Sinagogi hili la Siloam Ministries

Sinagogi hili la Siloam Ministries

Shika neno tenda neno mtumishi, ukiwa wa imani tofauti hata salamu hupati na wanaoana wao kwa wao, ukimtaka mtumishi lazima ukasali kanisani kwake na uvae kanzu/gauni jeupe na ushinde kanisani siku nzima
Hivi wao hawafanyi kazi? Mpk wanashinda kanisani muda wote
 
Mke wangu akifiwa na baba yake mkubwa,tukaenda kuzika. Kumbe alishahamia huko kwenye hilo dhehebu kutoka lutheran. Sasa sisi tunamfahamu kama mzee Tito,kumbe kule keshapewa jina jingine la UFAHAMU. Nilichoka. Wana mambo ya ajabu sijawahi kuona. Niliapa kukitokea msiba mwingine nyumba hiyo na wanaozika ni hao siloam sikanyagi. Bora ndoa ivunjike.
 
Hatari sana,kuna jirani yetu mkewe kaingia kwenye hiyo dini.
Kwa sasa anamuita mumewe kichwa.
namnukuu...jamani mmekutana na kichwa changu leo.?...
Duhhhhh eti umekutana na kichwa changu me namwambia Acha upumbavu kichwa chako unacho
 
Dini ya leo ni biashara inayolipa sana na kila mwenye uelewa kidogo wa theolojia hutaka kuanzisha kanisa lake
Kuna baadhi licha ya pesa Kuna mambo ya siri wanafanya au wana taratibu zao zenye kuacha maswali mengi
Hivi karibuni nilikutana na mwamimi aliyekimbia kanisa la Sialom mkoani pwani akanihadithia mengi ya kushangaza
-kwao majina si kama haya yetu bali majina yao ni kama haya..Siku yake!Ahadi!Agano! Kimbilio! Jaribu nk nk
-Chakula kwao wanaita karamu
-Maji yanaitwa damu yake
-wakipigiwa simu hawataji eneo husika bali wanasema wako mlima wa moto ili adui asijue uko wapi
-Wanaamini makombo ni tiba (makombo ya Chakula wanakula makuhani wao )
-viongozi wao wanajulikana kwa jina la makuhani
-ibada zao huanza saa sita alfajiri kwa kughani maneno ya kujirudiarudia tena kwa sauti ya juu (kupayuka)
-nguo zao ni suruari fupi nyeupe na kanzu
Maisha yao kwa sehemu kubwa wanategemea malipo kwa wale wanaokuja kuponywa kanisani
Hii ni imani lakini ni vema ukaamini kitu kisicho na ukakasi...muumini huyu amefanikiwa kukimbia na sasa yuko huru
saa sita alfajiri ikoje mkuu!!!
 
Wana bifu sababu ya hela.KANISA (Mke wa marehemu Eliya kizazi cha nne) anataka kuwapanda kichwani kina MIAKA 1000(Ambaye Eliya alimkabidhi huduma).Sasa WAKUU WA NJIA hawamkubali MIAKA 1000,wameenda kumchoma kwa KANISA.KANISA amepata kiburi akazira kusali hapo makao makuu mbezi.
 
Haya makanisa sasa balaa ....kuna Mchungaji nilikutana naye mbeya....aisee nilimweleza yanayonisibu kusudi nipate huduma duh!unaweza ukakimbia ..
1.Aliniambia nitafute laini imeishia namba Kumi au Tisa iwe voda au Tigo.
2.Kitambaa Cheupe kikubwa.
3.Kwenye bahasha niweke Sh.Elfu Saba kwa siku tatu mfululizo ninavyoenda kumwona niende nayo nisipunguze wala kuongeza.
4.Nitafute Mshumaa mkubwa mmoja.
5.Kuna chupa moja kubwa ya mafuta ninue jina limenitoka ila alisema mafuta ya mizeituni kitu kama hicho.....nikaenda Dukani kuulizia inauzwa Elfu ishirini.....Alfu ndo nianze naye kuwasiliana.....Duh!nilichoka mwwnyewe kiukweli siku nilivyoenda kwenye ibada zake sasa.....Alikuwa anapaka Mafuta kwenye mkono alafu waumini mnapanga Foleni kwenda kugusa ule mkono.....ila kabla kuugusa unaweka chini kuanzia Sh.Elfu moja kwenda mbele kusudi upate baraka na ufanikiwe....yani tangia siku hiyo sikurudi tena maana ni bonge la biashara jamaa anafanya .....Alfu njee alikuwa anapaki bonge moja ya Gari....
Huyo hana tofauti na waganga na wachawi mitaani
 
Kwa fikra zangu naona hiyo ni dini ya kiyahudi. wayahudi walimuona Yesu lakini hawaamini katika yeye, ndio maana hakuna alama ya msalaba kwenye masinagogi yao.
Ndiyo maana wanatumia majina ya kiyahudi kwa viongozi wao kama kuhani n.k.
Kuhusu kalenda, kama hutambui ujio wa Yesu hata kalenda yetu ya kawaida hutaifuata. kalenda zetu za kawaida zinazingati mwaka wa kuzaliwa Yesu kuwa ni mwaka wa kwanza, hadi leo ni miaka 2017 toka kuzaliwa Yesu.
Wanatumia biblia sawa, lakini huenda wanazingatia agano la kale tu maana hilo hata Yesu alilikuta.
Dini ni njia ya iimani kwa Mungu wetu, Wakristu wanaamini ktk YESU na kwamba njia sahihi ya kwenda mbinguni ni kupitia kwake. waislam wanamini katika Mtume Mohamed (SAW). Hawa nao wako poa!
 
  • Thanks
Reactions: dtj
Shika neno tenda neno ndio salamu yao
Muumini akifariki kwao ni sherehe hipika vyakula vya kila aina na hakuna kulia
Kuna msiba wa jirani yetu wakaja wachungaji wao si majirani yupo kwenye majonzi maana alifariki wakati anajifungua badala ya hosiptal wakampeleka kanisani damu zinavuja wanakemea kuja kuzinduka kumpeleka mwananyamala mama kafa kwenye msiba kama sherehe wanaimba wanasema mwenzetu kalala huyu haleluya amefika mbinguni
 
Kuna msiba wa jirani yetu wakaja wachungaji wao si majirani yupo kwenye majonzi maana alifariki wakati anajifungua badala ya hosiptal wakampeleka kanisani damu zinavuja wanakemea kuja kuzinduka kumpeleka mwananyamala mama kafa kwenye msiba kama sherehe wanaimba wanasema mwenzetu kalala huyu haleluya amefika mbinguni
Ndivyo walivyo mkuu!
Nimewahi hudhuria moja kati ya misiba yao
Nikabaki nashangaa tu
 
  • Thanks
Reactions: dtj
Kwa fikra zangu naona hiyo ni dini ya kiyahudi. wayahudi walimuona Yesu lakini hawaamini katika yeye, ndio maana hakuna alama ya msalaba kwenye masinagogi yao.
Ndiyo maana wanatumia majina ya kiyahudi kwa viongozi wao kama kuhani n.k.
Kuhusu kalenda, kama hutambui ujio wa Yesu hata kalenda yetu ya kawaida hutaifuata. kalenda zetu za kawaida zinazingati mwaka wa kuzaliwa Yesu kuwa ni mwaka wa kwanza, hadi leo ni miaka 2017 toka kuzaliwa Yesu.
Wanatumia biblia sawa, lakini huenda wanazingatia agano la kale tu maana hilo hata Yesu alilikuta.
Dini ni njia ya iimani kwa Mungu wetu, Wakristu wanaamini ktk YESU na kwamba njia sahihi ya kwenda mbinguni ni kupitia kwake. waislam wanamini katika Mtume Mohamed (SAW). Hawa nao wako poa!
Hamna lolote hili dhehebu ni tatizo Mimi nilishtuka na kuogopa waliponiambia kwamba shetani alishauwawa na huyo mwazilishi wao Elia. Bila maono ya Roho Mtakatifu wengi wataangamia.
 
  • Thanks
Reactions: dtj
Back
Top Bottom