Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,400
- 465,175
- Thread starter
- #281
Sehemu ya 92
Siku moja jioni baada ya kutoka matembezini, niliporudi nyumbani, wakati nafika getini nilimkuta Lawalawa akinongoja kwa shauku.
“Kuna ugeni. Ugeni wa wasiwasi.” Lawalawa aliniambia.
“Ugeni gani huo wa wasiwasi?”
“We’ ingia ndani uone.”
Nilipita ndani, Lawalawa akanifuata kwa nyuma. Nilipofika koridoni. Nilishituka sana kwa watu nilokuwa wamekaa kwenye viti mbele yangu.
Alikuwa ni mke wangu Pili na mwingine alikuwa ni mzee mwenye baraghashia kichwani. Baada ya wao kuniona, Kila mmoja alishituka.
Nilitembea kuwafauta. “Karibuni jamani,” niliwakaribisha, ingawa sikujua kule kuwakaribisha kama kulitoka moyoni ama nilijisemea tu ili mradi.
Mpenzi wangu Lawalawa aliniletea kiti na kuketi mbele yao. Yeye alisimama kando kusikiliza mazungumzo yetu.
“Pili hujambo?”
“Sijambo, ”alinijibu bila kuniangalia usoni.
“Mzee shikamoo.” “Marhabaa!. Bila shaka wewe ndiye Ajibu?”
“Naam! mimi ndiye,”nilimjibu mzee yule aliyeonekana kujawa na shari usoni mwake. “Nimekungoja kwa muda mrefu hapa, naomba tuongee pembeni ili niondoke zangu.” Alisema yule mzee.
“Kwani hampo wote pamoja?” nilimuliza, nikimaanisha kwamba ujio wao hakuwa wa pamoja na mke wangu Pili. Ujio wenye ajenda ya pamoja. “Hata!...” mzee yule alinijibu. Uso wake uliendelea kuonyesha hakuhitaji maswali zaidi ya kunieleza kilichomleta.
Akaendelea kuniambia:
“Huyu bibi amenikuta, ndio maana nakwambia nimefika hapa muda mrefu, hebu nakuomba kijana, tuongee kando ili niwahi kuondoka, mimi mgeni hapa Tabora ujue.”
Alaa!!... Kweli huu ni ugeni wa wasiwasi, huyu mzee anatokea wapi? ana shida gani na mimi? Amejuaje kwamba mimi naishi kwenye mji huu? Nilijiuliza bila majibu.
Nilisimama tukasogea hatua chache.
“Nakusikiliza mzee.” Nilisema. “Naitwa mzee Mwakanjara Kisu ni babu yake na Felix Kisu....”
Alipojitambulisha tu hivyo tumbo likapata joto, kimoyomoyo nikasema kumekucha. Akaendelea.
“Nimekuja hapa kutaka jambo moja tu baba, sio kukuomba, laah! Kutaka.” Alisema, akaweka kituo huku akiniangalia usoni kwa makini sana.
“Nimekuja kutaka ukafukue uchawi ulifukia makaburini ili mwanangu awe huru na maradhi uliyomtupia, vinginevyo nakupa siku tatu kisha utaona. Umesikia?”
Siku moja jioni baada ya kutoka matembezini, niliporudi nyumbani, wakati nafika getini nilimkuta Lawalawa akinongoja kwa shauku.
“Kuna ugeni. Ugeni wa wasiwasi.” Lawalawa aliniambia.
“Ugeni gani huo wa wasiwasi?”
“We’ ingia ndani uone.”
Nilipita ndani, Lawalawa akanifuata kwa nyuma. Nilipofika koridoni. Nilishituka sana kwa watu nilokuwa wamekaa kwenye viti mbele yangu.
Alikuwa ni mke wangu Pili na mwingine alikuwa ni mzee mwenye baraghashia kichwani. Baada ya wao kuniona, Kila mmoja alishituka.
Nilitembea kuwafauta. “Karibuni jamani,” niliwakaribisha, ingawa sikujua kule kuwakaribisha kama kulitoka moyoni ama nilijisemea tu ili mradi.
Mpenzi wangu Lawalawa aliniletea kiti na kuketi mbele yao. Yeye alisimama kando kusikiliza mazungumzo yetu.
“Pili hujambo?”
“Sijambo, ”alinijibu bila kuniangalia usoni.
“Mzee shikamoo.” “Marhabaa!. Bila shaka wewe ndiye Ajibu?”
“Naam! mimi ndiye,”nilimjibu mzee yule aliyeonekana kujawa na shari usoni mwake. “Nimekungoja kwa muda mrefu hapa, naomba tuongee pembeni ili niondoke zangu.” Alisema yule mzee.
“Kwani hampo wote pamoja?” nilimuliza, nikimaanisha kwamba ujio wao hakuwa wa pamoja na mke wangu Pili. Ujio wenye ajenda ya pamoja. “Hata!...” mzee yule alinijibu. Uso wake uliendelea kuonyesha hakuhitaji maswali zaidi ya kunieleza kilichomleta.
Akaendelea kuniambia:
“Huyu bibi amenikuta, ndio maana nakwambia nimefika hapa muda mrefu, hebu nakuomba kijana, tuongee kando ili niwahi kuondoka, mimi mgeni hapa Tabora ujue.”
Alaa!!... Kweli huu ni ugeni wa wasiwasi, huyu mzee anatokea wapi? ana shida gani na mimi? Amejuaje kwamba mimi naishi kwenye mji huu? Nilijiuliza bila majibu.
Nilisimama tukasogea hatua chache.
“Nakusikiliza mzee.” Nilisema. “Naitwa mzee Mwakanjara Kisu ni babu yake na Felix Kisu....”
Alipojitambulisha tu hivyo tumbo likapata joto, kimoyomoyo nikasema kumekucha. Akaendelea.
“Nimekuja hapa kutaka jambo moja tu baba, sio kukuomba, laah! Kutaka.” Alisema, akaweka kituo huku akiniangalia usoni kwa makini sana.
“Nimekuja kutaka ukafukue uchawi ulifukia makaburini ili mwanangu awe huru na maradhi uliyomtupia, vinginevyo nakupa siku tatu kisha utaona. Umesikia?”