingu aise
Hahahaha hatari hiyo mkuu lkn sio kwa mwendo huo...
Inamaana anakosoa hata jina alilopewa na wazazi wake(akitoka mungu ndio wazazi wake) daah sometimes ukibase kwenye dini saana (sio kwamba haitakiwi,ila imani yako ndio inakuponya aisee) unaharibikiwa kabisa...
 
Haya makanisa sasa balaa ....kuna Mchungaji nilikutana naye mbeya....aisee nilimweleza yanayonisibu kusudi nipate huduma duh!unaweza ukakimbia ..
1.Aliniambia nitafute laini imeishia namba Kumi au Tisa iwe voda au Tigo.
2.Kitambaa Cheupe kikubwa.
3.Kwenye bahasha niweke Sh.Elfu Saba kwa siku tatu mfululizo ninavyoenda kumwona niende nayo nisipunguze wala kuongeza.
4.Nitafute Mshumaa mkubwa mmoja.
5.Kuna chupa moja kubwa ya mafuta ninue jina limenitoka ila alisema mafuta ya mizeituni kitu kama hicho.....nikaenda Dukani kuulizia inauzwa Elfu ishirini.....Alfu ndo nianze naye kuwasiliana.....Duh!nilichoka mwwnyewe kiukweli siku nilivyoenda kwenye ibada zake sasa.....Alikuwa anapaka Mafuta kwenye mkono alafu waumini mnapanga Foleni kwenda kugusa ule mkono.....ila kabla kuugusa unaweka chini kuanzia Sh.Elfu moja kwenda mbele kusudi upate baraka na ufanikiwe....yani tangia siku hiyo sikurudi tena maana ni bonge la biashara jamaa anafanya .....Alfu njee alikuwa anapaki bonge moja ya Gari....
 
Pool of Siloam!


Pili... Kila mkoa Tanzania una jina lake, Kwa mfano Moshi panaitwa Ararati, Singida panaitwa Sayuni, Mwanza - Yericko,

Hata hapa DSM kila kitongoji kina jina lake, Mfano TABATA inaitwa, .... wanajua wenyewe

Nane: Hawatumii miezi yetu, sijui February, Janurary au March , wao miezi yao ni Zifa, n.k

Ukienda hapo utastaajabu....

Cha kushangaza jina la kanisa lao ni Sialom ministries,
 
Niliwahi kumpeleka mtu kanisani kwao kwa ajili ya maombi, nilipofanikiwa kutoka getini niliapa sitakuja kurudi tena eneo la kanisa lile
 
Kuuumbe,nashukuru nimejua,hao watu wamekuja kujenga kanisa lao hapa ila halina msalaba wala nn na hata jina majirani hatujui ila tunawajua kwa mavazi yao meupe,basi.na wanafijo hao na magari nahisi kila muumini ana gari
 
Back
Top Bottom